Umuhimu wa kutumia dawa za kujikinga na maambukizi ya ukimwi
Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kutumia dawa za kujikinga na maambukizi ya ukimwi, ni faida ambazo upatikana kwa watu wanaodhani wameambukizwa na virus vya ukimwi na kuweza kujikinga.
Faida za kutumia dawa za kujikinga na maambukizi ya ukimwi.
1. Kwanza kabisa wanaweza kujua afya zao wakoje, kwa sababu mtu akija kupewa dawa hizi ni lazima awe amepima kama ana maambukizi kama Hana anapewa dawa kwa kipindi cha mwezi mmoja au siku ishilini na nane na kama amekutwa na maambukizi anaendelea na dawa kama wateja wengine, kwa hiyo ni vizuri kwa sababu usaidia mtu kuja hali ya afya zao.
2. Inawasaidia wahudumu wa afya na watu wengi kuwa macho kuhusu maambukizi ya ukimwi, kwa sababu watu wanakua kuwa maambukizi yapo na wanakuwa macho kujikinga na ugonjwa huo na mara nyingi utawakuta wamevaa gloves Ili kujikinga.
3. Kuwasaidia wakina Mama wajawazito kutowaambukiza watoto wao kwa sababu dawa za kuzuia maambukizi utumiwa na akina Mama Ili kuzuia mtoto asipate akiwa tumboni , anapozaliwa na wakati wa kunyonya kwa hiyo ni vizuri kabisa dawa hizi zitumike, hasa kwa wahudumu wa afya walio wajawazito wanapaswa kuwa makini na kupima mara kwa mara kwa sababu ya usalama wa watoto walioko tumboni.
4. Kwa hiyo ni vizuri kabisa kwa wahudumu wa afya na watu wote walio kwenye hatari za kupata maambukizi ya ukimwi kupima mara kwa mara Ili kuweza kujua afya zao na kwa sababu ya mazingira yao, kwa mfano wanaofanya biashara za ngono,wanaovuta sigara kwa kutumia sindano Moja kwa watu zaidi ya mmoja na sindano hiyo utunzwa kwa matumizi ya siku nyingine, wanaume wanaojamiiana na wanaume wengine,wafungwa, watu wanaoishi kwenye kambi za wakimbizi. Wote Hawa wako kwenye hatari ya kupata ugonjwa wa ukimwi upimaji wa afya ni muhimu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 ai web app 👉5 web hosting 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Namna ya kuyatunza macho
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ya kuyatunza macho
Soma Zaidi...binadam akiwa mweupe mikononi atakuwa na upungufu wa vitamin gani?
Natak kufaham kuwa binadam akiwa mweupe mikononi atakuwa na upungufu wa vitamin gani?
Soma Zaidi...Upungufu wa damu wa madini (anemia ya upungufu wa madini)
upungufu wa damu wa madini ya chuma ni aina ya kawaida ya upungufu wa damu hali ambayo damu haina chembe nyekundu za damu zenye afya. Seli nyekundu za damu hubeba oksijeni kwa tishu za mwili. Bila chuma cha kutosha, mwili wako hauwezi kutoa dutu ya k
Soma Zaidi...Chanjo zinazotolewa nchini Tanzania
Posti hii inahusu zaidi chanjo ambazo utolewa nchini Tanzania, ni chanjo ambazo uzuia Magonjwa ambayo yako katika sehemu mbalimbali za nchi.
Soma Zaidi...Je, utamsaidia vipi mtu aliyeumwa na nyuki?
Posti hii inazungumzia kuhusiana na kumsaidia mwenye aliyeumwa na nyuki.nyuki na wadudu ambao wakikushambulia Sana na ukikosa msaada unaweza kufa au kuwa katika Hali mbaya.
Soma Zaidi...Zijue sehemu za mwili zinazochomwa chanjo.
Posti hii inahusu zaidi sehemu ambazo zinapaswa kudungwa chanjo, hizi ni sehemu zile zilizopendekezwa kwa ajili ya kuchoma chanjo kwa kadiri ya kazi ya chanjo.
Soma Zaidi...