Maumivu makali ya tumbo la chango wakati wa hedhi na sababu zake
Kwa nini unapata maumivu makali wakati wa kuingia hedhi, je unajuwa sababu za maumivu makali ya tumbo la chago.

MAUMIVU YA HEDHI MAKALI SANA
Maumivu ya tumbo la hedhi kikawaida yanatambulika kama tumbo la chango kwa wakinamama. Katika hali ya kawaida maumivu haya sio makali kiasi cha kuharibu ratiba za mwanamke. Lakini hutokea wakati mwingine yakawa makali sana kiasi cha kupelekwa hospitali, ama mwanamke kushindwa kufanya shughuli zake. Sasa nini sababu ya maumivu haya kupitiliza? Makala hii itakwenda kuangalia sababu za maumivu makali ya tumbo la chango au maumivu makali ya tumbo la hedhi.
Sababu za maumivu makali ya tumbo la hedhi
Kama mwanamke anaingia hedhi kwa na maumivu makali anaweza kutumia dawa za kupunguza maumivu kama ibuprofen. Lakini kama kuna sababu nyingine zinazopelekea maumivu kuwa makali hata akimeza dawa hii maumivu yatakuwa ni yenye kuendelea.
Dalili za maumivu makali ya hedhi ni
1.maumivu yasiyokata hata baada ya kumeza dawa za kupunguza maumivu
2.Kama maumivu makali kiasi cha kuharibu ratiba za shunguli za kawaida
3.Kama maumivu yanafuatana na damu nyingi ama kuganda kwa damu
Nini sababu ya maumivu makali ya hedhi?
1.kuota kwa tishu (nyamnyama) maeneo mengine tofauti na tumbo la mimba. Kitaalam hali hii inatambulika kama endometriosis. Hali pia inaweza kuwa na dalili zifuatazo:-
A.Kutokwa na damu nyingi sana wakati wa hedhi
B.Hedhi kuchukuwa siku zaidi ya 7
C.Kutokwa na damu kabla ya siku za hedhi kufika
D.Maumivu ya tumbo
E.Maumivu wakati wa tendo la ndoa
F.Kupata maumivu wakati wa haja kubwa.
G.Kuchelewa kupata ujauzito
2.Shida kwenye mfumo wa homoni, hali hii kitaalamu inatambulika kama Polycystic Ovary Syndrome (PCOS). hali hii ni ya kawaida sana takribani kwa kila wanawake 10 mmoja wao huwa na hali hii. Miongoni mwa sababu kuu ni kuwa na homoni za kiume nyingi (androgens) na kutokuwa na siku maalumu za kupata hedhi. Hali hii inaweza kuwa na dalili kama:
A.Kutokwa na damu nyingi sana
B.Kupata hedhi kwa muda mrefu
C.Kuota ndevu ama mwele kuwa nyingi maeneo mbali mbali ya mwili kama ilivyo kwa wanaume
D.Kuwa na uzito mwingi na usio rahisi kuupunguza
E.Kuota chunusi
F.Kunyonyoka kwa nywele na kukosa afya
G.Kuwa na madoa madoa meusi kwenye ngozi
3.kuwa na uvimbe kwenye kizazi kitaalamu hali hii hutambulika kama fibroids. Huu I uvimbe usio wa saratani unaoota kwenye tumb la mimba. Unaweza kuwa uvimbe mmoja ama zaidi. Unaweza pia kuwa na uvimbe bila ya kuonyesha dalili zozote hali hii ikichanganyika na maumivu ya chango inaweza kuonyesha dalili kaka:
A.Maumivu ya mgongo kwa chini
B.Maumivu ya miguu
C.Kupata damu nyingi ya hedhi
D.Kupata hedhi zaidi ya wiki
E.Kukosa choo kikubwa
F.Kukojoakojoa mara kwa mara
G.Kushindwa kumaliza mkojo wote.
4.kuwa na maambukizi ama mashambulizi ya bakteria, fangasi ama virusi kwenye kizazi. Kitaalamu hii huitwa Pelvic Inflammatory disease au maarufu kama PID. Miongoni mwa dalili zake ni:-
A.Maumivu wakati wa tendo la ndoa
B.Kutokwa na damu kabla ya hedhi na baada ya hedhi
C.Kutokwa na majimaji yanayotoa harufu kwenye uke
D.Maumivu wakati wa kukojoa
E.Homa
F.Kutokwa na damu kidogo kabla ya kuingia hedhi na baada ya kuingia hedhi
5. Maumbile ya kwenye shingo ya uzazi kitaalamu huitwa cervical stenosis, hii ji hali ambayo mlango wa shingo ya kizazi unakuwa ni mdogo sana. Huenda mwanamke amezaliwa ivyo ama mlango umeziba baadaye.
