Simulizi za Hadithi EP 6 Part24 : Kaka wa tatu wa kinyozi

Simulizi za Hadithi EP 6 Part24 : Kaka wa tatu wa kinyozi

Muendelezo

Download Post hii hapa

HADITHI YA KAKA WA TATU WA KINYOZI

 

 

 

Kaka yangu wa tatu alikuwa ni kipofu. Alipata upofu badala ya kupata ajali katika shughuli zake za kutafuta mali. Baada ya kupata upofu alikuwa akijipatia pesa kwa kuombaomba kutoka kwa watu. Kaka hakuwa na mke wala watotot. Ilitokea siku moja katika kuombaomba kwake alifika kwenye nyumba moja. Akagonga mwenyenyumba alipouliza kaka hakujibu kitu. Lengo lake ilikuwa mpaka ajemwenyeyumba ili atakapomuona ataweza kumsaidia. Kwa mara ya pili mwenyenyumba akauliza “wewe nani na unataka nini?”/ kaka hakujibu kitu hata akauliza kwa mara ya tatu bila ya majibu tena.

 

 

Mwenyenyumba alikasirika na akatoka kuja mlangoni. Alipofika mlangoni akamkuta kaka. Kaka akamweleza kuwa anahitaji msaada japo wa chakula ama pesa. Kwa hasira mwenyenyumba akamwambia nifate. Kaka akamfuata kwa kumshika kipande cha kanzu yake. Wakiwa wanapanda ngazi za gorofa kaka aligundua kuwa walikufika hadi gorofa la nne. Juu kileleni mwenyenyumba akamwambia kaka “umesema unahitaji nini” kaka akajibu “msaada, wa kifedha ama chakula”. mwenyenyumbq akajibu “ruka chini hapo msaada upo huko mbele” kaka akagunduwa kuwa endapo ataongeza hatua mbili mbele ataangukia chini. “kama hutaki kunisaidia si ungenieleza tu toka mwanzo” “nilipouliza nani aliyekuwepo mlangoni na nini unataka haukunijibu” yalikuwa ni maneno ya kaka na mwenyenyumba.

 

 

Kaka akagunduwa kuwa endapo ataendelea kupoteza muda anaweza kuuwawa ama kupata madhara zaidi. Kaka akashuka kwa haraka huku anahisabu vingazi alipokazibia chini kwa bahati mbaya alianguka na kuumia vibaya. Kaka akaelekea asikokujuwa akiwa anaugumia maumivu ya mguu. Katika kutembea huku na kule alikutana na vipofu wengine wawili. Kwa kuwa nao walikuwa hawakujui wendako wakaungana na kutengeneza mstari mmoja wa vipofu. Wakiwa wanatembetembea wakafika kwenye kajumba kamoja wakakaa. Wakiwa wamepumzika ghafla wakasikia sauti za watu zinawakaribia.

 

 

Kaka akashauri wenzie wazunguke nyuma ya nyumba wajifiche wasije onekana. Wakazunguka nyuma kimyamkimya, na baada ya muda wale watu wakaingia kwenye kijumba kile na kuakuzungumza. Katika mazungumzo ya watu wale kaka aligunduwa kuwa walikuwa ni wezi na pale walikuja kuficha pesa walizoiba. Walipatana warudi pale baada ya wiki moja huku wakisubiria mtaani kutulitulia. Waliziweka pesa zao kwenye moja ya sanduku la mbao lililopo pale ndani. Kisha wakaondoka zao.

 

 

Kaka na wenzie walikaa kule nyuma ya kijumba kile, kisha walipojiridhisha kuwa wale watu hawapo tena walirudi walipokuwa mwanzo. Wakajadiliana na kukubaliana kuwa wazitfute zile pesa na wagawane. Wakaingia ndani na kuzitafuta. Baada ya muda wakafanikiwa kuzipata. Loo ilikuwa ni viande 3000 vya dhahabu na 200 vya silva. Wakakubaliana kugawana kiasi kile cha pesa. Wakati wapo katika harakati za kugawana kaka aligunduwa kuwa kuna mgeni kati yao. Kaka akawaambia wenzake “mbona kuna mtu mwingine kati yetu”. Wakaanza kuchunguza wakamgundua mtu wa nne.

