picha

NJIA YA KUJIKINGA NA UGONJWA WA VIRUSI VYA VYA UKIMWI NA ATHARI ZAKE

Posti hii inahusisha maambukizi ya virusi vya ukimwi .pia  tutangalia  njia za kujikinga na  ugonjwa wa UKIMWI

 

        NJia za kujikinga na ugonjwa wa ukimwi.

  1. Kulingana na  ilivyoelezwa apo mwanzo  kwamba  tutangalia njia za maambukizi ya virusi vya ukimwi.hivyo hivyo mtu mwenye virusi vya ukimwi au mtu yoyote hambaye hana ni marufuku kutotumia miswaki mmoja.
  2. Kuacha kabisa kufanya ngono umri mdogo chini ya miaka 18.pia ata hivyo kuna njia nyingi za maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi.njia ya ngono ndo njia inayongoza kuwa na maambukizi mengi sana . Pia ukiangalia sahivi watu wanaoishi katika kundi ili wengi ni vijana walio na umri wa miaka hiyo .hivyo ukiacha ngono utakuwa umejiepusha na maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI kwa njia ya ngono.
  3. Kuepuka kishirikiana vifaa vyenye ncha kali kama  wembe, sindano ,mikasi ,na vifaa vya kutobolea masikio,pamoja na vifaa vya kunyolea nywele.
  4. Kuepuka kuchangia nguo za ndani na taulo.Nguo hizi zinaweza kusababisha maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI .
  5. Kutumia glavu unapokuwa unamuhudumia mgonjwa wa virusi kama atakuwa ametokwa na maji au damu
  6. Kuhakikisha kuwa wenye maambukizi ya virusi vya ukimwi wanapata ushauri wa daktari
  7. Kuhakikisha kuwa wenye maambukizi ya ugonjwa wa virusi vya ukimwi wanapata matibabu sahii.
  8. Mama mjamzito na mume wake kuhudhuria kiliniki mapema ili wachunguzwe kama wana maambukizi ya virusi vya ukimwi wakigundulika wapate tiba sahii .pia  mama lazima apate dawa ya kuzuia maambukizi kwa mtoto aliyetumboni mwake.

9.Mama mjamzito anashauriwa kujifungulia hospitalini ili kama mtoto ameathirika apate matibabu ya haraka iwezekanavyo.   

    

        Athari za maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi.

  1. KUtokana na hivyo tulivyoeleza kuhusu maambukizi ya  mgonjwa anashauriwa kuwahi hospitalini ili kuangalia hali yake
  2. Athari nyingine unafhoofika kwa mwili na kupungua kwa kinga ya mwili .pia huweza kusababisha magonjwa nyemelezi na hatimaye kifo.
  3. Kuharisha mara kwa mara.hii ni mojawapo ya athari ya virusi vya ukimwi.mtu kuharisha inatokana na virusi vya ukimwi kuwa vina nguvu nyingi kwenye mwili.
  4. Kukosa nguvu na kuchoka
  5. Kupata magonjwa ya ngozi kama chunusi sugu na mabakamabaka.
  6. Kupata homa mara kwa mara

        7.kukohoa mara kwa mara.

 

                Kulingana hayo kuna mambo pia ya kuzingatia kwa mtu anayeishi na virusi vya ukimwi.

1.usafi.mtu anayeishi na virusi vya ukimwi na ukimwi anatakiwa kuzingatia usafi wa mwili,nguo na mazingira yanayomzunguka.Anatakiwa kuoza na kuvaaa nguo safi.mgonjwa wa UKIMWI anaweza kushindwa kufanya usafi binafsi na sehemu za kulala.hivyo ni muhimu kumsaidia kufanya usafi wa mwili kama vile kukata kucha ,nywele na kumwogesha .nguo za kuvaaa zinapaswa kuwa safi mda wowote .pia ni muhimu kumfulia nguo zake za kuvaaa na matandikio .Ni vizuri kuchukua tahadhari wakati wa kumhudumia mgonjwa ili kuepuka kuambukizwa virusi.

 

2.lishe bora,.tumeangalia apo mwanzo kwamba virusi vya ukimwi husababisha kupungua kwa kinga mwilini.lishe bora huongeza kinga ya mwili .watu wanaoishi na virusi vya ukimwi huitaji lishe bora ili kiongozi kinga ya mwilini.

