Chanzo cha vita vya Ngamia Vita Kati ya Bibi Aisha na Khalifa Ali

Chanzo cha vita vya Ngamia Vita Kati ya Bibi Aisha na Khalifa Ali

Vita Kati ya Bibi Aisha na Khalifa Ali



Khabari za kutekwa Basra zilimchukua kwa mshangao mkubwa Khalifa Ali ambaye alikuwa aende Syria kumrudi Muawiya lakini alilazimika kwenda Basra kwanza kutuliza hali ya kule.


Alipofika Dhi-Qarโ€™a mahali karibu na Basra-alituma ujumbe kwa Aisha, Talha na Zubeir wafanye mazungumzo ya amani. Nafasi ilipatikana mazungumzo yakafanywa na wakawa karibu kukubaliana baada ya Ali kuahidi kuwa atawaadhibu wauwaji wa Uthman Dola itakapokuwa na amani. Lakini mpango wa amani haukuwa na maslahi kwa lile kundi la Ibn Sabaa ambalo lilifanya sehemu ya jeshi la Ali.


Walinongโ€™onezana kuwa Ali anataka kufikia makubaliano ya amani na ameahidi kuwaadhibu waliomuua Uthman. Kundi hili lilikuwa ndilo lililomuua Khalifa Uthman halikupendezwa na mpango huu, wakaunda hila iliyochochea kutokea vita. Mbinu mbili walizitumia. Kwanza walipeleka umbea Basra kuwa Ali akiingia Basra atawafanya watumwa wakazi wote na atawaua vijana wote. Kwa sababu hii watu wa Basra lazima wapigane.66 Ibn Sabaa na wachochezi wake usiku usiku walivamia jeshi la mama Aisha ambaye aliarifiwa na kwa namna hii vita vikaanza. Vita hivi vinajulikana kwa jina la Vita vya ngamia.


Vita vilikuwa vikali kwa vile ukubwa wa jeshi ulilingana. Baada ya mapigano makali na kuuawa Waislamu wapatao elfu kumi, Talha aliuwawa na , Zubair aliacha kupigana na akawa anaelekea Madina ndipo akauliwa njiani. Wakati wote wa vita mama Aisha alikuwa katika sehemu ya uwanja wa vita akiwa amepanda ngamia. Kuwepo kwake kulifanya mapigano yaendelee kwa kasi kubwa, bila kukoma, ndipo Ali alipoamuru ngamia wake akatwe miguu ya nyuma. Ngamia aliangukia miguu yake ya mbele na kwa heshima zote akatolewa mama Aisha ndani ya kikalio cha ngamia na vita vikaisha. Mama Aisha akasindikizwa Madinah na kaka yake Muhammad bin Abubakar.


Baada ya vita, Ali alizungumza na Waislamu katika msikiti wa Basra na Waislamu wakampa mkono wa utii. Alipoondoka alimuacha Abdallah bin Abbas kuwa Gavana wa Basra.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1643

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰2 Kitau cha Fiqh    ๐Ÿ‘‰3 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    ๐Ÿ‘‰5 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Historia ya Vijana wa Pangoni

Makafiri wa Kiquraish walikuwa na tabia ya kumghasi Mtume(s.

Soma Zaidi...
Uendeshaji wa dola ya uislamu madinah

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Nabii Ibrahiim(a.s) Afanywa Kiongozi wa Harakati za Uislamu Ulimwenguni

โ€œNa (kumbukeni habari hii) Mola wake alipomfanyia mtihani (Nabii) Ibrahiim kwa amri nyingi; naye akazitimiza.

Soma Zaidi...
Si Yesu Aliyesulubiwa (yesu hakufa msalabani wala hakusulubiwa

Katika Qur,an tukufu, Mwenyezi Mungu aliye muweza na mjuzi wa mambo anathibitisha kuwa aliyesulubiwa si Nabii Isa(a.

Soma Zaidi...
Maandalizi ya hijrah ya mtume na waislamu kuhamia madinah

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Msimamo wa Nabii Hud(a.s) Dhidi ya Makafiri wa Kaumu Yake

Pamoja na kwamba alipingwa na nguvu za Dola ya makafiri wa kaumu yake, Mtume Hud(a.

Soma Zaidi...
MTUME MUHAMMAD (S.A.W) KULELEWA NA BABA YAKE MDOGO MTUME (ABU TALIB)

KULELEWA NA BABA YAKE MDOGOBaada ya kufariki kwa mzee huyu, kiongozi mkubwa wa maquraysh na makkah, kiongozi ambaye jeshi la Abrah liliangamizwa ndani ya utawala wake.

Soma Zaidi...