picha

Bani Israil Kuabudu Ndama

Wakati Nabii Musa(a.

Bani Israil Kuabudu Ndama

Bani Israil Kuabudu Ndama


Wakati Nabii Musa(a.s) amekwenda kupokea Taurati, katika hizo siku arobaini alizoahidiwa na Mola Wake, Saamiriy alitengeneza sanamu la ndama wa ng'ombe linalotoa sauti unapovuma upepo na kuwashawishi Bani Israil walifanye mungu sanamu hilo la ndama.



"Na kumbukeni tulipomuahidi Musa siku arobaini (afanye ibada mfululizo) Mkamfanya ndama (kuwa Mungu) baada yake, na mkawa madhalimu (wa nafsi zenu)" (2:51).

Harun(a.s) aliyemkaimu Nabii Musa(a.s) aliwakataza watu wake wasiabudie sanamu la ndama. Baadhi wakamtii na wengine wakamuasi.




Na Harun aliwaambia zamani (akasema): "Enyi watu wangu! Hakika nyinyi mumefitinishwa tu kwa (kitu) hiki. Na kwa yakini Mola wenu ni yule Mungu Mwenye kurehemu. Basi nifuateni na tiini amri yangu (muache kuabudu Mungu huyu)".
Wakasema: "Hatutaacha kabisa kumuabudu mpaka Musa arejee kwetu, (aturudie)" (20:90-91).



Musa(a.s) aliporejea alimlaumu Harun(a.s) kwa kutomfuata huko alikokuwa baada ya watu wake kumuasi. Harun(a.s) alijitetea kuwa hakufanya hivyo kwa kuchelea kuwafarakanisha Bani Israil kwa kuondoka na kundi moja na kuliacha lingine nyuma kabla ya kauli yake (Musa(a.s)) - rejea (Qur'an 2:92-94).



Musa(a.s) aliondoa ile fitina kwa kumuadhibu Saamiriy na walioshirikiana naye na kuliangamiza lile sanamu.



Ikumbukwe kuwa ni muda mfupi sana toka Bani Israil walipokombolewa kutokana na utumwa wa Firauni. Lakini mara wanamsahau Mola wao na kuanza kuabudu ndama. Hii inaonesha ni kwa kiwango gani Bani Israil waliathiriwa na maisha ya ushirikina kwa kipindi walichoishi Misr. Ni muhimu basi tuone jinsi mazingira yanavyoathiri imani, maadili na mwenendo wa mtu.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1740

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app    👉2 web hosting    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Kazi na wajibu wa khalifa katika dola ya kiislamu

Kazi na Wajibu wa KhalifaKhalifa katika Serikali ya Kiislamu ndiye mtendaji mkuu wa Serikali kama alivyokuwa Mtume(s.

Soma Zaidi...
Kulingania Uislamu kwa Jamii Nzima

Baada ya miaka mitatu ya Utume, Muhammad(s.

Soma Zaidi...
NI UPI MKATABA WA AL-FUDHUL NA ASILI YAKE, ATHARI ZAKE NA WALOHUSIKA

MKATABA WA AL-FUDHULBaada ya vita hivi viongozi wa pande mbili hizi waliamuwa wakae chini na wakubaliane kuweka kanun i na utaratibu utakaozuia kutotokea uonevu kama huuu tena.

Soma Zaidi...
Mtume Muhammad alelewa na mama yake mzazi akiwa na umri wa miaka 4.

Sura na historia ya Mtume Muhammad S.A.W sehemu ya 8. Hapa utajifunza malezi ya Mtume kutokakwa Halimavkuja kwa mama yake.

Soma Zaidi...
Kujengwa upya al Kabah baada ya kuwa na mipasuko.

Sira na historia ya Mtume Muhammad s.a.w sehemu ya 18. Hapa utajifunza kuhusu tukio la kujengwa upya kwa al kaaba 🕋

Soma Zaidi...