Fahamu vitamini C na kazi zake, vyakula vya vitamini C na athari za upungufu wake.

kuhusu vitamini C, kuanzia chanzo chake, maana yake, upungufu wake na kazi zake kwenye miili yetu.

Fahamu vitamini C na kazi zake, vyakula vya vitamini C na athari za upungufu wake.



VYAKULA VYA VITAMINI C

Vitamini C ni katika vitamini muhimu sana katika mfumo wa kinga mwilini. Vitamini hivi vina sifa ya antioxidant. Antioxidant zenyewe ndani ya mwili ndizo ambazo husaidia kuupa mwili nguvu na kinga ya kupamba na na sumu, na vijidudu shambulizi. Vvitamini C ina pendelewa kuwepo ndani ya miili yetu kwa wingi muda wowote. Wapo wataalamu wa afya wanapendekeza kutumia vitamini C kwa ajili ya kupunguza uwezekeno wa kupata mafua na homa ya mafua mara lkwa mara. Katika makala hii nimekuandalia somo zima kuhusu vitamini C, kuanzia chanzo chake, maana yake, upungufu wake na kazi zake kwenye miili yetu.



YALIYOMO:

  1. Maana ya vitamini C
  2. Vyakula vya vitamini C
  3. Kazi zake mwilini
  4. Dalili za upungufu wa vitamini C
  5. Maradhi yaletwayo na upungufu wa vitamini c
  6. Athari za kuwa na vitamini C kupitiliza
  7. Ugonjwa wa Kiseyeye


Maana na Historia ya vitamini C

Vitamini C kitaalamu pia hufahamika kama โ€œascobic acidโ€ ama ascorbate. Vitamini C ni katika water soluble vitamini ambayo husaidia kukinga mwili dhidi ya maradhi ya kiseyeyee au kitaalamu scurvy. Ni maradhi hatari sana yanayodhurua afya. Kwa maelezo zaidi ya maradhi haya enelea kusoma makala hii.



Vitamini C vimegunduliwa miaka ya 1920 na Mwanasayansi aliyejulikana kwa jina la Albert von Szent Gyรถrgyi. Pia itambulike kuwa hapo mwanzo mwanasayansi aliyejulikana kwa jina la Kazimierz Funk yeye alieleza kuwa kuna maradhi yanasababishwa na upungufu wa virutubisho mwilini. Katika maradhi hayo aliyoyataja ugonjwa uitwao scurvy yaani kisehehe aliupa virutubicho kwa herufi C.



Baada ya ugunduzi wa Albert von Szent na haworth wakaipa herufi C kemikali iitwayo ascobic acid. Na hii ndiyo vitamini C. hivyo herufi C kwenye vitamini C ina maana ascobic acid hii ni tindikali. Wataalamu wa afya wanatueleza kuwa wanyama katu hawawezi kuishi bila ya vitamini C mwilini mwao.Vitamini C ndio vitamini vya kwanza kuweza kutengenezwa na binadamu kikemikali.



VYAKULA VYA VITAMINI C

Kwa kuwa tumeshajuwa sasa maana na historia ya vitamini C hapa nitakwenda kukueleza chanzo cha vitamini C na je ni katika vyakula vipi tunapata vitamini C. kwa ufupi wa somo ni kuwa vitamini C unaweza kuvipata kwenye matunda yenye ladha ya uchachu uchachu (citrus) na matunda vyenye rangi ya njano na kwenye mboga za majani



Vyakula vya vitamini c

  1. Pera
  2. Pilipili
  3. Papai
  4. Chungwa
  5. Limao/ndimu
  6. Zabibu
  7. Nanasi
  8. Pensheni
  9. Kabichi
  10. Embe
  11. Nyanya
  12. Tunguja
  13. Palachichi
  14. Kitunguu
  15. Karoti
  16. Epo


Tofauti na mboga za majani na matunda ya uchachu na yenye rangi ya njano pia tunaweza kupata vitamini C kwa kula maini, maziwa na mayai. Pia unaweza kupata vitamini C kwa kumezaa vidonge vya vitamini C.



