Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Taharuki kwa mfalme

Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Taharuki kwa mfalme

Muendelezo.....

Download Post hii hapa

TAHARUKI YA MFALME

 

 

Basi mfalme na waziri wake wakaenda mpaka kwenye bostani. Loo walikuta na geti lipo wazi. Waakingia bila hata ya tatizo. Walishangaa sana kukuta kuna watu watatu wakiwa katika furaha kubwa sana wakiimba na kunywa. Mfalme na waziri wake wakanyata ili wasionekane na mtu wasijewakavuruga burudani ya watu hawa. Basi wakanyata kwa kufuata miti ya matunda. Mfalme akapanda juu ya mti kuchunguli kupitia kwenye dirisha.

 

 

 

Loo alishangaa sana kumuona mzee ibrahimu akiwa amelewa. Hakika hajapatapo kumuona mzee Ibrahimu akiwa katika hali hii kwa miaka 13 sasa. Basi baada ya kushangaa kwa uda akashuka ili apate kutafakari. Akamwambia waziri wake Jafari panda na wewe ujionee maajabu ya watu hawa. Jaafari alipopanda alishangaa zaidi. Wakaanza kushauriana nini wafanye, ili wapate kujuwa hasa ni kitu gani kimewatokea watu hawa na mzee Ibrahim. Wakaamuwa wakabadili mavazi yao waingie kama watu wasiojulikana ili wapate kufahamu ukweli wamambo.

 

 

 

Wakati wanatafuta cha kufanya, mfalme akamuona kijana mmoja mvuvi aliyejulikana kwa jina la Karim. Mfalme akamwambia waziri amsubiri palepale asiondoke mpaka arudi. Waziri hakufahamu wapi mfalme anakwenda hata hivyo pia hakumuoona yile mvuvi. Karim hana ajualo alipofika karibu na geti akalikuta lipo wazi. Akaingia mule ndani kwa siri ili kavue samaki kwenye kajibwawa ka mfalme kwa siri wakati ule wa usiku.

 

 

 

Alipofika kwenye kibwawa akatupa nyavu yake kisha akaanza kusubiri inase samaki wengi. Kumbe mfalme alikuwa nyuma yake. Alipohakikisha samaki ni wengi akatoa nyavu yake. Loo kugeuka nyuma anamuona mfalme. Alijitupa chini ya muguu kuomba msamaha. Mfalme akamsamehe kisha wakabadilishana mavazi. Mfalme akachukuwa samaki wawili na kumuachia akarimu aondoke na samaki wake. Mflme akiwa katika mavazi ya Karim alirudi akiwa na samaki wake mpaka alipo Waziri wake. Akamsalimia, kwa hakika waziri alijuwa anaongea na Karimu. Loo kumbe alikuwa ni mfalme. Hapo mfalme akasema “kama wewe ambaye hujalewa umeshindwa kunijuwa vipi Ibrahim ambaye amelewa atanijuwa.

 

 

 

Basi mfalme akamwambia tena waziri wake amsubiri palepale asiondoke. Sasa mfalme akijifanya ni mvuvi akagonga hodo kwenye lile geti kwa sauti ya juu akijifananisha na Karim. Mzee Ibrahim akauliza nani wewe. Akajibu mfalme ni mimi karim, nimekuletea samaki. Sasa mzee ibrahi anafahamiana na Karim na huwa wanauziana samaki. Kijana Nurdin aliposikia samaki uchu ukamtoka. Akamlazimisha mzee aagize samaki aletewe. Wakaltwa samaki ila yule mrembo alipowaona ni wazima kwenye ndoo ya maji akaomba akaangiwe kwanza.

 

 

 

Mzee Ibrahimu bila ya kuelewa akamuagiza mvuvi akawakaange kisha aje nao. Mfalme akatoka hadi alipo waziri wake. Kisha akamueleza kuwa ameambiwa awakaange. Waziri akataka kulifanya yeye jukumu lake, ila mfalme akakataa alitaka kutimiza amri kama mvuri. Hivyo akaagiza aletewe kila kitu kinachohusika katika kukaanga mpaka chumvi. Alipoletewa aliwakaanga vyema sana kwa umakini mkubwa kisha akawapelekea kwa Mzee Ibrahim. Nurdini alifurahi sana na akampatia mvuvi kiasi kikubwa cha dhahabu ambapo ni mara 100 ya malipo halisi ya samaki wale.

 

 

 

Mfalme akiwa katika umbo la mvuvi alishukuru sana. Yule mtumwa (mke wa Nurdini) alifurahi zaidi na akaanza kuimba tena na kupiga gitaa. Mfalme alifurahi sana na kuonyesha furaha yake dhahiri. Bila ya kujuwa hili wala lile Nurdini akamwambia “mvuvi wewe ni mkarimu sana, umeleta samaki na ukawakaanga, ilaonyesha umependezwa sana na mtumwa wangu huyu. Kuanzia sasa nakupatia iwe kama zawadi yako. An-neese aliposikia maneno hayo alilalamika sana kwa kutumia mashairi, alionyesha dhahiri kuwa hakupenda uamuzi ule, hakupenda kutengena na Nurdini wake. Mfalme ilibidi aulize hasa nini kimetokea kati yao ama ana deni?

 

Kufikia hapo Nurdini akaanza kuhadithi kila ambacho kilichotokea. Kutoka baba yake akiwa karibu na Mfalme mpaka kununuliwa mtuwa. Kifo cha baba yake hata kukimbiwa na marafiki. Mwisho mpaka anakuja Baghadad na kukutana na mzee Ibrahimu. Mfalme akiwa anasikiliza maneno haya alikuwa akivijwa na machozi. Hakika yalukuwa ni maeneno yenye kutia huruma na simanzi.

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Mankaa image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Burudani File: Download PDF Views 306

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 19: Kinyozi
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 19: Kinyozi

Hii ni simulizi iliyopo ndani ya kitabi cha pili cha hadithi za HALIF LELA U LELA.....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 1 Part 2: Simulizi ya kisa cha mfugaji na mkewe
Simulizi za Hadithi EP 1 Part 2: Simulizi ya kisa cha mfugaji na mkewe

Simulizii hii ni inatoka katika kitabu cha kwanza cha HALIF LELA U LELA

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 8: Aliyekatwa kidole gumba
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 8: Aliyekatwa kidole gumba

Kojawapo ya simulizi iliyopo kwenye kitabu cha pili cha hadithi za HALIF LELA U LELA.....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 1: Hadithi ya chongo watatu, watoto wa mfalme na wanawake wa Baghdad.
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 1: Hadithi ya chongo watatu, watoto wa mfalme na wanawake wa Baghdad.

Skmulizii hii pia imetoka kitabu cha kwanza cha HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 15: Mji uliogeuzwa mawe
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 15: Mji uliogeuzwa mawe

Hadithi hii inapatikana katika kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 4: Kilema mtanashati asiye na mkono
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 4: Kilema mtanashati asiye na mkono

Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili.....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 3 Part 4: Kisa cha waziri aliyeadhibiwa
Simulizi za Hadithi EP 3 Part 4: Kisa cha waziri aliyeadhibiwa

Simulizii hii inapatikana katika kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA

Soma Zaidi...