6.kukaza kwa tishu (nyamnyama) za kwenye tumbo la mimba kitaalamu hai hii inatambulika kama (andenomyosis). hali hii hutokea pale nyamnayma laiki za kwenye tumbo la mimba zinapokuwa ngumu na kubadilika kuwa misuli.
7.matumizi ya baadhi ya njia za kuthibiti uzazi kama Intrauterine Device (IUD). hiki ni kifaa kidogo kinachowekwa kwenye tumbo la mimba. Kijikifaa hiki mwa wanawake wengine kinaweza kuwaletea shida za kiafya kama:
A. Maumivu makali wakati wa hedhi
B. Kutokuwa na siku maalumu za hedhi yaani hedhi inaruka ruka
C. Kutokwa na damu nyingi wakati wa hedhi
NINI NIFANYE KUKABILIANA NA MAUMIVU HAYA
1.fanya mazoezi mara kwa mara
2.Tumia pad zilizo kavu
3.Hakikisha huna stress yaani misongo ya mawazo kupitiliza
4.Oga maji ya moto
5.Tumia dawa za kupunguza maumivu ya chango kama ibuprofen na acetaminophen
6.Tumia vitamini kama vitamini B1, na B6, madini ya magnesium na omega-3 fatty acid.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 kitabu cha Simulizi π2 Bongolite - Game zone - Play free game π3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π4 Simulizi za Hadithi Audio π5 Kitau cha Fiqh π6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Kazi ya kongosho na athari za ugonjwa wa kisukari.
Kongosho ni kiungo muhimu katika mfumo wa mmeng'enyo wa chakula na udhibiti wa homoni mwilini. Ugonjwa wa kisukari hutokea pale kongosho inaposhindwa kufanya kazi zake ipasavyo, hasa katika uzalishaji wa insulini. Makala hii inachunguza kwa kina kazi za kongosho, uhusiano wake na ugonjwa wa kisukari, athari za muda mrefu za ugonjwa huu, na mbinu za kitaalamu za kuzuia na kudhibiti hali hii ili kulinda afya ya kongosho na mwili kwa ujumla.
Soma Zaidi...Ugonjwa wa kupooza (Stroke): Dalili za mwanzo na kinga.
βUgonjwa wa kupooza, unaojulikana kitabibu kama stroke au cerebrovascular accident (CVA), ni dharura kubwa ya kitabibu inayotokea wakati mtiririko wa damu kwenye sehemu ya ubongo unapoingiliwa au kukatika. Kila sekunde ni muhimu katika kuokoa tishu za ubongo na kupunguza ulemavu wa kudumu. Makala haya yanafafanua dalili za mwanzo, sababu za hatari, na mikakati madhubuti ya kuzuia ugonjwa huu kwa maisha yenye afya bora
Soma Zaidi...Kichwa kinaniuma mbele sielewi nini
Zijuwe sababu za kuumwa nankichwa upande mmoja wa kichwa.
Soma Zaidi...Kufunga uzazi (Tubal Ligation): Je, inaweza kurudishwa?
Kufunga uzazi kwa wanawake (Tubal Ligation) ni utaratibu wa upasuaji unaokusudiwa kuwa wa kudumu. Hata hivyo, mabadiliko ya kimaisha, kupoteza mtoto, au mabadiliko ya mazingira ya kifamilia huwafanya wanawake wengi kujiuliza kama utaratibu huu unaweza kubadilishwa. Makala haya yanachunguza kitaalamu uwezekano wa kurudisha uzazi (Tubal Reversal), viwango vya mafanikio, hatari zake, na mbadala mwingine kama In Vitro Fertilization (IVF
Soma Zaidi...Walio hatarini kupata gonorrhea (gonoria)
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu watu walio hatarini kupata gonorrhea gonoria
Soma Zaidi...Ugonjwa wa kisukari
Ugonjwa wa kisukari hurejelea kundi la magonjwa yanayoathiri jinsi mwili wako unavyotumia sukari kwenye damu (glucose). Glucose ni muhimu kwa afya yako kwa sababu ni chanzo muhimu cha nishati kwa seli zinazounda misuli na tishu zako. Pia ndio chanzo ki
Soma Zaidi...