Historia na asili ya kuzibiti uzazi na uzazi wa mpango

Historia na asili ya kuzibiti uzazi na uzazi wa mpango

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Historia na asili ya kuzibiti uzazi na uzazi wa mpango

Historia ya Kampeni ya Kudhibiti Uzazi



Upo ushahidi wa kutosha kuwa watu binafsi katika zama zote wamekuwa wakijitahidi kuzaa watoto wanaopishana miaka iii kuhifadhi afya ya mama na mtoto. Juhudi za serikali huko nyuma (yaani kabla ya kame ya 20) zilikuwa ni kuwashawishi raia kuoana na kuzaana. Lakini kuanzia karne ya 20 serikali zimejiingiza katika kampeni za kuwataka raia wadhibiti kizazi.



Neno kudhibiti uzazi (birth control) ambalo lilibuniwa na Margaret Sanger, mpiganiaji haki za wanawake wa huko Marekani, mwaka 1913 - 1915 lina maana ya njia za kuzuia mimba kwa kumtumia mwanamume au mwanamke, na hivi sasa zinajumuisha njia zote za kuzuia kizazi, ikiwa ni pamoja na kutoa mimba (abortion) au kuviza kizazi (sterilization). Hata hivyo jina Ia kampeni hii limekuwa likibadilika badilika. Katika miaka ya 1930 jina lilikuwa mpango wa familia (family planning) na katika miaka ya 1940 jina likawa mpango wa uzazi (planned parenthood). Baadaye yakazuka majina mengine mengi kama vile kuzuia mimba (controceptive), uzazi wa hiari (voluntary parenthood), kupunguza familia (family limitation), vita dhidi ya mimba (anti conception) na kadhalika.



Kampeni hizo zilipokuja Afrika Mashariki zilipewa majina mbali mbali kama vile uzazi wa majira, mpango wa familia, uzazi na malezi bora, na sasa kampeni hii imepewa jina Ia Elimu ya ngono (sex education) na Tanzania Elimu ya ngono hufundishwa mashuleni kwa jina Ia Elimu ya Afya na Uzazi.



Kwa vile tumemtaja Margaret Sanger kama mwanzilishi wa harakati za "bith control", ni vyema tumzungumzie kwa ufupi ili tupate kuelewa vyema uzito wa neno alilolizua.
Margret Sanger alizaliwa 1879 na kuolewa na William Sanger akiwa na umri kati ya miaka 20 na 25. Alijenga na kuitekeleza kwa vitendo dhana ya "mtu kuwa huru" kutembea na mwanamume yeyote anayemtaka. Alizikuza tamaa zake juu ya ngono na hivyo akawa kahaba mkubwa wa zama zake japo alikuwa kaolewa.



Yaonesha kuwa bwana William, kinyume na tabia ya mkewe, alikuwa ni mtu na heshima zake. Katika hatma ya mambo hakuwa na Ia kufanya ila kumwacha Margaret. Kwani kila alipojaribu kumsema juu ya uzinifu wake, Margret alimshauri mumewe naye azini.



Ndoa yake ya pili iliangukia kwa mume ambaye naye aliikubali dhana angamizi ya mtu kufanya zinaa apendavyo hata akiwa ndani ya ndoa. Na bwana huyu ndiye aliyezipa nguvu harakati za Margret za kampeni za kudhibiti uzazi.



Kiu ya Margret isiyokatika, na ulafi uliopindukia wa ngono, ulimfanya azini na wanaume wanne tofauti wakati yupo katika fungate ya ndoa yake ya pili. Huyo ndiye mwanzilishi wa sera ya kudhibiti uzazi:



Kwa mujibu wa Encyclopedia Britannica (1985) mojawapo ya sababu zilizopelekea kuenea kwa kampeni hii ni manufaa ya faida ya kibiashara iliyotokana na kuuza madawa au vifaa vya kuzuia mimba. Makampuni yanayotengeneza madawa hayo yalijikuta yanaingiza mamilioni ya dola. Hivyo, yakazidi kuitangaza biashara yao. Katika kuzivutia nchi changa, madawa hayo yamekuwa yakitolewa bure. Lakini sasa, baada ya kunogewa na sera hii, inabidi wasake madawa ya kuzuia mimba na magonjwa ya zinaa kwa bei mbaya.




                   


Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1072

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Ni ipi hukumu ya kutoa talaka hali ya kuwa umelazimishwa au ukiwa umerukwa na akili
Ni ipi hukumu ya kutoa talaka hali ya kuwa umelazimishwa au ukiwa umerukwa na akili

Endapo mtu atamuacha mke pasi na ridhaa yake yaani amelazimishwa ama amemuwacha wakati amerukwa na akili. Je ni ipo hukumu yake.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kiswali swala ya tahajud na swala za usiku yaani qiyamu layl
Jinsi ya kiswali swala ya tahajud na swala za usiku yaani qiyamu layl

Post hii itakujuza jinsi ya kiswali swala ya tahajudi. Pia utajifunza jinsi ya kuswali swala za usikubyaanibqiyamublayl

Soma Zaidi...
Ni ipi hukumu ya muislamu anayekula mwezi wa Ramadhani bila ya sababu ya kisheria
Ni ipi hukumu ya muislamu anayekula mwezi wa Ramadhani bila ya sababu ya kisheria

Endapo muislamu hatafunga mwezi wa Ramadhani bila ya ruhusa je atatakiwa afanye nini. Je ataweza kuilipa funga hiyo?

Soma Zaidi...
Watu hawa huruhusiwi kuwaoa katika uislamu
Watu hawa huruhusiwi kuwaoa katika uislamu

Hapa utajifunza watu ambao ni halali kuwaoa na wale ambao ni haramu kuwaoa.

Soma Zaidi...
Jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali
Jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali

Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali kulingana na ugonjwa wake.

Soma Zaidi...
Kusimamisha Swala na kuamrisha mema
Kusimamisha Swala na kuamrisha mema

Swala iliyosimamishwa vilivyo ndiyo nyenzo kuu ya kumtakasa Muislamu na kumpa sifa zinazomuwezesha kustahiki kufanya kazi takatifu ya kusimamisha Uislamu katika jamii.

Soma Zaidi...
Sharti za kutoa zaka
Sharti za kutoa zaka

Masharti ya Utoaji wa Zakat na Swadaqat Utoaji katika njia ya Allah (s.

Soma Zaidi...
Ni upibutaratibu wa kuingia eda na kutoka eda
Ni upibutaratibu wa kuingia eda na kutoka eda

Katika uislamu hakuna sheria ya mwanamke kuingizwa eda na kutolewa eda kama ilivyozoeleka. Endelea na post hii ujifunze zaidi

Soma Zaidi...