Mambo yasiyoharibu Swaumu na Kufunguza mwenye kufunga

Mambo yasiyoharibu Swaumu na Kufunguza mwenye kufunga

Yasiyobatilisha funga



Kuna baadhi ya mambo ambayo mtu aliyefunga akiyafanya, anaweza kujiona kuwa amefungua lakini bado hajafungua. Miongoni mwa mambo haya ni:



(i)Kula au Kunywa kwa Kusahau



Mtu akiwa amesahau kuwa amefunga akala au akanywa kiasi chochote, hata kiasi cha kushiba, bado atakuwa na swaumu kwa ushahidi wa Hadith zifuatazo:
Abu hurairah(r.a) amesema kuwa Mtume (s.a.w) amesema: 'Anayefungua Ramadhani kwa kusahau hatalipa wala hatatoa kafara' (Daral Qutni, Bayhaqi na Hakim).
Abu Hurairah ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: Yeyote yule atakayesahau akala au akanywa wakati amefunga, na amalizie funga yake kwa sababu Allah (s.w) amemlisha na kumnywesha '. (Bukhari na Muslim).



Hali kadhalika, kama mtu atalishwa au kunyweshwa au kufuturishwa kwa namna yoyote ile kwa kutezwa nguvu, saumu yake haitabatilika:
Ibn Abbas (r.a) ameeleza kwamba Mtume (s.a.w) amesema: 'Mwenyezi Mungu ameuondolea umati wangu (Jukumu la) kukosea, kusahau na waliotezwa nguvu.' (Ibn Majah, Ta bran na Hakim).



(ii)Kuoga wakati umefunga



Kuoga kwa kujimwagia maji au kujitumbukiza majini hakuharibu funga kwa maana imepokelewa kwamba Mtume (s.a.w) alikuwa akijimwagia maji kichwani kwa sababu ya kiu au joto, hali amefunga:



Mmoja wa Maswahaba ameeleza: Hakika nimemuona Mtume (s.a.w) akiwa Arji (bonde moja kati ya Makka na Madina) akijimwagilia maji kichwani mwake akiwa amefunga kwa sababu ya kiu au joto. (Malik, Abu Daud).


(iii)Kutokwa na Manii
Mtu akitokwa na manii kwa kuota au kwa namna ambayo hakukusudia, atakuwa hajafungua.



(iv)Kuamka na Janaba



Kuamka na janaba hakufunguzi kwani Mtume (s.a.w) wakati mwingine alikuwa anaamka na janaba na huku amefunga.
Aysha (r.a) ameeleza kuwa alfajiri iliingia wakati Mtume (s.a.w) yuko katika janaba. Kisha alioga na kuendelea na swaumu. (Bukhari na Muslim).
Hali kadhalika mwenye hedhi au nifasi, ambaye damu yake ilikoma kabla ya alfajiri, akiamka atafunga hata kama atakuwa hajaoga.
(v)Kubusiana na kukumbatiana Mume na Mke



Mtu kumbusu na kumkumbatia mkewe au mumewe wakati amefunga haiharibu funga iwapo kuna haja ya kufanya hivyo alimradi tu waweze kujizuia wasiendelee zaidi ya hapo. Hivi ndivyo tunavyojifunza katika Hadithi ifuatayo:
Aysha (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah alikuwa akimbusu na kumkumbatia wakati amefunga na alikuwa mw enye kumiliki matashi yake kuliko yeyote miongoni mw enu (Bukhari na Muslim).



Amehadithia baba wa Hisham kuwa: Aysha (r.a) amesema: 'Mtume wa Allah alikuwa akiwabusu baadhi ya wake zake akiwa amefunga: na kisha akacheka. (Bukhari).
Miongoni mwa Masahaba walioruhusu hili la mtu kumbusu na kukumbatia mkewe wakati amefunga ni Sayyidna Umar (r.a), Ibn Abbas (r.a.), Abu-Hurairah (r.a) na Bibi Aysha (r.a). Kwa maoni ya Imam Abu Hanifa na Shafii, kumbusu na kumkumbatia wakati mtu amefunga ni makruhu iwapo kutaamsha matamanio. Vinginevyo si makruhu, lakini ni bora kuacha iwapo hapana haja ya lazima kufanya hivyo.



(vi)Kupiga Mswaki



Si vibaya kupiga mswaki wakati mtu amefunga kwani Mtume (s.a.w) alikuwa akipiga mswaki wakati amefunga kama tunavyofahamishwa katika Hadith zifuatazo:
Amr bin Rabiyah (r.a) ameeleza: Nilimuona mtume (s.a.w) Mara nyingi nisizoweza kuhesabu akipiga msw aki akiwa amefunga.(Tirmidh na Abu Da ud).


