image

Hadhi na haki za mwanamke katika uislamu

4.

Hadhi na haki za mwanamke katika uislamu

4. HADHI NA HAKI ZA MWANAMKE KA11KAJAMII YA KIISLAMU.
Maadui wa Uislamu na watu wasio ufahamu Uislamu vizuri, wameuangalia Uislamu kama wanavyoziangalia jamii nyinginezo na kushutumu Sheria za Kiislamu kuwa nazo zinamkandamiza mwanamke. Kutokana na shutuma hizi imekuwa ni wajibu kwetu katika sehemu hii kuonesha kwa uwazi jinsi Uislamu unavyompa mwanamke hadhi na haki zake. Tumeshaona kuwa wale wote waliojipiga kifua kuwa wanamtetea mwanamke na kumpa hadhi yake anayostahiki, harakati zao ziliishia ukutani. Walivunja familia ambayo ndio msingi wa jamii na walizidi kumdhalilisha mwanamke mpaka kufikia uduni kuliko ule wa hayawani.


Bila shaka watetezi hawa wa haki na hadhi ya mwanamke hawakuwa na nia mbaya ya kuzidi kumdunisha na kumkandamiza bali kosa lao kubwa ni kule kujiingiza kwao kwenye kazi wasio na ujuzi nayo. Allah (s.w) ndiye aliyemuumba mwanaadamu na vyote vilivyomzunguka. Hivyo ni Allah (s.w) pekee mwenye haki na uwezo wa kumuwekea mwanaadamu muongozo wa maisha mwenye kumuelekeza namna ya kukiendea kila kipengele cha maisha yake ya binafsi, familia, uchumu, siasa, utamaduni na maisha yote ya kijamii kwa ujumla ili aweze kuishi kwa furaha na amani na hapo hapo afikie lengo Ia kuumbwa kwake.


Ni dhahiri kwamba watu wanaokana au wasiotambua kuwepo kwa Allah (s.w) na mwongozo wake, ambao hujiundia sheria za kuiongoza na kuilinda jamii kutokana na msukumo wa matashi yao, kamwe hawawezi kuweka utaratibu utakao mhakikishia kila mtu katika jamii kupata haki zake zote na kuishi kwa furaha na amani. Hivyo wale wote wasiofuata mwongozo wa Allah (s.w), wasitegemee kamwe kupata haki zao na kuishi kwa furaha na amani katika jamii zao.



Tofauti na sheria za jamii zinazotungwa na binaadamu baada ya haja kutokea, sheria za Kiislamu kwak uwa zimewekwa na Allah (s.w), Mjuzi Mwenye Hekima, haziko pale kutosheleza haja ya dharura, bali zimekuwa pale hata kabla ya Adam (a.s) kuja hapa ulimwenguni. Hivyo ni vyema ifahamike tangu mwanzo kuwa katika mjadala wetu huu utaratibu au sheria ya Kiislamu ambayo inamhakikishia mwanake kupata haki na hadhi yake, haikutungwa baada ya kuona kuwa mwanamke anakandamizwa na kupuuzwa, bali ilikuwepo sheria hiyo hata kabla ya kuumbwa Adam na Hawa. Allah (s.w) anamfahamu vyema mwanaadamu kuwa endapo hatapewa mwongozo kutoka kwake na kuufuata ni muhali kuepukana na maisha hayo ya kudhulumiana na hasa wenye nguvu kuwadhulumu wanyonge.



Ili kutofautisha hatua za kumkomboa mwanamke zilizochukuliwa na jamii zilizojitahidi kufanya hivyo na hatua zinazochukuliwa na sheria ya Kiislamu, hapa tutajihusisha na vipengele vitatu vifuatavyo:-
1.Mtizamo wa Uislamu juu ya Usawa kati ya mwanamume na mwanamke.
2.Haki za mwanamke katika Uislamu.
3.Hifadhi ya mwanamke na maadili ya Jamii.


                   




           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 163


Download our Apps
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Neno la awali
Asalaamu alykum warahmatullah wabarakaatuh Sifanjema zinamstahikia Allah Mola wa viumbe, muumba wa mbingu na ardhi na vilivyomo. Soma Zaidi...

(ix)Wenye kuhifadhi swala
Waumini wa kweli waliofuzu huhifadhi swala kwa kutekeleza kwa ukamilifu shuruti zote za swala nguzo zote za swala na huswali kama alivyoswali Mtume (s. Soma Zaidi...

MAADILI MEMA KATIKA UISLAMU
Yajuwe maadili mema yaliyotajwa katika quran Soma Zaidi...

Zoezi 2:2
Soma Zaidi...

jamii zoezi
Zoezi 2:1 1. Soma Zaidi...

Zoezi - 4
Soma Zaidi...

Kwanini Ni muhimu kusimamisha uislamu katika jamii
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

dharura
14. Soma Zaidi...

Epuka kukata tamaa, na yajuwe madhara ya kukata tamaa
37. Soma Zaidi...

quran na sayansi
QURANI KATIKA ZAMA ZA SAYANSI NA TEKNOLOJIAAsalaalaamu alykum warahmatullah wabarakaatuh. Soma Zaidi...

Madhara ya matusi katika jamii, na Kujiepusha na Matusi
15. Soma Zaidi...

Iv shekh haifai kufunga kwa nia utimize jambo labda kuna kitu unakitaka kwhy unaamua kugunga ili kama kuzidisha maombi kwa mungu jambo lifanikiwe
Ibada yavfubga ni katika ibadavanbazo hufanya nakaribia dini zote kubwa. Ibada hii imekuwaikikabiliw na naswlo mengi. Soma Zaidi...