KIKAO CHA KUMFUKUZA MTUME MUHAMMAD KUTOKA MAKKAH (MAKA), KIKAO ALICHOHUDHURIA IBLISI

KIKAO CHA KUMFUKUZA MTUME MUHAMMAD KUTOKA MAKKAH (MAKA), KIKAO ALICHOHUDHURIA IBLISI

KIKAO CHAKALIWA KUJADILI HATMA YA MUHAMMAD KATIKA MJI WA MAKAHiki ni kikao kizito hakijapata kutokea toka muhammad katika ji wa maka.

Download Post hii hapa

KIKAO CHA KUMFUKUZA MTUME MUHAMMAD KUTOKA MAKKAH (MAKA), KIKAO ALICHOHUDHURIA IBLISI

KIKAO CHAKALIWA KUJADILI HATMA YA MUHAMMAD KATIKA MJI WA MAKA

Hiki ni kikao kizito hakijapata kutokea toka muhammad katika ji wa maka. Ni katika jimba la mikutano lililofahamika kama AN-NADWAH hii ilikuwa ndio nyumba ya bunge la watu wa maka kujadili mambo yao. Lengo kubwa ni kupunguza kasi ya kuenea kwa uislamu na kumfanya muhammad aachane kabisa na jambo hili la kutangaza dini iliyo nje ya mila zao. Na hii ilitokea pale makabila ya Aws na Khazraj walipotishia kumpokea Muhammad endapo atakwenda Yathrib (Madina).


Kiakao kilikaliwa mnamo tarehe 12 mwezi wa tisa mwaka 622 B.K au ni sawa na tarehe 26 mfunguo tano (safar) kwa mujibu wa kalenda ya kiarabu.na tukio hili lilitokea miezi miwili na nusu baada ya mkataba wa ‘Aqabah. Katika siku hiyo mkutano ulifanyika kwa umakini zaidi, umakini ambao katu haujapata kutokea kabla.


1.Mkutano huu ulihudhuriwa na watu 14 karibia kutoka katika kila kabila. Watu hawa walikuwa nai:-
2.Abuu Jahal Ibn Hisham kutoka katika kabila la Banuu Makhzumi,
3.Jabir Ibn Mut’im, Tua’aima Ibn ‘Ady na Harith Ibn ‘Amir kutoka kabila la Banuu Naufal Ibn ‘Abd Manafi
4.Watoto wawili wa Ibn Rabia nao ni Shaiba na ‘Utbah, Abuu Sufian Ibn Harb kutoka katika kabila la Banii ‘Abd Shams Ibn ‘Abd Manaaf
5.Nadhr Ibn Haarith kutoka kkabila la Banii ‘Abd Dar
6.Abuu Bakhtar Ibn Hishaam na Zam’at Ibn Aswad, na hakim Ibn Hizaam kutoka katika kabila la Banii Asad ibn ‘Abd al-’Uzaa
7.Nubiyah na Munabih watoto wa Hajaaj kutoka kabila la banii Saham
8.Umayyah Ibn Khalaf kutoka kabila la banii Jumah.


Wakati wahudhuriaji walipokusanyika nje ya mlango wa jumba hili la mikutano, ghafla akaja mzee mmoja. Mzee aliyeonekana nadhifu sana. Mzee huyu akaja hadi mlangoni, walipomuuliza ni nani wewe akajibu kuwa yeye ni mtu kutoka maeneo ya Najd na amepetakhabari juu ya mkutano huu, hivyo atawakilisha watu wa najd na kutoa mawazo yake.


Watu walipojiridhisha wakamruhusu na kwa pamoja kundi likaingia ndani. Ukweli wa mambo ni kuwa mzee huyu hakuwa ni mtu wa Najid bali alikuwa ni iblisi na alikuja ili kuhakikisha inapatikana rai itakayokuwa ni mujarabu katika kummaliza Muhammad. Basi punde baada ya watu kuingia ndani mkutano ukaanza. Rai mbalimbali zikaanza kutolewa na huku mzee wa Najd (Iblis) akawa anapangua rai hizo kwa hija zilizo madhubuti. Miongoni mwa rai hizo ni kama zifuatazo:-


A.Basi mtu mmoja a;liyetambulika kwa jina la Abuu Aswad akazungumza kuwa “tumtoeni (tumfukuzeni) Muhammad kwenye mji wetu (Makkah) na aende kokote atakakotaka na katu tusijali popote atakapokwenda, tukifanya hivyo kwa hakika tutakuwa tumesalimika na mambo yatarudi kama yalivyokuwa.


