Namna ya kumsaidia mtoto mwenye UTI
Post hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia mtoto akiwa na ugonjwa wa UTI.
1. Mpatie mtoto dawa zilizoagizwa na daktari
Baada ya kugundua kuwa mtoto ana UTI dawa zilizoagizwa zinapaswa kutumika na kuendelea kuangalia maendeleo ya mtoto, dawa hizo zitumike kwa uhakika na kwa mda wake mtoto anapopaswa kupewa dawa hizo, kwa hiyo ni lazima kuangalia na matokea hasi ya dawa na mtoto anaweza kubadikishiwa dawa ambayo inapatana na mwili wake na kuendelea na matibabu yake ya kawaida.
2.Elimu inabidi utolewa kwa mama na walezi wa mtoto namna ya kuepukana na Maambukizi ya UTI kwa kufanya yafuatayo, kutawadha kutoka mbele kwenda nyuma, kumsafisha mtoto vizuri baada ya kujisaidia, kumtahiri mtoto kaama ni wa kiume, kumbadilisha mtoto nepi pindi tu anapijisaidia na anapokojoa ,kwa hiyo mtoto hasikae na nepi kwa mda mrefu maana bakteria kutoka kwenye mkojo urudi kwenye kibofu Cha mkojo na kukua na kuongezeka hatimaye usababisha maambukizi mapya.
3.Mtoto akiwa na UTI na Yuko kwenye matibabu hakikisha anapewa chakula Cha kutosha chenye mlo kamili na pia kama anatapika hakikisha unatibu kutapika Ili mtoto aweze kula chakula na chakula niendelee kukaa mwilini na kufanya kazi pamoja na dawa na hakikisha mtoto ananyonya vizuri Ili kuhakikisha kuwa dawa zinafanya kazi vizuri, na maendeleo ya mtoto yanakuwa Kawaida.
4. Hakikisha joto la mwili, msukumo wa damu, mapigo ya moyo na upumuaji wa mtoto vinakuwa sawia kwa kupima mara kwa mara kwa sababu maambukizi yoyote kwenye mwili usababisha hali y mwili kubadilika na kuleta kitu kingine ambacho ni matokeo ya maambukizi. Mfano joto la mwili likipanda kwa sababu ya ya UTI mtoto anaweza kuwa na degedege kwa hiyo tunapaswa kuhakikisha kuwa kila hali kwenye mwili Iko sawa kama haiko sawa tujitahidi kuiweka sawa Ili kuepusha madhara mbalimbali yanayoweza kutokea kwa sababu ya maambukizi.
5. Kama mtoto amepata changamoto ya UTI anapaswa kuwa na maji ya kutosha mwilini maana maambukizi kwa mtoto upunguza kiwango Cha maji mwilini na mtoto anaweza kuelekea pabaya, kwa hiyo kwanza mama na waangalizi wa mtoto wanapaswa kuangalia kiasi Cha maji mwilini kwa kuangalia kiasi Cha maji kinachoingia na kinachotoka kwa kufanya yafuatayo.
_ kuangalia kiasi kinachoingia kwa kuangalia anakunywa maji kiasi gani, uji , maziwa,juice na vitu vyote vinavyopungia mwilini kwa mfumo wa maji.
- kuangalia kiasi Cha maji yaliyotoka kwa kuangalia jinsi alivyokojoa yaani amekojoa kiasi gani,au kama anatoa jasho ,au labda anaharisha au kutapika.
Kama kiasi kinachoingia ni kikubwa zaidi ya kinachotoka mtoto anaweza kuendelea na dawa na uangalizi Ila kama kinachotoka ni kikubwa ya kinachoingia mtoto aongezwmewe maji.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Dalili za ugonjwa wa macho.
Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa macho, ugonjwa huu kwa kawaida una dalili kuu tano kadri ya maambukizi yanavyoongezeka na madhara yake kwa hiyo tunapaswa kujua dalili hizo Kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Dalili za mimba changa kutoka
Post hii inaenda kuzungumzia zaidi kuhusiana na mimba zinazoharibika . mimba huweza kuaribika au kutoka anzia miezi 3 na kuendelea .
Soma Zaidi...Mtu anaye umwaaa UTI anaweza kuona siku zake?
Kutokuona siku zake mwanamke ni ishara kuwa kuna shida kwenye umfumo wa uzazi. Wakati mwingine kutokuona siku ni ishara ya baraka ya kupata mtoto. Ijapokuwa kuna wengine wanadiriki kutoa mimba kwa sababu zisizo za msingi. Je unadhani UTI inaweza kusababi
Soma Zaidi...Nini chanzo cha malaria
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu chanzo cha ugonjwa wa malaria
Soma Zaidi...Fahamu ajali ambazo utokea kwenye kifua
Post hii inahusu Zaidi ajalia ambazo utokea kwenye kifua Kwa kitaalamu huitwa chest injury,Kwa kawaida kwenye kifua kua sehemu mbalimbali kama vile mapafu,moyo,koo na sehemu mbalimbali, sehemu hizi uweza kupata ajali na kusababisha madhara makubwa,Kwa hiy
Soma Zaidi...Njia za kuzuia ugonjwa wa kisonono
Posti hii inahusu zaidi njia ambazo utumiwa Ili kuweza kuzuia kuwepo ugonjwa wa kisonono, kwa kufuata njia hizi ugonjwa huu wa kisonono unaweza kupungua kwa kiasi au kuisha kabisa.
Soma Zaidi...