Umuhimu wa kutumia dawa za ARV
Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kutumia dawa za ARV kwa wathirika wa virusi vya ukimwi .pia tutangalia kwa undani mambo ya kuzingatia kwa wathirika wanaotumia ARV .pamoja na kujali watu wanaotumia dawa hizo .
Umuhimu wa kutumia dawa za " ARV" kwa wathirika wa VVU.
- Kutokana tulivyoeleza apo juu kuhusu umuhimu au matumizi kwa watu wanaotumia dawa za "ARV" .ambazo ni dawa za kupunguza makali ya virusi vya ukimwi .dawa hizi utakuwa kutumia kwa usahihi.mtu anayeishi na virusi vya ukimwi hutumia dawa hizi kwa maisha yake yote.Endapo mwathrika ataacha kutumia dawa hizo ,anaweza kupata madhara zaidi kama vile kufhoofu kiafya ,magonjwa nyemelezi na kifo ARV haziui virusi bali hufubaza virusi na kupunguza kasi ya kuongezeka.dawa hizi ufanya kinga ya mwili kuimarika.jukumu la kumwanzishia mwathrika dawa za kupunguza makali ya VVU ni la kitabibu mkwa hiyo,kuna umuhimu wa kupinda afya ili kukua hali halisi ya afya zetu.
- Huwaondolea wathirika wa VVU mateso ya kushambuliwa na maradhi nyemelezi ..maradhi nyemelezi ni kama .saratani ,kifua kikuu,fangasi,kuharisha na homa kali ya mapafu
- Huimarisha afya za wanaoishi na VVU. Kutokana na ilo watu wenye virusi vya ukimwi afya zao huwa vizuri kama vile watu wasio na ugonjwa wa UKIMWI. Hivyo hivyo mtu anaetumia hizi dawa inabidi awe anafanya sana mazoezi ya mwili .ili kuweza kulinda seli zake ziweze kufanya kazi.
- Wathirika wa VVU wanaweza kuishi maisha ya kawaida na kushiriki shughuli zao za kiuchumi na kukiongizia kipato.kutokana na hilo watu wanaotumia hizi dawa wanauwezo wa kuongoza maisha yao ya kila siku
5. Hupunguza kasi ya kuzaliana kwa wingi kwa VVU.hata hivyo hurefusha maisha.
. Mambo ya kuzingatia kwa waathrika wanaotumia "ARV"
Kama tulivyoona apo mwanzo wathirika wa VVU ni kundi linaloitaji kuishi kwa kufuata taratibu zilizoainishwa na watahalamu wa afya.mambo ya kuzingatia ni kama yafuatayo.
1.waathirika ni lazima wafuate ushauri wa kitaalamu wa kitibabu au watahalamu wa afya.
2.waathrika wanapaswa kutumia ARV kwa dozi sahii na kwa muda sahii .dawa zitumike kama ilivyoelezwa na daktari au mtaalamu wa afya .hii itasaidia kuboresha afya na kupunguza uwezekano wa VVU kuwa sugu kwa dawa zinazotumika.
3.waathrika wachukue tahadhari kwa kujikinga ili wasipate maambukizi mapya na kuambukiza wengine.ili kuondoa idadi ya maambukizi katika jamii.
4.mwathirika asiache kutumia dawa kwa muda na kisha kurudia tena dawa hizo bila ushauri wa daktari au mtaalamu wa afya.
5.waathirika wa VVU watoe taarifa kwa daktari au watoe huduma kuhusu matatizo na athari za "ARV" endapo zitajitokeza.
6.waathirika waepuke kufuata imani na mila potofu za jadi au za dini zinazozuia kuwa mfuasi mzuri wa ARV
7.waathirika wafuate ratiba ya kwenda kiliniki ya dawa za "ARV" bila kukosa ili kupata ushauri nasaa.
8.waathrika wazingatie ushauri kanuni za afya kwa mfano ,kuzingatia usafi wa mwili,lishe bora na mazingira safi.
9.waathirika wanashauriwa kuendelea kuishi kwa matumaini na wasikate tamaa .
10.mtumiaji wa "ARV" harusiwi kishirikiana dawa zake na mtu mwingine.
jinsi watu wanaotumia dawa za "ARV"
1. Wathirika wa VVU wanaotumia ARV wanahitaji kuthaminiwa katika jamii zao na kuwaona kama watu wengine bila kuwabuguzi na kuwatenga.ili kuwajali watu wanaotumia dawa hizo.ni muhimu sana kuwasaidia pale wanapoitaji msaada.
2.pia kuambatana nao wanapoitaji kuaindikizwa kwenda kiliniki kuchukua dawa zao.pia inabidi tuwafaliji wajione na wenyewe kama watu wengine wanapoitaji huduma hizo.
3.tuwasaidie wanapoitaji kuelekezwa matumizi sahihi ya " ARV" ili wasiweze kwenda kinyume badae wasije kupata athari zozote katika jamii zetu.
4.kuwapatia chakula bora na kwa wakati.pia inabidi tuwandalie chakula chenye kuwaongezea vitamin ndani ya mwili wao.ili waweze kuijenga miili ya sawa .chakula lazima kiwekwe kwenye mazingira masafi na yenye virutubisho.kifunikwe na kisiwe cha balidi sana.
5.kuwakumbusha muda sahihi wa kumeza dawa pale wanaposahau.
6.kuwahamasisha kuendelea na matumizi ya dawa.
7.kuepuka kuwanyanyapaa walioathirika na VVU.pia ni muhimu sana kuzingatia na kufuata ushauri unaotolewa na daktari au mtaalamu wa afya kwa ktumiaji hi wa ARV .
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 web hosting 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Fahamu dawa ya captopril katika matibabu ya magonjwa ya moyo
Post hii inahusu zaidi dawa ya captopril katika matibabu ya magonjwa ya moyo, ni dawa ambayo imo kwenye kundi la vasodilators na ufanya Kazi mbalimbali zinazousu magonjwa ya moyo.
Soma Zaidi...Njia zinazotumika Ili kumpatia mgonjwa dawa
Posti hii inahusu zaidi njia kuu nne ambazo utumika kumpatia mgonjwa dawa, Ili kumpatia mgonjwa dawa Kuna njia za kutumia kama ifuayavyo.
Soma Zaidi...Dawa ya penicillin ambayo uzuia asidi ya bakteria.
Post hii inahusu zaidi dawa ya phenoxy-methyl penicillin ambayo upambana na aina ya bakteria ambao utoa sumu Ili kuzuia dawa isifanye kazi.
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu dawa za kifua kikuu
Post hii inahusu dawa za kifua kikuu ni dawa ambazo utumika kutibu kifua kikuu, kwanza kabisa kabla ya kuanza kufahamu dawa hizo ni vizuri kabisa kufahamu kifua kikuu nini hili kuweza pia kufahamu dawa zake.
Soma Zaidi...