Nabii Ibrahiim(a.s) Kuulingania Uislamu kwa Jamii Yake

Nabii Ibrahiim(a.s) Kuulingania Uislamu kwa Jamii Yake

Nabii Ibrahim(a.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Nabii Ibrahiim(a.s) Kuulingania Uislamu kwa Jamii Yake

Nabii Ibrahiim(a.s) Kuulingania Uislamu kwa Jamii Yake


Nabii Ibrahim(a.s), baada ya kupingwa mawe na kufukuzwa na baba yake mzazi, hakukata tamaa bali aliamua kuikabili jamii na kuifikishia ujumbe wa Uislamu kwa hekima kwa kutumia hoja madhubuti.




(Na kumbukeni) Ibrahimu alipomwambia baba yake Azara “Unawafanya masanamu kuwa waungu? Hakika ninakuona wewe na watu wako mumo katika upotofu (upotevu) ulio dhahiri.(6:74)




Na namna hivi tulimwonyesha Ibrahimu Ufalme wa mbingu na ardhi (kuwa ni wa Mwenyezi Mungu), na ili awe miongoni mwa wenye yakini.(6:75)



Na usiku ulipomwingilia (Ibrahimu na hali kakaa na makafiri) akaona nyota, alinena “(Nyota) hii ni Mola wangu.” Ilipotua (ikapotea), alisema (kuwaambia wale makafiri kama kwamba yu pamoja nao katika Ibada ile): “Sipendi waola wanaopotea (hawawepo ila wakati makhsusi tu).(6:76)



Na (usiku wa pili) alipouona mwezi unachomoza alisema: “Huu (mwezi) ndio Mola wangu.” Ulipotua alisema: “Asiponiongoza Mola wangu, bila shaka nitakuwa miongoni mwa watu wapotofu(Na Mola huyu hawezi kuniongoza kwani anakuwa hayupo wakati mwingine).” (6:77).




Na (siku ya tatu) alipoliona jua linachomoza alisema (kuwaambia): “Hili (jua) ndilo Mola wangu. Huyu Mola mkubwa kabisa.” Lilipotua alisema “Enyi watu wangu! Mimi simo katika hayo mnayoyashirikisha (na Mungu).(6:78)



(Mimi) nimeuelekeza uso wangu kwa yule aliyeziumba mbingu na ardhi. Hali ya kuwa nimewacha dini za upotevu. Mimi (ni Mwislamu) si miongoni mwa washirikina.” (6:79)

Watu wa jamii yake walimshangaa kwa msimamo wake wa kumpwekesha Allah(s.w) na kujadiliana naye kama ifuatavyo:




Na watu wake wakajadiliana naye (kwa kumwambia Unaacha Ibada ya wazee! Utadhurika)! Akasema: “Je, Mnanihoji juu ya Mwenyezi Mungu, mnaowashirikisha naye. Isipokuwa Mola wangu akipenda jambo (kuwa, basi litakuwa). Mola wangu anakijua vyema kila kitu. Basi je, hamshiki mauidha (6:80)



“Na nitawaogopaje hao mnaowashirikisha, hali nyinyi hamwogopi kumshirikisha Mwenyezi Mungu na kile ambacho

hakukiteremshia dalili kwenu (yoyote ya kuonyesha kuwa ni mungu)? Basi kundi gani katika mawili haya (langu au lenu) linastahiki zaidi kupata amani? Kama nyinyi mnajua jambo (lijibuni hili).(6:81)



“(Hapana shaka kuwa) wale walioamini na hawakuchanganya imani yao na ushirikina kuwa hao ndio watakaopata amani, nao ndio walioongoka.(6:82)



Na hizi ndizo (baadhi ya) hoja zetu tulizompa Ibrahimu juu ya watu wake. Tunamyanyua katika vyeo yule tumtakaye (kwa kuwa anakwenda mwendo tunaoutaka). Hakika Mola wako ndiye Mwenye hikima (na) ndiye ajuaye. (6:83)



                   

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1275

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

NI UPI MKATABA WA AL-FUDHUL NA ASILI YAKE, ATHARI ZAKE NA WALOHUSIKA
NI UPI MKATABA WA AL-FUDHUL NA ASILI YAKE, ATHARI ZAKE NA WALOHUSIKA

MKATABA WA AL-FUDHULBaada ya vita hivi viongozi wa pande mbili hizi waliamuwa wakae chini na wakubaliane kuweka kanun i na utaratibu utakaozuia kutotokea uonevu kama huuu tena.

Soma Zaidi...
Historia ya Luqman mtu aliyesifika kuwa na Hikma
Historia ya Luqman mtu aliyesifika kuwa na Hikma

Luqman ni katika watu wema kabisa waliopita zama za nyuma.

Soma Zaidi...
Madhumuni ya dola ya uislamu
Madhumuni ya dola ya uislamu

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mafunzo yatokanayo na mkataba wa aqabah katika kuandaa ummah
Mafunzo yatokanayo na mkataba wa aqabah katika kuandaa ummah

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...