Tajwid somo la 9: hukumu za nun sakina na tanwin
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za kitajwid za nun sakina na tanwin
Maana ya Nuwn Sakina na Tanwin
Nuwn saakinah ni herufi ya nuwn (نْ) isiyokuwa na i’raab ambayo huthibiti katika kutamkwa, kuandikwa, kusimama, na katika kuunganisha. Tanwin hapa tunazungumzia hasa fatahateni, kasrteni na dhuma ten endapo zitakutana ha herufi nini kifanyike.
Wataalamu wa Tajwid wameeleza hukumu nne pindi nuwn sakina au tanwin zinapokutana na herufi. Hukumu hizo ni:
1. الإِظْهاَرْ (Al-Idh'har) - Kudhirisha
Maana: Kudhirisha kitu wazi. Katika hukumu za Tajwid, ni kuitoa kila herufi katika makhraj yake bila ya kuwepo ghunnah. Hii hutokea pale nuwn saakinah au tanwin inapofuatiwa na mojawapo wa herufi sita za al-halq (koo) ambazo ni ء, ه, ح, خ, ع, غ.
2. الإِدْغاَم (Al-Idghaam) - Kuingiza, Kuchanganya
Maana: Kuingiza kitu kwenye kitu. Katika hukumu za Tajwid, ni kuingiza herufi saakin kwenye herufi yenye i’raab na kuzipelekea herufi mbili hizi kuwa herufi moja ya pili nzito. Hii hutokea pale nuwn saakinah au tanwin inapofuatiwa na mojawapo ya herufi sita za idgham ambazo ni ي, ر, م, ل, ن, و.
Sharti za Idghaam
-
Idghaam inafanyika kwenye maneno mawili tu. Herufi ya mwisho ya neno la kwanza iwe na tanwin au nuwn saakinah na herufi ya kwanza ya neno linalofuata iwe ni mojawapo ya herufi za idgham.
Aina za Idghaam
-
Idgham Bighunnah: Kuingiza nuwn saakinah au tanwin kwenye herufi za ي, ن, م, و pamoja na kuleta ghunnah inayotokea puani.
-
Idgham Bighayri Ghunnah: Kuingiza nuwn saakinah au tanwin kwenye herufi za ر, ل bila ya ghunnah.
3. الإقْلاَبْ (Al-Iqlaab) - Kugeuza
Maana: Kugeuza kitu na kukifanya kuwa kitu kingine. Katika hukumu za Tajwid, ni kuigeuza nuwn saakinah au tanwin kwa kuitamka kama miym (م) pamoja na ghunnah. Hii hutokea pale tu nuwn saakinah au tanwin inapokutana na ب (baa).
Mifano
-
"أنبئهم" (anbi'uhum)
4. الإِخِفاء (Al-Ikhfaa) - Kuficha
Maana: Kuficha kitu. Katika hukumu za Tajwid, ni kuificha nuwn saakinah au tanwin katika herufi za ikhfaa. Hivyo nuwn saakinah au tanwin itatamkwa ikiwa baina ya idh'har na idgham kwa kuipa ghunnah isiyokuwa na shaddah. Herufi za ikhfaa ni: ث, ج, د, ذ, ز, س, ش, ص, ض, ط, ظ, ف, ق, ك.
Mifano
-
"من تفعل" (min taf'al)
Mwisho:
Katika somo linalofuata tutakwenda kujifunza zaidikuhusu idhhar na kuona mifano zaidi.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Tajwid somo la 15: hukumu za qalqala
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za Qalaqala katika usomaji wa tajwid.
Soma Zaidi...Tajwid somo la 18: hukumu za waqf wal ibtidai
Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu hukumuza waqfu katika usomajiwa quran.
Soma Zaidi...Tajwid somo la 1: Maana ya elimu ya Tajwid na kanuni zake
Katika somo hili utakwend akujifunza maana ya elimu ya tajwid kisheria. Pia utajifunza hukumu ya kusoma tajwid.
Soma Zaidi...Tajwid somo la 6: sifat al khuruf
hapa utakwenda kujifunza kuhusu sifa za herufi za kiarabu
Soma Zaidi...Tajwid somo la 21: hukumu za madd far’iy
Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu madd far’iy katika usomaji wa Quran tajwid.
Soma Zaidi...Tajwid somo la 20: hukumu za madd twab'iy yaani madd ya asili
Katika somo hili utakwend akujifunza kw akirefu kuhusu madd twab’iy yaani madd za asili.
Soma Zaidi...