image

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 4: Simulizi ya chongo wa kwanza mtoto wa Mfalme

Tusikilizie simulizii inahusu chongo wa kwanza wa mtoto wa mfalme iliyopo ndani ya kitabu cha kwanza cha Hadithi za HALIF LELA U LELA.....

CHONGO WA KWANZA MTOTO WA MFALME

 

kwanza utambue mimi ni mtoto wa mfalme na ni wa kipekee katika uzawa. Hivyo kwa upekee wangu nilipokea mapenzzi makubwa kutoka kwa baba na mama. Mama yangu alifariki nikiwa mdogo. Hivyo kwa muda mrefu nilibaki na baba yangu. Nilikuwa napenda kuwinda ndege kwa kutumia mishale. Nilikuwa nikitembea na waziri mkuu ninapokwenda kuwinda.

 

Sikumoja tulipokuwa mawindoni nilikuwa nikilenga shabaha shingo ya ndege aliyejificha kwenye kitundu chake. Bila ya kujuwa hili wala lile kumbe waziri alikuwa nyuma ya kile kitundu nae akimvizia yule ndege. Nikarusha mshale wangu na kumpata waziri kwenye jicho. Waziri aligugumia sana kwa maumivu makali yaliopelekea kupata chongo. Nilimuomba msamaha lakini alionesha kutokuridhia na kuamini kuwa nilifanya kwa makusudi.

 

Tulivofika nyumbani nikamueleza baba stori mzima hapo baba akamuita waziri na kutaka kumfariji. Waziri hakutaka chochote na mwisho aliahidi kuwa lazima alipe kisasi kwa yaliyompata. Tulikaa kwa muda mrefu hata nikasahau tukio lile. Nilipata safari ya kwenda kumuona mjomba wangu ambae pia ni mfalme aliyekuwa ni jirani na utawala wa baba. Mjomba huyu nae alinipenda sana. Wakati mwingiune hunambia anaponiona eti namkumbusha marehemu dada yake.

 

Mjomba alikuwa na kijana wake mmoja ambaye ni binamu yangu. Mimi na kaka huyu tulukuwa marafiki sana tulipokuwa wadogo. Hata hivyo urafiki wetu uliendelea hata nilivyokuwa mkubwa. Nilikwenda kwake kumsalimia. Kwakweli alifurahi sana uwepo wangu. Tulizungumza mengi sana na kufurahi pia. Tulipokula chakula cha usiku akanambia “kuna kitu nataka nikuoneshe, nilikuwa ninakiandaa toka ulipoondoka wakati ule”. Basi akachukuwa taa na kuniambia nimfate.

 

Tulikwenda kwa muda wa usiopungua dakika 20 na tukakuta nguzo mbili zilizokaa mfano wa mlango. Tulipofika pale akanambia nifukue pale chini. Bila kuchelewa nikatafuta mijiti na kuanza kuchimba pale. Urefu wa shibri moja nikakuta zege, akanambia “fungua huo ni mlango”. Nikafungua na kukuta ngazi. Tukachuka kwenye ngazi ile na kukutana chini kuna mfano wa mlango ndani ya handaki. Akfungua mlango ule na tukaona nyumba nzauri sana. Akanambia “turudi sasa hiki ndio kitu nilichokuwa naandaa, nakuomba usimwambie mtu jambo hili”.

 

Basi tuliporudi siku ile sikuweza kulala usiku nilikuwa nikiwaza ni la nini jumba lile na ni kwa nini anafanya siri. Niliwaza mengi mpaka nikapitiwa na usingizi. Siku ilofata tuliendelea kufanya mabo ya kawaida mpaka. Baada ya wiki tatu binamu yangu aliniita na kunambia niende nyumbani kwake muda wa usiku. Basi nikaenda na kunambia kuwa “kuna mwanamke atakuja hapa umchukuwe wende nae pale kwa siku ile na mimi nitakuja baadae.

 

Mambo yakawa kama vile haikupita muda yule mwanamke akaja na nikaenda nae mpaka pale. Hatukukaa sana binamu yangu akaja akiwa amebeba mfuko wa sementi na nyumdo na chepe. Bila ya kuzungumza na mtu alipofika pale akaanza kufukuwa mpaka akaikuta ile zege. Akafungua mlangomule na kushuka yeye na yule mwanamke kisha akanambia “ahasante sana nakushukuru wewe rudi na usimueleze yeyote jambo hili”. Basi akaziba ule mlango na mimi nikarejea nyumbani.

