Mapambano ya waislamu dhidi ya Makabila ya kiarabu wakati wa Mtume

Mapambano ya waislamu dhidi ya Makabila ya kiarabu wakati wa Mtume

Mapambano ya waislamu dhidi ya Makabila ya kiarabu wakati wa Mtume

Makabila Mengine ya Kiarabu


Makabila mengi ya Kiarabu yaliyoleta chokochoko dhidi ya Dola ya Kiislamu ya Madinah, Mtume(s.a.w) aliyashughulikia mpaka yakasalimu amri na kulipa jizya. Ukiacha Maquraish makabila ya Kiarabu yaliyokuwa na nguvu sana na kujiamini ni makabila ya Khawaizin na Thaqif yaliyokuwa yakiishi katika maeneo ya mji wa Taif. Makabila haya yalipambana na jeshi la Mtume(s.a.w) katika vita vya Hunain vilivyopiganiwa mwaka wa 8 A.H. mwezi mmoja baada ya Fat-h-Makka. Waislamu walipata ushindi mkubwa sana katika vita hivi vilivyokuwa mwisho wa mapambano na makabila ya Kiarabu kwani yote yalikuja silimu na kuwa chini ya Dola ya Kiislamu. Vita vya Hunain vinaelezwa katika Qur-an:




Bila shaka Mwenyezi Mungu amekunusuruni katika mapigano mengi, na siku ya Hunayni (pia); ambapo wingi wenu ulikupandisheni kichwa, lakini haukukufaeni chochote, na ardhi ikawa dhiki juu yenu; ingawa ilikuwa yenye wasaa, kisha mkageuka mkarudi nyuma (mnakimbia). Kisha Mwenyezi Mungu akateremsha utulivu wake juu ya Mtume wake na juu ya walioamini. Na akateremsha majeshi (ya Malaika) ambayo hamkuyaona, na akawaadhibu wale waliokufuru; na hayo ndiyo malipo ya makafiri. (9:25-26)



Aya hizi zinatupa picha halisi ya tukio la Hunain. Baadhi ya Waislamu mwanzo mwa vita walitelezeshwa na sheitani wakawa na fikra mbaya kuwa watashinda kutokana na ukubwa wa jeshi lao lililokuwa na askari 12,000 waliojizatiti vizuri, wakasahau kuwa ushindi wote unatoka kwa Allah(s.w). Mazingira ya vita yaliwadhihirishia kuwa wingi wao haukuwasaidia chochote. Mwanzoni wengi wa Waislamu walisambaratishwa na maadui na kumuacha Mtume(s.a.w) na waumini wachache kwenye uwanja wa mapambano wakiwa wamezungukwa na jeshi kubwa la maadui.



Mtume(s.a.w) na waumini wachache aliokuwa nao walipigana kwa ujasiri wakiwa na yakini kuwa Allah(s.w) yuko pamoja nao. Waislamu waliokimbia walipokumbushwa kuwa wamemuacha Mtume wa Allah na waumini wachache kwenye uwanja wa vita, walitanabahi na kujitupa tena kwenye uwanja wa vita bila ya woga wowote kwa kutegemea radhi za Allah(s.w) peke yake. Walipofanya hivyo, Allah(s.w) aliwasaidia kwa kuwashushia jeshi la Malaika na wakapata ushindi mkubwa kwa namna ya ajabu kabisa.





                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Download App yetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1417

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰2 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰3 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰5 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Maandalizi ya Kimafunzo aliyoandaliwa Mtume Muhammad

(i) Suratul- β€˜Alaq (96:1-5)β€œSoma kwa jina la Mola wako aliyeumba Aliyemuumba mwanaadamu kwa β€˜alaq.

Soma Zaidi...
Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Nuhu(a.s)

(i) Tuanze kulingania kwa Tawhiid – kumjua Allah(s.

Soma Zaidi...
Maswali kuhusu Quran

Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa Mtume(s.a.w) na Kufariki kwake

Miezi miwili baada ya Hijjat-al-Wada, Mtume(s.

Soma Zaidi...
Mtume Muhammad s.a. w amelewa na Baba yake mdogo

Historia na sura ya Mtume Muhammad, sehemu ya 10.

Soma Zaidi...