Menu



jamii

Zoezi - 1



1. Elimu ni nini?



2. “Sema, Je wanaweza kuwa sawa wale wanaojua na wale wasiojua?...” (39:9)
Ni kwasababu gani wanaojua hawawi sawa na wasiojuwa?



3. Unatoa maoni gani iwapo wanaojua na wasiojua wakawa sawa kiutendaji?



4. Toa maelezo yenye ushahidi wa Qur-an kuonyesha kuwa:



(a)Elimu ndio takrima ya kwanza aliyokirimiwa binaadamu na Mola wake.



(b)Kutafuta elimu ni amri ya kwanza kwa bin a adam u.



5. Onyesha kwa ushahidi wa Qur-an kuwa katika Uislamu mgawanyiko wa elimu katika “elimu ya dini” na “elimu ya dunia” haukubaliki.



6. “Soma kwa jina la Mola wako aliyeumba.” (96:1) Kusoma kwa jina la Mola wako maana yake nini?



7. “.... Soma na Mola wako ni karimu sana. Ambaye amemfundisha mwanaadamu kwa kalamu. Amemfundisha mwanaadamu mambo aliyokuwa hayajui”. (96:3-5)
Orodhesha njia tano anazozitumia Allah (SW) katika kuwasiliana na wanaadamu.



8. Elimu yenye manufaa kwa binaadamu ni ile .................................



9. Eleza sababu tatu zinazopelekea elimu kupewa nafasi ya kwanza katika Uislamu.
*******************************


Chanzo cha Elimu ni Allah (s.w) Kama tunavyojifunza katika surat ‘Alaq (96:4-5), chanzo cha elimu au mkufunzi wa binadamu ni Allah (s.w). Allah (s.w) huwasiliana na binadamu na kuwaelimisha kwa kutumia mojawapo ya njia zifuatazo zilizoainishwa katika aya ifuatayo: Na haikuwa kwa mtu kwamba Mwenyezi Mungu anasema naye ila kwa il-hamu (anayetiwa moyoni mwake) au kwa nyuma ya pazia au humtuma mjumbe (Malaika) naye humfunulia kiasi anachotaka kwa idhini yake (Allah), bila shaka yeye ndiye aliye juu mwenye hekima.” (42:51). Aya hii inatufahamisha kuwa binaadamu hupata habari kutoka kwa Allah (s.w) kwa njia tatu zifuatazo: (a)Il-hamu(Intution). (b)Nyu ma ya pazia. (c)Kutumwa Malaika na kufikisha ujumbe kama alivyotumwa. Pia katika Qur-an tunafahamishwa njia mbili nyingine anazozitumia Allah (s.w) katika kumfikishia binaadamu ujumbe kutoka kwake: (d)Ndoto za kweli (ndoto za Mitume).


                   


Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Dini File: Download PDF Views 343

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

jamii somo la 35

Hutekeleza ahadi zao wanapoahidiana na wanaadamu wenziwao maadamu ni katika mipaka ya Allah (s.

Soma Zaidi...
quran na sayansi

2:UUMBWAJI KWA MAJI YA UZAZIUumbwaji wa mwanadamu umepitia hatua mbalimbali na haya yote yamefanywa kwa sababumaalumu ili tipate mazingatio.

Soma Zaidi...
MAADILI MEMA KATIKA UISLAMU

Yajuwe maadili mema yaliyotajwa katika quran

Soma Zaidi...