Menu



Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Taharuki kwa mfalme

Muendelezo.....

TAHARUKI YA MFALME

 

 

Basi mfalme na waziri wake wakaenda mpaka kwenye bostani. Loo walikuta na geti lipo wazi. Waakingia bila hata ya tatizo. Walishangaa sana kukuta kuna watu watatu wakiwa katika furaha kubwa sana wakiimba na kunywa. Mfalme na waziri wake wakanyata ili wasionekane na mtu wasijewakavuruga burudani ya watu hawa. Basi wakanyata kwa kufuata miti ya matunda. Mfalme akapanda juu ya mti kuchunguli kupitia kwenye dirisha.

 

 

 

Loo alishangaa sana kumuona mzee ibrahimu akiwa amelewa. Hakika hajapatapo kumuona mzee Ibrahimu akiwa katika hali hii kwa miaka 13 sasa. Basi baada ya kushangaa kwa uda akashuka ili apate kutafakari. Akamwambia waziri wake Jafari panda na wewe ujionee maajabu ya watu hawa. Jaafari alipopanda alishangaa zaidi. Wakaanza kushauriana nini wafanye, ili wapate kujuwa hasa ni kitu gani kimewatokea watu hawa na mzee Ibrahim. Wakaamuwa wakabadili mavazi yao waingie kama watu wasiojulikana ili wapate kufahamu ukweli wamambo.

 

 

 

Wakati wanatafuta cha kufanya, mfalme akamuona kijana mmoja mvuvi aliyejulikana kwa jina la Karim. Mfalme akamwambia waziri amsubiri palepale asiondoke mpaka arudi. Waziri hakufahamu wapi mfalme anakwenda hata hivyo pia hakumuoona yile mvuvi. Karim hana ajualo alipofika karibu na geti akalikuta lipo wazi. Akaingia mule ndani kwa siri ili kavue samaki kwenye kajibwawa ka mfalme kwa siri wakati ule wa usiku.

 

 

 

Alipofika kwenye kibwawa akatupa nyavu yake kisha akaanza kusubiri inase samaki wengi. Kumbe mfalme alikuwa nyuma yake. Alipohakikisha samaki ni wengi akatoa nyavu yake. Loo kugeuka nyuma anamuona mfalme. Alijitupa chini ya muguu kuomba msamaha. Mfalme akamsamehe kisha wakabadilishana mavazi. Mfalme akachukuwa samaki wawili na kumuachia akarimu aondoke na samaki wake. Mflme akiwa katika mavazi ya Karim alirudi akiwa na samaki wake mpaka alipo Waziri wake. Akamsalimia, kwa hakika waziri alijuwa anaongea na Karimu. Loo kumbe alikuwa ni mfalme. Hapo mfalme akasema “kama wewe ambaye hujalewa umeshindwa kunijuwa vipi Ibrahim ambaye amelewa atanijuwa.

 

 

 

Basi mfalme akamwambia tena waziri wake amsubiri palepale asiondoke. Sasa mfalme akijifanya ni mvuvi akagonga hodo kwenye lile geti kwa sauti ya juu akijifananisha na Karim. Mzee Ibrahim akauliza nani wewe. Akajibu mfalme ni mimi karim, nimekuletea samaki. Sasa mzee ibrahi anafahamiana na Karim na huwa wanauziana samaki. Kijana Nurdin aliposikia samaki uchu ukamtoka. Akamlazimisha mzee aagize samaki aletewe. Wakaltwa samaki ila yule mrembo alipowaona ni wazima kwenye ndoo ya maji akaomba akaangiwe kwanza.

 

 

 

Mzee Ibrahimu bila ya kuelewa akamuagiza mvuvi akawakaange kisha aje nao. Mfalme akatoka hadi alipo waziri wake. Kisha akamueleza kuwa ameambiwa awakaange. Waziri akataka kulifanya yeye jukumu lake, ila mfalme akakataa alitaka kutimiza amri kama mvuri. Hivyo akaagiza aletewe kila kitu kinachohusika katika kukaanga mpaka chumvi. Alipoletewa aliwakaanga vyema sana kwa umakini mkubwa kisha akawapelekea kwa Mzee Ibrahim. Nurdini alifurahi sana na akampatia mvuvi kiasi kikubwa cha dhahabu ambapo ni mara 100 ya malipo halisi ya samaki wale.

 

 

 

Mfalme akiwa katika umbo la mvuvi alishukuru sana. Yule mtumwa (mke wa Nurdini) alifurahi zaidi na akaanza kuimba tena na kupiga gitaa. Mfalme alifurahi sana na kuonyesha furaha yake dhahiri. Bila ya kujuwa hili wala lile Nurdini akamwambia “mvuvi wewe ni mkarimu sana, umeleta samaki na ukawakaanga, ilaonyesha umependezwa sana na mtumwa wangu huyu. Kuanzia sasa nakupatia iwe kama zawadi yako. An-neese aliposikia maneno hayo alilalamika sana kwa kutumia mashairi, alionyesha dhahiri kuwa hakupenda uamuzi ule, hakupenda kutengena na Nurdini wake. Mfalme ilibidi aulize hasa nini kimetokea kati yao ama ana deni?

 

Kufikia hapo Nurdini akaanza kuhadithi kila ambacho kilichotokea. Kutoka baba yake akiwa karibu na Mfalme mpaka kununuliwa mtuwa. Kifo cha baba yake hata kukimbiwa na marafiki. Mwisho mpaka anakuja Baghadad na kukutana na mzee Ibrahimu. Mfalme akiwa anasikiliza maneno haya alikuwa akivijwa na machozi. Hakika yalukuwa ni maeneno yenye kutia huruma na simanzi.

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Mankaa image Tarehe 2024-09-10 15:02:55 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Masomo File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 183


Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zifazofanana:-

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 3: Uokozi kwenye kisiwa
Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza...... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Barua ya mfalme wa baghadad
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 3 Part 5: Simulizi ya samaki wa ajabu
Simulizii hii inapatikana kwenye hadhithi za HALIF LELA U LELA katika kitabu cha kwanza.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 10 Part 7: Taharuki
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 1: Hadithi ya safari saba za Sinbad
Hadithi hii inapatikana katika kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 10: Mapenzi kwenye mtihani
Simulizii hii inapatikana katika kitabu cha pili cha hadithi za HALIF LELA U LELA.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 7 Part 2: Aladini kwenye pango la utajiri
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 2 Part 1: Hadithi ya jini na mfanya biashara.
Hadithi hii ya jina na mfanya biashara imetoka katika kitabu cha kwanza cha simulizi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza karibu tusikilize simulizi nzuri na zakusisimua Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 19: Mfalme na waziri wake
Hadithi hii inapatikana katika kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 15: Mji uliogeuzwa mawe
Hadithi hii inapatikana katika kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA.... Soma Zaidi...