Tajwid somo la 4: umuhimu wa kusoma Tajwid
Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu umuhimu wa kusoma elimu ya tajwid.
Fadhila na Umuhimu wa Tajwid
Elimu ya Tajwid ina umuhimu mkubwa katika umma wa Kiislamu. Msomaji wa Qur'an kama hatachunga kisomo anaweza kubadilisha maana ya Qur'an kabisa. Hivyo, elimu ya Tajwid ni msingi wa kuchunga maana ya matamshi ya Qur'an katika usomaji.
Tunahitajia imamu mwenye kiraa nzuri kwa sauti pia awe anajua Tajwid na anaitumia ipasavyo. Mtume (s.a.w) amesema: "Kutoka kwa Abu Mas’uud Al-Answaariyy (r.a) amesema: Mtume (s.a.w) amesema: 'Awaswalishe watu yule mwenye kujua Kitabu cha Allah na wakiwa katika kusoma wako sawa, basi mwenye ujuzi zaidi wa Sunnah, na wakiwa kwenye Sunnah wako sawa, basi aliyetangulia Hijra, na wakiwa katika Hijra wako sawa, basi mkubwa wao kwa umri, wala asiswalishe mtu (mwengine) katika nyumba yake wala katika mamlaka yake wala asikae mahali pake pa heshima isipokuwa kwa idhini yake.'"
Watu hupenda kusikiliza kiraa cha mtu anayesoma vizuri kwa sauti na kuchunga hukumu za Tajwid. Mtume (s.a.w) amesema: "Kutoka kwa Abu Musa Al-’Ash’ariyy (r.a) kwamba Mtume kamwambia: 'Ungeliniona jana nilivyokuwa nakusikiliza kisomo chako. Hakika umepewa mizumari miongoni mwa mizumari ya aila ya Daud.'"
Msomaji wa Qur'an atakuwa pamoja na malaika wema wenye kuandika. 'Aaishah (r.a) amesema: Mtume (s.a.w) amesema: "Yule aliyekuwa hodari wa kusoma Qur'an atakuwa pamoja na Malaika Waandishi (wa Allah) watukufu wema, na yule ambaye anaisoma Qur'an kwa mashaka na huku anajitahidi kwa kudodosa atapata ujira mara mbili."
Mwisho:
Katika somo linalofuata utakwenda kujifunza kuhusu makharija al khuruf katika herufi za kiarabu
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Bongolite - Game zone - Play free game π2 web hosting π3 Madrasa kiganjani π4 Kitau cha Fiqh π5 Simulizi za Hadithi Audio π6 ai web app
Post zinazofanana:
Tajwid somo la 1: Maana ya elimu ya Tajwid na kanuni zake
Katika somo hili utakwend akujifunza maana ya elimu ya tajwid kisheria. Pia utajifunza hukumu ya kusoma tajwid.
Soma Zaidi...Tajwid somo la 14: kuhumu za mim sakina
Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu hukumu za ki tajwid za mim sakina.
Soma Zaidi...Tajwid somo la 8: hukumu za kusoma basmala na isti'adha
Katika somo hili utakwenda kujifunza kanuni za usomaji wa istiβadha na basmallah.
Soma Zaidi...Tajwid somo la 18: hukumu za waqf wal ibtidai
Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu hukumuza waqfu katika usomajiwa quran.
Soma Zaidi...Tajwid somo la 11: hukumu ya idgham
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za idgham katika tajwid
Soma Zaidi...Tajwid somo la 17: hukumu za idgham na idhhar katika laam.
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu idgham na idhhar katika laam.
Soma Zaidi...