Tajwid somo la 1: Maana ya elimu ya Tajwid na kanuni zake
Katika somo hili utakwend akujifunza maana ya elimu ya tajwid kisheria. Pia utajifunza hukumu ya kusoma tajwid.
Maana ya Elimu ya Tajwid
Neno "Tajwid" linatokana na neno la Kiarabu جَوَّدَ (jawwada) ambalo kilugha lina maana ya "ufundi," yaani kufanya kitu kwa uhodari au ustadi. Kwa mujibu wa Kishariah, maana ya Tajwid ni kuitamka kila herufi kama inavyotakiwa kutamkwa, kwa kuipa haki yake na sifa zake huku ukifuata hukumu zote za Tajwid.
Katika Qur'an na Sunnah, imehimizwa sana kusoma Qur'an kwa tajwid au tartila. Elimu hii ya Tajwid ilianza zamani toka enzi za masahaba na wakati Mtume Muhammad (s.a.w) akiwa hai. Mtume alikuwa akiwaelekeza masahaba kwa watu maalumu ili wapate kujifunza Qur'an kwa ufasaha. Imepokewa kuwa Mtume (s.a.w) amesema: "Mwenye kupenda kuisoma Qur'an kama vile ilivyoteremshwa basi na asome kwa Qiraa-ah (kisomo) cha ibn Ummi ‘Abd" (imepokelewa na Ibn Majah na Ahmad).
Pia, Allah amesema: "وَرَتِّلِ ٱلْقُرْءَانَ تَرْتِيلًا" ("na soma Qur'an kwa tartila" - kisomo cha utaratibu upasao). Katika kuonesha maana ya neno tartila, 'Aliy Ibn Abi Talib ambaye ni khalifa wa nne baada ya kufariki Mtume amesema: "التَّرتيلُ هُوَ تَجويد الحُروفَ ومَعرِفةِ الوقوفِ" ("Ni kuisoma Qur'an kwa ujuzi wa kutamka herufi ipasavyo na kuwa na ujuzi wa hukumu za kusimama").
Kanuni Zinazofungamana na Elimu ya Tajwid
-
Ujuzi wa kujua matamshi ya herufi na yanapopotamkiwa na yanavyotamkwa.
-
Ujuzi wa kujua tabia na sifa za herufi.
-
Ujuzi wa kujua namna ambavyo herufi zinabadilika kulingana na mpangilio wa maneno.
-
Kufanya mazoezi ya ulimi pamoja na kurudia rudia.
Hukumu ya Kujifunza Tajwid
Kusoma Qur'an bila ya Tajwid, yaani kuchunga herufi ipasavyo, ni katika makosa mbele ya maulamaa wa Tajwid. Maulamaa wa elimu hii wanasema kuwa kujifunza Tajwid ni faradhi kifaya (faradhi ya kutoshelezana) kwa kauli za walio wengi. Pia, wapo wanaosema ni faradhi 'ayn (faradhi ya lazima) kwa kila Mwislamu.
Hawa waliosema ni faradhi kifaya wanamaanisha sio faradhi ya lazima kwa wote ila inatosha kwa wachache wakiwa na elimu hii. Kundi hili pia linasema kuwa inapasa kwa msomaji asisome kwa kukosea ijapokuwa hajui hukumu za Tajwid. Yaani, achunge matamshi kama yalivyoandikwa ili asije akatamka vinginevyo na kubadilisha maana.
Mwisho:
Tukutane somo linalofuata utakwenda kujifunza kuhusu herufi saba katika usomaji wa tajwid.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Tajwid somo la 5: makharija al khuruf
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu makharijal khuruf
Soma Zaidi...Tajwid somo la 12: sheria za Iqlab
Katika somo hili utakwenda kujifunzakuhusu hukumu za iqlab katika usomaji wa tajwid.
Soma Zaidi...Tajwid somo la 10: hukumu ya idhhar
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za idhhar na mifano yake.
Soma Zaidi...Tajwid somo la 21: hukumu za madd far’iy
Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu madd far’iy katika usomaji wa Quran tajwid.
Soma Zaidi...Tajwid somo la 9: hukumu za nun sakina na tanwin
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za kitajwid za nun sakina na tanwin
Soma Zaidi...Tajwid somo la 17: hukumu za idgham na idhhar katika laam.
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu idgham na idhhar katika laam.
Soma Zaidi...