picha

NJIA YA KUJIKINGA NA UGONJWA WA VIRUSI VYA VYA UKIMWI NA ATHARI ZAKE

Posti hii inahusisha maambukizi ya virusi vya ukimwi .pia  tutangalia  njia za kujikinga na  ugonjwa wa UKIMWI

 

        NJia za kujikinga na ugonjwa wa ukimwi.

  1. Kulingana na  ilivyoelezwa apo mwanzo  kwamba  tutangalia njia za maambukizi ya virusi vya ukimwi.hivyo hivyo mtu mwenye virusi vya ukimwi au mtu yoyote hambaye hana ni marufuku kutotumia miswaki mmoja.
  2. Kuacha kabisa kufanya ngono umri mdogo chini ya miaka 18.pia ata hivyo kuna njia nyingi za maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi.njia ya ngono ndo njia inayongoza kuwa na maambukizi mengi sana . Pia ukiangalia sahivi watu wanaoishi katika kundi ili wengi ni vijana walio na umri wa miaka hiyo .hivyo ukiacha ngono utakuwa umejiepusha na maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI kwa njia ya ngono.
  3. Kuepuka kishirikiana vifaa vyenye ncha kali kama  wembe, sindano ,mikasi ,na vifaa vya kutobolea masikio,pamoja na vifaa vya kunyolea nywele.
  4. Kuepuka kuchangia nguo za ndani na taulo.Nguo hizi zinaweza kusababisha maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI .
  5. Kutumia glavu unapokuwa unamuhudumia mgonjwa wa virusi kama atakuwa ametokwa na maji au damu
  6. Kuhakikisha kuwa wenye maambukizi ya virusi vya ukimwi wanapata ushauri wa daktari
  7. Kuhakikisha kuwa wenye maambukizi ya ugonjwa wa virusi vya ukimwi wanapata matibabu sahii.
  8. Mama mjamzito na mume wake kuhudhuria kiliniki mapema ili wachunguzwe kama wana maambukizi ya virusi vya ukimwi wakigundulika wapate tiba sahii .pia  mama lazima apate dawa ya kuzuia maambukizi kwa mtoto aliyetumboni mwake.

9.Mama mjamzito anashauriwa kujifungulia hospitalini ili kama mtoto ameathirika apate matibabu ya haraka iwezekanavyo.   

    

        Athari za maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi.

  1. KUtokana na hivyo tulivyoeleza kuhusu maambukizi ya  mgonjwa anashauriwa kuwahi hospitalini ili kuangalia hali yake
  2. Athari nyingine unafhoofika kwa mwili na kupungua kwa kinga ya mwili .pia huweza kusababisha magonjwa nyemelezi na hatimaye kifo.
  3. Kuharisha mara kwa mara.hii ni mojawapo ya athari ya virusi vya ukimwi.mtu kuharisha inatokana na virusi vya ukimwi kuwa vina nguvu nyingi kwenye mwili.
  4. Kukosa nguvu na kuchoka
  5. Kupata magonjwa ya ngozi kama chunusi sugu na mabakamabaka.
  6. Kupata homa mara kwa mara

        7.kukohoa mara kwa mara.

 

                Kulingana hayo kuna mambo pia ya kuzingatia kwa mtu anayeishi na virusi vya ukimwi.

1.usafi.mtu anayeishi na virusi vya ukimwi na ukimwi anatakiwa kuzingatia usafi wa mwili,nguo na mazingira yanayomzunguka.Anatakiwa kuoza na kuvaaa nguo safi.mgonjwa wa UKIMWI anaweza kushindwa kufanya usafi binafsi na sehemu za kulala.hivyo ni muhimu kumsaidia kufanya usafi wa mwili kama vile kukata kucha ,nywele na kumwogesha .nguo za kuvaaa zinapaswa kuwa safi mda wowote .pia ni muhimu kumfulia nguo zake za kuvaaa na matandikio .Ni vizuri kuchukua tahadhari wakati wa kumhudumia mgonjwa ili kuepuka kuambukizwa virusi.

 

2.lishe bora,.tumeangalia apo mwanzo kwamba virusi vya ukimwi husababisha kupungua kwa kinga mwilini.lishe bora huongeza kinga ya mwili .watu wanaoishi na virusi vya ukimwi huitaji lishe bora ili kiongozi kinga ya mwilini.

