image

Hadhi na haki za mwanamke katika uislamu

4.

Hadhi na haki za mwanamke katika uislamu

4. HADHI NA HAKI ZA MWANAMKE KA11KAJAMII YA KIISLAMU.
Maadui wa Uislamu na watu wasio ufahamu Uislamu vizuri, wameuangalia Uislamu kama wanavyoziangalia jamii nyinginezo na kushutumu Sheria za Kiislamu kuwa nazo zinamkandamiza mwanamke. Kutokana na shutuma hizi imekuwa ni wajibu kwetu katika sehemu hii kuonesha kwa uwazi jinsi Uislamu unavyompa mwanamke hadhi na haki zake. Tumeshaona kuwa wale wote waliojipiga kifua kuwa wanamtetea mwanamke na kumpa hadhi yake anayostahiki, harakati zao ziliishia ukutani. Walivunja familia ambayo ndio msingi wa jamii na walizidi kumdhalilisha mwanamke mpaka kufikia uduni kuliko ule wa hayawani.


Bila shaka watetezi hawa wa haki na hadhi ya mwanamke hawakuwa na nia mbaya ya kuzidi kumdunisha na kumkandamiza bali kosa lao kubwa ni kule kujiingiza kwao kwenye kazi wasio na ujuzi nayo. Allah (s.w) ndiye aliyemuumba mwanaadamu na vyote vilivyomzunguka. Hivyo ni Allah (s.w) pekee mwenye haki na uwezo wa kumuwekea mwanaadamu muongozo wa maisha mwenye kumuelekeza namna ya kukiendea kila kipengele cha maisha yake ya binafsi, familia, uchumu, siasa, utamaduni na maisha yote ya kijamii kwa ujumla ili aweze kuishi kwa furaha na amani na hapo hapo afikie lengo Ia kuumbwa kwake.


Ni dhahiri kwamba watu wanaokana au wasiotambua kuwepo kwa Allah (s.w) na mwongozo wake, ambao hujiundia sheria za kuiongoza na kuilinda jamii kutokana na msukumo wa matashi yao, kamwe hawawezi kuweka utaratibu utakao mhakikishia kila mtu katika jamii kupata haki zake zote na kuishi kwa furaha na amani. Hivyo wale wote wasiofuata mwongozo wa Allah (s.w), wasitegemee kamwe kupata haki zao na kuishi kwa furaha na amani katika jamii zao.



Tofauti na sheria za jamii zinazotungwa na binaadamu baada ya haja kutokea, sheria za Kiislamu kwak uwa zimewekwa na Allah (s.w), Mjuzi Mwenye Hekima, haziko pale kutosheleza haja ya dharura, bali zimekuwa pale hata kabla ya Adam (a.s) kuja hapa ulimwenguni. Hivyo ni vyema ifahamike tangu mwanzo kuwa katika mjadala wetu huu utaratibu au sheria ya Kiislamu ambayo inamhakikishia mwanake kupata haki na hadhi yake, haikutungwa baada ya kuona kuwa mwanamke anakandamizwa na kupuuzwa, bali ilikuwepo sheria hiyo hata kabla ya kuumbwa Adam na Hawa. Allah (s.w) anamfahamu vyema mwanaadamu kuwa endapo hatapewa mwongozo kutoka kwake na kuufuata ni muhali kuepukana na maisha hayo ya kudhulumiana na hasa wenye nguvu kuwadhulumu wanyonge.



Ili kutofautisha hatua za kumkomboa mwanamke zilizochukuliwa na jamii zilizojitahidi kufanya hivyo na hatua zinazochukuliwa na sheria ya Kiislamu, hapa tutajihusisha na vipengele vitatu vifuatavyo:-
1.Mtizamo wa Uislamu juu ya Usawa kati ya mwanamume na mwanamke.
2.Haki za mwanamke katika Uislamu.
3.Hifadhi ya mwanamke na maadili ya Jamii.


                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 262


Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Kitabu cha Afya     ๐Ÿ‘‰2 Madrasa kiganjani     ๐Ÿ‘‰3 kitabu cha Simulizi     ๐Ÿ‘‰4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Assalam Baada yakufariki wazazi wake mtume alilelewa nanani???
Mtume Muhammad s.a.w amezaliwa yatima asiyena baba. Lakini hii haikumfanya asipate maelezo bora yaliyo mazuri. Je unajuwa aliyemlea baada ya kufariki kwa mama yake?. Soma Zaidi...

nini maana ya Unafiki na sifa za unafiki katika quran na sunnah
Mnafiki ni yule anayeukubaliย Uislamu mdomoni (kwa kauli tu) lakini moyoni mwake na katika matendo yake anaukanusha. Soma Zaidi...

Zoezi
Maswali mbalimbali yanayohusu elimu ya dini ya kiislamu na mwongozo wa elimu na elimu mazingira. Soma Zaidi...

Zingatio:
Swala husimama kwa kuhifadhiwa na kuswaliwa kwa khushui na kudumu na swala katika maisha yote. Soma Zaidi...

dharura
14. Soma Zaidi...

HUYU NDIYE MUUMINI WA KWELI KATIKA UISLAMU
ุนูŽู†ู’ ุฃูŽุจููŠ ุญูŽู…ู’ุฒูŽุฉูŽ ุฃูŽู†ูŽุณู ุจู’ู†ู ู…ูŽุงู„ููƒู ุฑูŽุถููŠูŽ ุงู„ู„ู‡ู ุนูŽู†ู’ู‡ู ุฎูŽุงุฏูู…ู ุฑูŽุณููˆู„ู ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุตู„ู‰ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆ ุณู„ู… ุนูŽู†ู’ ุงู„ู†ูŽู‘ุจููŠูู‘ ุตู„ู‰ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ?... Soma Zaidi...

Mtazamo wa Uislamu juu ya usawa kati ya mwanaume na mwanamke
Soma Zaidi...

kuwa mwenye huruma na faida zake
25. Soma Zaidi...

Maswali juu ya hadithi
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya) Soma Zaidi...

Zoezi - 4
Soma Zaidi...

HISTORIA YA UANDISHI WA HADITHI
Historia fupi ya uandishi wa Hadith za Mtume (s. Soma Zaidi...

Zoezi - 3:
1. Soma Zaidi...