Tajwid somo la 1: Maana ya elimu ya Tajwid na kanuni zake

Katika somo hili utakwend akujifunza maana ya elimu ya tajwid kisheria. Pia utajifunza hukumu ya kusoma tajwid.

Maana ya Elimu ya Tajwid

Neno "Tajwid" linatokana na neno la Kiarabu ุฌูŽูˆู‘ูŽุฏูŽ (jawwada) ambalo kilugha lina maana ya "ufundi," yaani kufanya kitu kwa uhodari au ustadi. Kwa mujibu wa Kishariah, maana ya Tajwid ni kuitamka kila herufi kama inavyotakiwa kutamkwa, kwa kuipa haki yake na sifa zake huku ukifuata hukumu zote za Tajwid.

 

Katika Qur'an na Sunnah, imehimizwa sana kusoma Qur'an kwa tajwid au tartila. Elimu hii ya Tajwid ilianza zamani toka enzi za masahaba na wakati Mtume Muhammad (s.a.w) akiwa hai. Mtume alikuwa akiwaelekeza masahaba kwa watu maalumu ili wapate kujifunza Qur'an kwa ufasaha. Imepokewa kuwa Mtume (s.a.w) amesema: "Mwenye kupenda kuisoma Qur'an kama vile ilivyoteremshwa basi na asome kwa Qiraa-ah (kisomo) cha ibn Ummi ‘Abd" (imepokelewa na Ibn Majah na Ahmad).

 

Pia, Allah amesema: "ูˆูŽุฑูŽุชู‘ูู„ู ูฑู„ู’ู‚ูุฑู’ุกูŽุงู†ูŽ ุชูŽุฑู’ุชููŠู„ู‹ุง" ("na soma Qur'an kwa tartila" - kisomo cha utaratibu upasao). Katika kuonesha maana ya neno tartila, 'Aliy Ibn Abi Talib ambaye ni khalifa wa nne baada ya kufariki Mtume amesema: "ุงู„ุชู‘ูŽุฑุชูŠู„ู ู‡ููˆูŽ ุชูŽุฌูˆูŠุฏ ุงู„ุญูุฑูˆููŽ ูˆู…ูŽุนุฑููุฉู ุงู„ูˆู‚ูˆูู" ("Ni kuisoma Qur'an kwa ujuzi wa kutamka herufi ipasavyo na kuwa na ujuzi wa hukumu za kusimama").

Kanuni Zinazofungamana na Elimu ya Tajwid

  1. Ujuzi wa kujua matamshi ya herufi na yanapopotamkiwa na yanavyotamkwa.

  2. Ujuzi wa kujua tabia na sifa za herufi.

  3. Ujuzi wa kujua namna ambavyo herufi zinabadilika kulingana na mpangilio wa maneno.

  4. Kufanya mazoezi ya ulimi pamoja na kurudia rudia.

 

Hukumu ya Kujifunza Tajwid

Kusoma Qur'an bila ya Tajwid, yaani kuchunga herufi ipasavyo, ni katika makosa mbele ya maulamaa wa Tajwid. Maulamaa wa elimu hii wanasema kuwa kujifunza Tajwid ni faradhi kifaya (faradhi ya kutoshelezana) kwa kauli za walio wengi. Pia, wapo wanaosema ni faradhi 'ayn (faradhi ya lazima) kwa kila Mwislamu.

Hawa waliosema ni faradhi kifaya wanamaanisha sio faradhi ya lazima kwa wote ila inatosha kwa wachache wakiwa na elimu hii. Kundi hili pia linasema kuwa inapasa kwa msomaji asisome kwa kukosea ijapokuwa hajui hukumu za Tajwid. Yaani, achunge matamshi kama yalivyoandikwa ili asije akatamka vinginevyo na kubadilisha maana.

 

Mwisho:

Tukutane somo linalofuata utakwenda kujifunza kuhusu herufi saba katika usomaji wa tajwid.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Darsa za Tajwid Main: Dini File: Download PDF Views 752

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    ๐Ÿ‘‰3 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰4 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Tajwid somo la 19: hukumu za madd na aina zake

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu madd na aina zake. Utajifunza herufi za madd na umuhimu wa madd katika tajwid.

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 11: hukumu ya idgham

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za idgham katika tajwid

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 15: hukumu za qalqala

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za Qalaqala katika usomaji wa tajwid.

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 12: sheria za Iqlab

Katika somo hili utakwenda kujifunzakuhusu hukumu za iqlab katika usomaji wa tajwid.

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 22: hukumu za sijdat tilawa

Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu sijda zinazotokea wakati wa kusoma Quran.

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 9: hukumu za nun sakina na tanwin

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za kitajwid za nun sakina na tanwin

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 5: makharija al khuruf

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu makharijal khuruf

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 21: hukumu za madd farโ€™iy

Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu madd farโ€™iy katika usomaji wa Quran tajwid.

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 13: sheria za Al-ikhfaa

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za Al ikhfaa katika usomaji wa Tajwid

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 7: haraka na irabu katika lugha ya kiarabu

Katika somo hili utakwenda kujifunzakuhusu haraka na irabu katika lugha ya kiarabu

Soma Zaidi...