NJIA YA KUJIKINGA NA UGONJWA WA VIRUSI VYA VYA UKIMWI NA ATHARI ZAKE
Posti hii inahusisha maambukizi ya virusi vya ukimwi .pia tutangalia njia za kujikinga na ugonjwa wa UKIMWI
NJia za kujikinga na ugonjwa wa ukimwi.
- Kulingana na ilivyoelezwa apo mwanzo kwamba tutangalia njia za maambukizi ya virusi vya ukimwi.hivyo hivyo mtu mwenye virusi vya ukimwi au mtu yoyote hambaye hana ni marufuku kutotumia miswaki mmoja.
- Kuacha kabisa kufanya ngono umri mdogo chini ya miaka 18.pia ata hivyo kuna njia nyingi za maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi.njia ya ngono ndo njia inayongoza kuwa na maambukizi mengi sana . Pia ukiangalia sahivi watu wanaoishi katika kundi ili wengi ni vijana walio na umri wa miaka hiyo .hivyo ukiacha ngono utakuwa umejiepusha na maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI kwa njia ya ngono.
- Kuepuka kishirikiana vifaa vyenye ncha kali kama wembe, sindano ,mikasi ,na vifaa vya kutobolea masikio,pamoja na vifaa vya kunyolea nywele.
- Kuepuka kuchangia nguo za ndani na taulo.Nguo hizi zinaweza kusababisha maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI .
- Kutumia glavu unapokuwa unamuhudumia mgonjwa wa virusi kama atakuwa ametokwa na maji au damu
- Kuhakikisha kuwa wenye maambukizi ya virusi vya ukimwi wanapata ushauri wa daktari
- Kuhakikisha kuwa wenye maambukizi ya ugonjwa wa virusi vya ukimwi wanapata matibabu sahii.
- Mama mjamzito na mume wake kuhudhuria kiliniki mapema ili wachunguzwe kama wana maambukizi ya virusi vya ukimwi wakigundulika wapate tiba sahii .pia mama lazima apate dawa ya kuzuia maambukizi kwa mtoto aliyetumboni mwake.
9.Mama mjamzito anashauriwa kujifungulia hospitalini ili kama mtoto ameathirika apate matibabu ya haraka iwezekanavyo.
Athari za maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi.
- KUtokana na hivyo tulivyoeleza kuhusu maambukizi ya mgonjwa anashauriwa kuwahi hospitalini ili kuangalia hali yake
- Athari nyingine unafhoofika kwa mwili na kupungua kwa kinga ya mwili .pia huweza kusababisha magonjwa nyemelezi na hatimaye kifo.
- Kuharisha mara kwa mara.hii ni mojawapo ya athari ya virusi vya ukimwi.mtu kuharisha inatokana na virusi vya ukimwi kuwa vina nguvu nyingi kwenye mwili.
- Kukosa nguvu na kuchoka
- Kupata magonjwa ya ngozi kama chunusi sugu na mabakamabaka.
- Kupata homa mara kwa mara
7.kukohoa mara kwa mara.
Kulingana hayo kuna mambo pia ya kuzingatia kwa mtu anayeishi na virusi vya ukimwi.
1.usafi.mtu anayeishi na virusi vya ukimwi na ukimwi anatakiwa kuzingatia usafi wa mwili,nguo na mazingira yanayomzunguka.Anatakiwa kuoza na kuvaaa nguo safi.mgonjwa wa UKIMWI anaweza kushindwa kufanya usafi binafsi na sehemu za kulala.hivyo ni muhimu kumsaidia kufanya usafi wa mwili kama vile kukata kucha ,nywele na kumwogesha .nguo za kuvaaa zinapaswa kuwa safi mda wowote .pia ni muhimu kumfulia nguo zake za kuvaaa na matandikio .Ni vizuri kuchukua tahadhari wakati wa kumhudumia mgonjwa ili kuepuka kuambukizwa virusi.
