ZIJUWE NAMNA ZA KUZUIA HASIRA, NA MADHARA YA HASIRA

ZIJUWE NAMNA ZA KUZUIA HASIRA, NA MADHARA YA HASIRA

28.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

ZIJUWE NAMNA ZA KUZUIA HASIRA, NA MADHARA YA HASIRA

28. Kudhibiti Hasira



Kujizuia na hasira ni tabia njema inayoambatana na tabia ya kusamehe. Hasira humpata mtu anapoudhiwa. Wakati mwingine huja ghafla na kumnyima mtu wakati wa kufikiri. Hasira zinaongozwa na shetani, hivyo humnyima mtu nafasi ya kutumia akili, hekima na busara. Hivyo humpelekea mtu kufanya matendo ambayo hugeuka kuwa majuto baadaye. Hasira hasara. Kujizuilia na hasira ni kitendo cha ucha Mungu chenye malipo makubwa mbele ya Allah (s.w). Rejea Qur-an (3:133-134) na (42:36-37). Pia ubora wa kujizuilia na hasira unadhihirika katika Hadithi zifuatazo:



Abu Hurairah(r.a) am esim ulia kuw a m tu mm oja alim uom ba Mtum e (s.a.w): “Niwaidhi’. Mtume akasema: “Usighadhibike”. Kisha akarudia mara nyingi akisema: Usighadhibike. (Bukhari)



Abu Hurairah(r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema “Mtu mwenye nguvu si bingwa wa mieleka bali mtu mwenye nguvu ni yule anayejizuilia na has ira ”. (Bukhari na Muslim).



Ibn Umar amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: “Hapana mja aliyemeza kidonge kichungu mbele ya Allah (s.w) kuliko kidonge cha hasira alichokimeza, huku akitaraji radhi ya Allah (s.w)”. (Ahmad).
Mbinu za kujizuia na hasira zimebainishwa katika Qur-an kama ifu atavyo:



“Shikamana na kusamehe na amrisha mema na wapuuze majahili (wajinga). Na kama wasi wasi wa shetani ukikusumbua basi (sema: Audhubillah) jikinge kwa Mwenyezi Mungu. Bila shaka yeye ndiye asikiaye na ajuaye.” (7:199-200).
Kutokana na aya hizi
hasira ni hizi zifuatazo:
(i) Kushikamana
(ii) Kushikamana
(iii) Kuwapuuza m
(iv) Kujikinga kwa tunajifunza kuwa mbinu za kujizuilia na


na kusamehe.
na kuamrisha mema.
ajah ili.
Allah (s.w) na uovu wa shetani.


Pia Mtume (s.a.w) anatupa mbinu nyingine za kupambana na hasira katika Hadithi zifuatazo:
Atiyyah bin Urw ah Ba ’id(r.a) ameeleza kuw a Mtume w a Allah amesema: “Hakika hasira zinatoka kwa Shetani, na Shetani ameumbwa kutokana na moto na hakika moto huzimishwa na maji. Kwa hiyo yoyote miongoni mwenu atakayepandwa na hasira, na atawadhe”. (Abu Daud).



Abu Dharr (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: “Wakati wowote mmoja wenu atakapopandwa na hasira akiwa amesimama, na akae chini. Kama (kwa kufanya hivyo) hasira itamtoka ni vyema; lakini kama haitatoka, na alale chini”. (Ahmad, Tirmidh).



Kutokana na Hadithi hizi Mtume (s.a.w) anatuelekeza tupunguze hasira zetu kwa:
(i)Kutia udhu.
(ii)Kukaa chini iwapo tumesimama.
(iii)Kulala chini.




                   


Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 1500

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

KUKUSANYIKA KATIKA DUA
KUKUSANYIKA KATIKA DUA

KUKUSANYIKA KATIKA DUA.

Soma Zaidi...
BAADHI YA DUA ZA KILA SIKU
BAADHI YA DUA ZA KILA SIKU

BAADHI YA DUA ZA KILA SIKU.

Soma Zaidi...
Sura za kujikinga na Uchawi na mashetani
Sura za kujikinga na Uchawi na mashetani

Post hii itakwenda kukufundisha sura katika Quran ambazo ni kinga dhidi ya Wachawi, uchawi na Masheitwani.

Soma Zaidi...
KUINGIA KWA WAGENI
KUINGIA KWA WAGENI

Download kitabu Hiki Bofya hapa KUINGIA KWA WAGENI Amina na Sadie walimuonea huruma wakamuomba Zubeid amruhusu abakie.

Soma Zaidi...
DUA 113 - 126
DUA 113 - 126

DUA ZA WAKATI WA SHIDA Dua ya wakati wa taabu “LAA ILAAHA ILLA-LLAHUL-’ADHIMUL-HALIIMU.

Soma Zaidi...
DUA na Adhkar  kutoka kwenye quran
DUA na Adhkar kutoka kwenye quran

hii ni orodha ya dua mbalimbali kutoka kwenye quran. Unaweza kuzitumia dua hizi kujipendekeza kwa Allah na kupata msamaha, neema na mengineyo.

Soma Zaidi...
DUA ZENYE MANENO HAYA HUJIBIWA
DUA ZENYE MANENO HAYA HUJIBIWA

SIFA ZA (MANENO NA MATAMSHI YA) DUA YENYE KUJIBIWA.

Soma Zaidi...