15.
15. Kujiepusha na Matusi
Mtu anayetukana ana lengo la kumdhalilisha mwingine. Waislamu tumekatazwa kutukanana na hata kuitana majina tusiyoyapenda kwa k ej eli.
“.... Wala msitukanane kwa kabila wala msiitane majina mabaya (ya kejeli). Jina baya kabisa kuitwa mtu ni “Fasiqi” baada ya kuwa yeye ni Muislamu. Na wasiotubu basi hao ndio madhalimu ”. (49:11)
Fasiq ni yule aliyebobea katika uasi. Yaani mtu anayejizatiti kumuasi Allah (s.w) kwa namna mbali mbali kama vile mwizi, mlevi,
mzinzi na kadhalika. Ni vibaya mno mbele ya Allah (s.w) kumsingizia au kumwita Muislamu ”mwizi” na huku si mwizi au kumwita “mnafiki” au “kafir” na huku ni Muislamu kamili. Tabia hii imekemewa vikali katika Qur-an:
“Kwa yakini wale wanaopenda uenee uovu kwa wale walioamini watapata adhabu iumizayo katika dunia na katika akhera, na Allah ndiye ajuaye, na nyinyi hamjui”. (24:19).
Kutokana na makemeo haya, Muumini wa kweli hana budi kujiepusha na tabia ya kuwaita watu kwa majina mabaya kwani kufanya hivyo mtu hujilaani mwenyewe kiasi kwamba hayo majina mabaya yatamgeukia, kama tunavyojifunza katika Hadithi zifuatazo:
Abu Dh-dhari(r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: Hapana mtu atakayemsingizia mwingine uasi kwa Allah au akamwita “kafiri”, ila hayo yatamgeukia yeye mwenyewe iwapo huyo aliyemsingizia hayuko hivyo”. (Bukhari)
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Mwenendo wa kati ni mwenendo ulioepukana na kibri na majivuno kwa upande mmoja na ulioepukkana na udhalili na unyonge kwa upande mwingine.
Soma Zaidi...Waumini wa kweli waliofuzu hutoa Zakat wakiwa na mali na hutoa misaada na huduma waziwezazo kwa wanaadamu wenziwe kwa kadiri ya haja ilivyojitokeza.
Soma Zaidi...Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Swala husimama kwa kuhifadhiwa na kuswaliwa kwa khushui na kudumu na swala katika maisha yote.
Soma Zaidi...Na kuwapambanua wale waliokuwa wanafiki.
Soma Zaidi...