picha

Umuhimu wa kutumia dawa za ARV

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kutumia dawa za ARV kwa wathirika wa virusi vya ukimwi .pia tutangalia kwa undani mambo ya kuzingatia kwa wathirika wanaotumia ARV .pamoja na kujali watu wanaotumia dawa hizo .

 Umuhimu wa kutumia dawa za " ARV" kwa wathirika wa VVU.

  1. Kutokana tulivyoeleza apo juu kuhusu umuhimu au matumizi kwa watu wanaotumia dawa za "ARV" .ambazo ni dawa za kupunguza makali ya virusi vya ukimwi .dawa hizi utakuwa kutumia kwa usahihi.mtu anayeishi na virusi vya ukimwi hutumia dawa hizi kwa maisha yake yote.Endapo mwathrika ataacha kutumia dawa hizo ,anaweza kupata madhara zaidi kama vile kufhoofu kiafya ,magonjwa nyemelezi na kifo  ARV haziui virusi bali hufubaza virusi na kupunguza kasi ya kuongezeka.dawa hizi ufanya kinga ya mwili kuimarika.jukumu la kumwanzishia mwathrika dawa za kupunguza makali ya VVU ni  la kitabibu mkwa hiyo,kuna umuhimu wa kupinda afya ili kukua hali halisi ya afya zetu.     
  2. Huwaondolea wathirika wa VVU mateso ya kushambuliwa na maradhi nyemelezi ..maradhi   nyemelezi ni kama .saratani ,kifua kikuu,fangasi,kuharisha na homa kali ya mapafu
  3. Huimarisha afya za wanaoishi na VVU.   Kutokana na ilo watu wenye virusi vya ukimwi afya zao huwa vizuri kama vile watu wasio na ugonjwa wa UKIMWI. Hivyo hivyo mtu anaetumia hizi dawa inabidi awe anafanya sana mazoezi ya mwili .ili kuweza kulinda seli zake ziweze kufanya kazi.
  4. Wathirika wa VVU wanaweza kuishi maisha ya kawaida na kushiriki shughuli zao za kiuchumi na kukiongizia kipato.kutokana na hilo watu wanaotumia hizi dawa wanauwezo wa kuongoza maisha yao ya kila siku 

        5. Hupunguza kasi ya kuzaliana kwa wingi kwa VVU.hata hivyo hurefusha maisha.

      .  Mambo ya kuzingatia kwa waathrika wanaotumia "ARV"

Kama tulivyoona apo mwanzo wathirika wa VVU ni kundi linaloitaji kuishi kwa kufuata taratibu zilizoainishwa na watahalamu wa afya.mambo ya kuzingatia ni kama yafuatayo.

1.waathirika ni lazima wafuate ushauri wa kitaalamu wa kitibabu au watahalamu wa afya.

2.waathrika wanapaswa kutumia ARV kwa dozi sahii na kwa muda sahii .dawa zitumike kama ilivyoelezwa na daktari au mtaalamu wa afya .hii itasaidia kuboresha afya na kupunguza uwezekano wa VVU kuwa sugu kwa dawa zinazotumika.

3.waathrika wachukue tahadhari kwa kujikinga ili wasipate maambukizi mapya na kuambukiza wengine.ili kuondoa idadi ya maambukizi katika jamii.

4.mwathirika asiache kutumia dawa kwa muda na kisha kurudia tena  dawa hizo bila ushauri wa daktari au mtaalamu wa afya.

5.waathirika wa VVU watoe taarifa kwa daktari au watoe huduma kuhusu matatizo na athari za "ARV" endapo zitajitokeza.

6.waathirika waepuke kufuata imani na mila potofu za jadi au za dini zinazozuia kuwa mfuasi mzuri wa ARV 

7.waathirika wafuate ratiba ya kwenda kiliniki ya dawa za "ARV" bila kukosa ili kupata ushauri nasaa.

8.waathrika wazingatie ushauri kanuni za afya kwa mfano ,kuzingatia usafi wa mwili,lishe bora na mazingira safi.

9.waathirika wanashauriwa kuendelea kuishi kwa matumaini na wasikate tamaa .

