picha

Tajwid somo la 9: hukumu za nun sakina na tanwin

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za kitajwid za nun sakina na tanwin

Maana ya Nuwn Sakina na Tanwin

Nuwn saakinah ni herufi ya nuwn (نْ) isiyokuwa na i’raab ambayo huthibiti katika kutamkwa, kuandikwa, kusimama, na katika kuunganisha. Tanwin hapa tunazungumzia hasa fatahateni, kasrteni na dhuma ten endapo zitakutana ha herufi nini kifanyike. 

Wataalamu wa Tajwid wameeleza hukumu nne pindi nuwn sakina au tanwin zinapokutana na herufi. Hukumu hizo ni:

1. الإِظْهاَرْ (Al-Idh'har) - Kudhirisha

Maana: Kudhirisha kitu wazi. Katika hukumu za Tajwid, ni kuitoa kila herufi katika makhraj yake bila ya kuwepo ghunnah. Hii hutokea pale nuwn saakinah au tanwin inapofuatiwa na mojawapo wa herufi sita za al-halq (koo) ambazo ni ء, ه, ح, خ, ع, غ.

2. الإِدْغاَم (Al-Idghaam) - Kuingiza, Kuchanganya

Maana: Kuingiza kitu kwenye kitu. Katika hukumu za Tajwid, ni kuingiza herufi saakin kwenye herufi yenye i’raab na kuzipelekea herufi mbili hizi kuwa herufi moja ya pili nzito. Hii hutokea pale nuwn saakinah au tanwin inapofuatiwa na mojawapo ya herufi sita za idgham ambazo ni ي, ر, م, ل, ن, و.

Sharti za Idghaam

Aina za Idghaam

  1. Idgham Bighunnah: Kuingiza nuwn saakinah au tanwin kwenye herufi za ي, ن, م, و pamoja na kuleta ghunnah inayotokea puani.

  2. Idgham Bighayri Ghunnah: Kuingiza nuwn saakinah au tanwin kwenye herufi za ر, ل bila ya ghunnah.

3. الإقْلاَبْ (Al-Iqlaab) - Kugeuza

Maana: Kugeuza kitu na kukifanya kuwa kitu kingine. Katika hukumu za Tajwid, ni kuigeuza nuwn saakinah au tanwin kwa kuitamka kama miym (م) pamoja na ghunnah. Hii hutokea pale tu nuwn saakinah au tanwin inapokutana na ب (baa).

Mifano

4. الإِخِفاء (Al-Ikhfaa) - Kuficha

Maana: Kuficha kitu. Katika hukumu za Tajwid, ni kuificha nuwn saakinah au tanwin katika herufi za ikhfaa. Hivyo nuwn saakinah au tanwin itatamkwa ikiwa baina ya idh'har na idgham kwa kuipa ghunnah isiyokuwa na shaddah. Herufi za ikhfaa ni: ث, ج, د, ذ, ز, س, ش, ص, ض, ط, ظ, ف, ق, ك.

Mifano

Mwisho:

Katika somo linalofuata tutakwenda kujifunza zaidikuhusu idhhar na kuona mifano zaidi.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-07-14 Topic: Darsa za Tajwid Main: Dini File: Download PDF Views 1797

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii    👉2 web hosting    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 ai web app    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Tajwid somo la 3: aina za viraa katika usomaji wa Quran

Katika somo hili utajifunza kuhusu viraa vya usomaji wa Quran. Viraa hivi ni tofauti na herufi saba

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 16: hukumu za tafkhim na tarqiq

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za tafkhim na tarqiq

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 1: Maana ya elimu ya Tajwid na kanuni zake

Katika somo hili utakwend akujifunza maana ya elimu ya tajwid kisheria. Pia utajifunza hukumu ya kusoma tajwid.

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 13: sheria za Al-ikhfaa

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za Al ikhfaa katika usomaji wa Tajwid

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 4: umuhimu wa kusoma Tajwid

Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu umuhimu wa kusoma elimu ya tajwid.

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 11: hukumu ya idgham

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za idgham katika tajwid

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 15: hukumu za qalqala

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za Qalaqala katika usomaji wa tajwid.

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 19: hukumu za madd na aina zake

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu madd na aina zake. Utajifunza herufi za madd na umuhimu wa madd katika tajwid.

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 12: sheria za Iqlab

Katika somo hili utakwenda kujifunzakuhusu hukumu za iqlab katika usomaji wa tajwid.

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 22: hukumu za sijdat tilawa

Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu sijda zinazotokea wakati wa kusoma Quran.

Soma Zaidi...