Post hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia mtoto akiwa na ugonjwa wa UTI.
1. Mpatie mtoto dawa zilizoagizwa na daktari
Baada ya kugundua kuwa mtoto ana UTI dawa zilizoagizwa zinapaswa kutumika na kuendelea kuangalia maendeleo ya mtoto, dawa hizo zitumike kwa uhakika na kwa mda wake mtoto anapopaswa kupewa dawa hizo, kwa hiyo ni lazima kuangalia na matokea hasi ya dawa na mtoto anaweza kubadikishiwa dawa ambayo inapatana na mwili wake na kuendelea na matibabu yake ya kawaida.
2.Elimu inabidi utolewa kwa mama na walezi wa mtoto namna ya kuepukana na Maambukizi ya UTI kwa kufanya yafuatayo, kutawadha kutoka mbele kwenda nyuma, kumsafisha mtoto vizuri baada ya kujisaidia, kumtahiri mtoto kaama ni wa kiume, kumbadilisha mtoto nepi pindi tu anapijisaidia na anapokojoa ,kwa hiyo mtoto hasikae na nepi kwa mda mrefu maana bakteria kutoka kwenye mkojo urudi kwenye kibofu Cha mkojo na kukua na kuongezeka hatimaye usababisha maambukizi mapya.
3.Mtoto akiwa na UTI na Yuko kwenye matibabu hakikisha anapewa chakula Cha kutosha chenye mlo kamili na pia kama anatapika hakikisha unatibu kutapika Ili mtoto aweze kula chakula na chakula niendelee kukaa mwilini na kufanya kazi pamoja na dawa na hakikisha mtoto ananyonya vizuri Ili kuhakikisha kuwa dawa zinafanya kazi vizuri, na maendeleo ya mtoto yanakuwa Kawaida.
4. Hakikisha joto la mwili, msukumo wa damu, mapigo ya moyo na upumuaji wa mtoto vinakuwa sawia kwa kupima mara kwa mara kwa sababu maambukizi yoyote kwenye mwili usababisha hali y mwili kubadilika na kuleta kitu kingine ambacho ni matokeo ya maambukizi. Mfano joto la mwili likipanda kwa sababu ya ya UTI mtoto anaweza kuwa na degedege kwa hiyo tunapaswa kuhakikisha kuwa kila hali kwenye mwili Iko sawa kama haiko sawa tujitahidi kuiweka sawa Ili kuepusha madhara mbalimbali yanayoweza kutokea kwa sababu ya maambukizi.
5. Kama mtoto amepata changamoto ya UTI anapaswa kuwa na maji ya kutosha mwilini maana maambukizi kwa mtoto upunguza kiwango Cha maji mwilini na mtoto anaweza kuelekea pabaya, kwa hiyo kwanza mama na waangalizi wa mtoto wanapaswa kuangalia kiasi Cha maji mwilini kwa kuangalia kiasi Cha maji kinachoingia na kinachotoka kwa kufanya yafuatayo.
_ kuangalia kiasi kinachoingia kwa kuangalia anakunywa maji kiasi gani, uji , maziwa,juice na vitu vyote vinavyopungia mwilini kwa mfumo wa maji.
- kuangalia kiasi Cha maji yaliyotoka kwa kuangalia jinsi alivyokojoa yaani amekojoa kiasi gani,au kama anatoa jasho ,au labda anaharisha au kutapika.
Kama kiasi kinachoingia ni kikubwa zaidi ya kinachotoka mtoto anaweza kuendelea na dawa na uangalizi Ila kama kinachotoka ni kikubwa ya kinachoingia mtoto aongezwmewe maji.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Post hii inahusu zaidi Sababu za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, hali hii uwatokea sana wanawake zaidi ya wanaume, kwa kitaalamu hali hii ya kuwa na uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo huitwa cystitis.
Soma Zaidi...Hivi umeshawahi kuwazakuwa jekipimo cha HIV ni sahihi kwa kiasi gani. Unadhani huwa kinakoseaga kutoa majibu?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia kuaribika kwa figo, hizi ni njia zinazotumika ili kuweza kupunguza tatizo la kuaribika kwa figo na hasa wale ambao hawajapata tatizo hili wazitumie ili tuone kama tutaweza kupunguza tatizo hili.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa wa vipele kwenye midomo na sehemu za siri ambao kwa kitaalamu huitwa herpes zoster. Kwa hiyo ili kugundua kubwa mtu ana Ugonjwa huu Dalili kama hizi zifuatazo zinaweza kutokea kwa mgonjwa.
Soma Zaidi...Je unapata dalili zisizoeleweka ni ni za mimba ama laa. Hapa nitakujuza hali baadhi ya wanawake zinazowatokea.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi hatua mbalimbali za Ugonjwa wa Ukimwi, kawaida Ugonjwa huu huwa na hatua kuu nne ila kila hatua huwa na sifa zake kwa hiyo tunapaswa kujua hatua za Ugonjwa huu na kujaribu kuzuia maambukizi yasisambae kabisa.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia Ugonjwa wa kaswende, tunajua wazi kuwa Ugonjwa huu unasambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kufanya ngono zembe na njia nyingine kwa hiyo tunaweza kuzuia kusambaa na kuenea kwa ugonjwa huu kwa n
Soma Zaidi...Malaria ni moja ya magonjwa hatari yanayoongoza katika vifo vya watoto wengi duniani walio chni ya umri wa miaka 5. Katika post hii utakwend akujifunza kuhusuugonjwa huu jinsi unavyotokea, hatuwa zake na dalili zake.
Soma Zaidi...