Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kutumia dawa za ARV kwa wathirika wa virusi vya ukimwi .pia tutangalia kwa undani mambo ya kuzingatia kwa wathirika wanaotumia ARV .pamoja na kujali watu wanaotumia dawa hizo .
Umuhimu wa kutumia dawa za " ARV" kwa wathirika wa VVU.
5. Hupunguza kasi ya kuzaliana kwa wingi kwa VVU.hata hivyo hurefusha maisha.
. Mambo ya kuzingatia kwa waathrika wanaotumia "ARV"
Kama tulivyoona apo mwanzo wathirika wa VVU ni kundi linaloitaji kuishi kwa kufuata taratibu zilizoainishwa na watahalamu wa afya.mambo ya kuzingatia ni kama yafuatayo.
1.waathirika ni lazima wafuate ushauri wa kitaalamu wa kitibabu au watahalamu wa afya.
2.waathrika wanapaswa kutumia ARV kwa dozi sahii na kwa muda sahii .dawa zitumike kama ilivyoelezwa na daktari au mtaalamu wa afya .hii itasaidia kuboresha afya na kupunguza uwezekano wa VVU kuwa sugu kwa dawa zinazotumika.
3.waathrika wachukue tahadhari kwa kujikinga ili wasipate maambukizi mapya na kuambukiza wengine.ili kuondoa idadi ya maambukizi katika jamii.
4.mwathirika asiache kutumia dawa kwa muda na kisha kurudia tena dawa hizo bila ushauri wa daktari au mtaalamu wa afya.
5.waathirika wa VVU watoe taarifa kwa daktari au watoe huduma kuhusu matatizo na athari za "ARV" endapo zitajitokeza.
6.waathirika waepuke kufuata imani na mila potofu za jadi au za dini zinazozuia kuwa mfuasi mzuri wa ARV
7.waathirika wafuate ratiba ya kwenda kiliniki ya dawa za "ARV" bila kukosa ili kupata ushauri nasaa.
8.waathrika wazingatie ushauri kanuni za afya kwa mfano ,kuzingatia usafi wa mwili,lishe bora na mazingira safi.
9.waathirika wanashauriwa kuendelea kuishi kwa matumaini na wasikate tamaa .
10.mtumiaji wa "ARV" harusiwi kishirikiana dawa zake na mtu mwingine.
jinsi watu wanaotumia dawa za "ARV"
1. Wathirika wa VVU wanaotumia ARV wanahitaji kuthaminiwa katika jamii zao na kuwaona kama watu wengine bila kuwabuguzi na kuwatenga.ili kuwajali watu wanaotumia dawa hizo.ni muhimu sana kuwasaidia pale wanapoitaji msaada.
2.pia kuambatana nao wanapoitaji kuaindikizwa kwenda kiliniki kuchukua dawa zao.pia inabidi tuwafaliji wajione na wenyewe kama watu wengine wanapoitaji huduma hizo.
3.tuwasaidie wanapoitaji kuelekezwa matumizi sahihi ya " ARV" ili wasiweze kwenda kinyume badae wasije kupata athari zozote katika jamii zetu.
4.kuwapatia chakula bora na kwa wakati.pia inabidi tuwandalie chakula chenye kuwaongezea vitamin ndani ya mwili wao.ili waweze kuijenga miili ya sawa .chakula lazima kiwekwe kwenye mazingira masafi na yenye virutubisho.kifunikwe na kisiwe cha balidi sana.
5.kuwakumbusha muda sahihi wa kumeza dawa pale wanaposahau.
6.kuwahamasisha kuendelea na matumizi ya dawa.
7.kuepuka kuwanyanyapaa walioathirika na VVU.pia ni muhimu sana kuzingatia na kufuata ushauri unaotolewa na daktari au mtaalamu wa afya kwa ktumiaji hi wa ARV .
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa
Mwandhishi Tarehe 2022/08/12/Friday - 11:36:09 am Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1971
Download our Apps
👉1 Kitabu cha Afya
👉2 Madrasa kiganjani
👉3 kitabu cha Simulizi
👉4 Kitau cha Fiqh