Amesimulia Abu Hurairah(r.a) kuwa Mtume (s.a.w) amesema: Si kwa kuw a ninahofia kuw a litakuw a jam bo zito kw a umm ati w angu, ningekuw a nimeshawaamrisha kutumia mswaki (kupiga mswaki) kila wakitawadha. (Bukh ari).



Hadith hii haikubagua mtu aliyefunga na asiyefunga. Bali tunapata fundisho kuwa kupiga mswaki ni kitendo kilichosisitizwa sana.
Bibi Aysha (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: 'Mswaki hutakasa mdomo na ni njia ya kutakia Radhi za Allah (s.w). ' (Bukhari).



(vii)Kusukutua na kupandisha Maji Puani



Wakati mtu anatawadha anaruhusiwa kusukutua na kupandisha maji puani lakini asifanye sana mpaka maji yakaingia ndani kwani hilo amelikataza Mtume (s.a.w) katika Hadith iliyopokelewa na Abu Daud, Tirmidh, Ibn Majah na Nasai.



(viii)Kupaka Wanja na Dawa ya Machoni



Kupaka wanja kunaruhusiwa kwa mtu aliyefunga Mtume (s.a.w) ameruhusu hilo katika Hadith ifuatayo:
Anas(r.a) ameeleza kuwa mtu mmoja amekuja kwa Mtume (s.a.w) na akasema: 'Ninaumwa macho. Ninaweza kupaka wanja wakati nimefunga? `Ndio' Alijibu Mtume (s.a.w).'



Pia dawa ya macho iwe ya mafuta au ya maji inaruhusiwa kutumiwa wakati mtu amefunga kwa sababu hapana tundu la kuungana moja kwa moja na koo kama yalivyo matundu ya pua na masikio.



(ix)Kumeza usichoweza kujizuia nacho
Ukimeza vitu usivyoweza kujizuia kama vile mate, kohozi, vumbi la njiani, vumbi la unga, kumeza mdudu aliyeingia kwa ghafla hadi kooni, n.k. utakuwa hujafungua.



(x)Kujipaka mafuta au manukato
Kujipaka mafuta au manukato mwilini au nguoni, kunusa manukato, kujifukiza udi na ubani, n.k. hakuharibu funga.



(xi)Kuumika au kutoa Damu
Kuumika hakufunguzi kwani Mtume (s.a.w) amefanya hivyo wakati akiwa amefunga kama tunavyofahamishwa katika Hadith ifuatayo:
Amehadithia Ibn Abbas (r.a) kwamba Mtume (s.a.w) aliumikwa akiwa katika 'Ihram' na pia akiwa amefunga. (Bukhari).


Hata hivyo, kama kuumika huko kutamfanya mtu awe dhaifu, basi itakuwa ni makruhu. Hali kadhalika mtu anaruhusiwa kutoa damu kwa ajili ya kuwasaidia wagonjwa (blood transfusion), akiwa amefunga.



(xii) Kupiga Sindano
Kupiga sindano ya dawa, iwe ya mshipa au chini ya ngozi, haifunguzi.




                   


Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 244

Post zifazofanana:-

Njama za Kumuua Nabii Yusufu(a.s)
Kwa tabia zake njema Yusufu(a. Soma Zaidi...

ATHARI ZA KUTOKUTIBU MINYOO: maumivu ya tumbo, kichwa, kutapika damu, kichefuchefu, miwasho
ATHARI ZA KUTOKUTIBU MINYOO Kukaa na minyoo na kutoitibu kwa muda mrefu kunaweza kusababisha madhara mengi hususani kwenye ini na maeneo mengine ya mfumo wa kumeng'enya chakula. Soma Zaidi...

ninasumbuliwa Sana na mapunye ya kichwani nimetumia dawa takribani miaka 3
Habari, samahani ninasumbuliwa Sana na mapunye ya kichwani nimetumia dawa takribani miaka 3 ila yanapona Tena baada ya Muda flani yanatokea. Soma Zaidi...

Je! vitu vichachu kama,machungwa twarusiwa kula wagonjwa wa vidonda vya tumbo?
Nashukuru kwa ushauri, Je! Soma Zaidi...

Utajiri wa Baba na kifo chake
UTAJIRI WA BABA NA KIFO CHAKE. Soma Zaidi...

DUA 61 - 84
61. Soma Zaidi...

Ni zipi siku ambazo ni haramu kufunga? na ni kwa nini hairuhusiwi kufunga katika siku hizo
Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII DAUD
Soma Zaidi...

Faida za kula Zaituni
Matunda ya zamani, matunda ya asili, Zaituni tunda lipendezalo, zijuwe faida zake leo Soma Zaidi...

nikiasi gani chaprotini kinachohitajika mwilini kwa siku kwa mtumzima
Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ayyuub(a.s)
Kutokana na kisha hiki cha Nabii Ayyuub(a. Soma Zaidi...

DARSA ZA TAWHID
Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala Soma Zaidi...