“Na wasiape wale wakarimu na wenye wasaa miongoni mwenu, kujizuia kuwasaidia jamaa zao, maskini na wale waliohama kwa ajili ya Dini ya Allah; na wasamehe na waachilie mbali (wapuuze yaliyopita).
“Na wasiape wale wakarimu na wenye wasaa miongoni mwenu, kujizuia kuwasaidia jamaa zao, maskini na wale waliohama kwa ajili ya Dini ya Allah; na wasamehe na waachilie mbali (wapuuze yaliyopita). Je, nyinyi hampendi Allah akusameheni? Na Allah ni msamehevu, mrehemevu. ”(24:22)
Tukirejea historia, Bi 'Aisha (r.a) amesema kuwa baada ya kuteremshwa aya za (24:11-21) zilizomtakasa na uzushi wa wanafiki, baba yake, Abu Bakr (r.a) aliapa kuwa hatamsaidia tena kwa mali Mistah bin Uthatha, miongoni mwa watu waliokuwa mstari wa mbele katika kueneza uzushi dhidi ya Bi 'Aisha (r.a).
Katika kufanya kitendo cha kueneza uzushi, Mistah hakuonyesha kabisa kujali mahusiano wala ihsani ambazo Abu Bakar (r.a) daima alikuwa anamfanyia yeye na familia yake. Hili lilimkasirisha sana Abu Bakar mpaka kumfikisha kwenye kuchukua kiapo cha kusitisha msaada wake kwa Mistah. Baada ya kushushwa aya hii, Abu Bakar aliomba msamaha kwa Allah (s.w) na akaanza tena kumsaidia Mistah kwa moyo mkunjufu zaidi kuliko hata hapo awali.
Kwa mujibu wa 'Abdullah bin 'Abbas (r.a), waumini wengine miongoni mwa maswahaba pia waliapa kuwa hawatawasaidia tena wale wote walioshiriki katika kusambaza masingizio dhidi ya Bi 'Aisha (r.a). Lakini baada ya kuteremshwa aya hii, wote walivibatilisha viapo vyao, na uhasama wote uliosababishwa na hayo 'masingizio' ukaisha.
Kwa mujibu wa aya hii na maelezo haya ya kihistoria tunajifunza kuwa:
(i) Katika maadili mema, hatuna budi kuendelea kuwafanyia wema wale waliotukosea, maadamu hatudhuriki tukiendelea kuwafanyia hivyo. Hekima ya kufanya hivyo Allah (s.w) anaibainisha katika aya zifuatazo:
"Mambo mazuri na mabaya hayawi sawa. Ondosha ubaya (unaofanyiwa) kwa wema, tahamaki yule ambaye baina yako na baina yake kuna uadui, anakuwa kama jamaa (yako) mwenye kukufia uchungu" Lakini jambo hili hawatapewa ila wale wanaosubiri, wala hawatapewa ila wenye hadhi kubwa (Mbele ya Allah (s.w))." (41:34-35)
(ii) Hatuna budi kuwa wepesi kuwasamehe wale walio tukosea ili iwe sababu na sisi kusamehewa makosa yetu na Allah (s.w)"
Je, nyinyi hampendi Allah akusameheni?……" (24:22)
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Kumzulia mtu mtwahirifu kuwa amefanya tendo la zinaa pasina kuleta ushahidi stahiki ni tendo ovu mno mbele ya Allah (s.
Soma Zaidi...Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Ushahidi wa kuthibitisha kutendeka kwa kosa la uzinifu unapatikana kwa namna tatu zifuatzo: (i)Kushuhudia tendo hilo likifanyika kwa wakati mmoja watu wanne Mukalafu (Walio baleghe na wenye akili timamu), wakiwa ni Waislamu waadilifu.
Soma Zaidi...Allah hutumia maandishi kuwafundisha wanadamu. Mfano mzuri ni nabii Musa ambaye alipewa vibao vya maandishi.
Soma Zaidi...Ni upi mgawanyo sahihi wa elimu kwa mtazamo wa uislamu (EDK form 1: mgawanyo sahihi wa elimu kwa mtazamo wa uislamu
Soma Zaidi..."Hakika wanaoamini kweli ni wale ambao anapotajwa Allah nyoyo zao hujaa khofu; na wanaposomewa aya zake huwazidishia imani na wanamtegemea Mola wao tu basi.
Soma Zaidi...Katika Uislamu elimu imegawanyika katika Elimu ya muongozo na elimu ya mazingira.
Soma Zaidi...