image

Historia ya Firaun, Qarun na Hamana

Karun na Hamana waliishi zama za Mtume Musa(a.

Historia ya Firaun, Qarun na Hamana

Historia ya Firaun, Qarun na Hamana


Karun na Hamana waliishi zama za Mtume Musa(a.s) na walikuwa viongozi waandamizi wa Firaun. Walikuwa ni watu maarufu katika jamii yao na walikuwa mstari wa mbele katika kumpinga Mtume Musa(a.s).



“Na kwa yakini tulimtuma Musa pamoja na miujiza yetu na hoja (dalili) zilizo dhahiri. (Tulimpeleka) kwa Firauni na Hamana na Karun, wakasema: “(Huyu ni) Mchawi, muongo mkubwa” (40:23-24).

Katika aya nyingine Mwenyezi Mungu anatufahamisha kuwa aliwaangamiza Firaun, Hamana na Qarun kwa sababu waliyakanusha mafundisho ya Mtume Musa na wakatakabari:



Na (vile vile) Qarun na Firauni na Hamana (waliangamizwa); na hakika aliwajia Musa kwa miujiza waziwazi, lakini walijivuna katika ardhi, lakini hawakuweza kumshinda Mwenyezi Mungu. Basi kila mmoja tulimtesa kwa sababu ya dhambi zake. Miongoni mwao wako tuliowapelekea kimbunga cha changarawe; na miongoni mwao wako waliotolewa roho kwa ukulele mkubwa, na miongoni mwao wako tuliowadidimiza ardhini na miongoni mwao wako tuliowagharikisha na hakuwa Mwenyezi Mungu Mwenye kuwadhulumu, lakini walikuwa wakijidhulumu (wenyewe) nafsi zao” (29:39-40).



Qarun alijaaliwa kuwa na mali nyingi sana. Lakini alilisahau lengo la maisha akatakabari. Watu walio karibu naye walimnasihi lakini hakuzinduka. Alijivuna na kuona kuwa utajiri aliokuwa nao kaupata kwa juhudi na elimu yake. Alisahau kuwa hiyo ni neema kutoka kwa Allah(s.w).




Hakika Qarun alikuwa katika watu wa Musa, lakini aliwafanyia dhulma. Na tulimpa hazina ambazo funguo zake zinawatopeza watu wenye nguvu (kuzichukua). Walimwambia watu wake: “Usijione (usijigambe), hakika Mwenyezi Mungu hawapendi wanaojigamba” (28:76).




Akasema: “Hakika nimepewa haya kwa sababu ya ilimu niliyo nayo”. Je, hakujua ya kwamba Mwenyezi Mungu amewaangamiza kabla yake watu waliokuwa wenye nguvu zaidi kuliko yeye na wenye mkusanyo mwingi zaidi (kuliko wake yeye)?” (28:78).

Kwa kutakabari kwake huko, Qarun aliangamizwa kwa kudidimizwa ardhini yeye na nyumba yake.




“Basi tukamdidimiza yeye (Qarun) na nyumba yake ardhini, wala hapakuwa na kundi lolote la kumsaidia kinyume na Mwenyezi Mungu, wala hakuwa miongoni mwa walioweza kujisaidia” (28:81).



Mafunzo:


Yapo mafunzo mengi kutokana na maisha ya Qarun. Funzo la kwanza ni kuwa kama utajiri hautatumiwa vyema, waweza kuzaa maovu yafuatayo:


(i) Humfanya mwenye mali kujisahau na kutakabari.

(ii) Humfanya mwenye mali kuwasahau wenye shida na wahitaji. Hali hii huzaa jamii ya wenye mali ambao hula na kusaza wakati wengine hubaki ombaomba wasio na msaada wowote.


Funzo la pili linalolandana na maisha ya Qaruni ni kuwa mali, cheo na mamlaka ya mtu hayawezi kumsaidia chochote Mwenyezi Mungu anapopitisha hukumu yake. Qaruni alitamba kwa mali yake, lakini hukumu ya Allah(s.w) ilipofika alididimizwa yeye na mali yake ardhini.



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 847


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Haki na Hadhi za Mwanamke katika jamii za mashariki: China, India na Japani hapo zamani
2. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII LUT(A.S) NA WATU WA SODOMA NA GOMORA
Mtume Lut(a. Soma Zaidi...

KIKAO CHA KUMFUKUZA MTUME MUHAMMAD KUTOKA MAKKAH (MAKA), KIKAO ALICHOHUDHURIA IBLISI
KIKAO CHAKALIWA KUJADILI HATMA YA MUHAMMAD KATIKA MJI WA MAKAHiki ni kikao kizito hakijapata kutokea toka muhammad katika ji wa maka. Soma Zaidi...

Mateso waliyoyapata waislamu wa mwanzo Maka, na orodha ya waislamu walioteswa vikali
Pili, Maquraish walimuendea Mtume(s. Soma Zaidi...

Mafunzo yatokanayo na upinzani wa maquraish dhidi ya uislamu
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Allah(s.w) Amnusuru Ibrahim (a.s) na Hila za Makafiri
Pamoja na kudhihirikiwa na ukweli wa udhaifu wa miungu wa kisanamu, watu wa NabiiIbrahiim(a. Soma Zaidi...

Si Yesu Aliyesulubiwa (yesu hakufa msalabani wala hakusulubiwa
Katika Qur,an tukufu, Mwenyezi Mungu aliye muweza na mjuzi wa mambo anathibitisha kuwa aliyesulubiwa si Nabii Isa(a. Soma Zaidi...

Imam Nasai na kitabu cha Sunan
Soma Zaidi...

Mafunzo yatokanayo na kuanzishwa kwa dola ya uislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

HISTORIA YA MTUME SULAIMAN(A.S)
Sulaiman(a. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII AYUBU
Soma Zaidi...

CHANZO CHA VITA VYA VITA VYA AL-FIJAR NA ATHARI ZAKE
MAPIGANO YA AL-FIJAR (MAPIGANO YA UOVU). Soma Zaidi...