(d) Ndoto za kweli
Njia nyingine ya kupata ujumbe kutoka kwa Allah ni njia ya ndoto za kweli. Historia inatuonyesha kuwa ndoto za Mitume daima zilikuwa zikitokea kweli; kwa hiyo ulikuwa ni ujumbe moja kwa moja kutoka kwa Allah (s.w). Ndio maana Nabii Ibrahim (a.s) alipoota kuwa anamchinja mwanawe, hakusita kutekeleza hilo kwa kuwa yeye na mtoto wake Ismail (a.s) walikuwa na uhakika kuwa ni amri kutoka kwa Allah kama inavyobaini katika Aya ifuatayo:
“… Ewe mwanangu! Hakika nimeona katika ndoto ya kwamba ninakuchinja. Basi fikiri, waonaje?” Akasema: “Ewe baba yangu! Fanya unayoamrishwa, utanikuta Insha-Allah miongoni mwa wanao subiri.” (37:102)
Kutokea kweli kwa ndoto ya Nabii Yusuf (a.s) kama inavyobainishwa katika Qur-an ni miongoni mwa ushahidi kuwa ndoto za Mitume ni ujumbe wa kweli na wa moja kwa moja (kama ndoto yen yewe ilivyo) kutoka kwa Allah (s.w). Hebu turejee kisa cha ndoto ya Nabii Yusuf (a.s) katika aya zifuatazo:
Kumbuka Yusuf alipomwambia baba yake: “Ewe baba yangu! Hakika nimeona katika ndoto nyota kumi na moja na jua na mwezi. Nimeviona vyote hivi vinanisujudia” (12:4)
Akasema (babaake): “Ewe mwanangu! Usiwasimulie ndoto yako (hii) nduguzo wasije wakakufanyia vitim bi (kwa ajili ya husda itakayow apanda). Hakika shetani kwa mw anaadam u ni adui aliye dhahiri (atawatia uchungu tu)”. (12:5)
Kutokea kweli kwa ndoto hii kunabainishwa katika aya ifuatayo:
(Na walipoingia kwa Yusuf), aliwainua wazazi wake na kuwaweka katika kiti (chake) cha ufalme. Na wote wakaporomoka kumsujudia. Na (Yusuf) akasema: “Ewe babaangu! Hii ndiyo (tafsiri) hakika ya ndoto yangu ya zamani. Bila shaka Mola wangu ameihakikisha. Na amen ifanyia ihsani akanitoa gerezani na akakuleteni nyinyi kutoka jangwani; baada ya shetani kuchochea baina yangu na ndugu zangu. Hakika Mola w angu ni mw enye kulifikia alitakalo. Bila shaka yeye ni mjuzi na mwenye hikima”. (12:100).
Kutokea kweli kwa ndoto ya Mtume (s.a.w) kuwa Waislamu watangia Makka kuhiji kwa salama bila ya kuzuiliwa na mtu yeyote. Ndoto hii ilitokea kweli kama tunavyofahamishwa katika aya ifuatayo:
Kw a yakini Mw enyezi Mungu amemhakikishia Mtume wake ndoto yake ya haki. Bila shaka nyinyi mtaingia katika Msikiti Mtukufu Insha-Allah kwa salama; mkinyoa vichwa vyenu na mkipunguza nywele (kama ilivyowajibu kufanya hivyo wakati wa Hija). Hamtakuwa na khofu. Na (Mwenyezi Mungu) anajua msiyoyajua. Basi kabla ya haya atakupeni kushinda kuliko karibu. (48:27)
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Na kuwapambanua wale waliokuwa wanafiki.
Soma Zaidi...Huwa wepesi wa kutoa msaada kwa hali na mali kwa wanaadamu wenziwe wanaohitajia msaada.
Soma Zaidi...Hutekeleza ahadi zao wanapoahidiana na wanaadamu wenziwao maadamu ni katika mipaka ya Allah (s.
Soma Zaidi...Waumini wa kweli waliofuzu huwa na khushui (unyenyekevu) katika swala.
Soma Zaidi...