image

ZIJUWE NAMNA ZA KUZUIA HASIRA, NA MADHARA YA HASIRA

28.

ZIJUWE NAMNA ZA KUZUIA HASIRA, NA MADHARA YA HASIRA

28. Kudhibiti Hasira



Kujizuia na hasira ni tabia njema inayoambatana na tabia ya kusamehe. Hasira humpata mtu anapoudhiwa. Wakati mwingine huja ghafla na kumnyima mtu wakati wa kufikiri. Hasira zinaongozwa na shetani, hivyo humnyima mtu nafasi ya kutumia akili, hekima na busara. Hivyo humpelekea mtu kufanya matendo ambayo hugeuka kuwa majuto baadaye. Hasira hasara. Kujizuilia na hasira ni kitendo cha ucha Mungu chenye malipo makubwa mbele ya Allah (s.w). Rejea Qur-an (3:133-134) na (42:36-37). Pia ubora wa kujizuilia na hasira unadhihirika katika Hadithi zifuatazo:



Abu Hurairah(r.a) am esim ulia kuw a m tu mm oja alim uom ba Mtum e (s.a.w): “Niwaidhi’. Mtume akasema: “Usighadhibike”. Kisha akarudia mara nyingi akisema: Usighadhibike. (Bukhari)



Abu Hurairah(r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema “Mtu mwenye nguvu si bingwa wa mieleka bali mtu mwenye nguvu ni yule anayejizuilia na has ira ”. (Bukhari na Muslim).



Ibn Umar amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: “Hapana mja aliyemeza kidonge kichungu mbele ya Allah (s.w) kuliko kidonge cha hasira alichokimeza, huku akitaraji radhi ya Allah (s.w)”. (Ahmad).
Mbinu za kujizuia na hasira zimebainishwa katika Qur-an kama ifu atavyo:



“Shikamana na kusamehe na amrisha mema na wapuuze majahili (wajinga). Na kama wasi wasi wa shetani ukikusumbua basi (sema: Audhubillah) jikinge kwa Mwenyezi Mungu. Bila shaka yeye ndiye asikiaye na ajuaye.” (7:199-200).
Kutokana na aya hizi
hasira ni hizi zifuatazo:
(i) Kushikamana
(ii) Kushikamana
(iii) Kuwapuuza m
(iv) Kujikinga kwa tunajifunza kuwa mbinu za kujizuilia na


na kusamehe.
na kuamrisha mema.
ajah ili.
Allah (s.w) na uovu wa shetani.


Pia Mtume (s.a.w) anatupa mbinu nyingine za kupambana na hasira katika Hadithi zifuatazo:
Atiyyah bin Urw ah Ba ’id(r.a) ameeleza kuw a Mtume w a Allah amesema: “Hakika hasira zinatoka kwa Shetani, na Shetani ameumbwa kutokana na moto na hakika moto huzimishwa na maji. Kwa hiyo yoyote miongoni mwenu atakayepandwa na hasira, na atawadhe”. (Abu Daud).



Abu Dharr (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: “Wakati wowote mmoja wenu atakapopandwa na hasira akiwa amesimama, na akae chini. Kama (kwa kufanya hivyo) hasira itamtoka ni vyema; lakini kama haitatoka, na alale chini”. (Ahmad, Tirmidh).



Kutokana na Hadithi hizi Mtume (s.a.w) anatuelekeza tupunguze hasira zetu kwa:
(i)Kutia udhu.
(ii)Kukaa chini iwapo tumesimama.
(iii)Kulala chini.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 607


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Mipaka katika kumtii mzazi, na mambo yasiyopasa kumtii mzazi
Soma Zaidi...

HADITHI NA SUNNAH
1. Soma Zaidi...

Nafasi ya Sunnah (suna) katika Uislamu.
Hapa utajifunza nafasi ya kufuata suna katika Uislamu Soma Zaidi...

DUA YA 1 - 10
1. Soma Zaidi...

Fadhila za udhu yaani faida za udhu
Katika makala hii utajifunza faida za kuwa na udhu Soma Zaidi...

DUA ZA WAKATI WA SHIDA
DUA ZA WAKATI WA SHIDA 1. Soma Zaidi...

AINA ZA HADITHI
Aina za HadithKuna aina kuu mbili za Hadith- (a) Hadith Nabawiyyi. Soma Zaidi...

Mafunzo ya hadithi zilizochaguliwa
Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

kujiepusha na uongo na sifa za uongo
Uwongo ni kinyume cha ukweli. Soma Zaidi...

DUA 11 - 20
11. Soma Zaidi...

Al-Arba'uwn An-Nawawiyyah hadithi ya 1: Nia
huu ni mwanzo wa kitabu hiki cha Matn arbaina Naway Soma Zaidi...

DUA 21 - 31
21. Soma Zaidi...