 

3.usalama wa lishe,.watu wanaoishi na virusi vya ukimwi wako katika hatari ya kuambukizwa maradhi mengine kwa urahisi .hii inatokana na kupungua kwa kinga mwilini.chakula kinaweza kuwa miongoni mwa chanzo cha maambukizi ya virusi vya ukimwi kama hakitandaliwa kwa kuzingatia usafi.ili chakula kiwe safi na salama ni muhimu kuzingatia usafi wa mara kwa mara wakati wa kuandaa chakula.unatakiwa uzumie vyombo safi wakati wa kuandaa kula chakula vyombo vinatakiwa kuishiwa vizuri kwa sabuni na maji safi na salama.vyombo lazima vianikwe au vipanguswe na kitambaa safi. 

   

Mtu anayeishi na virusi vya ukimwi anapaswa kula mlo kamili kila siku.chakula kinatakiwa kiwe safi na salama .chakula kifunikwe kwa kutumia mfuniko safi ili kuzuia vumbi na wadudu.mtu anayeishi na virusi vya ukimwi anatakiwa kula chakula cha moto .matunda na mboga mboga hasa zile zinazoliwa bila kupikwa zioshwe kwa maji safi na salama.

 

Pia mtu anayeishi na virusi vya ukimwi anatakiwa kuepuka vyakula viliyosindikwa .vyakula hivi mara nyingi husindikwa kwa kemikali ambazo zinaweza kuleta madhara kwa mgonjwa.vilevile ,haishauriwi kula chakula kilichokaa zaidi ya saa mbili bahada ya kupikwa kinatakiwa kipashwe moto mpaka kichemke kabla ya kula.

Kama ilivyo kwa watu wengine ,mtu anayeishi na virusi anatakiwa kunywa maji safi na salama ,maji ya kunywa yatunzwe katika chombo safi chenye mfuniko na kuweka mahali safi.

 

 

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 5483

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 web hosting     👉6 ai web app    

Post zinazofanana:

Choo kuwa kigumu (Constipation): Vyakula na vinywaji vya kusaidia.

Choo kigumu ni changamoto inayowatesa watu wengi, ikiwemo maumivu ya tumbo, kuhisi mzito, na kukosa raha. Mara nyingi, tatizo hili husababishwa na ukosefu wa nyuzi lishe (fiber), kutokunywa maji ya kutosha, au kutokuwa na utaratibu mzuri wa maisha. Habari njema ni kwamba, kwa kufanya mabadiliko machache kwenye lishe yako, unaweza kurudisha mfumo wako wa mmeng’enyo wa chakula kwenye hali ya kawaida.

Soma Zaidi...
Matumizi ya kondom: Njia sahihi ya kujikinga.

​Kondomu ni nyenzo yenye ufanisi mkubwa katika kuzuia maambukizi ya virusi vya UKIMWI (VVU), Kaswende, Klamidia, na magonjwa mengine ya zinaa, pamoja na uzazi wa mpango. Ufanisi wake hutegemea kwa kiasi kikubwa matumizi sahihi. Makala hii inatoa maelekezo ya kitaalamu juu ya hatua sahihi za kutumia kondomu, uhifadhi, na mambo ya kuzingatia ili kuhakikisha usalama wa juu.

Soma Zaidi...
Dawa za kutuliza maumivu na kazi zake

Post hii inahusu zaidi dawa za kupunguza maumivu na kazi zake, ni dawa ambazo upunguza maumivu kwenye mwili wa binadamu.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kujenga afya ya akili katika ulimwengu wa sasa.

​Katika ulimwengu wa kidijitali na wenye kasi kubwa, afya ya akili imekuwa rasilimali muhimu zaidi kwa binadamu. Makala haya yanachunguza mbinu za kisayansi na kivitendo za kujenga ustahimilivu wa kiakili, kudhibiti mfadhaiko wa teknolojia, na kukuza usawaziko wa maisha. Kupitia mwongozo huu, utajifunza jinsi ya kuweka mipaka, kuboresha mahusiano, na kutumia mazoea ya kujijali (self-care) ili kudumisha utulivu wa ndani katikati ya changamoto za kisasa.

Soma Zaidi...
Yajue magonjwa nyemelezi.

Posti hii inahusu zaidi magonjwa nyemelezi ambayo kwa kawaida utokea pale ambapo kinga ya mwili inashuka.

Soma Zaidi...
Fahamu Ugonjwa wa kipindupindu.

Kipindupindu ni ugonjwa wa bakteria ambao kawaida huenezwa kupitia maji machafu. Kipindupindu husababisha Kuhara na Upungufu wa maji mwilini.

Soma Zaidi...