picha

Umuhimu wa kutumia dawa za ARV

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kutumia dawa za ARV kwa wathirika wa virusi vya ukimwi .pia tutangalia kwa undani mambo ya kuzingatia kwa wathirika wanaotumia ARV .pamoja na kujali watu wanaotumia dawa hizo .

 Umuhimu wa kutumia dawa za " ARV" kwa wathirika wa VVU.

  1. Kutokana tulivyoeleza apo juu kuhusu umuhimu au matumizi kwa watu wanaotumia dawa za "ARV" .ambazo ni dawa za kupunguza makali ya virusi vya ukimwi .dawa hizi utakuwa kutumia kwa usahihi.mtu anayeishi na virusi vya ukimwi hutumia dawa hizi kwa maisha yake yote.Endapo mwathrika ataacha kutumia dawa hizo ,anaweza kupata madhara zaidi kama vile kufhoofu kiafya ,magonjwa nyemelezi na kifo  ARV haziui virusi bali hufubaza virusi na kupunguza kasi ya kuongezeka.dawa hizi ufanya kinga ya mwili kuimarika.jukumu la kumwanzishia mwathrika dawa za kupunguza makali ya VVU ni  la kitabibu mkwa hiyo,kuna umuhimu wa kupinda afya ili kukua hali halisi ya afya zetu.     
  2. Huwaondolea wathirika wa VVU mateso ya kushambuliwa na maradhi nyemelezi ..maradhi   nyemelezi ni kama .saratani ,kifua kikuu,fangasi,kuharisha na homa kali ya mapafu
  3. Huimarisha afya za wanaoishi na VVU.   Kutokana na ilo watu wenye virusi vya ukimwi afya zao huwa vizuri kama vile watu wasio na ugonjwa wa UKIMWI. Hivyo hivyo mtu anaetumia hizi dawa inabidi awe anafanya sana mazoezi ya mwili .ili kuweza kulinda seli zake ziweze kufanya kazi.
  4. Wathirika wa VVU wanaweza kuishi maisha ya kawaida na kushiriki shughuli zao za kiuchumi na kukiongizia kipato.kutokana na hilo watu wanaotumia hizi dawa wanauwezo wa kuongoza maisha yao ya kila siku 

        5. Hupunguza kasi ya kuzaliana kwa wingi kwa VVU.hata hivyo hurefusha maisha.

      .  Mambo ya kuzingatia kwa waathrika wanaotumia "ARV"

Kama tulivyoona apo mwanzo wathirika wa VVU ni kundi linaloitaji kuishi kwa kufuata taratibu zilizoainishwa na watahalamu wa afya.mambo ya kuzingatia ni kama yafuatayo.

1.waathirika ni lazima wafuate ushauri wa kitaalamu wa kitibabu au watahalamu wa afya.

2.waathrika wanapaswa kutumia ARV kwa dozi sahii na kwa muda sahii .dawa zitumike kama ilivyoelezwa na daktari au mtaalamu wa afya .hii itasaidia kuboresha afya na kupunguza uwezekano wa VVU kuwa sugu kwa dawa zinazotumika.

3.waathrika wachukue tahadhari kwa kujikinga ili wasipate maambukizi mapya na kuambukiza wengine.ili kuondoa idadi ya maambukizi katika jamii.

4.mwathirika asiache kutumia dawa kwa muda na kisha kurudia tena  dawa hizo bila ushauri wa daktari au mtaalamu wa afya.

5.waathirika wa VVU watoe taarifa kwa daktari au watoe huduma kuhusu matatizo na athari za "ARV" endapo zitajitokeza.

6.waathirika waepuke kufuata imani na mila potofu za jadi au za dini zinazozuia kuwa mfuasi mzuri wa ARV 

7.waathirika wafuate ratiba ya kwenda kiliniki ya dawa za "ARV" bila kukosa ili kupata ushauri nasaa.

8.waathrika wazingatie ushauri kanuni za afya kwa mfano ,kuzingatia usafi wa mwili,lishe bora na mazingira safi.

9.waathirika wanashauriwa kuendelea kuishi kwa matumaini na wasikate tamaa .

10.mtumiaji wa "ARV" harusiwi kishirikiana dawa zake na mtu mwingine.

      jinsi watu wanaotumia dawa za "ARV"

1. Wathirika wa VVU wanaotumia ARV wanahitaji kuthaminiwa katika jamii zao na kuwaona kama watu wengine bila kuwabuguzi na kuwatenga.ili kuwajali watu wanaotumia dawa hizo.ni muhimu sana kuwasaidia pale wanapoitaji msaada.

