image

Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat Al-Imran

Na kuwapambanua wale waliokuwa wanafiki.

Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat Al-Imran

Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat Al-Imran


Na kuwapambanua wale waliokuwa wanafiki. Nao waliambiwa: "Njooni mpigane katika njia ya Mwenyezi Mungu au mzuie (maadui pamoja na sisi)" Wakasema: "Tungejua kuwa kuna kupigana bila ya shaka tungelikufuateni." Wao siku ile walikuwa karibu na ukafiri kuliko na Uislamu (japokuwa siku zote wakidhihirisha Uislamu wa uwongo). Wanasema kwa midomo yao yasiyokuwa nyoyoni mwao. Na Mwenyezi Mungu anajua vyema (yote) wanayoyaficha. (3:167)


Wale waliosema juu ya ndugu zao - na (wao wenyewe) wamekataa kwenda (hawakwenda) vitani: "Wangalitutii wasingeuawa." Sema: "Jiondoleeni mauti (nyinyi) wenyewe msife maisha ikiwa mnasema kweli." (3:168)



"Wala usiwadhani wale waliouawa katika njia ya Mwenyezi Mungu kuwa ni wafu (maiti). Bali wahai, wanaruzukiwa kwa Mola wao." (3:169).
Kutokana na aya hizi tunapata sifa za wanafiki zifuatazo:



(i)Hawako tayari kujitoa muhanga kupigania dini ya Allah (s.w) isimame katika jamii au kuihami isiangushwe baada ya kusimama kwake.



(ii)Wanasema kwa midomo yao yasiyokuwa nyoyoni mwao. Baada ya mapambano dhidi ya maadui wa Dini ya Allah (s.w) kwisha, wanafiki hujikosha kwa kusema uwongo kuwa hawakuwa na taarifa juu ya mapambano ya Waislamu dhidi ya maadui zao, vinginevyo wangelikuwa Pamoja katika vita hivyo hali ya kuwa walijificha wasiende vitani kwa kuogopa kufa.



(iii)Huwabeza na kuwalaumu wale wanaouliwa au kupata misuko suko katika kuupigania Uislamu.
Katika aya ya 168 na 169 (3:168-1 69), Allah (s.w) anawasuta wanafiki na kuwakatisha tamaa kuwa mtu hafi kwa kuwa amepigania dini ya Allah (s.w), bali kila mtu atakufa kwa ajali yake aliyopangiwa:



โ€œโ€ฆ Sema: (uwaambia wanafiki): "Jiondosheeni mauti (nyinyi wenyewe msife milele) ikiwa mnasema kweli."



Pia Allah (s.w) anawakatisha tamaa wanafiki na kuwatumainisha waumini kuwa hapana jambo lililozuri na bora kwa mtu kuliko kufa katika njia ya Allah (s.w) (kufa shahidi).




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 230


Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Kitau cha Fiqh     ๐Ÿ‘‰2 Madrasa kiganjani     ๐Ÿ‘‰3 kitabu cha Simulizi     ๐Ÿ‘‰4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Mtazamo wa Uislamu juu ya usawa kati ya mwanaume na mwanamke
Soma Zaidi...

(viii)Wenye khushui katika swala
Waumini wa kweli waliofuzu huwa na khushui (unyenyekevu) katika swala. Soma Zaidi...

HISTORIA YA UANDISHI WA HADITHI
Historia fupi ya uandishi wa Hadith za Mtume (s. Soma Zaidi...

ndoto za kweli
Soma Zaidi...

KULA HALALI NA ZILICHO KIZURI NI AMRI KATIKA UISLAMU
ุนูŽู†ู’ ุฃูŽุจููŠ ู‡ูุฑูŽูŠู’ุฑูŽุฉูŽ ุฑูŽุถููŠูŽ ุงู„ู„ู‡ู ุนูŽู†ู’ู‡ู ู‚ูŽุงู„ูŽ: ู‚ูŽุงู„ูŽ ุฑูŽุณููˆู„ู ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุตู„ู‰ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆ ุณู„ู… "ุฅู†ูŽู‘ ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ูŽ ุทูŽูŠูู‘ุจูŒ ู„ูŽุง ูŠูŽู‚ู’ุจูŽู„ู ุฅู„ูŽู‘ุง ุทูŽูŠ... Soma Zaidi...

Nini maana ya Husda, na ni yapi madhara yake
34. Soma Zaidi...

Uandishi wa hadithi wakati wa tabiina (wafuasi wa maswahaba)
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

DARSA LA KUJIFUNZA KUHUSU QURAN NA SUNNAH
Soma Zaidi...

HADITHI YA MZEE WA KWANZA NA MBUZI
Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA MZEE WA KWANZA NA MBUZI WAKE. Soma Zaidi...

Kitabu Cha Darsa za Funga
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet. Soma Zaidi...

Kitabu Cha Dua 120
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet. Soma Zaidi...

nini maana ya Unafiki na sifa za unafiki katika quran na sunnah
Mnafiki ni yule anayeukubaliย Uislamu mdomoni (kwa kauli tu) lakini moyoni mwake na katika matendo yake anaukanusha. Soma Zaidi...