Tajwid somo la 9: hukumu za nun sakina na tanwin

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za kitajwid za nun sakina na tanwin

Maana ya Nuwn Sakina na Tanwin

Nuwn saakinah ni herufi ya nuwn (نْ) isiyokuwa na i’raab ambayo huthibiti katika kutamkwa, kuandikwa, kusimama, na katika kuunganisha. Tanwin hapa tunazungumzia hasa fatahateni, kasrteni na dhuma ten endapo zitakutana ha herufi nini kifanyike. 

Wataalamu wa Tajwid wameeleza hukumu nne pindi nuwn sakina au tanwin zinapokutana na herufi. Hukumu hizo ni:

1. الإِظْهاَرْ (Al-Idh'har) - Kudhirisha

Maana: Kudhirisha kitu wazi. Katika hukumu za Tajwid, ni kuitoa kila herufi katika makhraj yake bila ya kuwepo ghunnah. Hii hutokea pale nuwn saakinah au tanwin inapofuatiwa na mojawapo wa herufi sita za al-halq (koo) ambazo ni ء, ه, ح, خ, ع, غ.

2. الإِدْغاَم (Al-Idghaam) - Kuingiza, Kuchanganya

Maana: Kuingiza kitu kwenye kitu. Katika hukumu za Tajwid, ni kuingiza herufi saakin kwenye herufi yenye i’raab na kuzipelekea herufi mbili hizi kuwa herufi moja ya pili nzito. Hii hutokea pale nuwn saakinah au tanwin inapofuatiwa na mojawapo ya herufi sita za idgham ambazo ni ي, ر, م, ل, ن, و.

Sharti za Idghaam

Aina za Idghaam

  1. Idgham Bighunnah: Kuingiza nuwn saakinah au tanwin kwenye herufi za ي, ن, م, و pamoja na kuleta ghunnah inayotokea puani.

  2. Idgham Bighayri Ghunnah: Kuingiza nuwn saakinah au tanwin kwenye herufi za ر, ل bila ya ghunnah.

3. الإقْلاَبْ (Al-Iqlaab) - Kugeuza

Maana: Kugeuza kitu na kukifanya kuwa kitu kingine. Katika hukumu za Tajwid, ni kuigeuza nuwn saakinah au tanwin kwa kuitamka kama miym (م) pamoja na ghunnah. Hii hutokea pale tu nuwn saakinah au tanwin inapokutana na ب (baa).

Mifano

4. الإِخِفاء (Al-Ikhfaa) - Kuficha

Maana: Kuficha kitu. Katika hukumu za Tajwid, ni kuificha nuwn saakinah au tanwin katika herufi za ikhfaa. Hivyo nuwn saakinah au tanwin itatamkwa ikiwa baina ya idh'har na idgham kwa kuipa ghunnah isiyokuwa na shaddah. Herufi za ikhfaa ni: ث, ج, د, ذ, ز, س, ش, ص, ض, ط, ظ, ف, ق, ك.

Mifano

Mwisho:

Katika somo linalofuata tutakwenda kujifunza zaidikuhusu idhhar na kuona mifano zaidi.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Darsa za Tajwid Main: Dini File: Download PDF Views 760

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Tajwid somo la 1: Maana ya elimu ya Tajwid na kanuni zake

Katika somo hili utakwend akujifunza maana ya elimu ya tajwid kisheria. Pia utajifunza hukumu ya kusoma tajwid.

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 17: hukumu za idgham na idhhar katika laam.

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu idgham na idhhar katika laam.

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 15: hukumu za qalqala

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za Qalaqala katika usomaji wa tajwid.

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 22: hukumu za sijdat tilawa

Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu sijda zinazotokea wakati wa kusoma Quran.

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 20: hukumu za madd twab'iy yaani madd ya asili

Katika somo hili utakwend akujifunza kw akirefu kuhusu madd twab’iy yaani madd za asili.

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 11: hukumu ya idgham

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za idgham katika tajwid

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 5: makharija al khuruf

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu makharijal khuruf

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 12: sheria za Iqlab

Katika somo hili utakwenda kujifunzakuhusu hukumu za iqlab katika usomaji wa tajwid.

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 7: haraka na irabu katika lugha ya kiarabu

Katika somo hili utakwenda kujifunzakuhusu haraka na irabu katika lugha ya kiarabu

Soma Zaidi...
Tajwid somo la 8: hukumu za kusoma basmala na isti'adha

Katika somo hili utakwenda kujifunza kanuni za usomaji wa isti’adha na basmallah.

Soma Zaidi...