Hadhi na haki za mwanamke katika uislamu

Hadhi na haki za mwanamke katika uislamu

4.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Hadhi na haki za mwanamke katika uislamu

4. HADHI NA HAKI ZA MWANAMKE KA11KAJAMII YA KIISLAMU.
Maadui wa Uislamu na watu wasio ufahamu Uislamu vizuri, wameuangalia Uislamu kama wanavyoziangalia jamii nyinginezo na kushutumu Sheria za Kiislamu kuwa nazo zinamkandamiza mwanamke. Kutokana na shutuma hizi imekuwa ni wajibu kwetu katika sehemu hii kuonesha kwa uwazi jinsi Uislamu unavyompa mwanamke hadhi na haki zake. Tumeshaona kuwa wale wote waliojipiga kifua kuwa wanamtetea mwanamke na kumpa hadhi yake anayostahiki, harakati zao ziliishia ukutani. Walivunja familia ambayo ndio msingi wa jamii na walizidi kumdhalilisha mwanamke mpaka kufikia uduni kuliko ule wa hayawani.


Bila shaka watetezi hawa wa haki na hadhi ya mwanamke hawakuwa na nia mbaya ya kuzidi kumdunisha na kumkandamiza bali kosa lao kubwa ni kule kujiingiza kwao kwenye kazi wasio na ujuzi nayo. Allah (s.w) ndiye aliyemuumba mwanaadamu na vyote vilivyomzunguka. Hivyo ni Allah (s.w) pekee mwenye haki na uwezo wa kumuwekea mwanaadamu muongozo wa maisha mwenye kumuelekeza namna ya kukiendea kila kipengele cha maisha yake ya binafsi, familia, uchumu, siasa, utamaduni na maisha yote ya kijamii kwa ujumla ili aweze kuishi kwa furaha na amani na hapo hapo afikie lengo Ia kuumbwa kwake.


Ni dhahiri kwamba watu wanaokana au wasiotambua kuwepo kwa Allah (s.w) na mwongozo wake, ambao hujiundia sheria za kuiongoza na kuilinda jamii kutokana na msukumo wa matashi yao, kamwe hawawezi kuweka utaratibu utakao mhakikishia kila mtu katika jamii kupata haki zake zote na kuishi kwa furaha na amani. Hivyo wale wote wasiofuata mwongozo wa Allah (s.w), wasitegemee kamwe kupata haki zao na kuishi kwa furaha na amani katika jamii zao.



Tofauti na sheria za jamii zinazotungwa na binaadamu baada ya haja kutokea, sheria za Kiislamu kwak uwa zimewekwa na Allah (s.w), Mjuzi Mwenye Hekima, haziko pale kutosheleza haja ya dharura, bali zimekuwa pale hata kabla ya Adam (a.s) kuja hapa ulimwenguni. Hivyo ni vyema ifahamike tangu mwanzo kuwa katika mjadala wetu huu utaratibu au sheria ya Kiislamu ambayo inamhakikishia mwanake kupata haki na hadhi yake, haikutungwa baada ya kuona kuwa mwanamke anakandamizwa na kupuuzwa, bali ilikuwepo sheria hiyo hata kabla ya kuumbwa Adam na Hawa. Allah (s.w) anamfahamu vyema mwanaadamu kuwa endapo hatapewa mwongozo kutoka kwake na kuufuata ni muhali kuepukana na maisha hayo ya kudhulumiana na hasa wenye nguvu kuwadhulumu wanyonge.



Ili kutofautisha hatua za kumkomboa mwanamke zilizochukuliwa na jamii zilizojitahidi kufanya hivyo na hatua zinazochukuliwa na sheria ya Kiislamu, hapa tutajihusisha na vipengele vitatu vifuatavyo:-
1.Mtizamo wa Uislamu juu ya Usawa kati ya mwanamume na mwanamke.
2.Haki za mwanamke katika Uislamu.
3.Hifadhi ya mwanamke na maadili ya Jamii.


                   


Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Dini File: Download PDF Views 866

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰2 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰3 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰4 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

ZOEZI
ZOEZI

Zoezi laΒ 1 (a) Ainisha maana ya sunnah kilugha na kisheria.

Soma Zaidi...
Husimamisha swala
Husimamisha swala

Husimamisha swala katika maisha yao yote.

Soma Zaidi...
Matukio ya kihistoria katika masiku 10 ya Dhul Hija -Mfunguo tatu
Matukio ya kihistoria katika masiku 10 ya Dhul Hija -Mfunguo tatu

Haya ni matukio ya kihistoria yanayoamiika kutokea ndani ya masiku 10 ya Mfunguo tatu.

Soma Zaidi...
Zoezi
Zoezi

Maswali mbalimbali yanayohusu elimu ya dini ya kiislamu na mwongozo wa elimu na elimu mazingira.

Soma Zaidi...
(viii)Wenye khushui katika swala
(viii)Wenye khushui katika swala

Waumini wa kweli waliofuzu huwa na khushui (unyenyekevu) katika swala.

Soma Zaidi...
Uandishi wa hadithi wakati wa maswahaba wa mtume (s.a.w)
Uandishi wa hadithi wakati wa maswahaba wa mtume (s.a.w)

Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...