Tajwid somo la 4: umuhimu wa kusoma Tajwid
Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu umuhimu wa kusoma elimu ya tajwid.
Fadhila na Umuhimu wa Tajwid
Elimu ya Tajwid ina umuhimu mkubwa katika umma wa Kiislamu. Msomaji wa Qur'an kama hatachunga kisomo anaweza kubadilisha maana ya Qur'an kabisa. Hivyo, elimu ya Tajwid ni msingi wa kuchunga maana ya matamshi ya Qur'an katika usomaji.
Tunahitajia imamu mwenye kiraa nzuri kwa sauti pia awe anajua Tajwid na anaitumia ipasavyo. Mtume (s.a.w) amesema: "Kutoka kwa Abu Mas’uud Al-Answaariyy (r.a) amesema: Mtume (s.a.w) amesema: 'Awaswalishe watu yule mwenye kujua Kitabu cha Allah na wakiwa katika kusoma wako sawa, basi mwenye ujuzi zaidi wa Sunnah, na wakiwa kwenye Sunnah wako sawa, basi aliyetangulia Hijra, na wakiwa katika Hijra wako sawa, basi mkubwa wao kwa umri, wala asiswalishe mtu (mwengine) katika nyumba yake wala katika mamlaka yake wala asikae mahali pake pa heshima isipokuwa kwa idhini yake.'"
Watu hupenda kusikiliza kiraa cha mtu anayesoma vizuri kwa sauti na kuchunga hukumu za Tajwid. Mtume (s.a.w) amesema: "Kutoka kwa Abu Musa Al-’Ash’ariyy (r.a) kwamba Mtume kamwambia: 'Ungeliniona jana nilivyokuwa nakusikiliza kisomo chako. Hakika umepewa mizumari miongoni mwa mizumari ya aila ya Daud.'"
Msomaji wa Qur'an atakuwa pamoja na malaika wema wenye kuandika. 'Aaishah (r.a) amesema: Mtume (s.a.w) amesema: "Yule aliyekuwa hodari wa kusoma Qur'an atakuwa pamoja na Malaika Waandishi (wa Allah) watukufu wema, na yule ambaye anaisoma Qur'an kwa mashaka na huku anajitahidi kwa kudodosa atapata ujira mara mbili."
Mwisho:
Katika somo linalofuata utakwenda kujifunza kuhusu makharija al khuruf katika herufi za kiarabu
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
๐1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina ๐2 Kitau cha Fiqh ๐3 kitabu cha Simulizi ๐4 Simulizi za Hadithi Audio ๐5 Bongolite - Game zone - Play free game ๐6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Tajwid somo la 15: hukumu za qalqala
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za Qalaqala katika usomaji wa tajwid.
Soma Zaidi...Tajwid somo la 8: hukumu za kusoma basmala na isti'adha
Katika somo hili utakwenda kujifunza kanuni za usomaji wa istiโadha na basmallah.
Soma Zaidi...Tajwid somo la 9: hukumu za nun sakina na tanwin
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za kitajwid za nun sakina na tanwin
Soma Zaidi...Tajwid somo la 7: haraka na irabu katika lugha ya kiarabu
Katika somo hili utakwenda kujifunzakuhusu haraka na irabu katika lugha ya kiarabu
Soma Zaidi...Tajwid somo la 21: hukumu za madd farโiy
Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu madd farโiy katika usomaji wa Quran tajwid.
Soma Zaidi...Tajwid somo la 22: hukumu za sijdat tilawa
Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu sijda zinazotokea wakati wa kusoma Quran.
Soma Zaidi...