picha

NAMNA YA KUBORESHA MBEGU ZA KIUME, NA VYAKULA VYA KUBORESHA NGUVU ZA KIUME

Njoo ujifunze vyakula vya kuboresha mbegu za kiume na nguvu za kiume.

NAMNA YA KUBORESHA MBEGU ZA KIUME, NA VYAKULA VYA KUBORESHA NGUVU ZA KIUME

VYAKULA VYA KUBORESHA MBEGU ZA KIUME




Ugumba si kwa wanawake tu, wapo hata wanaume wanatatizo hili. Lakini kutokubebesha mimba ama kubeba mimba pekee haimaanishi kuwa wewe ni mgumba. Mwanaume kumbebesha mimba mwanamke kunategemea mambo mengi kutoka kwa mwanaume mwenyewe na kwa mwanamke mwenyewe. Katika makala hii nitazungumzia kipengele kimoja tu nacho ni tatizo la kutokuwa na mbegu bora za kiume.



Mwnaume anapokojoa bao moja anatoa mbegu zaidi ya milioni 300. katika mbegu hizo ni moja tu ndiyo intakayofanikiwa kitungisha mimba. Mamimioni ya mbegu haya yanakufa bila hata ya kulifikia yai, kutokana na udhaifu wao, kutoweza kuogelea vyema, ukali wa tindikali katika tumbo la mwanamke n.k. sasa ili mwanaume aweze kubebesha ujauzito anatakiwa atoe mbegu bora na imara zinazoweza kuishi ndani ya tumbo la mimba kwa muda mrefu.



Inatokea baadhi ya wanaume mbegu zao zinakuwa sio imara kutosheleza. Hii inakuwa ni ngumu kubebesha ujauzito. Lakini kumbuka kama mambo mengine yakiwa sawa hata mwenye mbegu dhaifu inaweza kubebesha mimba endapo itakuwa ni siku sahihi ya kukutana na yai, hazitachukuwa muda kukutana na yai ama zilitolewa nyingi.



Sasa ikiwa tatizo ni hili la mbegu ni dhaifu, je nitawezaje kuboresha mbegu zangu? Yes ni swali zuri sana, na inapasa hasa kulijuwa jibu lake. Mbegu utaweza kuziporesha kwa kubadilisha mlo ama kutumia dawa ama njia nyinginezo. Miongoni mwa njia hizo ni:-



Njia za kuboresha mbegu za kiume.
1.Badili mlo wako.
Muonekano wako leo ni sawa na chakula unachokila. Ladha na ubora wa manii na mbegu za kiume pia hutegemeana na unachokila. Kama unataka kuboresha mbegu za kiume kwanza anza na kubadili mlo wako. Jitahidi kula vyakula vifuatavyo:-



A.Vitamini B-12
Vitamini hivi unaweza kuvipata kwenye nyama, samaki na maziwa. Vitamini hivi husaidia sana katika afya ya mbegu za kiume.



B.Vitamini C
Hivi unaweza kuvipata kwenye machungwa, viaz mbatatai, nyanya, apinach na kwenye matunda yenye uchachu na mapapai na mananasi. Vitamini C pia ni muhumu kwa afya ya mfumo wa kinga



C.Kula vyakula jamii ya korosho na karanga



D.Kula vyakula vyenye lycopene. Vyakula hivi kuwa na rangi nyekundu kama tikiti na nyanya



E.Kula vyakula vyenye madini ya zinc kwa wingi. Unaweza kupata madini haya kwenye nyama, samaki wa baharini kwenye magobeta jamii ya kaa, mimea jamii ya kunde, kula mbegu kama mbegu za maboga na nyingine, maziwa, mayai, jamii ya korosho, baadhi ya mboga za majani kama maharagwe ya kijani na nafaka nzima.



2.Fanya mazoezi ya mara kwa mara.
Mazoezi si kwa ajuli ya hili tu bali pia ni kwa ajili ya kuboresha afya kwa ujumla. Si lazima ufanye mazoezi mareefu, hapana kwa uchache pia inatosha.



3.Punguza kuvaa nguo za ndani zenye joto.
Afya ya mbegu za kiume inategemea pia joto la mwili wako. Hakikisha korodani unazipa hewa ya kutosha. Usivae nguo za kubana nyingi kama chupi, si salama kwa wanaume. Boxa kama haibani sana inatosha.



4.Punguza unywaji wa pombe, na soda kama unakunywa kwa kiasi kikubwa.





                   



Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 13874

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 web hosting     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Damu, majimaji na uteute unaotoka kwenye uke wa Mjamzito, sababu zake na dalili zake

Unataka kujuwa sababu za mjamzito kutokwa na damu, utelezi ama majimaji kwenye uke wake. Na dalili gani zinaashiriwa na majimaji haya

Soma Zaidi...
Mwanaune anapataje fangasi kwenye uume

Post hii itakujulishs kwa namna gani mwanaune anaweza kupata fangasi kwenye uume wake

Soma Zaidi...
Kuwepo kwa maziwa wakati wa ujauzito.

Posti hii inahusu zaidi kuwepo kwa maziwa kwa akina Mama wakati wa ujauzito ni kawaida kwa sababu ya kuzaliwa kwa homoni ambayo usaidia kutoa maziwa.

Soma Zaidi...
Huduma kwa mama mwenye mimba ambayo inataka kutoka.

Post hii inahusu zaidi huduma kwa mama ambaye mimba inataka kutoka, mimba za aina hiyo kwa kitaalamu huitwa inevitable pregnant ni lazima itoke tu hata kama kuna juhudi mbalimbali za wataalamu mimba hii utoka kabisa.

Soma Zaidi...
Dalili ya mimba ya wiki moja(1)

Mwanaume na mwanamke wanapo kutana na kujamiina kama mwanamke yupo kwenye ferlile process ni rahisi kupata mbimba. Sparm Zaid ya million moja huingia kwenye mfuko wa lakin sparm moja ndio huweza kuingia kwenye ovum(yai)lakin nyingine hubaki kwenye follopi

Soma Zaidi...
Njia za kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito

Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito, ni mojawapo ya njia ambazo utumiwa na wahudumu wa afya ili kuweza kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito.

Soma Zaidi...