Dalili za kuvimba kwa ovari.
 Posti hii inazungumzia kuhusiana na kuvimba kwa ovari kunakosababishwa na maambukizo ya bakteria na kawaida huweza kusababishwa na magonjwa sugu katika Maambukizi ya mfumo wa Uzazi wa mwanamke.
Dalili na ishara za Mgonjwa aliye vimba ovari
1.maumivu katika tumbo la chini. Kutokana na uvimbe uliojitokeza kwenye ovari.
2.damu ya hedhi ambayo ni nzito kuliko kawaida kutokana na viuvimbe vidogovidogo vilivyopo kwenye Njia ya Uzazi
3.kutokwa na damu kati ya mzunguko wa hedhi.Na hedhi hii huwa na maumivu makali kuliko Kawaida .
4. maumivu au kutokwa na damu wakati wa kujamiiana.hii Ni mbaya kwasababu hupelekea maumivu wakati wa tendo la ndoa pia na Damu kutoka.
5.kutokwa na uchafu mwingi wa uke, ambao unaweza kuwa na harufu mbaya.na uchafu huu huaribu mfumo mzima wa Uzazi pia kupelekea kansa ya kizazi.
6.kuungua au maumivu wakati wa kukojoa,mkojo kutoka na Moto (burning urination) ambapo hupelekea maamivu makali wakati tu wa kukojoa
7. ugumu wa kukojoa. Muda mwingine hupelekea kushindwa kukojoa kabisa au mkojo kutoka kidogo Sana au kutokutoka kabisa.
8. homa, baridi kichefuchefu na kutapika, kutoka na maumivu makali ya tumbo.
Mwisho,kwa mwenye Dalili za ovari anatakiwa kupata huduma ya haraka, pia anashauriwa aache kufanya tendo la ndoa mara atakapogundua anaugonjwa huu na anashauriwa asishikiri tendo la ndoa wakati wa matibabu mpaka atakapopona.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Mambo ya kuzingatia kwa mama ili apate huduma endelevu.
Posti hii inazungumzia kuhusiana na huduma kwa mama wajawazito na waliojifungua.
Soma Zaidi...Utaratibu kwa wajawazito na wanaonyonshesha wakiwa na virusi vya ukimwi na ukimwi
Je kuna madhara kwa mwenye virusi vya ukimwi kunyonyesha ama kubeba mimba, na nini afyanye kama ameshabeba mimba ama kama ananyonyesha
Soma Zaidi...Imani potofu kwa mwanamke mwenye mimba
Posti hii inahusu zaidi imani potofu kwa mwanamke mwenye mimba, ni Imani ambazo zimekuwepo kwenye jamii kuhusu wanawake wenye mimba.
Soma Zaidi...Je endapo mama atafanya tendo la ndoa wiki moja kabla ya kuingia hedhi anaweza kupata ujauzito?
Zipo siku maalumu ambazo mwanamke hupata mimba. Siku hizi huzoeleka kwa jina la siku hatari. Je ungependa kufahamu mengi kuhusu siku hatari, endelea na makala hii.
Soma Zaidi...Namna za kujilinda na fangasi ukeni
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuepuka fangasi za ukeni, ni njia ambazo usaidia kuepuka madhara ya fangasi za ukeni.
Soma Zaidi...