jamii somo la 35

Hutekeleza ahadi zao wanapoahidiana na wanaadamu wenziwao maadamu ni katika mipaka ya Allah (s.

Wenye kutekeleza ahadi

Hutekeleza ahadi zao wanapoahidiana na wanaadamu wenziwao maadamu ni katika mipaka ya Allah (s.w).


Ahadi kubwa wanayotoa Waislamu mbele ya Allah (s.w) ni shahada; pale wanapo ahidi kuwa hawatamshirikisha Allah (s.w) na chochote na kwamba wataishi maisha yao yote kwa kufuata mwongozo wa Allah (s.w) kupitia kwa Mtume wake, Muhammad (s.a.w). Rejea (6: 162 -163)Katika Suratul-Fur-qaan sifa za Waumini zinabainishwa tena kama ifuatavyo:


“Na waja wa Rahmaan; Ni wale wanaokwenda ulimwenguni kwa unyenyekevu; na wajinga wakisema nao (maneno mabaya) huwajibu (maneno ya) salama. (25:63).



Na wale wanaopitisha baadhi ya saa za usiku kwa ajili ya Mola wao kwa kusujudu na kusimama. Na wale wanaosema:“Mola wetu! Tuondolee adhabu ya Jahannam, bila shaka adhabu yake ni yenye kuendelea(25 :64-65).


Hakika hiyo (Jahannamu) ni kituo kibaya na mahali (pabaya kabisa) pa kukaa ”.Na wale ambao wanapotumia hawatumii kwa fujo wala hawafanyi ubakhili, bali wanakuwa katikati baina ya hayo. (25:66-6 7)


Na wale wasiomuomba mungu mwingine pamoja na Allah, wala hawaui nafsi aliyoiharamisha Allah ila kwa haki, wala hawazini; na atakayefanya hayo atapata madhara (papa hapa ulimwenguni).(25:68).


Na atazidishiwa adhabu siku ya Kiyama na atakaa humo kwa kufedheheka milele (25:69).



Ila yule atakayetubia na kuamini na kufanya vitendo vizuri, basi hao ndio Mwenyezi Mungu atawabadilishia maovu yao kuwa mema; na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwingi wa ku reh em u. (25:70).


Na aliyetubia na kufanya wema, basi kwa hakika yeye anatubu kw eli kw eli kw a Mwenyezi Mungu.(25:71)


Na wale ambao hawashuhudii shahada za uwongo, na wanapopita penye upuuzi, hupita kwa hishima (yao). (25:72)


Na wale ambao wanapokumbushwa aya za Mola wao haw aziangukii kw a uziw i na upofu.(25:73)



Na wale wanaosema: “Mola wetu! Tupe katika wake zetu na wototo wetu yaburudishayo macho (yetu) (nyoyo zetu), na Utujaalie kuwa waongozi kwa wamchao (Mungu). (25:74).


Hao ndio watakaolipwa ghorofa (za Peponi) kwa kuwa walisubiri, na watakuta humo hishima na am ani(25 :75).


Wakae humo milele; kituo kizuri na mahali pazuri (kabisa pa kukaa.) (25:76)
Kutokana na aya hizi tunajifunza kuwa sifa za Waumini ambao hapa wameitwa “Waja wa Rahman” ni pamoja na:




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Dini File: Download PDF Views 392

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 web hosting    👉2 Dua za Mitume na Manabii    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

ZOEZI

Zoezi la 1 (a) Ainisha maana ya sunnah kilugha na kisheria.

Soma Zaidi...
(ix)Wenye kuhifadhi swala

Waumini wa kweli waliofuzu huhifadhi swala kwa kutekeleza kwa ukamilifu shuruti zote za swala nguzo zote za swala na huswali kama alivyoswali Mtume (s.

Soma Zaidi...
Zingatio:

Swala husimama kwa kuhifadhiwa na kuswaliwa kwa khushui na kudumu na swala katika maisha yote.

Soma Zaidi...
Kitabu Cha Darsa za dua

Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.

Soma Zaidi...