Menu



NGUZO ZA IMAN

Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala

NGUZO ZA IMAN

.Dhana ya Imani katika Uislamu.
Maana ya Tawhiid.
- Ni fani inayohusiana na imani ya kuwepo Allah (s.w) na siku ya mwisho pamoja na vipengele vyote vya nguzo za imani.
- Ni kumpwekesha Allah (s.w) katika kila kitu kwa Upweke na Umoja wake na uweza wake juu ya kila kitu.
Matapo (makundi) ya Tawhiid.
- Tawhiid imegawanyika makundi makuu matatu:
1)Tawhiid – Rubbuubiyya: Ni Kumpwekesha Allah (s.w) katika Utawala wake.
2)Tawhiid – Asmaa Wassifaat: Kumpwekesha Allah katika Majina na Sifa zake.
3)Tawhiid – Ibaadah: Kumpwekesha Allah (s.w) katika Uungu na Kuabudiwa.

Maana ya imani kwa mujibu wa Qur’an (Uislamu).
- Ni kuwa na yakini moyoni juu ya kuwepo kitu au jambo fulani lisiloonekana kwa macho bali kwa dalili zinazothibitisha kuwepo kwake.

Imani kwa mtazamo wa Uislamu na ule wa dini zingine:
- Katika Uislamu imani ni ile inayodhihirishwa katika vitendo vya mtu tofauti na dini zingine.
- Katika Uislamu imani juu ya kitu au jambo fulani lisiloonekana hutokana na dalili au ushahidi wa kuonesha uwepo wake tofauti na dini zingine.

Nguzo za Imani.
Nguzo za imani ya Kiislamu ni Sita:
1.Kumuamini Mwenyezi Mungu (s.w).
2.Kuamini Malaika wa Mwenyezi Mungu (s.w).
3.Kuamini Vitabu vya Mwenyezi Mungu (s.w).
4.Kuamini Mitume wa Mwenyezi Mungu (s.w).
5.Kuamini Siku ya Mwisho.
6.Kuamini Qadar ya Mwenyezi Mungu (s.w) kuwa kheri na shari vyote vinatokana kwake.
Rejea Qur’an (2:285), (4:136), (57:22) na (11:6).

Nguzo ya Ihsani.
- Nayo ni ‘kumuabudu Allah (s.w) kana kwamba unamuona na kama humuoni basi yeye anakuona’.
Nani muumini wa kweli? (Sifa za muumini wa kweli).
- Ni yule ambaye imani yake inathibitishwa katika matendo ya kila kipengele cha maisha yake ya kila siku.
Rejea Qur’an (2:8-9).

- Ni yule anayejipamba na sifa za waumini zilizoainishwa katika Qur’an na Sunnah katika kukiendea kila kipengele cha maisha yake ya kila siku.
Rejea Qur’an (23:1-11), (25:63-77), (33:35-36), n.k.
- Ni yule anayeendea kila kipengele cha maisha yake kwa mujibu wa vipengele vyote vya nguzo za imani ya Kiislamu.
oHawi muumini wa kweli kwa imani isiyoendana na matendo wala kwa kuamini baadhi ya nguzo za imani.


                   

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 1228


Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Hukumu ya zakat Al-Fitir na namna ya kuitoa zaka ya fitir
Soma Zaidi...

fadhila za sura kwenye quran
FADHILA ZA BAADHI YA SURA Umuhimu na ubora wa baadhi ya sura na aya. Soma Zaidi...

2.3.Kuamini Vitabu Vya Mwenyezi Mungu (s.w Quran, tawrat, Zabur na injili
2. Soma Zaidi...

Kwa Nini Mwanaadamu Hawezi Kuunda Dini Sahihi ?
1. Soma Zaidi...

nguzo za uislamu
Soma Zaidi...

Madai ya Makafiri Dhidi ya Qur’an na Udhaifu Wake
i. Soma Zaidi...

Kitabu Cha Dua 120
Sifanjema zinamstahikia Allah Mola wa viumbe vyote. Soma Zaidi...

Sababu za kushuka sura kwenye quran na fadhila za sura mbalimbali kwenye quran
Soma Zaidi...

Muda wa kuhiji na mwenendo wa mwenye kuhiji
Soma Zaidi...

maana na asili ya dini, kazi zake na nadharia potofu za makafiri kuhusu dini
2. Soma Zaidi...