Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu umuhimu wa kusoma elimu ya tajwid.
Elimu ya Tajwid ina umuhimu mkubwa katika umma wa Kiislamu. Msomaji wa Qur'an kama hatachunga kisomo anaweza kubadilisha maana ya Qur'an kabisa. Hivyo, elimu ya Tajwid ni msingi wa kuchunga maana ya matamshi ya Qur'an katika usomaji.
Tunahitajia imamu mwenye kiraa nzuri kwa sauti pia awe anajua Tajwid na anaitumia ipasavyo. Mtume (s.a.w) amesema: "Kutoka kwa Abu Mas’uud Al-Answaariyy (r.a) amesema: Mtume (s.a.w) amesema: 'Awaswalishe watu yule mwenye kujua Kitabu cha Allah na wakiwa katika kusoma wako sawa, basi mwenye ujuzi zaidi wa Sunnah, na wakiwa kwenye Sunnah wako sawa, basi aliyetangulia Hijra, na wakiwa katika Hijra wako sawa, basi mkubwa wao kwa umri, wala asiswalishe mtu (mwengine) katika nyumba yake wala katika mamlaka yake wala asikae mahali pake pa heshima isipokuwa kwa idhini yake.'"
Watu hupenda kusikiliza kiraa cha mtu anayesoma vizuri kwa sauti na kuchunga hukumu za Tajwid. Mtume (s.a.w) amesema: "Kutoka kwa Abu Musa Al-’Ash’ariyy (r.a) kwamba Mtume kamwambia: 'Ungeliniona jana nilivyokuwa nakusikiliza kisomo chako. Hakika umepewa mizumari miongoni mwa mizumari ya aila ya Daud.'"
Msomaji wa Qur'an atakuwa pamoja na malaika wema wenye kuandika. 'Aaishah (r.a) amesema: Mtume (s.a.w) amesema: "Yule aliyekuwa hodari wa kusoma Qur'an atakuwa pamoja na Malaika Waandishi (wa Allah) watukufu wema, na yule ambaye anaisoma Qur'an kwa mashaka na huku anajitahidi kwa kudodosa atapata ujira mara mbili."
Mwisho:
Katika somo linalofuata utakwenda kujifunza kuhusu makharija al khuruf katika herufi za kiarabu
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya hapa chini kuipakua sasa!
Umeionaje Makala hii.. ?
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za idhhar na mifano yake.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu hukumuza waqfu katika usomajiwa quran.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza maana ya elimu ya tajwid kisheria. Pia utajifunza hukumu ya kusoma tajwid.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza kuhusu viraa vya usomaji wa Quran. Viraa hivi ni tofauti na herufi saba
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za idgham katika tajwid
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza kw akirefu kuhusu madd twabโiy yaani madd za asili.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za Al ikhfaa katika usomaji wa Tajwid
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu madd farโiy katika usomaji wa Quran tajwid.
Soma Zaidi...hapa utakwenda kujifunza kuhusu sifa za herufi za kiarabu
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu makharijal khuruf
Soma Zaidi...