2.pia kuambatana nao wanapoitaji kuaindikizwa kwenda kiliniki kuchukua dawa zao.pia inabidi tuwafaliji  wajione na wenyewe kama watu wengine wanapoitaji huduma hizo.

3.tuwasaidie wanapoitaji kuelekezwa matumizi sahihi ya  " ARV" ili wasiweze kwenda kinyume badae wasije kupata athari zozote katika jamii zetu.

4.kuwapatia chakula bora na kwa wakati.pia inabidi tuwandalie chakula chenye kuwaongezea vitamin ndani ya mwili wao.ili waweze kuijenga miili ya sawa .chakula lazima kiwekwe kwenye mazingira masafi na yenye virutubisho.kifunikwe na kisiwe cha balidi sana.

5.kuwakumbusha muda sahihi wa kumeza dawa pale wanaposahau.

6.kuwahamasisha kuendelea na matumizi ya dawa.

7.kuepuka kuwanyanyapaa walioathirika na VVU.pia ni muhimu sana kuzingatia na kufuata ushauri unaotolewa na daktari au mtaalamu wa afya kwa ktumiaji hi wa ARV .

 

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/08/12/Friday - 11:36:09 am Topic: Dawa Main: Afya File: Download PDF Views 4074

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

Dawa ya fangasi ukeni

Makala hii itakueleza dawa ya kutibu fangasi wa ukeni

Soma Zaidi...
Ifahamu dawa ya kupunguza maumivu

Post hii inahusu dawa ya aspirin katika kupunguza maumivu,ni dawa ambayo upunguz maumivu ya Kawaida, kushusha homa na pia usaidia kwenye magonjwa ya moyo hasa kuzuia stroke kama imetokea mda ndani ya masaa ishilini na manne

Soma Zaidi...
Matibabu ya macho

Somo Hili linakwenda kukuletea matibabu ya macho

Soma Zaidi...
Faida za dawa za NMN

Posti hii inahusu zaidi faida za dawa za NMN maana yake ni Nicotinamide mononucleotide ni dawa ambazo usaidia kutibu magonjwa mbalimbali kama vile.

Soma Zaidi...
Dawa mbadala za vidonda vya tumbo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa mbadala za vidonda vya tumbo

Soma Zaidi...
Fahamu matumizi ya Dawa iitwayo paracetamol.

Paracetamol kwa jina kingine hujulikana kama(acetaminophen) ni dawa ya kawaida ya kutuliza maumivu ambayo hutumiwa kupunguza aina mbalimbali za maumivu. Paracetamol ndilo jina linalojulikana zaidi katika kutuliza maumivu ya kawaida. Paracetamol inajulik

Soma Zaidi...
Miungurumo haiishi tumboni nikishika upande wa kushoto wa tumbo kuna maumivu kwa mbali je mm nitumie dawa gan kuondoa tatizo hilo

Kukawa na gesi tumboni kunaweza kuwa ni dalili ya shida kwenye afya, hasa katika mfumo wa chakula. Hali itakuwa sio nzuri endapo utakosea hamu ya kula na kuhisivkushiba muda wowote.

Soma Zaidi...
Dawa ya kutibu fangasi wa kwenye mdomo na kinywa

Zipo dawa nyingi ambazo hufahamika katika kutibu fangasi kwenye mdomo ama kinywa. Miongoni mwa dawa hizo hapa nitakuletea baadhi yao. kama wewe pia unasumbuliwa na fangasi wa mdomo basi post hii itakusaidi sana.

Soma Zaidi...
Fahamu dawa za kutuliza magonjwa ya akili inayoitwa Chlorpromazine

Post hii inahusu zaidi dawa zinazosaidis katika kutuliza magonjwa ya akili, dawa hii kwa kitaamu huiitwa chlorpromazine ni dawa ambayo utumiwa na watu wenye tatizo la magonjwa ya akili na kwa kiasi kikubwa huwa sawa.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya propranolol ambayo hutibu magonjwa ya moyo

Post hii inahusu zaidi dawa ya propranolol katika matibabu ya magonjwa ya moyo, dawa hii ipo kwenye kundi la beta blockers na ufanya Kazi mbalimbali hasa kwa wagonjwa wa moyo.

Soma Zaidi...