image

Tajwid somo la 2: herufi saba katikausomaji wa quran

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu herufi saba katika usomaji wa tajwid.

Herufi Saba

Wataalamu wa Tajwid wanaeleza kuhusu herufi saba za usomaji wa Qur'an. Qur'an imeshuka kwa lugha ya Kiarabu, na Waarabu wenyewe walitofautiana katika lahaja za lugha ya Kiarabu. Lahaja hizi zilikuwa za makabila saba ya Kiarabu yaliyopo Makkah. Hii ina maana kuwa Waarabu walikuwa na makabila saba wakati huo, na ingawa walizungumza Kiarabu, walitofautiana katika maneno, utamkaji, na hata uandishi. Lahaja hizi zilijulikana kama herufi saba za usomaji wa Qur'an.

 

Lahaja hizi saba ndizo chanzo cha hizi herufi saba. Hili linathibitika katika maneno ya Mtume Muhammad (s.a.w) aliposema: "Jibriyl alinisomea kwa herufi moja, nikaifanyia marudio mpaka akanifundisha nyingine, nikaendelea kumuomba nyinginezo mpaka mwishowe zikawa herufi (lahaja) saba" (Bukhari na Ahmad).

Makabila haya yalikuwa Quraysh, Hudhayl, Thaqiyf, Hawaazin, Kinaanah, Tamiym, na Yemen. Hivyo, Qur'an ilishuka katika lahaja saba kulingana na makabila haya, na kila kabila linasoma Qur'an kwa namna ambavyo lahaja yao inawafanya waelewe. Wakawa watu wanaandika Qur'an kwa namna wanavyoelewa wao kulingana na lahaja ya kabila lao. Hali hii ilifanya usomaji wa Qur'an utofautiane. Mifano ni kama ifuatavyo: "‘alayhim" wengine walitamka "‘alayhimuw," neno "swiraatw" walitamka wengine "zwiraatw" na wengine "siraatw," na "muumin" wengine walitamka "muwmin."

 

Amesimulia ‘Umar Ibn Al-Khatab kuwa: “Nilimsikia Hishaam ibn Hakiym akisoma Suratul-Furqan tofauti na vile ninavyoisoma na alivyonifundisha Mtume (s.a.w). Nilikaribia kumsimamisha (asiswalishe) lakini nikamvumilia mpaka akamaliza, kisha nikamshika nguo yake shingoni na kumvuta mpaka kwa Mtume (s.a.w) na kusema: "Nimesikia huyu mtu akisoma (Suratul-Furqan) kinyume na ulivyonifundisha." Mtume (s.a.w) akasema: "Mwachie!" Akamwambia (Hishaam): "Soma." Akasoma. Akasema: "Hivi ndivyo ilivyoteremshwa." Kisha akaniambia mimi: "Soma." Nikasoma. Akasema: "Hivi ndivyo ilivyoteremshwa. Hakika Qur'an imeteremshwa kwa herufi saba, hivyo someni iliyokuwa sahali kwenu."

 

Kuenea kwa Uislamu na Uhitaji wa Msahafu Moja

Uislamu ulipoenea zaidi, ikaonekana haja ya kuiandika Qur'an katika lahaja moja ili kuepuka makosa katika usomaji. Katika utawala wa Uthman (r.a), kikundi cha maswahaba kilichokuwa kikiongozwa na Hudhayfah bin al-Yamaaniy kilikuja kwa Uthman (r.a) na kumsihi "auokoe ummah wa Kiislamu kabla haujatofautiana juu ya Qur'an." Uthman (r.a) akaamrisha chini ya uongozi wa Zayd bin Thaabit (r.a) nakala za Qur'an ziandikwe na nakala zote zisizo rasmi zichomwe moto.

 

Lahaja iliyotumika kuandika Qur'an ilikuwa ile ya Kikuraysh, na msahafu ukajulikana kama 'Msahafu wa Uthman'. Nakala hizo zilisambazwa miji mikuu ya Waislamu kama nuskhah (nakala) rasmi, na nuskhah ya asili ikabakishwa kwa Mama wa Waumini Hafsah (r.a). Zayd bin Thaabit alibaki Madina, 'Abdullah bin Swa’ib alitumwa Makkah, Mughiyrah bin Shu'bah alitumwa Syria, Abu 'Abdur-Rahmaan As-Sulamy alitumwa Kufa, na 'Aamir bin 'Abdil-Qays alitumwa Basra.

 

Baada ya msahafu huu kusambazwa katika dola ya Kiislamu, lahaja zote zisizo rasmi zilipotea. Msahafu huu ndio chimbuko la misahafu tuliyonayo leo. Ingawa kuna tofauti kubwa za kiuandishi kati ya misahafu ya leo na msahafu huu, kwa mfano, msahafu huu haukuwa na nukta kwenye herufi au irabu pia hazikuwepo. Hayo yalifanyika baadaye kadiri Uislamu ulipoenea maeneo mbalimbali ya dunia na ikaonekana ugumu wa kutumia msahafu ule kwa watu wasiokuwa Waarabu.

Mwisho:

Tukutane somo linalofuata tutakwenda kujifunza kuhusu aina za viraa katika usomaji wa Tajwid

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-07-14 16:35:11 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 79


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Tajwid somo la 2: herufi saba katikausomaji wa quran
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu herufi saba katika usomaji wa tajwid. Soma Zaidi...

Tajwid somo la 9: hukumu za nun sakina na tanwin
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za kitajwid za nun sakina na tanwin Soma Zaidi...

Tajwid somo la 4: umuhimu wa kusoma Tajwid
Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu umuhimu wa kusoma elimu ya tajwid. Soma Zaidi...

Tajwid somo la 18: hukumu za waqf wal ibtidai
Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu hukumuza waqfu katika usomajiwa quran. Soma Zaidi...

Tajwid somo la 12: sheria za Iqlab
Katika somo hili utakwenda kujifunzakuhusu hukumu za iqlab katika usomaji wa tajwid. Soma Zaidi...

Tajwid somo la 1: Maana ya elimu ya Tajwid na kanuni zake
Katika somo hili utakwend akujifunza maana ya elimu ya tajwid kisheria. Pia utajifunza hukumu ya kusoma tajwid. Soma Zaidi...

Tajwid somo la 19: hukumu za madd na aina zake
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu madd na aina zake. Utajifunza herufi za madd na umuhimu wa madd katika tajwid. Soma Zaidi...

Tajwid somo la 20: hukumu za madd twab'iy yaani madd ya asili
Katika somo hili utakwend akujifunza kw akirefu kuhusu madd twab’iy yaani madd za asili. Soma Zaidi...

Tajwid somo la 5: makharija al khuruf
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu makharijal khuruf Soma Zaidi...

Tajwid somo la 10: hukumu ya idhhar
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za idhhar na mifano yake. Soma Zaidi...

Tajwid somo la 7: haraka na irabu katika lugha ya kiarabu
Katika somo hili utakwenda kujifunzakuhusu haraka na irabu katika lugha ya kiarabu Soma Zaidi...

Tajwid somo la 16: hukumu za tafkhim na tarqiq
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu hukumu za tafkhim na tarqiq Soma Zaidi...