Nini maana ya Kibri, madhara yake na kujiepusha na kibri

17.

Nini maana ya Kibri, madhara yake na kujiepusha na kibri

17. Kuepuka kujisifu na kujitukuza


Waislamu tumekatazwa kujisifu sisi wenyewe na pia tumekatazwa kuwasifu wengine kupita kiasi.Mtume (saw) amekataza jambo hili katika Hadith zifuatazo:
Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuwa Mtume (saw) amependekeza kwetu kuwa tumtupie mchanga (vumbi) usoni yule anayejihusisha na kuw asifus ifu w atu kupita kiw ango kinachos tahili. (Tirim idh).


Abu Bakar (ra) amesimulia kuwa mtu mmoja alimsifu mtu mwingine mbele ya Mtume (saw). Mtume (saw) alisema mara tatu. β€œOle wako umekata kichwa cha ndugu yako!” (Kisha anasema Mtume); Yeyote miongoni mwenu ambaye ataona hapana budi kumsifu mwingine na aseme; Nafikiri fulani yuko hivi na hivi ( ana sifa hizi na hizi) na Allah (sw) atamuhesabu hivyo kama kweli mbele yake anastahiki sifa hizo. Lakini asithubutu mtu kumpachika yeyote sifa ya Ucha-Mungu(wema) juu ya Allah.” (Bukhari na Muslim)
Aidha Allah (sw) ametukataza kujisifu sifu katika aya ifuatayo:

β€œβ€¦Yeye (Allah) ndiye anayekujueni sana tangu alipokuumbeni katika ardhi na mlipokuwa mimba matumboni mwa mama zenu. Basi msizitakase nafsi zenu; Yeye (Allah) anamjua sana aliyetakasika ”. (53:32)


Kuwasifu sana watu kupita kiasi huwapelekea wale wenye kusifiwa kuvimba vichwa na kujihisi kuwa wao ni watukufu na bora zaidi kuliko wengine katika jamii. Tunayaona madhara makubwa yaliyojitokeza katika jamii ya waislamu kutokana na sifa za kupita kiasi tulizowapachika masheikhe zetu na watu wengine tuliowapachika usharifu, uwalii, ucha-mungu,n.k. Mgawanyiko wa waislamu tunaoushuhudia hivi leo kwenye madh-habu, twarika na matapo mengine mbali mbali, unatokana na dhambi hii ya kuwasifu viongozi wa hayo makundi kupita kiasi.


Pia tunajifunza katika historia kuwa chanzo cha Mitume wa Allah (sw) na watu wema kushirikishwa na Allah (s.w) ni kuwasifu kupita

kiasi. Katika Qur’an (9:30) tunafahamishwa kuwa kuwaiga washirikina waliowatangulia katika kuwasifu kupita kiasi viongozi wao, Mayahudi walimfaya Uzair (Mtu mwema) mwana wa Mungu na wakristo wakamfanya Isa Bin Maryam mwana wa Mungu. Kwa kuchelea watu wa Ummah nao wasijetumbukia kwenye shirki hii ya sifa, Mtume (saw) anatuasa katika Hadith ifuatayo:


β€œ Imepokelewa kutoka kwa Umar(r.a) kuwa amesema Mtume wa Allah (saw) Msizidishe kwenye kunisifu kama walivyozidisha wakristo ( manasara) katika kums ifu mwana wa Maryam. Mimi ni mja wa Allah tu; kwa hiyo niiteni ;”Mja wa Allah na Mtume wake ”. (Bukhari)
Hivyo muumini wa mkweli hanabudi kujiepusha na kujisifu sifu au kuwasifusifu watu. Na ikiwa hapana budi kumsifu mtu tuzingatie mipaka na tuseme kama alivyotuelekeza Mtume (saw) katika Hadith tuliyoirejea hapa juu. Tabia ya kujisifusifu au kuwasifusifu watu ni tabia ya uwongo, unafiki na ushirikina.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Dini File: Download PDF Views 3293

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰2 Dua za Mitume na Manabii    πŸ‘‰3 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰4 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰5 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

Uchambuzi wa hadithi za mtume

Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
(xvi)Huepuka ugomvi na mabishano

Waumini wa kweli huepuka kabisa tabia ya ugomvi na mabishano.

Soma Zaidi...
quran na sayansi

2; mbegu ya uhai uliyo changanyikaUmbile la mwanadamu limepitia hatua nyingi sana kama tutakavyoendelea mbele kuonalakini ukiachilia mbali na hatua zote alizopitia mwanadamu wakati wa kuumbwa lakiniumbile la mwanadamu bado limebakia kuwa dhalili kama ALLA

Soma Zaidi...
jamii somo la 35

Hutekeleza ahadi zao wanapoahidiana na wanaadamu wenziwao maadamu ni katika mipaka ya Allah (s.

Soma Zaidi...
ZOEZI

Zoezi laΒ 1 (a) Ainisha maana ya sunnah kilugha na kisheria.

Soma Zaidi...
(ix)Wenye kuhifadhi swala

Waumini wa kweli waliofuzu huhifadhi swala kwa kutekeleza kwa ukamilifu shuruti zote za swala nguzo zote za swala na huswali kama alivyoswali Mtume (s.

Soma Zaidi...
Maswali juu ya hadithi

Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya)

Soma Zaidi...