Haki na wajibu wa mtoto kwa wazazi na katika jamii

Haki na wajibu wa mtoto kwa wazazi na katika jamii

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Haki na wajibu wa mtoto kwa wazazi na katika jamii

Wajibu wa Watoto kwa Wazazi



Wajibu wa watoto kwa wazazi wao ni kuwatii katika kiwango cha hali ya juu, kuwaheshimu na kuwahurumia hasa wanapokuwa wazee. Kuwatii wazazi ni kitendo kinachochukua nafasi ya juu sana katika Uislamu. Utii kwa wazazi huchukuwa nafasi baada tu ya Kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Msisitizo wa kuwatii wazazi, kuwaonea huruma na kuwafanyia ihsani uko wazi katika Qur-an:


Na Mola wako amehukumu kuwa msimuabudu yeyote ila Yeye tu. Na (ameagiza) kuwafanyia wema (mkubwa) wazazi. Kama mmoja wao akifikia uzee pamoja nawe, au wote wawili, usiwaambie hata A/i! Wala usiwakemee. Na useme nao kwa msemo wa heshima kabisa. Na uwainamishie bawa ?a unyenyekevu kwa (kuwaonea) huruma na useme: 'Mola wangu! Warehemu (wazee wangu) kama walivyonilea katika utoto ". (17:23-24).



Wazazi, hasa mama, wamestahiki kutiiwa kwa kiwango cha hali ya juu, kuwafanyia ihsani na kuhurumiwa na watoto wao hasa wanapokuwa wazee, iii iwe kama malipo ya kazi ngumu ya kuwalea watoto wao. Mtoto hana malipo ya kumlipa mzazi wake kwa kumzaa na kumlea mpaka kufikia utu uzima wake. Malipo anayotakiwa na Mwenyezi Mungu (s.w)


awalipe wazazi wake kwa taabu zote walizochukua katika kumlea ni kumshukuru Mwenyezi Mungu (s.w) na wazazi wake kwa kumtii Mwenyezi Mungu (s.w) na Mtume na kisha kuwatii wazazi wake, kuwafanyia ihsani na kuwahurumia kama tunavyojifunza katika Qur-an:


Na tumemuusia mwanaadamu (kuwafanyia ihsani) wazazi wake - mama yake amechukua mimba yake kwa udhafujuu ya udhafu na kumnyonyesha katika kipindi cha miaka miwili - (tumemuusia) ya kwamba unishukuru Mimi na wazazi wako, marejeo yenu ni kwangu. (31:14)


Na tumemuusia mwanaadamu afanye wema kwa wazazi wake,.Mama yake amechukua mimba yake kwa taabu. Na ku be ha mimba yake hata kumwachisha ziwa, (uchache wake) ni miezi thelathini (46:15). Pia mtoto mwema, pamoja na kuwatii na kuwahurumia wazazi wake kwa kuwapa kila msaada wanaohitajia, huwaombea dua wakiwa hai au wakiwa wametangulia kufa kwa kusema:


Mola wetu! Unighufirie mimi na wazazi wangu wote wawili na wanaoamini Siku ya Hisabu. (14:41). Utii kwa wazazi unatakiwa uendelezwe hata baada ya kufa kwao kama tunavyojifunza katika hadithi: Abu Usaydi as-Said (r.a) amesimulia: Tulikuwa karibu na Mtume (s.a.w) wakati alpomjia mtu wa ukoo wa Salimah na kumuuliza: Ee Mtume wa mwenyezi Mungu! Kuna utii


mwingine uliobakia kwa wazazi baada ya kutawafu kwao? "Ndio" alUibu Mtume. "Kuwaombea dua, kuwaombea msamaha na maghfira kwa Mwenyezi Mungu (s.w), kutekeleza wasia wao, kuwa na uhusiano mwema na wale mliofahamiana kutokana na wao na kuwaheshimu rafiki zao ". (Abu Daud, Ibn Majah)



Pia katika hadithi iliyosimuliwa na Ibn Umar mtume (s.a.w) amesema:
Utii wa hali ya juu kwa wazazi ni mtu kufanya urafiki na marafiki wa baba yake baada ya kufa kwake. (Muslim).
Hata hivyo, kiwango cha utii na huruma ya mtoto kwa wazazi wawili kinatofautiana. Mama anastahiki kupata nafasi ya kwanza ndio baba afuatie kama tunavyojifunza katika hadithi:



Abu Hurairah amesimulia kuwa mtu mmoja aliuliza: Ee Mtume wa Mwenyezi Mungu! Ni nani hasa anayestahiki upendo wangu wa hali ya juu? 'Mama yako ", alijibu Mtume. Kisha akauliza tena: Nani anayefuatia? "Mama yako ", alijibu Mtume. Akauliza tena: Nani anayefuatia? 'Mama yako ' alj/ibu Mtume. Katika maelezo mengine al/ibu Mtume: Mama yako, kisha mama yako, kisha mama yako, kisha baba yako, kisha jamaa zako wa karibu, (Bukhari na Muslim).




                   


Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2491

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Jukumu la serikali katika kuzuia dhuluma
Jukumu la serikali katika kuzuia dhuluma

Serikali ina nafasi kubwa katika kuzuia dhulma na kufanya uchumibuwe huru kuyokana na dhulma.

Soma Zaidi...
Taratibu za mirathi katika zama za ujahilia
Taratibu za mirathi katika zama za ujahilia

Kabla ya kuhubiriwa uislamu watu wa Maka walikuwa na tarayibu zenye dhuluma ndani yake katika ugawaji wa mirathi.

Soma Zaidi...
 Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga
Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga

Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga.

Soma Zaidi...
Zijuwe nguzo 17 za swala.
Zijuwe nguzo 17 za swala.

Ili swala itimie utahitajika kutimiza nguzo zake na masharti yake. Hapa utajifunza nguzo 17 za swala.

Soma Zaidi...
Maana ya hadathi na aina zake
Maana ya hadathi na aina zake

Post hii inakwenda kukugundisha maana ya hadathi pamoja na kutaja aina za hadathi

Soma Zaidi...
Mambo yaliyo haramu kwa mwenye hedhi na nifasi
Mambo yaliyo haramu kwa mwenye hedhi na nifasi

Katika post hii utakwenda kujifunza mambo ambayo ni haramu kwa mwanamke aliye na hedhi na nifasi

Soma Zaidi...
Nguzo za kufunga ramadhani
Nguzo za kufunga ramadhani

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Taratibu za kumiliki hisa na mali ya shirika
Taratibu za kumiliki hisa na mali ya shirika

Katika Uislamu kuwa na hisa kwenye mali inaruhusiwa. Hapa utajifunza taratibu za kumiliki hisa.

Soma Zaidi...