Kuzuka Imani ya Kishia
Baada ya kuuwawa Ali(r.a), kundi la marafiki wa Ali(Shi’a Ali) lilianzisha imani mpya ya ushia. Walifuata itikaqadi iliyo buniwa na ‘Abdallah bin Sabaa kuwa Ali ni Mrithi wa Mtume(s.a.w) kama Haruna(a.s) alivyokuwa mrithi Musa(a.s). Hivyo kundi hili liliitaqidi kuwa Ali(r.a) ndiye aliyekuwa Khalifa halali pekee na kuwaona Abubakar, ‘Umar na Uthmani kuwa walikuwa madhalimu waliopora nafasi hiyo. Siku zilivyosonga mbele mashia waliandika vitabu vyao vya sheria, Hadith, Historia ya Uislamu na ufafanuzi wa Qur’an unaolandana na imani yao mpya. Kwa mujibu wa Imani ya kishia, kiongozi wa jamii lazima aweImam ambaye uteuzi wakeunatokana na Mtume(s.a.w).
Baada yakut awafu Mtume(s.a.w),kulingana na Imani ya kishia Uimamu ulimshukia Ali(r.a) kupitia kwa mkewe Fatma bint Muhammed(s.a.w). Baada ya kuuliwa Ali(r.a) Uimamu uliwashukia watoto wa kiume wa Fatma hadi akafikia Imam wa kumi na moja anayeitwa Hassan al-Askari ambaye alifariki 874 A.D./260 A.H. katika utawala wa Abasi, ambao Khalifa wake alikuwa Matamid. Alipofariki Imam Hassan al- Askari Uimam ulimshukia mwanae Muhammad anayejulikana kwa jina la Mahdi, Imam wa mwisho.
Tarekh ya maimamu wa nyumba ya Mtume (Ahlul-Bayt) inatatanisha. Inaaminika Baba yake Hassan alihamishwa kutoka Madinah na kupelekwa Summara na dikteta Mutawakkil aliyekuwa Khalifa wakati huo, aliwekwa kizuizini huko Summara hadi akafa. Hassan naye aliwekwa kizuizini na aliyechukua nafasi ya Mutawakkil, mtoto wa Hassan aliyekaribia umri wa miaka mitano alianza kumtafuta baba yake katika pango lililokuwa karibu ya nyumba yao. Mtoto huyu hakurudi kutoka pangoni. Tukio hili limewapelekea Mashia kujaa matumaini kuwa mtoto huyu atarudi kuja kuikoa dunia kutokana na mzigo wa madhambi na uonevu.
Mtindo huu haumo katika mfumo wa Uislamu ingawa wafuasi wake wanatumia jina la Uislamu. Kwa nini mtindo huu haumo katika Uislamu tumeshazitaja sababu zake kuwa utume haurithiwi ila hapa tunataka kuongezea kuwa Imani hii ambayo ilipandikizwa baadaye katika historia ya Uislamu ina mizizi ya dini ya Uzoroastrian na Ukristu, dini ambazo zote zinamshirikisha Mwenyezi Mungu.
Angalizo(Tanbih)
Kwa Waislamu hivi leo, mfumo wa usia kama wanavyofanya wafuasi wanaojiita Mashia si katika utaratibu unaokubalika katika Uislamu. Mtume hakulifanya, na hata Ali alipokuwa katika kitanda cha mauti baada ya kujeruhiwa aliulizwa na mtu mmoja kuwa Waislamu wampe mkono wa ahadi ya utii mwanae mkubwa, Hassan, awe Khalifa? Ali alijibu, “Nawaachia Waislamu waamue”. Au mfumo wa ufalme (Royal Family) kama ule wa Saudia Arabia, Moroko, Oman, Qatar au mfumo wa vyama vingi au kimoja kama Pakistan, Misri, Libya, Syria n.k. siyo mifumo ya Kiislamu na nchi zinazofuata mifumo hiyo si za Kiislamu.
Hivyo ni dhahiri wajumbe wa Shura katika dola ya Kiislamu wanalazimika kwa kushirikiana na kiongozi aliyepo madarakani kumteua anayefaa kuwa kiongozi kisha jina liwasilishwe kwa waumini kwa ajili ya kupitishwa au kukataliwa. Hivyo ni kweli kuwa jina linalotolewa na utaratibu unaotumika sasa wa chama kuteua mgombea katika chaguzi za Marais duniani kote ni mawazo yaliyoazimwa kutoka katika mfumo huu wa Kiislamu.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 772
Sponsored links
👉1
kitabu cha Simulizi
👉2
Madrasa kiganjani
👉3
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉4
Kitabu cha Afya
👉5
Simulizi za Hadithi Audio
👉6
Kitau cha Fiqh
Hawa ndio waaasi wakwanza wa Dola ya kiislamu wakati wa makhalifa
Soma Zaidi...
Tukio la kupasuliwa kifua Mtume Muhammad S.A.W
Sura na historia ya Mtume Muhammad S.A.W, sehemu ya 7 Soma Zaidi...
Khalifa ‘Umar bin Abdul Aziz
Soma Zaidi...
Mafunzo yatokanayo na maandalizi haya ya ki ilhamu
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Miujiza Kama Ushahidi wa Utume wa Nabii Musa(a.s)
Allah(s. Soma Zaidi...
Historia ya Vijana wa Pangoni
Makafiri wa Kiquraish walikuwa na tabia ya kumghasi Mtume(s. Soma Zaidi...
Waliomshambulia na kumuuwa Ali, makhawariji na si muawiya
Soma Zaidi...
Mtume Muhammad alelewa na mama yake mzazi akiwa na umri wa miaka 4.
Sura na historia ya Mtume Muhammad S.A.W sehemu ya 8. Hapa utajifunza malezi ya Mtume kutokakwa Halimavkuja kwa mama yake. Soma Zaidi...
Historia ya Vijana wa Pangoni
Makafiri wa Kiquraish walikuwa na tabia ya kumghasi Mtume(s. Soma Zaidi...
HISTORIA YA KUPASULIWA KWA KIFUA AU TUMBO CHA MTUME MUHAMMAD (S.A.W) AKIWA MTOTO KWA BI HALIMA
KUPASULIWA KWA KIFUA MTUMEWAKATI AKIWA MTOTO. Soma Zaidi...