 

 

Wakamkamata na kuanza kumshambulia kwa kumpiga. Kaka akachukuwa zile pesa na kuzificha tena. Kakana wenzake wakamburuza yule mwingine hadi mbali kidogo na lile eneo a kuanza kumshambulia tena. Haukupita muda watu wakaanza kujaa. Yule mtu mwingine akajichokowa kwenye macho na kuwa kama kipofu. Kisha akaanza kuguta kelele “jamani naombeni msaada, hawa wenzangu wananionea na kunidhulumu, naombeni msaada”. watu wakaona wawapeleke wote kwa kadhi apate kutoa hukumu kati yao.

 

 

Kadhi alipouliza hasa kilichotokea yue mtu akasema “kadhi niadhibu kwanza kisha nitakueleza kila kitu” basi kadha akaamrisha apingwe viboko 25. kisha akaanza kueleza “sisi unaotuona hapa wote si vipofu. Tumeigiza kuwa vipofu ili tupate kuwaibia watu na kuapata msaada wa bure kifedaha. Na kwa kutumia njia hii tumenufaika vyema” kisha akafumbuwa macho yake Loo!! hakuwa kipofu hata kidogo kisha akaendelea kusema “leo tulipata pesa vipande 300 vya dhahabu na 200 vya silva. Lakini tulipokuwa tunagawana wenzangu wakanidhulumu wakati mimi ndiye niliyepata pesa hiyo. Ninakuomba uwaadhibu vikali ili wafunguwe macho yao, na waseme ukweli”.

 

 

Basi kaka na wenzake wakaanza kuadthibiwa kwa mijeledi . walichapwa viboko 25, waliposhindwa kufungua macho yao wakaongezwa viboko 25 hata wakashindwa kukaa wala kuzungumza. Kisha wakamuelekea yule mtu wakambana vyema aeleze ukweli vinginevyo ataadhibiwa tena. Ndipo akaanza kutaja kuwa pesa zimefichwa sehem flani, na kama kadhi ataahidi kuwa naye atapewa shea atawaonyesha mahali pesa ilipofichwa. Pia aliongezea kwa kusema “hawa hawatafumbua macho kwa hofu, hivyo kuthibitisha utapeli wetu na wao na kutaka kunidhulumu kwao nitakwenda kuonyesha mahali esa ilipo”.

 

 

Kadhi akachaguwa kundi la askari limfate. Akaenda nao mpaka kwenye kale kajumba na kuzitowa zile pesa. Kadhi akampatia yule mtu fungu lake na zilizobakia zikawekwa kwenye hazina ya nchi. Kaka na wenzake wakafukuzwa mjini na hawakutakiwa kuonekana tena. Mimi nilipopata habari hizi nikaenda kumchukuwa kaka kwa siri. Mpaka kufikia hapa kinyozi akamaliza stori ya kaka wake wa tatu. Kisha akaendelea kuhadithia kilichompata kaka wa nne kama ifuatavyo:-

 

 

 

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Mankaa image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Burudani File: Download PDF Views 332

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Simulizi za Hadithi EP 3 Part 2:  Simulizi ya tabibu wa mfalme
Simulizi za Hadithi EP 3 Part 2:  Simulizi ya tabibu wa mfalme

Simulizi ni nzuri sana maana zinafundisha na hazibagui mkubwa wala mdogo... tusikilize na kusoma kisa cha tabibu wa mfalme....kutoka katika kitabu cha kwanza cha HALIF LELA U LELA...

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 3 Part 5: Simulizi ya samaki wa ajabu
Simulizi za Hadithi EP 3 Part 5: Simulizi ya samaki wa ajabu

Simulizii hii inapatikana kwenye hadhithi za HALIF LELA U LELA katika kitabu cha kwanza....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 2: Kisa cha kinyozi msiri..
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 2: Kisa cha kinyozi msiri..

Karibuni tuendelee kusimuliana stori za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza, stori nzuri sana na za kuvutia zimeandaliwa kwaajili ya kujifunza na kujiburudisha pia.....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Hadithi ya Nurdini Mtoto wa Waziri
Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Hadithi ya Nurdini Mtoto wa Waziri

Hii ni hadithi ya kitabu cha tatu cha hadithi za HALIF LELA U LELA...

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 6: Hadithi ya Ndoa ya siri
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 6: Hadithi ya Ndoa ya siri

Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili muendelezo....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 2 Part 3: Hadithi ya mzee wa pili na mbwa wawili weusi.
Simulizi za Hadithi EP 2 Part 3: Hadithi ya mzee wa pili na mbwa wawili weusi.

Simulizi za HALIF LELA U LELA ni nziri sana tuwe pamoja kusikiliza kisa cha mzee wa pili na mbwa wawili weusi...

Soma Zaidi...