picha

Namna ya kumsaidia mtoto mwenye UTI

Post hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia mtoto akiwa na ugonjwa wa UTI.

1. Mpatie mtoto dawa zilizoagizwa na daktari

Baada ya kugundua kuwa  mtoto ana UTI dawa zilizoagizwa zinapaswa kutumika na kuendelea kuangalia maendeleo ya mtoto, dawa hizo zitumike kwa uhakika na kwa mda wake mtoto anapopaswa kupewa dawa hizo, kwa hiyo ni lazima kuangalia na matokea hasi ya dawa na mtoto anaweza kubadikishiwa dawa ambayo inapatana na mwili wake na kuendelea na matibabu yake ya kawaida.

 

2.Elimu inabidi utolewa kwa mama na walezi wa mtoto namna ya kuepukana na Maambukizi ya UTI kwa kufanya yafuatayo, kutawadha kutoka mbele kwenda nyuma, kumsafisha mtoto vizuri baada ya kujisaidia, kumtahiri mtoto kaama ni wa kiume, kumbadilisha mtoto nepi pindi tu anapijisaidia na anapokojoa ,kwa hiyo mtoto hasikae na nepi kwa mda mrefu maana bakteria kutoka kwenye mkojo urudi kwenye kibofu Cha mkojo na kukua na kuongezeka hatimaye usababisha maambukizi mapya.

 

3.Mtoto akiwa na UTI na Yuko kwenye matibabu hakikisha anapewa chakula Cha kutosha chenye mlo kamili na pia kama anatapika hakikisha unatibu kutapika Ili mtoto aweze kula chakula na chakula niendelee kukaa mwilini na kufanya kazi pamoja na dawa na hakikisha mtoto ananyonya vizuri Ili kuhakikisha kuwa dawa zinafanya kazi vizuri, na maendeleo ya mtoto yanakuwa Kawaida.

 

4. Hakikisha joto la mwili, msukumo wa damu, mapigo ya moyo na upumuaji wa mtoto vinakuwa sawia kwa kupima mara kwa mara kwa sababu maambukizi yoyote kwenye mwili usababisha hali y mwili kubadilika na kuleta kitu kingine ambacho ni matokeo ya maambukizi. Mfano joto la mwili likipanda kwa sababu ya ya UTI mtoto anaweza kuwa na degedege kwa hiyo tunapaswa kuhakikisha kuwa kila hali kwenye mwili Iko sawa kama haiko sawa tujitahidi kuiweka sawa Ili kuepusha madhara mbalimbali yanayoweza kutokea kwa sababu ya maambukizi.

 

5. Kama mtoto amepata changamoto ya UTI anapaswa kuwa na maji ya kutosha mwilini maana maambukizi kwa mtoto upunguza kiwango Cha maji mwilini na mtoto anaweza kuelekea pabaya, kwa hiyo kwanza mama na waangalizi wa mtoto wanapaswa kuangalia kiasi Cha maji mwilini kwa kuangalia kiasi Cha maji kinachoingia na kinachotoka kwa kufanya yafuatayo.

_ kuangalia kiasi kinachoingia kwa kuangalia anakunywa maji kiasi gani, uji , maziwa,juice na vitu vyote vinavyopungia mwilini kwa mfumo wa maji.

- kuangalia kiasi Cha maji yaliyotoka kwa kuangalia jinsi alivyokojoa yaani amekojoa kiasi gani,au kama anatoa jasho ,au labda anaharisha au kutapika.

Kama kiasi kinachoingia ni kikubwa zaidi ya kinachotoka mtoto anaweza kuendelea na dawa na uangalizi Ila kama kinachotoka ni kikubwa ya kinachoingia mtoto aongezwmewe maji.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 6493

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉2 web hosting     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Madrasa kiganjani    

Post zinazofanana:

Maumivu, kizunguzungu, kichefuchefu na kutoka na damu ni dalili zamimba?

Je unapata dalili zisizoeleweka ni ni za mimba ama laa. Hapa nitakujuza hali baadhi ya wanawake zinazowatokea.

Soma Zaidi...
Vidonda vya tumbo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu ugonjwa wa vidonda vya tumbo

Soma Zaidi...
Kazi ya figo: Dalili za awali za kushindwa kufanya kazi.

​Katika ulimwengu wa sasa wenye kasi kubwa, uchovu wa mwili umekuwa changamoto sugu kwa wengi. Makala hii inachunguza kwa kina vyanzo mbalimbali vya uchovu—kuanzia mambo ya mtindo wa maisha, matatizo ya kisaikolojia, hadi magonjwa ya msingi ya kiafya. Lengo ni kutoa ufahamu wa kina kuhusu jinsi ya kutambua dalili, sababu za kisayansi, na mikakati madhubuti ya kurejesha nishati yako ya mwili na akili.

Soma Zaidi...
Dalili na ishara za shambulio la moyo

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Dalili na ishara za shambulio la moyo. Shambulio la moyo huzuia damu yenye oksijeni kufika kwenye moyo hivyo hupelekea tishu kufa. Na Ugonjwa huu mtu akicheleweshewa matibabu huweza kupata mshtuko wa moyo mpaka kifo.

Soma Zaidi...
Dalili za UKIMWI

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za UKIMWI

Soma Zaidi...
Saratani ya tishu zinazounda Damu mwilini (leukemia)

Post hii inaelezea kuhusiana na Saratani ya tishu zinazounda damu mwilini, ikijumuisha uboho na mfumo wa limfu.ugonjwa huu kitaalamu huitwa leukemia.

Soma Zaidi...