2.lishe bora,.tumeangalia apo mwanzo kwamba virusi vya ukimwi husababisha kupungua kwa kinga mwilini.lishe bora huongeza kinga ya mwili .watu wanaoishi na virusi vya ukimwi huitaji lishe bora ili kiongozi kinga ya mwilini.
3.usalama wa lishe,.watu wanaoishi na virusi vya ukimwi wako katika hatari ya kuambukizwa maradhi mengine kwa urahisi .hii inatokana na kupungua kwa kinga mwilini.chakula kinaweza kuwa miongoni mwa chanzo cha maambukizi ya virusi vya ukimwi kama hakitandaliwa kwa kuzingatia usafi.ili chakula kiwe safi na salama ni muhimu kuzingatia usafi wa mara kwa mara wakati wa kuandaa chakula.unatakiwa uzumie vyombo safi wakati wa kuandaa kula chakula vyombo vinatakiwa kuishiwa vizuri kwa sabuni na maji safi na salama.vyombo lazima vianikwe au vipanguswe na kitambaa safi.
Mtu anayeishi na virusi vya ukimwi anapaswa kula mlo kamili kila siku.chakula kinatakiwa kiwe safi na salama .chakula kifunikwe kwa kutumia mfuniko safi ili kuzuia vumbi na wadudu.mtu anayeishi na virusi vya ukimwi anatakiwa kula chakula cha moto .matunda na mboga mboga hasa zile zinazoliwa bila kupikwa zioshwe kwa maji safi na salama.
Pia mtu anayeishi na virusi vya ukimwi anatakiwa kuepuka vyakula viliyosindikwa .vyakula hivi mara nyingi husindikwa kwa kemikali ambazo zinaweza kuleta madhara kwa mgonjwa.vilevile ,haishauriwi kula chakula kilichokaa zaidi ya saa mbili bahada ya kupikwa kinatakiwa kipashwe moto mpaka kichemke kabla ya kula.
Kama ilivyo kwa watu wengine ,mtu anayeishi na virusi anatakiwa kunywa maji safi na salama ,maji ya kunywa yatunzwe katika chombo safi chenye mfuniko na kuweka mahali safi.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 ai web app 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
IJUE HOMA YA CHIKUNGUNYA (CHIKV) DALILI ZAKE, TIBA YAKE, CHANJO YAKE, NA MBU ANAYESAMBAZA HOMA HII
Haya ni maradhi ambayo husambazwa kutoka kwa mtu kwenda kwa mtu kwa kupitia mbu.
Soma Zaidi...Madhara ya kutotibu ngiri.
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea pale ambapo Ugonjwa wa ngiri unaposhindwa kutibiwa mapema.
Soma Zaidi...WAJUE FANGASI, AINA ZAKE, DALILI ZAKE NA MATIBABU YAKE
Fangasi huweza kuishi na kuathiri maeneo mbalimbali ndani ya mwili.
Soma Zaidi...Sababu za maumivu ya matiti na chuchu
Maumivu ya matiti yanaweza kuanzia kidogo hadi makali. Inaweza kukuathiri siku chache tu kwa mwezi, kwa mfano kabla tu ya kipindi chako, au inaweza kudumu kwa siku saba au zaidi kila mwezi. Maumivu ya matiti yanaweza kukuathiri kabla tu ya kipindi chako
Soma Zaidi...Yajue mashambulizi ya bacteria kwenye Ngozi (cellulitis)
Mashambulizi ya bacteria kwenye Ngozi hujitokeza sehemu yenye jeraha pia huonyesha wekundu wenye upele,Uvimbe na malengelenge.
Soma Zaidi...Fahamu Ugonjwa wa kifua kikuu kwa watoto chini ya miaka mitano
Posti hii inaonyesha mambo mbalimbali yanayoweza kusababisha Ugonjwa wa kifua kikuu kwa watoto chini ya miaka mitano.
Soma Zaidi...