B.Basi hapo mzee wa Najd (Iblis) akasema kuwa: kwa hakika jambo hili sio salama kabisa kwenu. Akasema “hivi hamjaona jinsi yalivyo matamu maneno yake?, na utamu na ufasaha wa matamko yake, kama mkimtoa atakwenda kupata wafuasi wengine wasiokuwa nyinyi, na atakuwa na nguvu kisha atakuvamieni na kukutoeni kwenye miji yenu, na afanye atakachokitaka. Kwa hakika rai hii sio salama toeni rai nyingine isiyokuwa hii.


C.Mtu mwingine aliyefahamika kwa jina la Abuu Al-Bakhtar akasema “mfungieni kwenye chumba chenye milango madhubuti, na kisha abakie humo na yampate yele yalowapata waliotangulia kabla yenu (baada ya kupewa adhabu kama hii) mpaka mauti yamkute”


D.Baada ya kutolewa rai hii mzee wa Nadj (Iblis) akaipinga tena rai hii kwa kusema hapana hili pia si jema, kwa hakika naapa kwa Allah kuwa kama mtafanya hivyo wafuasi wake watakuja kumtoa. Watu walionekana pia kukubali wazo hilo kuwa rai hii pia sio salama. Kwani hata nduguzake wangemtoa wasingeweza kumuacha, kwani walisha mfungia kabla hapo yeye na familia yake.


E.Basi baada ya muda mkuu wa makafiri wa Makkah Abuu Jahal akazungumza “kwa hikika naapa kwa Allah kuwa njina rai ambayo hamjaitoa” watu wakasema ni ipi rai hiyo? Akasema “na tuchukuwe kutoka katika kabila mtukijana mmoja mwenye nguvu na afya njema, kisha tumpatie upanga ulio safi na mkali kisha kila mmoja katia vijana hawa akampige (Muhammad) upanga mmoja na wamuue na wakifanya hivi atakuwa ameuliwa na kabila zote za watu wa Makkah hivyo hata familia yake haitaweza kulipiza kisasi.


F.Watu walionekana kuikubali rai hii na hata mzee wa Najd (Iblis) hakuweza kuipinga rai hii hata kidogo. Na kisha akasema mzee wa Najd “hii ndio rai ambayo hakuna rai nyingine (bora zaidi) kuliko hii.

Baada ya kumaliza kikao kwa kukubaliana kutekeleza hoja ya kumuua Muhammad, watu wote walitawanyika. Vijana kutoka katika kila kabila walichukuliwa tayari kwa akwenda kummaliza Muhammad. Mambo makubwa na miujiza ya hali ya juu ilitokea, darasa lijalo tutaendelea na kipande kijacho.



                   

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 945

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Msonge wa uongozi na siasa katika serikali ya kiislamu mafinah
Msonge wa uongozi na siasa katika serikali ya kiislamu mafinah

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Sababu ya uislamu kuwa ndiyo dini sahihi pekee
Sababu ya uislamu kuwa ndiyo dini sahihi pekee

Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
MJADALA JUU YA NDOA YA MTUME S.A.W NA BI KHADIJA (HADIJA)
MJADALA JUU YA NDOA YA MTUME S.A.W NA BI KHADIJA (HADIJA)

LAKINI UMRI WANGU MKUBWABaada ya kuwaza na kufikiri muda mrefu, bibi Khadija (Radhiya Llahu anha) akafikia uamuzi wa kutaka kuolewa na Muhammad (Swalla Laahu alayhi wa sallam).

Soma Zaidi...
Mfumo wa ulinzi na usalama katika fola ya uislamu madinah
Mfumo wa ulinzi na usalama katika fola ya uislamu madinah

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Chokochoko na Upinzani wakati wa khalifa uthman khalifa wa Tatu
Chokochoko na Upinzani wakati wa khalifa uthman khalifa wa Tatu

KUPOROMOKA KWA DOLA YA KIISLAMU ALIYOICHA MTUME(S.

Soma Zaidi...
tarekh 06
tarekh 06

MAISHA YA UTOTONI YA MTUME S.

Soma Zaidi...
HISTORIA YA MTUME ILYASA(A.S)
HISTORIA YA MTUME ILYASA(A.S)

Mtume Ilyasa ni mmoja wa Mitume waliotumwa kupitia kizazi cha Bani Israil.

Soma Zaidi...
Nasaba ya mtume
Nasaba ya mtume

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...