Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu umuhimu wa kusoma elimu ya tajwid.
Elimu ya Tajwid ina umuhimu mkubwa katika umma wa Kiislamu. Msomaji wa Qur'an kama hatachunga kisomo anaweza kubadilisha maana ya Qur'an kabisa. Hivyo, elimu ya Tajwid ni msingi wa kuchunga maana ya matamshi ya Qur'an katika usomaji.
Tunahitajia imamu mwenye kiraa nzuri kwa sauti pia awe anajua Tajwid na anaitumia ipasavyo. Mtume (s.a.w) amesema: "Kutoka kwa Abu Mas’uud Al-Answaariyy (r.a) amesema: Mtume (s.a.w) amesema: 'Awaswalishe watu yule mwenye kujua Kitabu cha Allah na wakiwa katika kusoma wako sawa, basi mwenye ujuzi zaidi wa Sunnah, na wakiwa kwenye Sunnah wako sawa, basi aliyetangulia Hijra, na wakiwa katika Hijra wako sawa, basi mkubwa wao kwa umri, wala asiswalishe mtu (mwengine) katika nyumba yake wala katika mamlaka yake wala asikae mahali pake pa heshima isipokuwa kwa idhini yake.'"
Watu hupenda kusikiliza kiraa cha mtu anayesoma vizuri kwa sauti na kuchunga hukumu za Tajwid. Mtume (s.a.w) amesema: "Kutoka kwa Abu Musa Al-’Ash’ariyy (r.a) kwamba Mtume kamwambia: 'Ungeliniona jana nilivyokuwa nakusikiliza kisomo chako. Hakika umepewa mizumari miongoni mwa mizumari ya aila ya Daud.'"
Msomaji wa Qur'an atakuwa pamoja na malaika wema wenye kuandika. 'Aaishah (r.a) amesema: Mtume (s.a.w) amesema: "Yule aliyekuwa hodari wa kusoma Qur'an atakuwa pamoja na Malaika Waandishi (wa Allah) watukufu wema, na yule ambaye anaisoma Qur'an kwa mashaka na huku anajitahidi kwa kudodosa atapata ujira mara mbili."
Mwisho:
Katika somo linalofuata utakwenda kujifunza kuhusu makharija al khuruf katika herufi za kiarabu
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu madd farโiy katika usomaji wa Quran tajwid.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za kitajwid za nun sakina na tanwin
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu madd na aina zake. Utajifunza herufi za madd na umuhimu wa madd katika tajwid.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za idgham katika tajwid
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza kuhusu viraa vya usomaji wa Quran. Viraa hivi ni tofauti na herufi saba
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu hukumuza waqfu katika usomajiwa quran.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu hukumu za ki tajwid za mim sakina.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza kw akirefu kuhusu madd twabโiy yaani madd za asili.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu herufi saba katika usomaji wa tajwid.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za Al ikhfaa katika usomaji wa Tajwid
Soma Zaidi...