Sahihi Muslim
Sahihi Muslim ni kitabu cha Hadith sahihi kinachofuatia sahihi al-Bukhari kilichokusanywa na Abul Husain Muslim bin al-Hajjaj anayejulikana kwa jina la Imamu Muslim. Imamu Muslim alizaliwa katika mji wa Misabur, 202 A.H./817 A.D. na alifariki 261 A.H./875
A.D. katika mji huo huo. Kama alivyokuwa Imamu Bukhar, naye alisafiri sana huku na huko katika nchi za Uarabuni, Misr, Syria (Sham) na Iraq ambapo alipata fursa ya kusoma kwa wanazuoni wengi waliokuwa mashuhuri. Miongoni mwa wanazuoni mashuhuri ambao alisoma kwao ni Ahmad bin Hambal, mwanafunzi wa Imam Shafii.
Imam Muslim alikusanya Hadith 300,000 na katika hizo ni Hadith 9,200 tu alizoziandika katika kitabu chake kinachojulikana kwa jina mashuhuri "Sahihi Muslim". Alimpenda sana Imam Bukhari na kazi yake. Kama imam Bukhari, Muslim naye amekifuma kitabu chake kulingana na mada za fiq-h. Naye alichukua uangalifu mkubwa mno katika kuchagua Hadith zilizo sahihi kwa kiasi ambacho Hadith zake nyingi zimeku baliana na zile za Al-Bukhari. Alikuwa mwangalifu sana katika kuchambua sehemu ya upokezi (isnad) kwa kiasi ambacho Hadith moja ilikuwa na isnad nyingi (misururu mingi ya wapokeaji). Kwa msomaji, Sahihi Muslim imekuwa katika mpango mzuri zaidi kuliko ule wa Sahihi al-Bukhari.
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1280
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉2 Kitabu cha Afya
👉3 kitabu cha Simulizi
👉4 Simulizi za Hadithi Audio
👉5 Kitau cha Fiqh
👉6 Madrasa kiganjani
Kifo cha Nabii Sulaiman
Pamoja na utukufu na umadhubuti wa ufalme wake Nabii Sulaiman muda wake wa kuishi ulipokwisha aliondoka kama walivyoondoka Mitume,wafalme na wanaadamu wengine. Soma Zaidi...
Upinzani Dhidi ya Ujumbe wa Mtume(s.a.w)
Mtume(s. Soma Zaidi...
Miujiza Kama Ushahidi wa Utume wa Nabii Musa(a.s)
Allah(s. Soma Zaidi...
Utekwaji wa Misri na Gavana Muawiya
Soma Zaidi...
Mbinu walizotumia makafiri wa kiqureish katika kuupinga uislamu makkah
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Mjadala juu ya ndoa ya Mtume Muhammad s.a.w na bi Khadija.
Sara na historia ya Mtume Muhammad s.a.w sehemu ya 16. Hapa utajifunza maandalizi wa mjadala wa ndoa hizi. Soma Zaidi...
Mbinu Alizozitumia Nabii Shu’ayb(a.s) Katika Kufikisha Ujumbe Wake
Soma Zaidi...
Kuporomoka kwa Dola ya Kiislamu
Soma Zaidi...
Haki na Hadhi za Mwanamke katika jamii za mashariki: China, India na Japani hapo zamani
2. Soma Zaidi...
Sababu ya uislamu kuwa ndiyo dini sahihi pekee
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Vita vya Uhud na sababu ya kutokea kwake, Mafunzo ya Vita Vya Uhud
Vita vya Uhudi. Soma Zaidi...
Zakaria(a.s) Akabidhiwa Ulezi wa Maryam
Baada ya kupigwa kura juu ya nani awe mlezi wa Maryam, Nabii Zakaria akachaguliwa kuwa mlezi wa Maryam. Soma Zaidi...