Tajwid somo la 8: hukumu za kusoma basmala na isti'adha

Katika somo hili utakwenda kujifunza kanuni za usomaji wa isti’adha na basmallah.

Hukumu ya Basmala na Isti'adha

Tamko la "Bismillahir-Rahmanir-Rahim" hujulikana kama Basmala, na "A'udhu Billahi Minash-Shaytanir-Rajim" hujulikana kama Isti'adha. Matamko yote haya yana hukumu zake za usomaji mbele ya maulamaa wa Tajwid. Allah amesema: "...pindi unaposoma Qur'an, tafuta hifadhi kwa Allah kutokana na Shetani aliye mbali na rehema za Allah" (yaani, anza kusoma kwa Isti'adha).

Hukumu ya Isti'adha

Pindi utakapoanza kusoma Qur'an na ukataka kuanza na Isti'adha mwanzoni mwa sura, unatakiwa kuleta Basmala kabla ya kuanza sura. Hivyo basi, kutakuwa kumekutana Isti'adha, Basmala, na sura unayotaka kusoma. Hapa katika kusoma kwake kuna hukumu nne kama ifuatavyo:

  1. Kukata zote: Kusoma kila moja kivyake kwa kusimama kati ya vitatu hivi. Yaani, utasoma Isti'adha kisha utasimama, halafu utasoma Basmala kisha utasimama na baadaye utaanza sura.

  2. Kuunga zote: Kunganisha Isti'adha, Basmala, na sura bila kusimama.

  3. Kuunga Basmala na sura: Kusoma Isti'adha kisha utasimama, halafu utasoma Basmala na sura kwa kuunganisha bila kusimama.

  4. Kuunga Isti'adha na Basmala: Kusoma Isti'adha na Basmala kwa pamoja kisha unasimama, kisha unasoma sura.

Hukumu ya Basmala Kati ya Sura Mbili

Inapotokea umemaliza sura moja na unataka kuingia sura nyingine, hapa kuna hukumu zifuatazo:

  1. Kukata zote: Kusoma mwisho wa sura, kisha unasoma Basmala, na kisha unasoma sura inayofuata.

  2. Kuunga zote: Kuunganisha mwisho wa sura kisha unasoma Basmala, kisha unaanza kusoma sura mpya bila kupumzika.

  3. Kuunga Basmala na mwanzo wa sura: Kumaliza sura kisha utasimama, kisha utasoma Basmala pamoja na kuanza sura mpya bila kusimama.

Mwisho:

Katika somo linalofuata tutakwend akujifunza hukumu za NUN sakina na tanwinkatika usomaji wa Quran.

 

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Darsa za Tajwid Main: Dini File: Download PDF Views 279

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Tajwid somo la 20: hukumu za madd twab'iy yaani madd ya asili

Katika somo hili utakwend akujifunza kw akirefu kuhusu madd twab’iy yaani madd za asili.

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 6: sifat al khuruf

hapa utakwenda kujifunza kuhusu sifa za herufi za kiarabu

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 13: sheria za Al-ikhfaa

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za Al ikhfaa katika usomaji wa Tajwid

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 12: sheria za Iqlab

Katika somo hili utakwenda kujifunzakuhusu hukumu za iqlab katika usomaji wa tajwid.

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 17: hukumu za idgham na idhhar katika laam.

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu idgham na idhhar katika laam.

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 1: Maana ya elimu ya Tajwid na kanuni zake

Katika somo hili utakwend akujifunza maana ya elimu ya tajwid kisheria. Pia utajifunza hukumu ya kusoma tajwid.

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 9: hukumu za nun sakina na tanwin

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za kitajwid za nun sakina na tanwin

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 14: kuhumu za mim sakina

Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu hukumu za ki tajwid za mim sakina.

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 3: aina za viraa katika usomaji wa Quran

Katika somo hili utajifunza kuhusu viraa vya usomaji wa Quran. Viraa hivi ni tofauti na herufi saba

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 2: herufi saba katikausomaji wa quran

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu herufi saba katika usomaji wa tajwid.

Soma Zaidi...