image

Tajwid somo la 8: hukumu za kusoma basmala na isti'adha

Katika somo hili utakwenda kujifunza kanuni za usomaji wa isti’adha na basmallah.

Hukumu ya Basmala na Isti'adha

Tamko la "Bismillahir-Rahmanir-Rahim" hujulikana kama Basmala, na "A'udhu Billahi Minash-Shaytanir-Rajim" hujulikana kama Isti'adha. Matamko yote haya yana hukumu zake za usomaji mbele ya maulamaa wa Tajwid. Allah amesema: "...pindi unaposoma Qur'an, tafuta hifadhi kwa Allah kutokana na Shetani aliye mbali na rehema za Allah" (yaani, anza kusoma kwa Isti'adha).

Hukumu ya Isti'adha

Pindi utakapoanza kusoma Qur'an na ukataka kuanza na Isti'adha mwanzoni mwa sura, unatakiwa kuleta Basmala kabla ya kuanza sura. Hivyo basi, kutakuwa kumekutana Isti'adha, Basmala, na sura unayotaka kusoma. Hapa katika kusoma kwake kuna hukumu nne kama ifuatavyo:

  1. Kukata zote: Kusoma kila moja kivyake kwa kusimama kati ya vitatu hivi. Yaani, utasoma Isti'adha kisha utasimama, halafu utasoma Basmala kisha utasimama na baadaye utaanza sura.

  2. Kuunga zote: Kunganisha Isti'adha, Basmala, na sura bila kusimama.

  3. Kuunga Basmala na sura: Kusoma Isti'adha kisha utasimama, halafu utasoma Basmala na sura kwa kuunganisha bila kusimama.

  4. Kuunga Isti'adha na Basmala: Kusoma Isti'adha na Basmala kwa pamoja kisha unasimama, kisha unasoma sura.

Hukumu ya Basmala Kati ya Sura Mbili

Inapotokea umemaliza sura moja na unataka kuingia sura nyingine, hapa kuna hukumu zifuatazo:

  1. Kukata zote: Kusoma mwisho wa sura, kisha unasoma Basmala, na kisha unasoma sura inayofuata.

  2. Kuunga zote: Kuunganisha mwisho wa sura kisha unasoma Basmala, kisha unaanza kusoma sura mpya bila kupumzika.

  3. Kuunga Basmala na mwanzo wa sura: Kumaliza sura kisha utasimama, kisha utasoma Basmala pamoja na kuanza sura mpya bila kusimama.

Mwisho:

Katika somo linalofuata tutakwend akujifunza hukumu za NUN sakina na tanwinkatika usomaji wa Quran.

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-07-14 17:17:06 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 65


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Tajwid somo la 5: makharija al khuruf
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu makharijal khuruf Soma Zaidi...

Tajwid somo la 8: hukumu za kusoma basmala na isti'adha
Katika somo hili utakwenda kujifunza kanuni za usomaji wa isti’adha na basmallah. Soma Zaidi...

Tajwid somo la 12: sheria za Iqlab
Katika somo hili utakwenda kujifunzakuhusu hukumu za iqlab katika usomaji wa tajwid. Soma Zaidi...

Tajwid somo la 2: herufi saba katikausomaji wa quran
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu herufi saba katika usomaji wa tajwid. Soma Zaidi...

Tajwid somo la 19: hukumu za madd na aina zake
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu madd na aina zake. Utajifunza herufi za madd na umuhimu wa madd katika tajwid. Soma Zaidi...

Tajwid somo la 20: hukumu za madd twab'iy yaani madd ya asili
Katika somo hili utakwend akujifunza kw akirefu kuhusu madd twab’iy yaani madd za asili. Soma Zaidi...

Tajwid somo la 11: hukumu ya idgham
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za idgham katika tajwid Soma Zaidi...

Tajwid somo la 18: hukumu za waqf wal ibtidai
Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu hukumuza waqfu katika usomajiwa quran. Soma Zaidi...

Tajwid somo la 9: hukumu za nun sakina na tanwin
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za kitajwid za nun sakina na tanwin Soma Zaidi...

Tajwid somo la 7: haraka na irabu katika lugha ya kiarabu
Katika somo hili utakwenda kujifunzakuhusu haraka na irabu katika lugha ya kiarabu Soma Zaidi...

Tajwid somo la 1: Maana ya elimu ya Tajwid na kanuni zake
Katika somo hili utakwend akujifunza maana ya elimu ya tajwid kisheria. Pia utajifunza hukumu ya kusoma tajwid. Soma Zaidi...

Tajwid somo la 17: hukumu za idgham na idhhar katika laam.
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu idgham na idhhar katika laam. Soma Zaidi...