KAZI ZA VITAMINI C MWALINI

Kama tulivyowkisha kuona kuwa vitamini C hulunda mwili dhidi ya mashambulizi na sumu za vyakula. Pia basi vitamini C husaidia katika kulinda mwili dhidi ya magonjwa mbalimbali kma kiseyeye, magonjwa ya ngozi, mifupa na moyo. Katika kipengele hiki utakwenda kuona kwa undani zaidi kuhusu kazi hizi za vitamini c mwilini:



Kazi kuu tatuza vitamini C

  1. Husaidia katika utengenezwaji wa collagen hizi ni protini ambazo huhusika katika utengenezwaji wa tishu kitaalamu zinazotambulika kama connective tissue na pia husaidia katika uponaji wa vidonda na majeraha. Mtu mwenye upungufu wa vitamini C vidonda vyake vitachelewa sana kupona ukilinganisha na mwenye vitamini C vya kuatosha.


Tishu hizi ndizo ambazo zilitupa umbo letu, kwa lugha nyepesi hizi nyama zinazoonekana kwenye miili yetu, zilizofunika mbavu, mifupa, magoti, kichwa na maeneo yote ya mwili. Tishu hizi pia zinapatikana kwenye viungio vya miili yetu. Mifupa laini ya kwenye viungio vyetu pia ni katika tishu hizi. Hivyo protini huhusika katika utengenezwaji wa hizi tishu.



  1. Vitamini C ni antioxidant katika miili yetu antioxidanti hufanyakazi ya kulinda miili dhidi ya mipambano ya kikemikali ya melecule ndani ya miili yetu.. Antioxidant ni chembechembe za kikemikali ambazo husaidia katika uuguzwaji wa oksijeni mwilini. Husaidia kuzui antioxidant hupunguza sumu za vyakula wilini. Miili yetu inahitaji antioxidant ili iweze kujilinda na kuwa madhubuti. Zipo antioxidant nyingia mbazo tunaweza kuzipata kwa vyakula. Mifano hiyo ni:-
  • Caroteese ambayo tunaweza kuipata kwenye karot.
  • Vitamini E
  • Vitamini C
  • Uric acid


  1. Husaidia katika uupa mfumo wa kinga nguvu na uwezo wa kuulinda mwili dhidi ya mashambulizi na uvamizi dhidi ya maradhi.


Kazi nyingine za vitamini C

  1. Hulinda mwili dhidi ya maradhi ya kiseyeye (scurvy):


Ugonjwa wa kiseyeye (scurvy)

Ugonjwa wa kiseyeye husababishwa na upungufu wa vitamini C na kutibiwa kwa kupata vitamini C aidha kwa kutumia vyakula ama vidonge vya vitamini C. dalili za ugonjwa huu huanza kutokea mwezi mmoja toka upungufu wa vitamini C uanze kutokea mwilini.



Dalili za ugonjwa wa kiseyeye:

  1. Kushindwa kuhema vizuri
  2. Maumivu ya mifupa
  3. Mafinzi kutoka damu
  4. Uponaji ulio hafifu wa vidonda
  5. Homa
  6. Mwili kukosa nguvu
  7. Maumivu ya misuli na viungio
  8. Kifo




  1. Kulinda mwili zidi ya maambukizi na mashambulizi:

Tafiti mbalimbali zilizofanya zinaonesha kuwa vitamini C inaweza kusaidia kupunguza nguvu za virusi waletao mafua na homa ya mafua. Baadhi ya tafiti zinadiriki kusema kuwa vitamini hivi kuponyesha mafua yaa kwa haraka, lakini ambalo halina shaka ni kuwa vitamini c vinaweza kupunguza kupata mafua ya mara kwa mara au kufanya mafua yaondoke kwa haraka.



Vitamini C ni muhimu sana katika mfumo wa kinga mwilini. Kwani vitamini C husaidia katika Antimicrobial yaani katika kuzuia vijidudu shambulizi mwilini kama bakteria na virusi, pia vitamini C husaidia katika Natural killer cell yaani katika kuuwa vijidudu shambulizi ama kuvizuia visiendelee kukua mwilini, pia vitamini C husaidia katika kuimarisha mfumo wa kinga kwa kuimarisha seli hai nyeupe ziitwazo lymphocyte hizi ndizo seli ambazo askari mkuu wa mwili dhidi ya vimelea vya maradhi kama virisi, fangasi, protozoa na bakteria.



