ZIJUWE NAMNA ZA KUZUIA HASIRA, NA MADHARA YA HASIRA

28.

ZIJUWE NAMNA ZA KUZUIA HASIRA, NA MADHARA YA HASIRA

28. Kudhibiti Hasira



Kujizuia na hasira ni tabia njema inayoambatana na tabia ya kusamehe. Hasira humpata mtu anapoudhiwa. Wakati mwingine huja ghafla na kumnyima mtu wakati wa kufikiri. Hasira zinaongozwa na shetani, hivyo humnyima mtu nafasi ya kutumia akili, hekima na busara. Hivyo humpelekea mtu kufanya matendo ambayo hugeuka kuwa majuto baadaye. Hasira hasara. Kujizuilia na hasira ni kitendo cha ucha Mungu chenye malipo makubwa mbele ya Allah (s.w). Rejea Qur-an (3:133-134) na (42:36-37). Pia ubora wa kujizuilia na hasira unadhihirika katika Hadithi zifuatazo:



Abu Hurairah(r.a) am esim ulia kuw a m tu mm oja alim uom ba Mtum e (s.a.w): “Niwaidhi’. Mtume akasema: “Usighadhibike”. Kisha akarudia mara nyingi akisema: Usighadhibike. (Bukhari)



Abu Hurairah(r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema “Mtu mwenye nguvu si bingwa wa mieleka bali mtu mwenye nguvu ni yule anayejizuilia na has ira ”. (Bukhari na Muslim).



Ibn Umar amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: “Hapana mja aliyemeza kidonge kichungu mbele ya Allah (s.w) kuliko kidonge cha hasira alichokimeza, huku akitaraji radhi ya Allah (s.w)”. (Ahmad).
Mbinu za kujizuia na hasira zimebainishwa katika Qur-an kama ifu atavyo:



“Shikamana na kusamehe na amrisha mema na wapuuze majahili (wajinga). Na kama wasi wasi wa shetani ukikusumbua basi (sema: Audhubillah) jikinge kwa Mwenyezi Mungu. Bila shaka yeye ndiye asikiaye na ajuaye.” (7:199-200).
Kutokana na aya hizi
hasira ni hizi zifuatazo:
(i) Kushikamana
(ii) Kushikamana
(iii) Kuwapuuza m
(iv) Kujikinga kwa tunajifunza kuwa mbinu za kujizuilia na


na kusamehe.
na kuamrisha mema.
ajah ili.
Allah (s.w) na uovu wa shetani.


Pia Mtume (s.a.w) anatupa mbinu nyingine za kupambana na hasira katika Hadithi zifuatazo:
Atiyyah bin Urw ah Ba ’id(r.a) ameeleza kuw a Mtume w a Allah amesema: “Hakika hasira zinatoka kwa Shetani, na Shetani ameumbwa kutokana na moto na hakika moto huzimishwa na maji. Kwa hiyo yoyote miongoni mwenu atakayepandwa na hasira, na atawadhe”. (Abu Daud).



Abu Dharr (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: “Wakati wowote mmoja wenu atakapopandwa na hasira akiwa amesimama, na akae chini. Kama (kwa kufanya hivyo) hasira itamtoka ni vyema; lakini kama haitatoka, na alale chini”. (Ahmad, Tirmidh).



Kutokana na Hadithi hizi Mtume (s.a.w) anatuelekeza tupunguze hasira zetu kwa:
(i)Kutia udhu.
(ii)Kukaa chini iwapo tumesimama.
(iii)Kulala chini.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 1819

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Fadhila za udhu yaani faida za udhu

Katika makala hii utajifunza faida za kuwa na udhu

Soma Zaidi...
MAANA NA FADHILA ZA KUOMBA DUA

DUA Kwa ufupi dua ni kumuomba Allah akuondoshee lililobaya, ama linalo kuudhi ama akupe jambo fulani.

Soma Zaidi...
Ijuwe swala ya Mtume na fadhila zake na jinsi ya kumswalia Mtume.

Post hii itakufundisha jinsi ya kumswalia mtume, pamoja na kuzijuwa fadhila unazopata kwa kumswalia Mtume

Soma Zaidi...
TANZU ZA HADITHI

Tanzu za Hadith(1) Tanzu ya UsahihiKulingana na kiwango cha usahihi wa Hadith, Hadith zimegawanywa katika makundi makuu manne:(a) Sahihi (b) Hasan/Nzuri.

Soma Zaidi...
Hukumu ya kukusanyika kwenye dua na umuhimu wa dua ya watu wengi

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu umuhimu wa kukusanyika katika kuomba dua.

Soma Zaidi...
Namna ambazo Allah hujibu dua ya mwenye kuomba.

Post hii inakwenda kukufundisha namna ama staili ambazo Allah hujibu dua za watu.

Soma Zaidi...
Historia ya uandishi wa Hadithi, na ni kwa nini wakati wa Mtunme hakukuwa na uandishibmkubwa wa hadithi

Hapa utakwendabkuijuwabhistoria ya uandishi wa hadithi. Pia utaijuwa sababu iliyopelekea uandishi wa hadithi kuwa mdogo .

Soma Zaidi...
Matamshi ambayo ukimwambia Allah kwenye dua yako basi hujibiwa kwa haraka dua hiyo

Post hii inakwenda kukufundisha matamshi ambayo mtu akiyatamka Allah hujibu dua hiyo kwa urahisi.

Soma Zaidi...
NAMNA AMBAZO DUA HUJIBIWA

NAMNA AMBAYO ALLAH HUJIBU DUA.

Soma Zaidi...
DUA ZA WAKATI WA SHIDA

DUA ZA WAKATI WA SHIDA 1.

Soma Zaidi...