HISTORIA YA MTUME ZAKARIA(A.S) NA YAHYA(A.S)

Zakaria(a.

HISTORIA YA MTUME ZAKARIA(A.S) NA YAHYA(A.S)

HISTORIA YA MTUME ZAKARIA(A.S) NA YAHYA(A.S)
Nabii Zakaria(a.s) ni miongoni mwa mitume wa Bani Israil (Mayahud) na anatokana na kizazi cha Nabii Sulaiman(a.s). Alikuwa mwangalizi mkuu wa nyumba ya Ibada na alikuwa anapta riziki yake kwa kazi ya useremala.




Zakaria(a.s) Kumlea Marymam na Kuomba Mtoto Mwema Zakaria(a.s) alichaguliwa na ukoo kumlea Maryamu, mama yake Nabii Issa(a.s). Alimlea vyema katika malezi ya kiislamu.

Katika kumlea Marymu, Zakaria(a.s) siku moja alishangaa kumkuta Maryam binti Imraan na vyakula mezani ambavyo hakumpa yeye, ikabidi amuulize:-

“.........Ewe Maryam! unapta wapi hivi ? Akasema: Hivi vinatoka kwa Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu humruzuku amtakaye bila ya hisabu” (3:37)



Jibu hili la Maryamu lilimsisimua na kumuhamasisha Mzee Zakaria kiasi cha kumfanya naye amuelekee Mola wake na kumuomba mtoto mwema atakaye mrithi katika ucha-mungu na kusimamisha Dini ya Allah(s.w) katika jamii. Zakaria(a.s) alimuelekea Mola wake na kulalama.


Akasema: “Mola wagu. Bila shaka mifupa yangu imekuwa dhaifu na kichwa kinawaka (kinan’gara) kwa mvi,wala sikuwa mweye bahati mbaya (mwenye kukhasirika) Mola wangu, kwa kukuomba wewe. Na hakika mimi nawahofia jamaa zangu baada yangu(kuharibu Dini). Na mke wangu ni tasa. Basi nipe mrithi (anijie) kutoka kwako. Atakaye nirithi na kuwa na kuwarithi(wazee wake wengine)kizazi cha Ya‘aquub. Na umfanye, Mola wangu mwenye kukuridhisha”(19:4-6)



Yahya(a.s) Jibu la Dua ya Mzee Zakaria(a.s)

Dua ya Zakaria(a.s) ilijibiwa kwa kubashiriwa kupata mtoto, Yahya (Akaambiwa): “Ewe Zakaria! Tunakupa habari njema ya (kuwa utazaa)mtoto, jina lake ni Yahya: Hatujafanya kabla yake aliye na jina namna hilo.” (19:7)



Yahya(a.s) Kupewa Utume


Alizaliwa mtoto Yahya na kupewa utume akingali mtoto na akainukia kuwa mtu mwema kwa wazazi wake na kwa walimwengu wote kwa ujumla. Alijitoa muhanga kwa ajili ya kulingania Dini ya Allah(s.w).




“Ewe Yahya! kishike kitabu (hiki unachopewa) kwa hima kubwa.” Na tulimpa hikima angali mtoto. Na (tukamfanya ni) huruma kutoka kwetu, na utakaso na akawa mcha-Mungu. Na mwema kwa wazazi wake wala hakuwa jeuri ,asi. Na amani ilikuwa juu yake siku aliyozaliwa na siku aliyokufa na siku atakayofufuliwa hai.(19:12-15)

Nabii Zakaria na Yahya(a.s),wote waliuliwa na Mayahud.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 3695

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Msafara wa vita vya Tabuk Dhidi ya Warumi

Ukombozi wa mji wa Makka (Fat-h Makka) mwaka 8 A.

Soma Zaidi...
Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Salih(a.s)

Mafunzo tuyapatayo hayatofautiani na yale yatokanayo na Historia ya Nabii Hud(a.

Soma Zaidi...
Nani alikuwa ni Sahaba wa kwanza kufariki akiwa Shahidi

Sahaba wa kwanz akufariki akiwa shahidi, alifariki kwa sababu ya mateso aliyoyapata kutoka kwa Makafiri wa ki Quraysh

Soma Zaidi...
vita vya ahzab, sababu ya kutokea vita hivi na mafunzo tunayoyapata

Vita vya Ahzab- Maquraish waliungana na mayahudi, wanafiki na makabila mengine ya waarabu baada ya kuona kuwa wao peke yao hawawezi kuufuta Uislamu.

Soma Zaidi...
Kuchimbwa upya kwa kisima cha Zamzam

Sura na historia ya mtume Muhammad S.A.W sehemu ya 3.Hapa utajifunza kuhusu kufukuliwa kwa kisima cha Zamzam baada ya kufukiwa muda mrefu.

Soma Zaidi...
Kuhajiri Waislamu wa Makka Kwenda Madinah

Baada ya mikataba miwili ya ‘Aqabah na baada ya Waislamu 75 kufika Yathrib salama, Mtume(s.

Soma Zaidi...
Yusufu(a.s.) Akutana na Ndugu Zake

Njaa ilitokea na ikawa hapana sehemu nyingine yoyote yenye chakula ila Misri.

Soma Zaidi...