Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala
1.2.Shirk.
Maana : Shirk ni kinyume cha Upweke au Umoja (Tawhiid)
Maana ya Kumshirikisha Mwenyezi Mungu (s.w):
Ni kujaalia kinadharia au kiutendaji kuwa kuna miungu wengine wanaoshirikiana na Mwenyezi Mungu (s.w) katika kuongoza na kuendesha Ulimwengu.
Aina za Shirk.
Kuna aina kuu nne za shirk,
1.Shirk katika Dhati ya Mwenyezi Mungu – (Shirk fiy Dhaat).
2.Shirk katika Sifa za Mwenyezi Mungu – (Shirk fiy Sifaat).
3.Shirk katika Mamlaka ya Mwenyezi Mungu – (Shirk fiy Ikhtiyaar).
4.Shirk katika Hukumu za Mwenyezi Mungu – (Shirk fiy Ah-kaam).
1. Shirk katika Dhati ya Mwenyezi Mungu (s.w).
Ni kujaalia au kuvinasibisha viumbe na uungu kwa kuvipa majina rasmi kama washirika wa Mwenyezi Mungu (s.w) na kuviendea kwa unyenyekevu na ibada maalum kama, kuvisujudia, kuchinja na kuviomba msaada.
Rejea Qur’an (25:2-3), (22:73) na (29:41).
2. Shirk katika Sifa za Mwenyezi Mungu (s.w).
Ni kuwasifu au kuwatukuza viumbe kiwango anachostahiki kusifiwa au kutukuzwa Allah (s.w) peke yake. Kama kuomba dua, baraka na msaada kupitia kwa Wacha-Mungu, mfano kwa baraka za Mtume, Abdul-Qadir, Sharifu au Sheikh fulani n.k.
Rejea Qur’an (53:32), (10:62-64), (2:180), (17:110) na (40:60).
3. Shirk katika Mamlaka ya Mwenyezi Mungu (s.w).
Ni kuwakabidhi viumbe mamlaka kamili ya Mwenyezi Mungu (s.w) na kuwatii kwayo kama vile kuongoza, kulisha, kulea, kulinda n.k katika maisha ya kila siku kinyume na nafasi au uwezo wao.
Rejea Qur’an (9:31) na (2:208).
4. Shirk katika Hukumu za Mwenyezi Mungu (s.w).
Ni kutunga sheria au hukumu kinyume na sheria au hukumu za Mwenyezi Mungu (s.w) alizoziainisha katika vitabu vyake vitukufu na kuzitumia kuhukumu kwazo katika uendeshaji wa maisha ya kila siku.
Rejea Qur’an (5:38), (24:2), (33:36), (5:44-45, 47) na (5:50).
Kina cha Uovu wa Shirk.
oNi dhulma kubwa kuliko zote na ndio chanzo cha matatizo yote ulimwenguni.
Rejea Qur’an (31:13) na (10:35-36).
oNi dhambi kubwa kuliko zote isiyosameheka ila apende Mwenyezi Mungu (s.w) na kutubia kikweli kweli kabla ya kufa.
oNi dhambi inayofuta mema yote ya mtu aliyoyafanya kabla ya kushirikisha.
Rejea Qur’an (4:48), (4:116) na (39:65).
Maana ya Kumuamini Mwenyezi (s.w) katika maisha ya kila siku.
Ni kumpwekesha Mwenyezi Mungu (s.w) kwa kufuata barabara mwongozo wake katika utendaji wa wetu wa kila kipengele cha maisha yetu ya kila siku kwa kufanya moja kati ya mambo yafuatayo;
oKusimamisha Tawhiid (Umoja na Upweke wa Mwenyezi Mungu) na
oKujiepusha na Shirk za aina zote.
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 709
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio
👉2 Kitabu cha Afya
👉3 Kitau cha Fiqh
👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉5 Madrasa kiganjani
👉6 kitabu cha Simulizi
nmna ya kufanya istikhara na kuswali swala ya Istikhara
Soma Zaidi...
swala za tahiyatu al masjid, qabliya na baadiya
Muislamu anapoingia Msikitini kabla hajakaa anatakiwa aswali rakaa mbili za maamkizi ya msikiti, Tahiyyatul-Masjid. Soma Zaidi...
Je mahari inashusha hadhi ya mwanamke?
Je, Mahari inashusha hadhi ya mwanamke? Soma Zaidi...
maana ya swala kilugha na kisheria
Soma Zaidi...
SHIRK
Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala Soma Zaidi...
Umuhimu wa ndoa na kuoa ama kuolwa katika jamii
Matamanio ya jimai ni katika maumbile na hayaepukiki. Soma Zaidi...
MAFUNZO YA QURAN: QURAN NA SAYANSI NA TEKNOLOJIA
Soma Zaidi...
MAANA YA HADITHI SUNNAH
Maana ya SunnahKilugha: Neno sunnah katika lugha ya Kiarabu lina maana ya mwenendo au mila. Soma Zaidi...
Sifa na vigezo vya dini sahihi
1. Soma Zaidi...
Hadithi aliyoisimulia Kijakazi kwa sultan
Soma Zaidi...
NDANI YA SHIMO LA KABURI
Download kitabu Hiki Bofya hapa NDANI YA PANGO LA MAKABURI Mmoja wapo akatowa kamba na kulifunga jeneza vizuri na kuanza kulishusha chini ya mapango kwa kamba ile. Soma Zaidi...