Wakati Nabii Musa(a.
Wakati Nabii Musa(a.s) amekwenda kupokea Taurati, katika hizo siku arobaini alizoahidiwa na Mola Wake, Saamiriy alitengeneza sanamu la ndama wa ng'ombe linalotoa sauti unapovuma upepo na kuwashawishi Bani Israil walifanye mungu sanamu hilo la ndama.
"Na kumbukeni tulipomuahidi Musa siku arobaini (afanye ibada mfululizo) Mkamfanya ndama (kuwa Mungu) baada yake, na mkawa madhalimu (wa nafsi zenu)" (2:51).
Harun(a.s) aliyemkaimu Nabii Musa(a.s) aliwakataza watu wake wasiabudie sanamu la ndama. Baadhi wakamtii na wengine wakamuasi.
Na Harun aliwaambia zamani (akasema): "Enyi watu wangu! Hakika nyinyi mumefitinishwa tu kwa (kitu) hiki. Na kwa yakini Mola wenu ni yule Mungu Mwenye kurehemu. Basi nifuateni na tiini amri yangu (muache kuabudu Mungu huyu)".
Wakasema: "Hatutaacha kabisa kumuabudu mpaka Musa arejee kwetu, (aturudie)" (20:90-91).
Musa(a.s) aliporejea alimlaumu Harun(a.s) kwa kutomfuata huko alikokuwa baada ya watu wake kumuasi. Harun(a.s) alijitetea kuwa hakufanya hivyo kwa kuchelea kuwafarakanisha Bani Israil kwa kuondoka na kundi moja na kuliacha lingine nyuma kabla ya kauli yake (Musa(a.s)) - rejea (Qur'an 2:92-94).
Musa(a.s) aliondoa ile fitina kwa kumuadhibu Saamiriy na walioshirikiana naye na kuliangamiza lile sanamu.
Ikumbukwe kuwa ni muda mfupi sana toka Bani Israil walipokombolewa kutokana na utumwa wa Firauni. Lakini mara wanamsahau Mola wao na kuanza kuabudu ndama. Hii inaonesha ni kwa kiwango gani Bani Israil waliathiriwa na maisha ya ushirikina kwa kipindi walichoishi Misr. Ni muhimu basi tuone jinsi mazingira yanavyoathiri imani, maadili na mwenendo wa mtu.
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu
Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF
Share On
Facebook
or
Whatsapp
Imesomwa mara 310
Sponsored links
๐1 Madrasa kiganjani
๐2 Kitau cha Fiqh
๐3 kitabu cha Simulizi
๐4 Kitabu cha Afya
Mafunzo yatokanayo na kuanzishwa kwa dola ya uislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
MTUME MUHAMMAD (S.A.W) KULELEWA NA BABA YAKE MDOGO MTUME (ABU TALIB)
KULELEWA NA BABA YAKE MDOGOBaada ya kufariki kwa mzee huyu, kiongozi mkubwa wa maquraysh na makkah, kiongozi ambaye jeshi la Abrah liliangamizwa ndani ya utawala wake. Soma Zaidi...
Nini maana ya tabii tabiina
Soma Zaidi...
Hadhi na haki za Mwanamke katika jamii za Mashariki ya Kati bara la arabu hapo zamani
Soma Zaidi...
HISTORIA YA MTUME YUNUS(A.S)
Nabii Yunus(a. Soma Zaidi...
Kuhajiri Waislamu wa Makka Kwenda Madinah
Baada ya mikataba miwili ya โAqabah na baada ya Waislamu 75 kufika Yathrib salama, Mtume(s. Soma Zaidi...
MAMA YAKE MTUME MUHAMMAD (S.A.W) ANAMLEA MTUME MUHAMAD AKIWA NA UMRI WA MIAKA MINNE (4)
KULELEWA NA MAMA YAKE ALIPOFIKA MIAKA MINNEMtume (s. Soma Zaidi...
Jinsi tukio la Karatasi lilivyotokea wakati wa Mtume siku chache kabla ya kifo chake
Tukio la kartasiTukio la โkartasiโ lililonakiliwa katika vitabu vya Muslim na Bukhari kuwa siku tatu kabla ya kutawafu Mtume (s. Soma Zaidi...
Je, Nabii Isa(a.s) ni Mtoto wa Mungu?
Mwenyezi Mungu si kiumbe. Soma Zaidi...
Kuchaguliwa kwa Makhalifa wanne baada ya kutawaf (kufariki) kwa Mtume muhammad (s.a.w)
8. Soma Zaidi...
Mafunzo yatokanayo na hijrah ya mtume na maswahaba wake
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...