Namna ya kumsaidia mtoto mwenye UTI
Post hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia mtoto akiwa na ugonjwa wa UTI.
1. Mpatie mtoto dawa zilizoagizwa na daktari
Baada ya kugundua kuwa mtoto ana UTI dawa zilizoagizwa zinapaswa kutumika na kuendelea kuangalia maendeleo ya mtoto, dawa hizo zitumike kwa uhakika na kwa mda wake mtoto anapopaswa kupewa dawa hizo, kwa hiyo ni lazima kuangalia na matokea hasi ya dawa na mtoto anaweza kubadikishiwa dawa ambayo inapatana na mwili wake na kuendelea na matibabu yake ya kawaida.
2.Elimu inabidi utolewa kwa mama na walezi wa mtoto namna ya kuepukana na Maambukizi ya UTI kwa kufanya yafuatayo, kutawadha kutoka mbele kwenda nyuma, kumsafisha mtoto vizuri baada ya kujisaidia, kumtahiri mtoto kaama ni wa kiume, kumbadilisha mtoto nepi pindi tu anapijisaidia na anapokojoa ,kwa hiyo mtoto hasikae na nepi kwa mda mrefu maana bakteria kutoka kwenye mkojo urudi kwenye kibofu Cha mkojo na kukua na kuongezeka hatimaye usababisha maambukizi mapya.
3.Mtoto akiwa na UTI na Yuko kwenye matibabu hakikisha anapewa chakula Cha kutosha chenye mlo kamili na pia kama anatapika hakikisha unatibu kutapika Ili mtoto aweze kula chakula na chakula niendelee kukaa mwilini na kufanya kazi pamoja na dawa na hakikisha mtoto ananyonya vizuri Ili kuhakikisha kuwa dawa zinafanya kazi vizuri, na maendeleo ya mtoto yanakuwa Kawaida.
4. Hakikisha joto la mwili, msukumo wa damu, mapigo ya moyo na upumuaji wa mtoto vinakuwa sawia kwa kupima mara kwa mara kwa sababu maambukizi yoyote kwenye mwili usababisha hali y mwili kubadilika na kuleta kitu kingine ambacho ni matokeo ya maambukizi. Mfano joto la mwili likipanda kwa sababu ya ya UTI mtoto anaweza kuwa na degedege kwa hiyo tunapaswa kuhakikisha kuwa kila hali kwenye mwili Iko sawa kama haiko sawa tujitahidi kuiweka sawa Ili kuepusha madhara mbalimbali yanayoweza kutokea kwa sababu ya maambukizi.
5. Kama mtoto amepata changamoto ya UTI anapaswa kuwa na maji ya kutosha mwilini maana maambukizi kwa mtoto upunguza kiwango Cha maji mwilini na mtoto anaweza kuelekea pabaya, kwa hiyo kwanza mama na waangalizi wa mtoto wanapaswa kuangalia kiasi Cha maji mwilini kwa kuangalia kiasi Cha maji kinachoingia na kinachotoka kwa kufanya yafuatayo.
_ kuangalia kiasi kinachoingia kwa kuangalia anakunywa maji kiasi gani, uji , maziwa,juice na vitu vyote vinavyopungia mwilini kwa mfumo wa maji.
- kuangalia kiasi Cha maji yaliyotoka kwa kuangalia jinsi alivyokojoa yaani amekojoa kiasi gani,au kama anatoa jasho ,au labda anaharisha au kutapika.
Kama kiasi kinachoingia ni kikubwa zaidi ya kinachotoka mtoto anaweza kuendelea na dawa na uangalizi Ila kama kinachotoka ni kikubwa ya kinachoingia mtoto aongezwmewe maji.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Maambukizi ya VVU: Dalili za mwanzo na jinsi ya kuishi nayo.
Makala hii inachunguza kwa kina virusi vya VVU (Virusi vya Upungufu wa Kinga Mwilini), ikianzia na utambuzi wa dalili za mwanzo (acute HIV infection), umuhimu wa upimaji wa mapema, na mikakati ya kisayansi ya kuishi maisha marefu na yenye tija kwa kutumia tiba ya kufubaza virusi (ART). Lengo ni kuondoa unyanyapaa na kutoa mwongozo wa kitaalamu kwa watu wanaoishi na VVU.
Soma Zaidi...Homa ya dengue: Dalili na jinsi inavyoenezwa na mbu.
Homa ya Dengue ni ugonjwa unaosababishwa na virusi vinavyoambukizwa kwa binadamu kupitia kuumwa na mbu aina ya Aedes aegypti. Ugonjwa huu ni tishio kubwa katika maeneo ya kitropiki na mikoa yenye joto. Ingawa visa vingi ni vya wastani, baadhi ya watu wanaweza kupata Dengue kali (Dengue Hemorrhagic Fever) ambayo inahitaji uangalizi wa haraka wa kimatibabu. Makala hii inaelezea mzunguko wa uenezaji wa virusi hivi na umuhimu wa usafi wa mazingira katika kudhibiti mbu.
Soma Zaidi...Ugonjwa wa ngozi (Eczema): Sababu na jinsi ya kutunza ngozi.
Muhtasari Eczema, inayofahamika kitaalamu kama atopic dermatitis, ni hali ya ngozi kuwa kavu, kuwasha, na kupata vipele vinavyoweza kujitokeza mara kwa mara. Makala haya yameandaliwa kwa kina kuchunguza visababishi vya eczema, vichochezi vyake, na kutoa mwongozo wa kitaalamu wa jinsi ya kutunza ngozi ili kudhibiti hali hii na kuboresha maisha ya kila siku.
Soma Zaidi...Hofu ya kufanya makosa (Perfectionism) na jinsi ya kuikabili.
Katika ulimwengu wa ushindani na mitandao ya kijamii, wengi wetu tunajikuta tukinyongwa na mzigo wa kutaka kila kitu kiwe "kamilifu." Makala hii inachunguza kwa kina dhana ya perfectionism—hofu inayozuia ubunifu na maendeleo. Tutachambua kwa nini tunahofu kufanya makosa, athari zake katika afya ya akili na tija, na kutoa mwongozo wa hatua kwa hatua wa jinsi ya kuachana na tabia hii ili kufikia mafanikio ya kweli kupitia kukubali mapungufu.
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Bawasili
Posti hii inahusu zaidi juu ya ugonjwa wa Bawasili, ni ugonjwa unaotokea kwenye njia ya haja kubwa hali ambayo upelekea kuwepo kwa uvimbe au nyama ambazo uonekana hadi nje, kwa lugha ya kitaalamu ujulikana kama haemorrhoid au pokea.
Soma Zaidi...Tatizo la tezi koo
Posti hii inahusu zaidi tatizo la tezi koo, ni tatizo ambalo uwapata watu mbalimbali ambapo Usababisha koo kuvimba na mgonjwa huwa na maumivu mbalimbali na pengine mgonjwa upata kikohozi kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye koo.
Soma Zaidi...