Historia ya Kuzuka Imani ya Kishia waliodai kuwa ni wafuasi wa Ally

Historia ya Kuzuka Imani ya Kishia waliodai kuwa ni wafuasi wa Ally

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Historia ya Kuzuka Imani ya Kishia waliodai kuwa ni wafuasi wa Ally

Kuzuka Imani ya Kishia



Baada ya kuuwawa Ali(r.a), kundi la marafiki wa Ali(Shi’a Ali) lilianzisha imani mpya ya ushia. Walifuata itikaqadi iliyo buniwa na ‘Abdallah bin Sabaa kuwa Ali ni Mrithi wa Mtume(s.a.w) kama Haruna(a.s) alivyokuwa mrithi Musa(a.s). Hivyo kundi hili liliitaqidi kuwa Ali(r.a) ndiye aliyekuwa Khalifa halali pekee na kuwaona Abubakar, ‘Umar na Uthmani kuwa walikuwa madhalimu waliopora nafasi hiyo. Siku zilivyosonga mbele mashia waliandika vitabu vyao vya sheria, Hadith, Historia ya Uislamu na ufafanuzi wa Qur’an unaolandana na imani yao mpya. Kwa mujibu wa Imani ya kishia, kiongozi wa jamii lazima aweImam ambaye uteuzi wakeunatokana na Mtume(s.a.w).


Baada yakut awafu Mtume(s.a.w),kulingana na Imani ya kishia Uimamu ulimshukia Ali(r.a) kupitia kwa mkewe Fatma bint Muhammed(s.a.w). Baada ya kuuliwa Ali(r.a) Uimamu uliwashukia watoto wa kiume wa Fatma hadi akafikia Imam wa kumi na moja anayeitwa Hassan al-Askari ambaye alifariki 874 A.D./260 A.H. katika utawala wa Abasi, ambao Khalifa wake alikuwa Matamid. Alipofariki Imam Hassan al- Askari Uimam ulimshukia mwanae Muhammad anayejulikana kwa jina la Mahdi, Imam wa mwisho.


Tarekh ya maimamu wa nyumba ya Mtume (Ahlul-Bayt) inatatanisha. Inaaminika Baba yake Hassan alihamishwa kutoka Madinah na kupelekwa Summara na dikteta Mutawakkil aliyekuwa Khalifa wakati huo, aliwekwa kizuizini huko Summara hadi akafa. Hassan naye aliwekwa kizuizini na aliyechukua nafasi ya Mutawakkil, mtoto wa Hassan aliyekaribia umri wa miaka mitano alianza kumtafuta baba yake katika pango lililokuwa karibu ya nyumba yao. Mtoto huyu hakurudi kutoka pangoni. Tukio hili limewapelekea Mashia kujaa matumaini kuwa mtoto huyu atarudi kuja kuikoa dunia kutokana na mzigo wa madhambi na uonevu.


Mtindo huu haumo katika mfumo wa Uislamu ingawa wafuasi wake wanatumia jina la Uislamu. Kwa nini mtindo huu haumo katika Uislamu tumeshazitaja sababu zake kuwa utume haurithiwi ila hapa tunataka kuongezea kuwa Imani hii ambayo ilipandikizwa baadaye katika historia ya Uislamu ina mizizi ya dini ya Uzoroastrian na Ukristu, dini ambazo zote zinamshirikisha Mwenyezi Mungu.



Angalizo(Tanbih)



Kwa Waislamu hivi leo, mfumo wa usia kama wanavyofanya wafuasi wanaojiita Mashia si katika utaratibu unaokubalika katika Uislamu. Mtume hakulifanya, na hata Ali alipokuwa katika kitanda cha mauti baada ya kujeruhiwa aliulizwa na mtu mmoja kuwa Waislamu wampe mkono wa ahadi ya utii mwanae mkubwa, Hassan, awe Khalifa? Ali alijibu, “Nawaachia Waislamu waamue”. Au mfumo wa ufalme (Royal Family) kama ule wa Saudia Arabia, Moroko, Oman, Qatar au mfumo wa vyama vingi au kimoja kama Pakistan, Misri, Libya, Syria n.k. siyo mifumo ya Kiislamu na nchi zinazofuata mifumo hiyo si za Kiislamu.


Hivyo ni dhahiri wajumbe wa Shura katika dola ya Kiislamu wanalazimika kwa kushirikiana na kiongozi aliyepo madarakani kumteua anayefaa kuwa kiongozi kisha jina liwasilishwe kwa waumini kwa ajili ya kupitishwa au kukataliwa. Hivyo ni kweli kuwa jina linalotolewa na utaratibu unaotumika sasa wa chama kuteua mgombea katika chaguzi za Marais duniani kote ni mawazo yaliyoazimwa kutoka katika mfumo huu wa Kiislamu.





                   


Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1016

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Mtume amezaliwa mwaka gani?
Mtume amezaliwa mwaka gani?

Na tumemuusia mwanaadamu afanye wema kwa wazazi wake.

Soma Zaidi...
MJADALA JUU YA NDOA YA MTUME S.A.W NA BI KHADIJA (HADIJA)
MJADALA JUU YA NDOA YA MTUME S.A.W NA BI KHADIJA (HADIJA)

LAKINI UMRI WANGU MKUBWABaada ya kuwaza na kufikiri muda mrefu, bibi Khadija (Radhiya Llahu anha) akafikia uamuzi wa kutaka kuolewa na Muhammad (Swalla Laahu alayhi wa sallam).

Soma Zaidi...
Historia ya Firaun, Qarun na Hamana
Historia ya Firaun, Qarun na Hamana

Karun na Hamana waliishi zama za Mtume Musa(a.

Soma Zaidi...
Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Salih(a.s)
Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Salih(a.s)

Mafunzo tuyapatayo hayatofautiani na yale yatokanayo na Historia ya Nabii Hud(a.

Soma Zaidi...
Kusilimu kwa Wachawi wa Firaun
Kusilimu kwa Wachawi wa Firaun

Mawaziri waliokuwa washauri wakuu wa Firauni wakataka wakusanywe magwiji waliobobea katika uchawi nchi nzima, kisha wapambanishwe na Nabii Musa(as).

Soma Zaidi...
Njama za Kumuua Nabii Yusufu(a.s)
Njama za Kumuua Nabii Yusufu(a.s)

Kwa tabia zake njema Yusufu(a.

Soma Zaidi...