Kutowatii Wazazi katika kumuasi Allah (s.w)

Kutowatii Wazazi katika kumuasi Allah (s.w)

"Na (wazazi wako) wakikushurutisha kunishirikisha na (yale) ambayo huna ilimu nayo, usiwatii; lakini kaa nao kwa wema hapa duniani (Maadamu ni wazee wako, ila usiwafuate tu mwenendo wao mbaya); Shika mwenendo wa wale wanaoelekea kwangu, kisha marejeo yenu

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Kutowatii Wazazi katika kumuasi Allah (s.w)

(d)Kutowatii Wazazi katika kumuasi Allah (s.w)


"Na (wazazi wako) wakikushurutisha kunishirikisha na (yale) ambayo huna ilimu nayo, usiwatii; lakini kaa nao kwa wema hapa duniani (Maadamu ni wazee wako, ila usiwafuate tu mwenendo wao mbaya); Shika mwenendo wa wale wanaoelekea kwangu, kisha marejeo yenu ni kwangu, hapo nitakuambieni mliyokuwa mkiyatenda." (31:15).



Aya inabainisha wazi kuwa hatupaswi kuwatii wazazi wetu pale watakapotuamrisha kumuasi Allah (s.w). Tukiwatii tutakuwa tumemshirikisha Allah (s.w) kwa kuwafanya wazazi wetu miungu badala yake kama inavyo bainika katika Qur'an.



โ€œMayahudi na Wakristo) wamewafanya wanavyuoni wao na watawa wao kuwa ni miungu badala ya Allah (s.w) โ€ฆ." (9:31)



Iliposhushwa aya hii Adi bin Hatimu (r.a) ambaye alisilimu kutoka kwenye Ukristo, alimtaka Mtume (s.a.w) atoe ufafanuzi kwa sababu alidai kuwa kinadharia hawakuwa wanawafanya watawa wao miungu. Katika kufafanua, Mtume (s.a.w) alimuuliza Adi, "Je hawakuwa watawa wenu wanawahalalishia alivyo viharamisha Allah (s.w) na nyinyi mkawatii?" Alijibu Adi, "Ndiyo" Mtume (s.a.w) akamuuliza tena, "Je watawa wenu hawakuwa wanakuharamishieni alivyo halalisha Allah (s.w) na nyinyi mkawatii? Adi akajibu tena "Ndiyo." Basi Mtume (s.a.w) akasema, "Huko ndio kuwafanya miungu".



Hivyo, kumtii mzazi au kiongozi au yeyote yule katika kumuasi Allah (s.w) ni kumfanya mungu badala ya Allah (s.w). Pia ukitii matashi ya nafsi yako kinyume na amri au makatazo ya Allah (s.w) utakuwa umeifanya nafsi yako mungu badala ya Allah (s.w).


"Je, umemuona yule aliyefanya matamanio yake, (kile anachikipenda), kuwa Mungu wake? Basi je, utaweza kuwa mlinzi wake (ukamhifadhi na hayo, na hali ya kuwa hataki?). "(25:43).



Lakini, tunaamrishwa katika aya hii (31:15) kuwa pamoja na kutowatii wazazi wetu katika kumshirikisha Allah (s.w), tusiwe jeuri na fedhuli kwao, bali tuzungumze nao kwa upole kwa kauli njema na tuendelee kuwatii na kuwafanyia wema katika mambo yote ya halali.


Wakati mwingine wazazi wanaweza kutishia kuacha laana tutakapowakatalia kwa kauli nzuri kutowatii katika yale yatakayotupelekea kumuasi na kumshirikisha Allah (s.w). Tusiyumbishwe na tishio hili kwa sababu marejeo yetu sote ni kwa Allah (s.w) na ni mjuzi kamili juu ya dhamira (nia) zetu na vitendo vyetu - "โ€ฆkisha marejeo yenu ni kwangu, Hapo nitakuambieni mliyokuwa mkiyatenda" (31:15).




                   


Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 1047

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰3 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰5 Madrasa kiganjani    ๐Ÿ‘‰6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu

Faradhi kwa maiti ya muislamu (edk form 2:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kuamini mitume wa mwenyezi Mungu
Kuamini mitume wa mwenyezi Mungu

Nguzo za Imani (EDK form 2:. Dhana ya elimu ya uislamu

Soma Zaidi...
Kwa nini Uislamu ndio dini pekee inayostahiki kufuatwa
Kwa nini Uislamu ndio dini pekee inayostahiki kufuatwa

Kwa nini uislamu ndio dini pekee ya haki ambayo watu wanatakiwa waifuate.

Soma Zaidi...
Kumuamini mwenyezi Mungu (S.W)
Kumuamini mwenyezi Mungu (S.W)

Nguzo za imani (EDK form 2: elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Taathira ya Imani ya Malaika katika maisha ya kila siku
Taathira ya Imani ya Malaika katika maisha ya kila siku

Kuamini Malaika ni imani ambayo pindi ikithibiti vema moyoni, huleta taathira kubwa sana katika maisha ya kila siku na hivyo kubadili kabisa tabia na mwenendo wa Muumini.

Soma Zaidi...
 zijue Nguzo za uislamu, imani, ihsani pamoja na dalili za qiyama
zijue Nguzo za uislamu, imani, ihsani pamoja na dalili za qiyama

ุนูŽู†ู’ ุนูู…ูŽุฑูŽ ุฑูŽุถููŠูŽ ุงู„ู„ู‡ู ุนูŽู†ู’ู‡ู ุฃูŽูŠู’ุถู‹ุง ู‚ูŽุงู„ูŽ: " ุจูŽูŠู’ู†ูŽู…ูŽุง ู†ูŽุญู’ู†ู ุฌูู„ููˆุณูŒ ุนูู†ู’ุฏูŽ ุฑูŽุณููˆู„ู ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุตู„ู‰ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆ ุณู„ู… ุฐูŽุงุชูŽ ูŠูŽูˆู’ู…ูุŒ ุฅุฐู’ ?...

Soma Zaidi...
Sifa za waumini zilizotajwa katika surat Al-Anfal (8:2-4) na Al-Hujurat
Sifa za waumini zilizotajwa katika surat Al-Anfal (8:2-4) na Al-Hujurat

"Hakika wanaoamini kweli ni wale ambao anapotajwa Allah nyoyo zao hujaa khofu; na wanaposomewa aya zake huwazidishia imani na wanamtegemea Mola wao tu basi.

Soma Zaidi...