Tajwid somo la 8: hukumu za kusoma basmala na isti'adha

Tajwid somo la 8: hukumu za kusoma basmala na isti'adha

Katika somo hili utakwenda kujifunza kanuni za usomaji wa isti’adha na basmallah.

Hukumu ya Basmala na Isti'adha

Tamko la "Bismillahir-Rahmanir-Rahim" hujulikana kama Basmala, na "A'udhu Billahi Minash-Shaytanir-Rajim" hujulikana kama Isti'adha. Matamko yote haya yana hukumu zake za usomaji mbele ya maulamaa wa Tajwid. Allah amesema: "...pindi unaposoma Qur'an, tafuta hifadhi kwa Allah kutokana na Shetani aliye mbali na rehema za Allah" (yaani, anza kusoma kwa Isti'adha).

Hukumu ya Isti'adha

Pindi utakapoanza kusoma Qur'an na ukataka kuanza na Isti'adha mwanzoni mwa sura, unatakiwa kuleta Basmala kabla ya kuanza sura. Hivyo basi, kutakuwa kumekutana Isti'adha, Basmala, na sura unayotaka kusoma. Hapa katika kusoma kwake kuna hukumu nne kama ifuatavyo:

  1. Kukata zote: Kusoma kila moja kivyake kwa kusimama kati ya vitatu hivi. Yaani, utasoma Isti'adha kisha utasimama, halafu utasoma Basmala kisha utasimama na baadaye utaanza sura.

  2. Kuunga zote: Kunganisha Isti'adha, Basmala, na sura bila kusimama.

  3. Kuunga Basmala na sura: Kusoma Isti'adha kisha utasimama, halafu utasoma Basmala na sura kwa kuunganisha bila kusimama.

  4. Kuunga Isti'adha na Basmala: Kusoma Isti'adha na Basmala kwa pamoja kisha unasimama, kisha unasoma sura.

Hukumu ya Basmala Kati ya Sura Mbili

Inapotokea umemaliza sura moja na unataka kuingia sura nyingine, hapa kuna hukumu zifuatazo:

  1. Kukata zote: Kusoma mwisho wa sura, kisha unasoma Basmala, na kisha unasoma sura inayofuata.

  2. Kuunga zote: Kuunganisha mwisho wa sura kisha unasoma Basmala, kisha unaanza kusoma sura mpya bila kupumzika.

  3. Kuunga Basmala na mwanzo wa sura: Kumaliza sura kisha utasimama, kisha utasoma Basmala pamoja na kuanza sura mpya bila kusimama.

Mwisho:

Katika somo linalofuata tutakwend akujifunza hukumu za NUN sakina na tanwinkatika usomaji wa Quran.

 

Bongoclass
Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya hapa chini kuipakua sasa!

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Darsa za Tajwid Main: Dini File: Download PDF Views 346

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Tajwid somo la 3: aina za viraa katika usomaji wa Quran
Tajwid somo la 3: aina za viraa katika usomaji wa Quran

Katika somo hili utajifunza kuhusu viraa vya usomaji wa Quran. Viraa hivi ni tofauti na herufi saba

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 10: hukumu ya idhhar
Tajwid somo la 10: hukumu ya idhhar

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za idhhar na mifano yake.

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 12: sheria za Iqlab
Tajwid somo la 12: sheria za Iqlab

Katika somo hili utakwenda kujifunzakuhusu hukumu za iqlab katika usomaji wa tajwid.

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 14: kuhumu za mim sakina
Tajwid somo la 14: kuhumu za mim sakina

Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu hukumu za ki tajwid za mim sakina.

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 19: hukumu za madd na aina zake
Tajwid somo la 19: hukumu za madd na aina zake

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu madd na aina zake. Utajifunza herufi za madd na umuhimu wa madd katika tajwid.

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 11: hukumu ya idgham
Tajwid somo la 11: hukumu ya idgham

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za idgham katika tajwid

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 17: hukumu za idgham na idhhar katika laam.
Tajwid somo la 17: hukumu za idgham na idhhar katika laam.

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu idgham na idhhar katika laam.

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 7: haraka na irabu katika lugha ya kiarabu
Tajwid somo la 7: haraka na irabu katika lugha ya kiarabu

Katika somo hili utakwenda kujifunzakuhusu haraka na irabu katika lugha ya kiarabu

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 21: hukumu za madd far’iy
Tajwid somo la 21: hukumu za madd far’iy

Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu madd far’iy katika usomaji wa Quran tajwid.

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 5: makharija al khuruf
Tajwid somo la 5: makharija al khuruf

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu makharijal khuruf

Soma Zaidi...