 

Nilikaa siku tatu kisha nikarejea kwa baba. Nilipofika kule nilishangaa sana mambo yamebadilika sana. Nilipouliza wakaniambia kuwa baba yangu amepinduliwa na mfalme wa sasa ni waziri mkuu yule niliyemtoboaga jicho lake. Nilishangaa sana na haukupita muda nikakamatwa na kuingizwa mahabusu. Waziri akaja na kunambia sasa umefika muda wake wa kilipiza kisasi. Nilimuomba sana msamaha lakini alikataa.akaamrisha askari wake anichukuwe na akaniuwe na kunitowa jicho moja la kulia.

 

Basi askari yule akanichukuwa mpaka mbali na kunambia “ nikifikiria wema alotufanyia baba yako siwezi kukuuwa lakini naomba uniridhie nikutoe jicho ili kumridhisha mfalme wa sasa na nitamwambia nimesha kuuwa”. Nilikubali nikamuomba niingie porini na kutafuta dawa ya kunifanya nipoteze fahamu. Dawa hii nilifundishwaga na binamu yangu. Yeye alikuwa akiitumia dawa hii anapokuwa na mawazo mengi hivyo hujipoteza fahamu kwa muda.

 

Nilitafuta dawa hivyo kwa muda na nikaipata nikayafikicha majani yake na yalipotowa mai nikayanywa na nikapoteza fahamu muda ulelule na sikujuwa kinacho endelea. Nakuja kuamka nikiwa na maumivu makali sana kichwani na jichoni nikiwa chongo asiye na jicho moja la kulia. Askari akanambia niondoke aneo lile na nisirudi tena nchi ile. Nilirudi kule kwenye utawala wa mjomba wangu.

 

Kufika kwamjomba nae alikuwa katika hali nzito ya kumtafuta mtoto wake. Alifurahi pindi aliponiona maana aliamini nitakuwa na taarifa kuhusu mtoto wake. Aliponambia ni mwezi sasa hajaonekana nilipatwa na hofu, hivyo nikamueleza mjomba kuhusu stori nzima. Usiku ulipoingia nilitoka na mjomba kwa siri na kuelekea kule kwenye ule mjumba wa ardhini. Basi tukaingia palele baada ya kuvunja mlango. Tulipofika kwenye jumba ile tukaingia na tukakuta kuna moshi pale ndani. Tulipopita moshi ule tukamkuta binamu yangu amelala chini akiwa amekauka kama amebanikwa nyama.

 

Kuona hali ile mjomba alilia sana na akanambia tutoke na tumuache palelpale. Tulipofika pale nje akanambia “nilijuwa tu nilipomuaona anakaana mwanamke yule nikajua kuwa atakufa tuu, yule mwanamke ni jini”. Basi akanambia nisimwambie yeyote habari ile. Niliishi na mjomba kwa muda ila alifariki na nikachukuwa madaraka yake.

 

Siku moja nilishangaa kuona ufalme wangu umezungukwa na askari wa ile nchi ya mjomba. Kumbe yule waziri aliyempindua baba amekuja kupindua na utawala wa mjomba wangu. Kwakuwa nchi yangu haijajiandaa kwa vita niliamua kukimbia ilikuepusha vifo vya watu. Niliondoka pale nikawa nalanda mpaka nikafika nchi hii ya baghdad nikanyoa nyusi zangu na nikakutana na wenzangu wawili hawa maka tukafika hapa. Hii ndio stori yangu. Zubeida kusikia maneno yale alifurahi sana kwa stori ile na kumwambia umeokoka. Akamfata chongo wa pili na kumwambia tuambia na wewe stoti yako. Naye akaanza kama ifuatavyo:-





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Mankaa Tarehe 2024-09-09 13:49:59 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Masomo File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 34


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 1: Muuaji ni nani?
Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 13: Sehemu ya sita ya safari ya Sinbad
Muendelezo wa safari ya Sinbad iliyopo ndani ya kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Barua ya mfalme wa baghadad
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 6: Sehemu ya tatu ya safari ya Sinbad
Muendelezo wa sehemu ya tatu ya safari ya Sinbad iliyopo kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 10 Part 7: Taharuki
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 11: Hadithi ya kisiwa cha mawe yanayolia
Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 7 Part 2: Aladini kwenye pango la utajiri
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 16: Viatu vya ajabu vyaondoka na mkono wangu
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 15: Baba tajiri na kifo chake
Muendelezo....... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 2 Part 4: Hadithi ya mzee wa tatu na mbwa wake mwekundu.
Hadithi za HALIF LELA U LELA hii ni moja wapo imetoka katika kitabu cha kwanza imaelezea kisa cha mzee wa tatu.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP7  Part 17: Jaribio la tatu kwa Aladini
Muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 17: Siri ya wageni yafichuka
Muendelezo........ Soma Zaidi...