10.mtumiaji wa "ARV" harusiwi kishirikiana dawa zake na mtu mwingine.

      jinsi watu wanaotumia dawa za "ARV"

1. Wathirika wa VVU wanaotumia ARV wanahitaji kuthaminiwa katika jamii zao na kuwaona kama watu wengine bila kuwabuguzi na kuwatenga.ili kuwajali watu wanaotumia dawa hizo.ni muhimu sana kuwasaidia pale wanapoitaji msaada.

2.pia kuambatana nao wanapoitaji kuaindikizwa kwenda kiliniki kuchukua dawa zao.pia inabidi tuwafaliji  wajione na wenyewe kama watu wengine wanapoitaji huduma hizo.

3.tuwasaidie wanapoitaji kuelekezwa matumizi sahihi ya  " ARV" ili wasiweze kwenda kinyume badae wasije kupata athari zozote katika jamii zetu.

4.kuwapatia chakula bora na kwa wakati.pia inabidi tuwandalie chakula chenye kuwaongezea vitamin ndani ya mwili wao.ili waweze kuijenga miili ya sawa .chakula lazima kiwekwe kwenye mazingira masafi na yenye virutubisho.kifunikwe na kisiwe cha balidi sana.

5.kuwakumbusha muda sahihi wa kumeza dawa pale wanaposahau.

6.kuwahamasisha kuendelea na matumizi ya dawa.

7.kuepuka kuwanyanyapaa walioathirika na VVU.pia ni muhimu sana kuzingatia na kufuata ushauri unaotolewa na daktari au mtaalamu wa afya kwa ktumiaji hi wa ARV .

 

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/08/12/Friday - 11:36:09 am Topic: Dawa Main: Afya File: Download PDF Views 3948

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Dua za Mitume na Manabii    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Fahamu matumizi ya Dawa iitwayo Aspirin.

Aspirini Ni dawa ya kutuliza maumivu.Majina yanayoaminika zaidi katika kutuliza maumivu sasa yanapatikana kwa njia mbadala inayookoa gharama kwa kutumia Aspirini. Aspirini inayopendwa na familia kwa miongo kadhaa, mara nyingi hutumiwa kupunguza maumivu y

Soma Zaidi...
Dawa ya kutibu UTI

Nitakujuza dalili za UTI na dawa za kutibu UTI. Pia tutaona njia za kujikinga na UTI pamoja na dalili za UTI

Soma Zaidi...
Fahamu dawa ya kutibu kikohozi inayoitwa expectorant

Post hii inahusu zaidi dawa aina ya expectorant katika matibabu ya kikohozi,ni dawa ambayo usaidia au uzuia kikohozi kuendelea kutokea.

Soma Zaidi...
Kazi za Dawa ya Artesunate katika kutibu Malaria

Posti hii inahusu zaidi kazi za dawa ya Artesunate katika kutibu Malaria kali, ni dawa ambayo inatumika sana kutibu Malaria kali.

Soma Zaidi...
Dawa ya fangasi na dalili za fangasi

hapa utajifunza dalili za fangasi, dawa ya fangasi na aina za fangasi, pia nitakujuza njia za kukabiliana na fangasi

Soma Zaidi...
Namna ya kutumia tiba ya jino.

Posti hii inahusu zaidi namna au njia ya kufanya Ili kuweza kutumia tiba hii ya jino, kwa sababu ya mchanganyiko ambao umekwisha kuwepo kwa hiyo unachumua mchanganyiko unafanya kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya griseofulvin

Post hii inahusu zaidi dawa ya griseofulvin ni dawa inayotumika kutibu fangasi za kwenye ngozi ambazo usababisha mabaka mabaka kwenye ngozi.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya fluoroquinolones/quinolones

Post hii inahusu dawa ya kupambana na bakteria, hili kundi la fluoroquinolones lina dawa kuu mbili ambazo ni ciprofloxin na ofloxacin.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya parental Artusnate dawa ya kutibu malaria sugu

Post hii inahusu zaidi dawa ya Parental Artusnate ni dawa inayotumika kutibu ugonjwa wa malaria sugu kama tutakavyoona hapo baadaye.

Soma Zaidi...
Mebendazole kama dawa ya kutibu Minyoo.

Post hii inahusu zaidi dawa ya Mebendazole kama Dawa ya kutibu Minyoo, ni dawa inayotumiwa na watu wengi pale wanapokuwa na minyoo, walio wengi wamefanikiwa kupona kwa kutumia Dawa hii.

Soma Zaidi...