Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu herufi saba katika usomaji wa tajwid.
Wataalamu wa Tajwid wanaeleza kuhusu herufi saba za usomaji wa Qur'an. Qur'an imeshuka kwa lugha ya Kiarabu, na Waarabu wenyewe walitofautiana katika lahaja za lugha ya Kiarabu. Lahaja hizi zilikuwa za makabila saba ya Kiarabu yaliyopo Makkah. Hii ina maana kuwa Waarabu walikuwa na makabila saba wakati huo, na ingawa walizungumza Kiarabu, walitofautiana katika maneno, utamkaji, na hata uandishi. Lahaja hizi zilijulikana kama herufi saba za usomaji wa Qur'an.
Lahaja hizi saba ndizo chanzo cha hizi herufi saba. Hili linathibitika katika maneno ya Mtume Muhammad (s.a.w) aliposema: "Jibriyl alinisomea kwa herufi moja, nikaifanyia marudio mpaka akanifundisha nyingine, nikaendelea kumuomba nyinginezo mpaka mwishowe zikawa herufi (lahaja) saba" (Bukhari na Ahmad).
Makabila haya yalikuwa Quraysh, Hudhayl, Thaqiyf, Hawaazin, Kinaanah, Tamiym, na Yemen. Hivyo, Qur'an ilishuka katika lahaja saba kulingana na makabila haya, na kila kabila linasoma Qur'an kwa namna ambavyo lahaja yao inawafanya waelewe. Wakawa watu wanaandika Qur'an kwa namna wanavyoelewa wao kulingana na lahaja ya kabila lao. Hali hii ilifanya usomaji wa Qur'an utofautiane. Mifano ni kama ifuatavyo: "‘alayhim" wengine walitamka "‘alayhimuw," neno "swiraatw" walitamka wengine "zwiraatw" na wengine "siraatw," na "muumin" wengine walitamka "muwmin."
Amesimulia ‘Umar Ibn Al-Khatab kuwa: “Nilimsikia Hishaam ibn Hakiym akisoma Suratul-Furqan tofauti na vile ninavyoisoma na alivyonifundisha Mtume (s.a.w). Nilikaribia kumsimamisha (asiswalishe) lakini nikamvumilia mpaka akamaliza, kisha nikamshika nguo yake shingoni na kumvuta mpaka kwa Mtume (s.a.w) na kusema: "Nimesikia huyu mtu akisoma (Suratul-Furqan) kinyume na ulivyonifundisha." Mtume (s.a.w) akasema: "Mwachie!" Akamwambia (Hishaam): "Soma." Akasoma. Akasema: "Hivi ndivyo ilivyoteremshwa." Kisha akaniambia mimi: "Soma." Nikasoma. Akasema: "Hivi ndivyo ilivyoteremshwa. Hakika Qur'an imeteremshwa kwa herufi saba, hivyo someni iliyokuwa sahali kwenu."
Uislamu ulipoenea zaidi, ikaonekana haja ya kuiandika Qur'an katika lahaja moja ili kuepuka makosa katika usomaji. Katika utawala wa Uthman (r.a), kikundi cha maswahaba kilichokuwa kikiongozwa na Hudhayfah bin al-Yamaaniy kilikuja kwa Uthman (r.a) na kumsihi "auokoe ummah wa Kiislamu kabla haujatofautiana juu ya Qur'an." Uthman (r.a) akaamrisha chini ya uongozi wa Zayd bin Thaabit (r.a) nakala za Qur'an ziandikwe na nakala zote zisizo rasmi zichomwe moto.
Lahaja iliyotumika kuandika Qur'an ilikuwa ile ya Kikuraysh, na msahafu ukajulikana kama 'Msahafu wa Uthman'. Nakala hizo zilisambazwa miji mikuu ya Waislamu kama nuskhah (nakala) rasmi, na nuskhah ya asili ikabakishwa kwa Mama wa Waumini Hafsah (r.a). Zayd bin Thaabit alibaki Madina, 'Abdullah bin Swa’ib alitumwa Makkah, Mughiyrah bin Shu'bah alitumwa Syria, Abu 'Abdur-Rahmaan As-Sulamy alitumwa Kufa, na 'Aamir bin 'Abdil-Qays alitumwa Basra.
Baada ya msahafu huu kusambazwa katika dola ya Kiislamu, lahaja zote zisizo rasmi zilipotea. Msahafu huu ndio chimbuko la misahafu tuliyonayo leo. Ingawa kuna tofauti kubwa za kiuandishi kati ya misahafu ya leo na msahafu huu, kwa mfano, msahafu huu haukuwa na nukta kwenye herufi au irabu pia hazikuwepo. Hayo yalifanyika baadaye kadiri Uislamu ulipoenea maeneo mbalimbali ya dunia na ikaonekana ugumu wa kutumia msahafu ule kwa watu wasiokuwa Waarabu.
Mwisho:
Tukutane somo linalofuata tutakwenda kujifunza kuhusu aina za viraa katika usomaji wa Tajwid
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu idgham na idhhar katika laam.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu madd farβiy katika usomaji wa Quran tajwid.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu madd na aina zake. Utajifunza herufi za madd na umuhimu wa madd katika tajwid.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu hukumu za ki tajwid za mim sakina.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za Qalaqala katika usomaji wa tajwid.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu sijda zinazotokea wakati wa kusoma Quran.
Soma Zaidi...hapa utakwenda kujifunza kuhusu sifa za herufi za kiarabu
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu makharijal khuruf
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za idgham katika tajwid
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za idhhar na mifano yake.
Soma Zaidi...