picha

NAMNA YA KUBORESHA MBEGU ZA KIUME, NA VYAKULA VYA KUBORESHA NGUVU ZA KIUME

Njoo ujifunze vyakula vya kuboresha mbegu za kiume na nguvu za kiume.

NAMNA YA KUBORESHA MBEGU ZA KIUME, NA VYAKULA VYA KUBORESHA NGUVU ZA KIUME

VYAKULA VYA KUBORESHA MBEGU ZA KIUME




Ugumba si kwa wanawake tu, wapo hata wanaume wanatatizo hili. Lakini kutokubebesha mimba ama kubeba mimba pekee haimaanishi kuwa wewe ni mgumba. Mwanaume kumbebesha mimba mwanamke kunategemea mambo mengi kutoka kwa mwanaume mwenyewe na kwa mwanamke mwenyewe. Katika makala hii nitazungumzia kipengele kimoja tu nacho ni tatizo la kutokuwa na mbegu bora za kiume.



Mwnaume anapokojoa bao moja anatoa mbegu zaidi ya milioni 300. katika mbegu hizo ni moja tu ndiyo intakayofanikiwa kitungisha mimba. Mamimioni ya mbegu haya yanakufa bila hata ya kulifikia yai, kutokana na udhaifu wao, kutoweza kuogelea vyema, ukali wa tindikali katika tumbo la mwanamke n.k. sasa ili mwanaume aweze kubebesha ujauzito anatakiwa atoe mbegu bora na imara zinazoweza kuishi ndani ya tumbo la mimba kwa muda mrefu.



Inatokea baadhi ya wanaume mbegu zao zinakuwa sio imara kutosheleza. Hii inakuwa ni ngumu kubebesha ujauzito. Lakini kumbuka kama mambo mengine yakiwa sawa hata mwenye mbegu dhaifu inaweza kubebesha mimba endapo itakuwa ni siku sahihi ya kukutana na yai, hazitachukuwa muda kukutana na yai ama zilitolewa nyingi.



Sasa ikiwa tatizo ni hili la mbegu ni dhaifu, je nitawezaje kuboresha mbegu zangu? Yes ni swali zuri sana, na inapasa hasa kulijuwa jibu lake. Mbegu utaweza kuziporesha kwa kubadilisha mlo ama kutumia dawa ama njia nyinginezo. Miongoni mwa njia hizo ni:-



Njia za kuboresha mbegu za kiume.
1.Badili mlo wako.
Muonekano wako leo ni sawa na chakula unachokila. Ladha na ubora wa manii na mbegu za kiume pia hutegemeana na unachokila. Kama unataka kuboresha mbegu za kiume kwanza anza na kubadili mlo wako. Jitahidi kula vyakula vifuatavyo:-



A.Vitamini B-12
Vitamini hivi unaweza kuvipata kwenye nyama, samaki na maziwa. Vitamini hivi husaidia sana katika afya ya mbegu za kiume.



B.Vitamini C
Hivi unaweza kuvipata kwenye machungwa, viaz mbatatai, nyanya, apinach na kwenye matunda yenye uchachu na mapapai na mananasi. Vitamini C pia ni muhumu kwa afya ya mfumo wa kinga



C.Kula vyakula jamii ya korosho na karanga



D.Kula vyakula vyenye lycopene. Vyakula hivi kuwa na rangi nyekundu kama tikiti na nyanya



E.Kula vyakula vyenye madini ya zinc kwa wingi. Unaweza kupata madini haya kwenye nyama, samaki wa baharini kwenye magobeta jamii ya kaa, mimea jamii ya kunde, kula mbegu kama mbegu za maboga na nyingine, maziwa, mayai, jamii ya korosho, baadhi ya mboga za majani kama maharagwe ya kijani na nafaka nzima.



2.Fanya mazoezi ya mara kwa mara.
Mazoezi si kwa ajuli ya hili tu bali pia ni kwa ajili ya kuboresha afya kwa ujumla. Si lazima ufanye mazoezi mareefu, hapana kwa uchache pia inatosha.



3.Punguza kuvaa nguo za ndani zenye joto.
Afya ya mbegu za kiume inategemea pia joto la mwili wako. Hakikisha korodani unazipa hewa ya kutosha. Usivae nguo za kubana nyingi kama chupi, si salama kwa wanaume. Boxa kama haibani sana inatosha.



4.Punguza unywaji wa pombe, na soda kama unakunywa kwa kiasi kikubwa.





                   



Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 9223

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Dua za Mitume na Manabii    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Sababu za mimba ya miezi 4-6 kutoka.

Posti hii inahusu zaidi sababu za mimba ya miezi kuanzia minne mpaka sita kutoka , Kuna kipindi mimba kuanzia miezi mimne mpaka sita utoka kwa sababu mbalimbali.

Soma Zaidi...
Je? Naomba kuuliza mkewangu ali ingiya kwenye hezi siku tatu damu ikakata nikakutana nae siku ya nane je? Anaweza pata ujauzito

Idadi ya siku hatari za kupata mimba hutofautiana kutoka kwa mwanamke mmoja namwinhine. Kinda ambao idadivyavsikuvzao za hatari ni nyingi kuliko wengine.

Soma Zaidi...
Nataka nijue Kuwa njia yakuzuia mimba wakati Wakufany tendo La ndoa

Je ungependa kuijuwa Njia ya kuzuia mimba wakati wa tendo la ndoa?. Posti hii itakwenda kukufundisha ujanja huu.

Soma Zaidi...
Mapendekezo muhimu kwa wajawazito

Posti hii inahusu zaidi mapendekezo muhimu kwa wajawazito, haya ni mapendekezo yaliyotolewa na wataalamu wa afya ili wajawazito waweze kule mimba zao vizuri na kuweza kujifungua vizuri na kupata watoto wenye afya njema na makuzi mazuri pasipokuwepo na ule

Soma Zaidi...
mpenzi wangu nimeshiriki nae tendo la ndoa akiwa siku zake za hatar kwa siku 3 lakin hajashika mimba tatizo linaweza kuwa ni nini?

Kupata ujauzito hufungamana na mambo mengi ikiwepo afya vya wawili yaani me na mume na mengineyo. Unaweza kushiriki sikuvhatari na usiupate mimba. Postivhii ibakwendavkukufahamisha undani wa jambo hili.

Soma Zaidi...
Kuwepo kwa mabonge ya damu wakati wa hedhi

Posti hii inahusu zaidi kuwepo kwa mabonge ya damu wakati wa hedhi, tunajua kabisa wakati wa hedhi damu inapaswa kuwa nyepesi na ya kawaida ila kuna wakati mwingine inakuwa na mabonge zifuatazo ni sababu za kuwepo kwa mabonge ya damu wakati wa hedhi.

Soma Zaidi...
Njia za kugundua kama mtoto amevunjika baada ya kuzaliwa

Post hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo mtoa huduma anaweza kuzitumia kuangalia kama mtoto amevunjika baada ya kuzaliwa.

Soma Zaidi...
Dawa hatari kwa mwenye ujauzito

Hii ni orodha ya dawa ambazo hutumiwa sana na watu kutoka maduka ya dawa lakini sio salama kwa wajawazito.

Soma Zaidi...
Mbinu za kuwakinga watoto na saratani.

Posti hii inahusu zaidi mbinu ambazo tunaweza kuzitumia ili kuwakinga watoto dhidi ya saratani, kama tulivyotangulia kusema kwamba saratani ya watoto mara nyingi Usababishwa na akina Mama hasa kwa sababu ya mtindo wa maisha wakati wa ujauzito kwa hiyo tun

Soma Zaidi...