  1. Kulinda miili yetu dhidi ya saratani (cancer):

Tafiti mbalimbali zimefanywa kuhusu aina ya saratani na zinavyohusiana na vitamini C kama saratani ya matiti na mapafu. Ijapokuwa tafiti hizi hazikuweza kuthibitisha moja kwa moja kuwa vitamini C vinasaidia kuondoa saratani hizi kalaki kuna mambo ambayo tafiti hizi yametufungua mawazo:

  1. Vitamini C husaidia kuborsha afya na kuishi vyema kwa wagonjwa wa saratani
  2. Vitamini C inaweza kuuwa seli zinazotengeneza uvimbe wa saratani


  1. Husaidia kulind miili yetu dhidi ya maradhi yanayohusu mishipa ya damu na moyo (cardiovascular)
  2. Husaidia kulinda miili yetu dhidi ya maradhi ya ubongona kusahasahau


UPUNGUFU WA VITAMINI C

Endapo kutatokea upungufu wa vitamini C mwilini kuna athari kubwa itakayotokea mwilini ikiwemo:

  • Kupata ugonjwa wa kiseyeye
  • Kuchelewa kupona kwa vidonda
  • Kutokwa na damu kwenye mafinzi
  • Maumivu ya mifupa
  • Maumivu ya misuli na viungio


ATHARI ZA KULA VITAMINI C KUPITILIZA

Kila kirutibisho kinahitajika ndani ya miili yetu kwa kiwango maalumu. Endapo kirutubisho kitakuwa kingi kupitiliza athari zinaweza kutokea katika afya ya mtu. Miongoni mwa athari za kuwa na vitamini C kupitiliza ni kama zifuatazo:-

  • Kichefuchefu
  • Maumivu ya tumbo
  • Kuharisha
  • Kufanyika kwa vijiwe ndani ya figo
  • Kujaa kwa tumbo


Mwisho

Kwakuwa sasa unatambua umuhimu wa vitamini C ndani ya mwili wako. Hakikisha kula vyakula vyema ili kusaidia katika kuboresha afya yako. Endelea kuwa pamoja na si kwa makala nyingine za Afya.



MAKALA NYINGINE ZINAZOHUSU:

  1. Vyakula vya Vitamini na faida zake
  2. Afya ya uzazi
  3. magonjwa na Afya
  4. Kitabu cha matunda
  5. Dondoo 100 za Afya


                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Vyakula Main: Afya File: Download PDF Views 4131

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰2 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰3 Madrasa kiganjani    ๐Ÿ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Faida za kiafya za kula nyama

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula nyama

Soma Zaidi...
Faida za ubuyu

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula ubuyu

Soma Zaidi...
NI ZIPI KAZI ZA PROTINI MWILINI?

Makala hii inakwenda kukuletea kazi kuu za protini na vyakula vya protini katika miili yetu. Mkala hii itakusaiidia kujuwa namna ya kupangilia lishe yako kiusalama zaidi baada ya kujuwa kazi za protini katika miili yetu.

Soma Zaidi...
Faida za kafya za kula asali

Post hii itakwenda kukufundisha faida za kiafya za kula asali

Soma Zaidi...
Faida za kula tikiti

Somo hili linalenga kukujuza juu ya umuhimu wa tikiti kwenye afya ya mwili

Soma Zaidi...
Vyakula muhimu kwa kulinda afya ya macho - Epuka upofu kwa kula vyakula hivi

Matatizo ya macho yanaweza kuruthiwa kutoka kwa wazazi kwenda kwa mtoto. hata hivyo shughuli zetu na vyakula tunavyokula vinaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa matatizo haya. Hapa nitakuletea vyakula muhimu kwa afya ya macho yako.

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kula magimbi/ taro roots

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula magimbi

Soma Zaidi...
Vijuwe vyakula vya madini na kazi za madini mwilini

Post hii inakwenda kukieleza kuhusu vyakula vya madini na kazi zake mwilini

Soma Zaidi...