Namna ya kumsaidia mtoto mwenye UTI
Post hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia mtoto akiwa na ugonjwa wa UTI.
1. Mpatie mtoto dawa zilizoagizwa na daktari
Baada ya kugundua kuwa mtoto ana UTI dawa zilizoagizwa zinapaswa kutumika na kuendelea kuangalia maendeleo ya mtoto, dawa hizo zitumike kwa uhakika na kwa mda wake mtoto anapopaswa kupewa dawa hizo, kwa hiyo ni lazima kuangalia na matokea hasi ya dawa na mtoto anaweza kubadikishiwa dawa ambayo inapatana na mwili wake na kuendelea na matibabu yake ya kawaida.
2.Elimu inabidi utolewa kwa mama na walezi wa mtoto namna ya kuepukana na Maambukizi ya UTI kwa kufanya yafuatayo, kutawadha kutoka mbele kwenda nyuma, kumsafisha mtoto vizuri baada ya kujisaidia, kumtahiri mtoto kaama ni wa kiume, kumbadilisha mtoto nepi pindi tu anapijisaidia na anapokojoa ,kwa hiyo mtoto hasikae na nepi kwa mda mrefu maana bakteria kutoka kwenye mkojo urudi kwenye kibofu Cha mkojo na kukua na kuongezeka hatimaye usababisha maambukizi mapya.
3.Mtoto akiwa na UTI na Yuko kwenye matibabu hakikisha anapewa chakula Cha kutosha chenye mlo kamili na pia kama anatapika hakikisha unatibu kutapika Ili mtoto aweze kula chakula na chakula niendelee kukaa mwilini na kufanya kazi pamoja na dawa na hakikisha mtoto ananyonya vizuri Ili kuhakikisha kuwa dawa zinafanya kazi vizuri, na maendeleo ya mtoto yanakuwa Kawaida.
4. Hakikisha joto la mwili, msukumo wa damu, mapigo ya moyo na upumuaji wa mtoto vinakuwa sawia kwa kupima mara kwa mara kwa sababu maambukizi yoyote kwenye mwili usababisha hali y mwili kubadilika na kuleta kitu kingine ambacho ni matokeo ya maambukizi. Mfano joto la mwili likipanda kwa sababu ya ya UTI mtoto anaweza kuwa na degedege kwa hiyo tunapaswa kuhakikisha kuwa kila hali kwenye mwili Iko sawa kama haiko sawa tujitahidi kuiweka sawa Ili kuepusha madhara mbalimbali yanayoweza kutokea kwa sababu ya maambukizi.
5. Kama mtoto amepata changamoto ya UTI anapaswa kuwa na maji ya kutosha mwilini maana maambukizi kwa mtoto upunguza kiwango Cha maji mwilini na mtoto anaweza kuelekea pabaya, kwa hiyo kwanza mama na waangalizi wa mtoto wanapaswa kuangalia kiasi Cha maji mwilini kwa kuangalia kiasi Cha maji kinachoingia na kinachotoka kwa kufanya yafuatayo.
_ kuangalia kiasi kinachoingia kwa kuangalia anakunywa maji kiasi gani, uji , maziwa,juice na vitu vyote vinavyopungia mwilini kwa mfumo wa maji.
- kuangalia kiasi Cha maji yaliyotoka kwa kuangalia jinsi alivyokojoa yaani amekojoa kiasi gani,au kama anatoa jasho ,au labda anaharisha au kutapika.
Kama kiasi kinachoingia ni kikubwa zaidi ya kinachotoka mtoto anaweza kuendelea na dawa na uangalizi Ila kama kinachotoka ni kikubwa ya kinachoingia mtoto aongezwmewe maji.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
๐1 ai web app ๐2 Dua za Mitume na Manabii ๐3 Kitabu cha Afya ๐4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) ๐5 Simulizi za Hadithi Audio ๐6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Dalili za kuvunjika kwa nyonga
Kuvunjika kwa nyonga ni jeraha kubwa, na matatizo ambayo yanaweza kuhatarisha maisha. Hatari ya kupasuka kwa nyonga huongezeka na umri.
Soma Zaidi...Mtoto Kutokwa na matongo tongo tiba ake nin sababu
Hili ni swali lililowahi kuulizwa na moja ya wasomaji wetu
Soma Zaidi...Dalili za mimba wakati wa ovulation
โKipindi cha baada ya yai kuachiliwa (ovulation) hadi kufikia tarehe ya hedhi inayofuata hujulikana kama Luteal Phase. Hapa ndipo wanawake wengi wanaotafuta ujauzito huanza kuchunguza mabadiliko ya miili yao. Makala haya yanajadili dalili za mapema za mimba zinazoweza kujitokeza siku chache baada ya ufertilishaji, jinsi ya kutofautisha dalili hizi na zile za hedhi ya kawaida (PMS), na ukweli wa kitaalamu kuhusu lini unapaswa kupima mimba.
Soma Zaidi...Sababu za Mtoto Kuharisha Mara kwa Mara
โUharishaji kwa watoto ni changamoto ya kawaida inayoweza kusababishwa na maambukizi, lishe, au mabadiliko ya kifizikia. Makala haya yatafafanua sababu kuu za tatizo hili, jinsi ya kukabiliana nalo nyumbani, na wakati mwafaka wa kumpeleka mtoto hospitalini.
Soma Zaidi...