ndoto za kweli

(d) Ndoto za kweli



Njia nyingine ya kupata ujumbe kutoka kwa Allah ni njia ya ndoto za kweli. Historia inatuonyesha kuwa ndoto za Mitume daima zilikuwa zikitokea kweli; kwa hiyo ulikuwa ni ujumbe moja kwa moja kutoka kwa Allah (s.w). Ndio maana Nabii Ibrahim (a.s) alipoota kuwa anamchinja mwanawe, hakusita kutekeleza hilo kwa kuwa yeye na mtoto wake Ismail (a.s) walikuwa na uhakika kuwa ni amri kutoka kwa Allah kama inavyobaini katika Aya ifuatayo:


โ€œโ€ฆ Ewe mwanangu! Hakika nimeona katika ndoto ya kwamba ninakuchinja. Basi fikiri, waonaje?โ€ Akasema: โ€œEwe baba yangu! Fanya unayoamrishwa, utanikuta Insha-Allah miongoni mwa wanao subiri.โ€ (37:102)
Kutokea kweli kwa ndoto ya Nabii Yusuf (a.s) kama inavyobainishwa katika Qur-an ni miongoni mwa ushahidi kuwa ndoto za Mitume ni ujumbe wa kweli na wa moja kwa moja (kama ndoto yen yewe ilivyo) kutoka kwa Allah (s.w). Hebu turejee kisa cha ndoto ya Nabii Yusuf (a.s) katika aya zifuatazo:


Kumbuka Yusuf alipomwambia baba yake: โ€œEwe baba yangu! Hakika nimeona katika ndoto nyota kumi na moja na jua na mwezi. Nimeviona vyote hivi vinanisujudiaโ€ (12:4)



Akasema (babaake): โ€œEwe mwanangu! Usiwasimulie ndoto yako (hii) nduguzo wasije wakakufanyia vitim bi (kwa ajili ya husda itakayow apanda). Hakika shetani kwa mw anaadam u ni adui aliye dhahiri (atawatia uchungu tu)โ€. (12:5)
Kutokea kweli kwa ndoto hii kunabainishwa katika aya ifuatayo:


(Na walipoingia kwa Yusuf), aliwainua wazazi wake na kuwaweka katika kiti (chake) cha ufalme. Na wote wakaporomoka kumsujudia. Na (Yusuf) akasema: โ€œEwe babaangu! Hii ndiyo (tafsiri) hakika ya ndoto yangu ya zamani. Bila shaka Mola wangu ameihakikisha. Na amen ifanyia ihsani akanitoa gerezani na akakuleteni nyinyi kutoka jangwani; baada ya shetani kuchochea baina yangu na ndugu zangu. Hakika Mola w angu ni mw enye kulifikia alitakalo. Bila shaka yeye ni mjuzi na mwenye hikimaโ€. (12:100).
Kutokea kweli kwa ndoto ya Mtume (s.a.w) kuwa Waislamu watangia Makka kuhiji kwa salama bila ya kuzuiliwa na mtu yeyote. Ndoto hii ilitokea kweli kama tunavyofahamishwa katika aya ifuatayo:



Kw a yakini Mw enyezi Mungu amemhakikishia Mtume wake ndoto yake ya haki. Bila shaka nyinyi mtaingia katika Msikiti Mtukufu Insha-Allah kwa salama; mkinyoa vichwa vyenu na mkipunguza nywele (kama ilivyowajibu kufanya hivyo wakati wa Hija). Hamtakuwa na khofu. Na (Mwenyezi Mungu) anajua msiyoyajua. Basi kabla ya haya atakupeni kushinda kuliko karibu. (48:27)




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Dini File: Download PDF Views 844

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰2 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰3 Madrasa kiganjani    ๐Ÿ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    ๐Ÿ‘‰6 web hosting   

Post zinazofanana:

Elimu

Uwanja wa elimu na maarifa

Soma Zaidi...
jamii somo la 35

Hutekeleza ahadi zao wanapoahidiana na wanaadamu wenziwao maadamu ni katika mipaka ya Allah (s.

Soma Zaidi...
HUYU NDIYE MUUMINI WA KWELI KATIKA UISLAMU

ุนูŽู†ู’ ุฃูŽุจููŠ ุญูŽู…ู’ุฒูŽุฉูŽ ุฃูŽู†ูŽุณู ุจู’ู†ู ู…ูŽุงู„ููƒู ุฑูŽุถููŠูŽ ุงู„ู„ู‡ู ุนูŽู†ู’ู‡ู ุฎูŽุงุฏูู…ู ุฑูŽุณููˆู„ู ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุตู„ู‰ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆ ุณู„ู… ุนูŽู†ู’ ุงู„ู†ูŽู‘ุจููŠูู‘ ุตู„ู‰ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ?...

Soma Zaidi...
Assalam Baada yakufariki wazazi wake mtume alilelewa nanani???

Mtume Muhammad s.a.w amezaliwa yatima asiyena baba. Lakini hii haikumfanya asipate maelezo bora yaliyo mazuri. Je unajuwa aliyemlea baada ya kufariki kwa mama yake?.

Soma Zaidi...
HISTORIA YA UANDISHI WA HADITHI

Historia fupi ya uandishi wa Hadith za Mtume (s.

Soma Zaidi...
Kitabu Cha Dua 120

Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.

Soma Zaidi...