picha

mgawanyiko wa elimu

Mgawanyo wa Elimu katika Faradh ‘Ain na Faradh Kifaya



Faradh ya elimu inaweza kugawanywa kwenye faradhi ‘Ain na faradh Kifaya. Faradh ‘Ain ni faradh inayomhusu kila mtu binafsi isiyo na uwakilishi. Mfano, kusimamisha swala, kutoa Zakat, kufunga, n.k. ni katika faradh ‘ain.



Faradh Kifaya ni faradh inayoweza kufanywa kwa uwakilishi. Ni faradhi ya kijamii. Wachache wanaweza kuitekeleza kwa niaba ya jamii. Kwa mfano swala ya maiti na yale yote ya faradh anayostahiki kufanyiwa maiti wa Kiislamu ni katika faradh kifaya.


Elimu ya Maarifa ya Uislamu, itakayompelekea mja kumtambua, Mola wake, vilivyo na kumuabudu inavyostahiki katika kila kipengele cha maisha ni faradh ‘Ain.


Kwa maana nyingine ni faradh kwa kila Muislamu kuujua Uislamu vilivyo na kujitahidi kuutekeleza kwa kadiri ya uwezo wake katika kila kipengele cha maisha.



Elimu juu ya fani mbalimbali zinazohitajika katika maisha ya jamii ni faradhi kifaya kwa jamii ya Kiislamu. Kwa mfano ni faradhi kwa jamii ya Kiislamu kuwa na madaktari, wahandisi, wanasheria, wanasiasa, wanauchumi, waalimu na wataalamu wengineo katika kila fani ya maisha ya jamii wa kutosha kukidhi mahitajio ya jamii katika kuendea nyanja zote za maisha.


Ikitokezea Waislamu wamezembea kiasi cha kushindwa kutoa wataalamu wanaohitajika kuendesha kila fani ya maisha ya jamii mpaka inapelekea Waislamu kushindwa kumuabudu Mola wao ipasavyo katika kila kipengele cha maisha, jamii yote ya Waislamu itakuwa katika lawama (itapata dhambi) na itaathirika kutokana na dhambi hii.



Hivyo ili Waislamu waweze kusimamisha Uislamu (Ukhalifa wa Allah) katika jamii, kila Muislamu hanabudi kuufahamu Uislamu vilivyo na pawekwe mazingira ya makusudi yatakayomuwezesha kila Muislamu kujielimisha katika fani maalumu ya maisha inayohitajika katika jamii kwa kadiri ya vipaji alivyoruzukiwa na Mola wake.


Kwa maana nyingine kila Muislamu mwenye vipaji vya kuwa Daktari au Mhandisi au Mwanasheria au Mchumi au Mwalimu au …. ajizatiti kuiendea taaluma hiyo na jamii ijizatiti kumuwezesha. Endapo, kwa mfano Muislamu mwenye kipaji cha kuwa Daktari, akazembea asiwe Daktari atakuwa mas-uli mbele ya Allah (s.w). Pia endapo jamii ya Waislamu itazembea isitoe Madaktari wanaohitajika itakuwa mas-uli mbele ya Allah (s.w).




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 1891

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Uchambuzi wa Neema Alizopewa Nabii Sulaiman(a.s)

(i) Kutiishiwa Upepo Qur'an inatufahamisha kuwa Nabii Sulaiman alitiishiwa upepo akaweza kuutumia apendavyo kwa amri yake.

Soma Zaidi...
Lengo la ibada maalumu

Lengo la ibada maalumu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Elimu ya mwingozo na elimu ya mazingira katika uislamu

Mahusiano kati ya elimu ya mwongizo na elimu ya mazingira katika uislamu.

Soma Zaidi...
mitume

Labda itaulizwa: Kwanini Mtume Muhammad (s.

Soma Zaidi...
Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika surat Hashir

Huwaoni wale wanafiki wanawaambia ndugu zao walio makafiri miongoni mwa watu waliopewa Kitabu (kabla yenu) Mayahudi (Wanawaambia): "Kama mkitolewa, (mkifukuzwa hapa) tutaondoka pamoja nanyi, wala hat utamtii yoyote kabisa juu yenu.

Soma Zaidi...
UMBILE LA MBINGU NA ARDHI

“Katika kuumbwa mbingu na ardhi na mfuatano wa usiku na mchana,ziko alama (hoja) za kuonyesha kuwepo Allah (s.

Soma Zaidi...
Mafundisho yao kutoathiriwa na mazingira ya jamii zao

Takriban Mitume wote walitokea katika jamii zilizozama katika ujahili, lakini kamwe ujumbe wao haukuathiriwa na mitazamo ya ujahili kwa ujumla, walahawakuingizautamaduni wa kijahili katika dini ya Allah (s.

Soma Zaidi...
Mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini kutokana na maumbile yake

Kuwa ni kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini kutokana na umbile la mwanadamu.

Soma Zaidi...