picha

FANGASI SEHEMU ZA SIRI: DALILI ZAKE, CHANZO CHAKE NA NJIA ZA KUPAMBANA NAO

FANGASI SEHEMU ZA SIRI: DALILI ZAKE, CANZO CHAKE NA NJIA ZA KUPAMBANA NAO

FANGASI

Fangasi huweza kuishi na kuathiri maeneo mbalimbali ndani ya mwili. Fangasi ni hatari sana, kwani wanaweza kusababisha madhara makubwa ya kiafya na kiakili kama wasipitibiwa mapema. Kuna aina nyingi za fangasi ambao wanaweza kuathiri mwili wa binadamu.

 

Kuna mamilioni ya aina hizi za fangasi, katika hawa kuna kuna mamia ya aina za fangasi ambazo huweza kumfanya mtu kuumwa. Fangasi wanaweza kuathiri makwapa, vidole, sehemu za siri kwenye tumbo na maeneo mengine.

 

Fangasi wa sehemu za siri husababishwa na fangasi waitwao candida. Hawa wanaweza kuathiri sehemu za siri kuzungukia uume ama uke. Kunatafiti zinaonesha kuwa fangasi hawa wanaweza kuambukizwa kwa kufanya mapenzi. Japo tafiti zaidi zinahitajika ili kuthibitisha hili.

 

FANGASI WA SEHEMU ZA SIRI DALILI ZAO KWA WANAUME

  1. Kuvimba kwa kichwa cha uume
  2. Kuwasha kwa sehemu za siri, hususan kichwa cha uume
  3. Uume kuwa mwekundu kwa kuchubuka ama kuvumba ama kwa mashambulizi ya fangasi hawa.
  4. Kuota kwa mapele na maruturutu kwenye uume
  5. Kuwasha uume ama kuungua moto kwa uume.
  6. Kutokwa na majimaji meupe kwenye uume, majimaji haya huwa na harufu mbaya.
  7. Maumivu wakati wa kukojoa na kufanya tendo la ndoa.

DALILI ZA FANGASI WA SEHEMU ZA SIRI KWA WANAWAKE

  1. Maumivu na miwasho kwenye mashavu ya uke na sehemu ya juu ya uke
  2. Maumivu wakati wa kukojoa ama kufanya tendo la ndoa
  3. Uuke kuwaka moto kwa ndani
  4. Kuvimba kwa mashavu ya uke na kuwa mekundu
  5. Kuot mapele na maruturutu kwenye uke
  6. Kutokwa na majimaji kwenye uke
  7. Kutokwa na majimaji mazito meupe na yenye harufu mbaya kwenye uke.

 

WATU WALIO HATARINI KUPATA FANGASI HAWA

  1. Wachafu
  2. Kuwa na mikunjomikunjo kwenye ngozi kama kitambi
  3. Wenye kisukari
  4. Wenye HIV
  5. Wenye saratani
  6. Wenye kutumia baadhi ya madawa ya kuzuia mimba
  7. Wajawazito

 

NJIA ZA KUPAMBANA NA FANGASI HAWA

  1. Kuwacha kutumia madawa ya kusafishia ama kuunga uke
  2. Kutokuvaa nguo mbichi
  3. Kutokuvaa nguo za kubana hususani za mpira
  4. Kuwa msafi muda wowote
  5. Kuosha kichwa cha uume na ngozi ya govi mara kwa mara
  6. Kuosha uke mara kwa mara
  7. Kutumia pedi zilizo kavua na safi na kubadilisha mara kwa mara
 


                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 7059

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 ai web app     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Bongolite - Game zone - Play free game     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Ugonjwa wa kuporomoka kwa mapafu (pneumothorax)

Posti hii inazungumzia Ugonjwa wa mapafu ambao hujulikana Kama pafu lililoporomoka (Pneumothorax) hutokea wakati hewa inavuja kwenye nafasi kati ya mapafu yako na ukuta wa kifua. Hewa hii hutoka nje ya pafu lako. Ugonjwa huu unaweza kusababishwa na jera

Soma Zaidi...
dalili za ukimwi kwa mwanaume

Katika post hii utakwenda kujifunza zaidi khusu dalili za ukimwi ama HIV kwa wanaume

Soma Zaidi...
Dalili na ishara za jipu la Jino

Jipu la jino ni mfuko wa usaha unaosababishwa na maambukizi ya bakteria.

Soma Zaidi...
Dalili na ishara za Ugonjwa wa kuambukiza.

Magonjwa ya kuambukiza ni maradhi yanayosababishwa na vijidudu kama vile bakteria, virusi, fangasi au vimelea. Viumbe vingi vinaishi ndani na kwenye miili yetu. Kwa kawaida hazina madhara au hata kusaidia, lakini chini ya hali fulani, baadhi ya viumbe

Soma Zaidi...
Dalili za miguu kufa ganzi

Posti hii inahusu zaidi dalili mbalimbali ambazo Uweza kujitokeza na kuona kwamba ni Dalili za miguu kufa ganzi, pengine utokea kwa watu wote na pengine huwa ni kwa ghafla

Soma Zaidi...
Matatizo ya unene kwa watoto (childhood obesity)

post Ina onyesha madhara na matatizo ya Unene Utoto ni hali mbaya ya kiafya inayoathiri watoto na vijana. Inatokea wakati mtoto yuko juu ya uzito wa kawaida kwa umri na urefu wake

Soma Zaidi...