Tajwid somo la 8: hukumu za kusoma basmala na isti'adha
Katika somo hili utakwenda kujifunza kanuni za usomaji wa isti’adha na basmallah.
Hukumu ya Basmala na Isti'adha
Tamko la "Bismillahir-Rahmanir-Rahim" hujulikana kama Basmala, na "A'udhu Billahi Minash-Shaytanir-Rajim" hujulikana kama Isti'adha. Matamko yote haya yana hukumu zake za usomaji mbele ya maulamaa wa Tajwid. Allah amesema: "...pindi unaposoma Qur'an, tafuta hifadhi kwa Allah kutokana na Shetani aliye mbali na rehema za Allah" (yaani, anza kusoma kwa Isti'adha).
Hukumu ya Isti'adha
Pindi utakapoanza kusoma Qur'an na ukataka kuanza na Isti'adha mwanzoni mwa sura, unatakiwa kuleta Basmala kabla ya kuanza sura. Hivyo basi, kutakuwa kumekutana Isti'adha, Basmala, na sura unayotaka kusoma. Hapa katika kusoma kwake kuna hukumu nne kama ifuatavyo:
-
Kukata zote: Kusoma kila moja kivyake kwa kusimama kati ya vitatu hivi. Yaani, utasoma Isti'adha kisha utasimama, halafu utasoma Basmala kisha utasimama na baadaye utaanza sura.
-
Kuunga zote: Kunganisha Isti'adha, Basmala, na sura bila kusimama.
-
Kuunga Basmala na sura: Kusoma Isti'adha kisha utasimama, halafu utasoma Basmala na sura kwa kuunganisha bila kusimama.
-
Kuunga Isti'adha na Basmala: Kusoma Isti'adha na Basmala kwa pamoja kisha unasimama, kisha unasoma sura.
Hukumu ya Basmala Kati ya Sura Mbili
Inapotokea umemaliza sura moja na unataka kuingia sura nyingine, hapa kuna hukumu zifuatazo:
-
Kukata zote: Kusoma mwisho wa sura, kisha unasoma Basmala, na kisha unasoma sura inayofuata.
-
Kuunga zote: Kuunganisha mwisho wa sura kisha unasoma Basmala, kisha unaanza kusoma sura mpya bila kupumzika.
-
Kuunga Basmala na mwanzo wa sura: Kumaliza sura kisha utasimama, kisha utasoma Basmala pamoja na kuanza sura mpya bila kusimama.
Mwisho:
Katika somo linalofuata tutakwend akujifunza hukumu za NUN sakina na tanwinkatika usomaji wa Quran.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Tajwid somo la 7: haraka na irabu katika lugha ya kiarabu
Katika somo hili utakwenda kujifunzakuhusu haraka na irabu katika lugha ya kiarabu
Soma Zaidi...Tajwid somo la 3: aina za viraa katika usomaji wa Quran
Katika somo hili utajifunza kuhusu viraa vya usomaji wa Quran. Viraa hivi ni tofauti na herufi saba
Soma Zaidi...Tajwid somo la 10: hukumu ya idhhar
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za idhhar na mifano yake.
Soma Zaidi...Tajwid somo la 9: hukumu za nun sakina na tanwin
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za kitajwid za nun sakina na tanwin
Soma Zaidi...Tajwid somo la 6: sifat al khuruf
hapa utakwenda kujifunza kuhusu sifa za herufi za kiarabu
Soma Zaidi...Tajwid somo la 19: hukumu za madd na aina zake
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu madd na aina zake. Utajifunza herufi za madd na umuhimu wa madd katika tajwid.
Soma Zaidi...