Mafundisho ya Mitume

Mafundisho ya Mitume

Mafundisho ya mitume ni eneo lingine linalo thibitisha kuwepo Allah (s.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Mafundisho ya Mitume

Mafundisho ya Mitume


Mafundisho ya mitume ni eneo lingine linalo thibitisha kuwepo Allah (s.w).Dalili zinazodhihirisha kuwepo Allah (s.w) katika eneo hili ni pamoja na:



(a)Umoja wa ujumbe wa mitume



(b)Mafundisho yao kutoathiriwa na mazingira ya jamii zao



(c)Upeo wa elimu waliyokuwa nayo mitume.

Kitu kinachodhihirisha kuwa Mitume ambao baadhi yao ulimwengu mzima una shuhudia historia yao, kama vile historia ya Nabii Ibrahim (a.s), Musa (a.s), Isa (a.s) na Muhammad (s.a.w) kuwa ni wajumbe kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w) wenye ujuzi na hekima, ni kule kufanana kwa ujumbe wao.


Kama dhana ya kutokuwepo Mwenyezi Mungu (s.w) ingelikuwa kweli, ingelikuwa muhali kwa Mitume waliotokea sehemu tofauti nyakati tofauti, kutoa ujumbe unaofanana. Turejee katika Qur-an mifano michache ya mafundisho ya msingi waliyotoa Mitume kwa watu wa o:Tulipompeleka Nuhu kwa watu wake, naye akasema: “Enyi watu wangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu.


Nyinyi hamna Mungu ila Yeye.Hakika mimi ninakuhofieni adhabu ya siku (hiyo) iliyo kuu ”. (7:59).Na kwa Adi (tulimpeleka) ndugu yao Hudi, akasema: “Enyi kaumu yangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu, nyinyi hamna Mungu ila Yeye. Basi hamuogopi? (7:65).


Na kwa thamud (tulimpeleka) ndugu yao, Saleh. Akasema “Enyi watu w angu! Muabuduni Mwenyezi Mungu, nyinyi hamna Mola ila Yeye. Hakika umekwisha kukufikieni muujiza ulio dhahiri kutoka kwa Mola wenu. Huyu ni ngamia jike wa Mwenyezi Mungu aliye na ishara kwenu (ya Utume wangu).


Basi muacheni ale katika ardhi ya Mungu, wala msimtie katika dhara yoyote, isije ikakushikeni adhabu iumizayo. (7:73).


(iv) Shu’ayb (a.s)
Na kwa watu wa Madyan (tulimpeleka) ndugu yao, Shu’ayb, akasema:


‘Enyi kaumu yangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu, hamna Mungu mwingine isipokuwa Yeye. Zimekwisha kufikieni hoja dhahiri kutoka kwa Mola wenu. Basi kamilisheni sawa sawa vipimo (vya vibaba) na mizani (pia) wala msiwapunguzie watu vitu vyao wala msifanye uharibifu katika ardhi badala ya kutengenea kwake. Hivi ndivyo bora kwenu ikiwa nyinyi mumeamini. (7:85).


Na hakika Mwenyezi Mungu ni Mola wangu na Mola wenu. Basi muabuduni. Hii ni njia iliyonyooka. (19:36)
(vi) Muhammad (s.a.w)



Sema (ewe Muhammad): “Enyi watu! Hakika mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu nyinyi nyote; (Mungu) ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi, hakuna aabudiwaye (kwa haki) ila yeye, yeye ndiye ahuishaye na ndiye afishaye.Basi muaminini Mwenyezi Mungu na Mtume wake, aliye Nabii Ummiyyi (asiyejua kusoma wala kuandika) ambaye humuamini Mwenyezi Mungu na maneno yake. Na mfuateni yeye ili mpate kuongoka”. (7:158)


“Na bila shaka tulimpeleka mtume katika kila umma ya kwamba, “Muabuduni Mwenyezi Mungu na mwepukeni twaghuti. Basi wako miongoni mwao ambao Mwenyezi Mungu amewaongoa na wako miongoni mwao ambao upotofu umethubutu juu yao. Basi tembeeni katika ardhi na mwangalie ulikuwaje mwisho wa wale waliokadhibisha ”. (16:36)
Ukirejea katika Qur-an utaona kuwa Mitume wote kwa ujumla wamefundisha yafuatayo:-



(i)Tawh iid
Wamewafundisha watu juu ya kuwepo Allah (s.w) na upweke wake kwa kuwaonyesha dalili zilizo waziwazi.



(ii)Lengo
Waliwafundisha watu kuwa lengo la kuumbwa kwao ni kumuabudu Allah (s.w) na kusimamisha ukhalifa wake hapaulimwenguni na kisha waliwafundisha namna ya kumuabudu Mola wao katika kila kipengele cha maisha.



(iii)Kubashiria
Waliwabashiria watu malipo mema ya kudumu ya huko Peponi kwa wale watakaoamini vilivyo na kutenda mema katika maisha yao ya hapa duniani.



(iv)Kuhofisha
Waliwahofisha watu juu adhabu kali watakayopata huko Akhera wale watakao mkufuru Allah (s.w) na kumwabudu twaghu ti.




                   


Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 1648

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Nguzo za imani
Nguzo za imani

Zifuatazo ni nguzo za imani (EDK form 2: elimu ya dini ya kiislamu)

Soma Zaidi...
Elimu ya mwingozo na elimu ya mazingira katika uislamu
Elimu ya mwingozo na elimu ya mazingira katika uislamu

Mahusiano kati ya elimu ya mwongizo na elimu ya mazingira katika uislamu.

Soma Zaidi...
Athari za kumuamini mwenyezi Mungu katika maisha ya kila siku
Athari za kumuamini mwenyezi Mungu katika maisha ya kila siku

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mafundisho yao kutoathiriwa na mazingira ya jamii zao
Mafundisho yao kutoathiriwa na mazingira ya jamii zao

Takriban Mitume wote walitokea katika jamii zilizozama katika ujahili, lakini kamwe ujumbe wao haukuathiriwa na mitazamo ya ujahili kwa ujumla, walahawakuingizautamaduni wa kijahili katika dini ya Allah (s.

Soma Zaidi...
Kwa namna gani nabii Musa na Bi Mariam waliweza kuzungumza na Allah nyuma ya pazia
Kwa namna gani nabii Musa na Bi Mariam waliweza kuzungumza na Allah nyuma ya pazia

Nabii Musa na Mama yake nabii Isa bi Mariam waliweza kuwasiliana na Allah nyuma ya pazia.

Soma Zaidi...
Kujiepusha na kukaribia zinaa
Kujiepusha na kukaribia zinaa

Si zinaa tu iliyoharamishwa bali hata yale yote yanayotengeneza mazingira na kuchochea kufanyika kwa zinaa nayo pia yameharamishwa.

Soma Zaidi...
mitume
mitume

Labda itaulizwa: Kwanini Mtume Muhammad (s.

Soma Zaidi...
Ni ipi maana ya Imani katika Uislamu, na ni zipi sifa za muumini.
Ni ipi maana ya Imani katika Uislamu, na ni zipi sifa za muumini.

Katika Uislamu imani inanguzo kuu 6.Pia muumini anatakiwa ajipambe na sifa za waumini. Posti hii itakufundisha kuhusu imani katika Uislamu.

Soma Zaidi...