Menu



Jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali

Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali kulingana na ugonjwa wake.

Swala tano za Faradh katika Nyakati za Dharura

Amri ya kusimamisha swala tano imeambatana na nyakati makhususi kama tunavyojifunza katika aya ifuatayo:

 

“Basi simamisheni swala Kwa hakika swala kwa waislamu ni faradhi iliyowekewa nyakati makhsusi” (4:103)
Hivyo swala ya mja haitakubaliwa iwapo ataiswali nje ya wakati wake makhsusi. Hapana “kadha” katika swala.

 


Pamoja na amri ya kuiswali kila swala ya faradhi katika wakati wake makhsusi, Allah (s.w) aliye Mwingi wa Rehma haikalifishi nafsi yoyote katika kuipa amri zake ila huitaraji kila nafsi itekeleze amri hizo kwa kadiri ya uwezo aliyoijaalia kuwa nao. Mara kwa mara katika kutufahamisha huruma zake juu yetu, Allah(s.w.) anakariri:

 


“Mwenyezi Mungu haikalifishi nafsi yoyote ila yaliyosawa na uwezo wake...” (2:286)
Baada ya kutoa ruhusa ya kutofunga wagonjwa na wasafiri, wakati wa mwezi wa Ramadhani na badala yake walipe “kadha” siku walizokula anatudhihirishia Rehma zake kwa kutufahamisha:

 

“... Mw enyezi Mungu anakutakieni yaliyo m epesi, w ala hakutakieni yaliyo mazito...” (2:185)
Pia baada ya kutoa ruhusa ya kutayammam, baada ya kukosa maji, au kwa ajili ya maradhi au mtu anapokuwa safarini, katika Sura ya 5 aya ya 6, Allah (s.w) anamalizia kwa kusema:-

 

“... Hapendi Mwenyezi Mungu kukutieni katika taabu, bali anataka kukutakaseni na kutimiza neema yake juu yenu ili mpate kushukuru”. (5:6)

 

 

 

“.. .Na ka m a m kiw a w agonjw a (mm eka tazw a ku tumia m aji) a u mm o safarini au mmoja wenu ametoka msalani (chooni) au mmewagusa(mmewajamii), wanawake - na msip ate maji basi ukusudieni (tayamamuni) udongo safi, mpake nyuso zenu na mikono yenu. Hakika Mw enyezi Mungu ni Mwenye kusamehe (na) Mw enye kughufiria ”. (4:43)

 


“... Na mkiwa wagonjwa au mmo safarini, au mmoja wenu ametoka chooni au mmeingiliana na wanawake, na hamkupata maji, basi kusudieni (tayammamuni) udongo ulio safi na kuupaka nyuso zenu na mikono yenu. Hapendi Mwenyezi Mungu kukutieni katika taabu, bali anataka kukutakaseni na kutimiza neema Yake juu yenu ili mpate kushukuru”. (5:6)

 


(2) Iwapo mgonjwa hajimudu na hana wa kumtwaharisha kwa maji au kwa udongo itabidi atayammamu kifikra na kuswali hivyo hivyo. Hili ni sahali kwa kauli ya Allah (s.w):

 

“Hapendi Allah kukutieni katika taabu, bali anataka kukutakaseni na kutimiza neema Yake juu yenu”. (5:6)

 


(3)Mgonjwa anaruhusiwa kuswali akiwa amekaa na kuelekea Qibla iwapo ana uwezo huo, vinginevyo ataelekea popote pale kwa kadiri ya uwezo wake. Atarukuu na kusujudu katika hali hiyo ya kukaa iwapo anaweza, vinginevyo atarukuu na kusujudu kwa ishara tu.
(4)Iwapo mgonjwa hawezi hata kukaa ataswali akiwa amelala kwa ubavu huku akiwa ameelekea Qibla kama ana uwezo wa kufanya hivyo, vinginevyo ataelekea popote pale. Pia kama hawezi kulala kwa ubavu atalala chali. Kama hawezi kulala chali ataswali kwa ishara akiwa amelala vyovyote vile awezavyo.

 

(5) Pia mgonjwa anaruhusiwa kuchanganya swala kama msafiri (rejea swala ya msafiri) kama hivyo ndivyo hali ya mazingira ya ugonjwa inavyotaka.
Kutokana na tahfifu hizi, ugonjwa si udhuru wa kumruhusu mtu asiswali swala ya faradh kwa wakati wake hata kama mgonjwa huyo atakuwa mahututi kitandani akiwa nyumbani au hospitalini maadamu bado ana akili timamu.

 

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 946


Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Eda ya kufiwa na hukumu zake
Soma Zaidi...

Mambo yenye kufunguza swaumu (funga)
Soma Zaidi...

darsa nzuri zenye kuelimisha hasa katika ndoa ya kiislam.
Assalaam alykum warahmatullah wabarakatuh. Soma Zaidi...

TAKBIRA YA KWANZA, DUA BAADA YA TAKBIRA YA KUHIRIMIA SWALA NA KUSOMA ALHAMDU (SURAT AL-FATIHA KWENYE SWALA
2. Soma Zaidi...

Tofauti ya uchumi wa kiislamu na uchumi wa kikafiri
Uchumi wa kiislamu unatofautiana sana na uchumi wa kikafiri. Hapa utajifunza tofauti hizo. Soma Zaidi...

Nini maana ya Kushahadia nguzo ya kwanza ya uislamu
Soma Zaidi...

Miiko au Mambo yanayoharibu/kubatilisha funga
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Misingi na Maadili Katika Uislamu
5. Soma Zaidi...

Kwanini lengo la zakat na sadaqat halifikiwi katika jamii yetu
Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kumuandaa maiti kabla ya kufa na baada ya kufa, mambo muhimu anayopasa kufanyiwa maiti wa kiislamu
3. Soma Zaidi...