Katika somo hili utakwenda kujifunza kanuni za usomaji wa isti’adha na basmallah.
Tamko la "Bismillahir-Rahmanir-Rahim" hujulikana kama Basmala, na "A'udhu Billahi Minash-Shaytanir-Rajim" hujulikana kama Isti'adha. Matamko yote haya yana hukumu zake za usomaji mbele ya maulamaa wa Tajwid. Allah amesema: "...pindi unaposoma Qur'an, tafuta hifadhi kwa Allah kutokana na Shetani aliye mbali na rehema za Allah" (yaani, anza kusoma kwa Isti'adha).
Pindi utakapoanza kusoma Qur'an na ukataka kuanza na Isti'adha mwanzoni mwa sura, unatakiwa kuleta Basmala kabla ya kuanza sura. Hivyo basi, kutakuwa kumekutana Isti'adha, Basmala, na sura unayotaka kusoma. Hapa katika kusoma kwake kuna hukumu nne kama ifuatavyo:
Kukata zote: Kusoma kila moja kivyake kwa kusimama kati ya vitatu hivi. Yaani, utasoma Isti'adha kisha utasimama, halafu utasoma Basmala kisha utasimama na baadaye utaanza sura.
Kuunga zote: Kunganisha Isti'adha, Basmala, na sura bila kusimama.
Kuunga Basmala na sura: Kusoma Isti'adha kisha utasimama, halafu utasoma Basmala na sura kwa kuunganisha bila kusimama.
Kuunga Isti'adha na Basmala: Kusoma Isti'adha na Basmala kwa pamoja kisha unasimama, kisha unasoma sura.
Inapotokea umemaliza sura moja na unataka kuingia sura nyingine, hapa kuna hukumu zifuatazo:
Kukata zote: Kusoma mwisho wa sura, kisha unasoma Basmala, na kisha unasoma sura inayofuata.
Kuunga zote: Kuunganisha mwisho wa sura kisha unasoma Basmala, kisha unaanza kusoma sura mpya bila kupumzika.
Kuunga Basmala na mwanzo wa sura: Kumaliza sura kisha utasimama, kisha utasoma Basmala pamoja na kuanza sura mpya bila kusimama.
Mwisho:
Katika somo linalofuata tutakwend akujifunza hukumu za NUN sakina na tanwinkatika usomaji wa Quran.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Katika somo hili utakwend akujifunza kw akirefu kuhusu madd twab’iy yaani madd za asili.
Soma Zaidi...hapa utakwenda kujifunza kuhusu sifa za herufi za kiarabu
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za Al ikhfaa katika usomaji wa Tajwid
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunzakuhusu hukumu za iqlab katika usomaji wa tajwid.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu idgham na idhhar katika laam.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza maana ya elimu ya tajwid kisheria. Pia utajifunza hukumu ya kusoma tajwid.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za kitajwid za nun sakina na tanwin
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu hukumu za ki tajwid za mim sakina.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza kuhusu viraa vya usomaji wa Quran. Viraa hivi ni tofauti na herufi saba
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu herufi saba katika usomaji wa tajwid.
Soma Zaidi...