 

3.usalama wa lishe,.watu wanaoishi na virusi vya ukimwi wako katika hatari ya kuambukizwa maradhi mengine kwa urahisi .hii inatokana na kupungua kwa kinga mwilini.chakula kinaweza kuwa miongoni mwa chanzo cha maambukizi ya virusi vya ukimwi kama hakitandaliwa kwa kuzingatia usafi.ili chakula kiwe safi na salama ni muhimu kuzingatia usafi wa mara kwa mara wakati wa kuandaa chakula.unatakiwa uzumie vyombo safi wakati wa kuandaa kula chakula vyombo vinatakiwa kuishiwa vizuri kwa sabuni na maji safi na salama.vyombo lazima vianikwe au vipanguswe na kitambaa safi. 

   

Mtu anayeishi na virusi vya ukimwi anapaswa kula mlo kamili kila siku.chakula kinatakiwa kiwe safi na salama .chakula kifunikwe kwa kutumia mfuniko safi ili kuzuia vumbi na wadudu.mtu anayeishi na virusi vya ukimwi anatakiwa kula chakula cha moto .matunda na mboga mboga hasa zile zinazoliwa bila kupikwa zioshwe kwa maji safi na salama.

 

Pia mtu anayeishi na virusi vya ukimwi anatakiwa kuepuka vyakula viliyosindikwa .vyakula hivi mara nyingi husindikwa kwa kemikali ambazo zinaweza kuleta madhara kwa mgonjwa.vilevile ,haishauriwi kula chakula kilichokaa zaidi ya saa mbili bahada ya kupikwa kinatakiwa kipashwe moto mpaka kichemke kabla ya kula.

Kama ilivyo kwa watu wengine ,mtu anayeishi na virusi anatakiwa kunywa maji safi na salama ,maji ya kunywa yatunzwe katika chombo safi chenye mfuniko na kuweka mahali safi.

 

 

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/08/06/Saturday - 07:50:51 pm Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 4954

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Maradhi ya macho, dalili zake na matibabu yake

Makala hii itakufundisha maradho makuu ya macho, matibabu yake na tiba zake

Soma Zaidi...
Dalili ya pressure ya kupanda

Post ya leo inaenda kufundisha dalili na hatari za presha ya kupanda. Presha ni ugonjwa unaosababishwa na baadhi ya vitu mbalimbali.pressure hujulikana kwa jina lingine ambolo ni hypertension (pressure ya kupanda). presha hugundulika pale ambapo presha ya

Soma Zaidi...
Magonjwa yanayowashambulia watoto wachanga

Watoto wachanga ni watoto wenye umri chini ya miaka mitano, watoto hawa hushambulia na maginjwa mara kwa mara na kusababisha ukuaji wao kuwa dunk,

Soma Zaidi...
Tiba ya vidonda vya tumbo na dawa zake

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu Tina ya vidonda vya tumbo na dawa zake

Soma Zaidi...
Maambukizi ya tishu ya Matiti.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na maambukizi ya tishu ya matiti ambayo husababisha maumivu ya matiti, uvimbe, joto na uwekundu. Pia unaweza kuwa na Homa na baridi. Ugonjwa huu huwapata zaidi wanawake wanaonyonyesha ingawa wakati mwingine hali hi

Soma Zaidi...
Yajuwe maradhi mbalmbali ya ini na chano chake

Ini ni moja ya ogani za mwili ambazo husumbuliwa na maradhi hatari sana. Katika post hii utakwend akuyajuwa maradh hatari ambayo hushambulia ini. Pia utajifunza jinsi a kujikinga na maradhi hayo.

Soma Zaidi...
Madhara ya mwili kujaa sumu

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kupatikana ikiwa mwili unaweza kujaa sumu, kwa sababu mwili unapaswa kuwa huru Ili kuweza kufanya vizuri kazi yake ila ikiwa utajaa Sumu Kuna hatari mbalimbali zinaweza kutokea kama vile.

Soma Zaidi...
Njia za kuzuia ugonjwa wa kisonono

Posti hii inahusu zaidi njia ambazo utumiwa Ili kuweza kuzuia kuwepo ugonjwa wa kisonono, kwa kufuata njia hizi ugonjwa huu wa kisonono unaweza kupungua kwa kiasi au kuisha kabisa.

Soma Zaidi...
Kupambana na kisukari

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kupambana na kisukari

Soma Zaidi...
VIRUSI VYA KORONA AU CORONA (CORONAVIRUS)

Virusi vya korona ni katika aina za virusi ambavyo asili yake ni kutoka kwa wanyama na kuja kwa binadamu.

Soma Zaidi...