picha

Shahada mbili

Kwenye mada hii tutajifunza shahada mbili,tafsiri ya shahada kstika maisha ya kila siku.

6.2.Shahada Mbili.

 “Nashuhudia kuwa hapana Mola ila Allah”

 

-     Kiutendaji maana yake ni kuahidi kwa dhati utaishi kila kipengele cha maisha yako kwa kumtii Allah (s.w) katika maamrisho na makatazo yake.

 

-     Pia ni kuahidi kuwa hutamtii yeyote isipokuwa Allah (s.w) na kuendesha maisha yote kwa mujibu wa Qur’an na Sunnah.

 

“Na ninashuhudia kuwa Muhammad ni Mtume wa Allah”

 

-    Kiutendaji maana yake ni kuahidi kuishi kwa kufuata mafundisho ya Mtume (s.a.w) na kuacha aliyoyakataza.

Rejea Qur’an (59:7).

 

-    Pia ni kuahidi kufuata mwenendo na tabia za Mtume (s.a.w) kama kiigizo cha maisha yetu yote.

Rejea Qur’an (33:21).

 

 

-     Shahada haikamiliki kwa kutoa shahada ya kwanza tu ni lazima uongeze na ya pili kwa sababu Mtume (s.a.w) ndiye mwalimu aliyeteuliwa na Allah (s.w) kuufundisha wahyi kwa wanaadamu ili kumtambua na kuweza kumuabudu yeye ipasavyo.

 

  1. Shahada ya Moyoni.

-     Ni ile inayoyakinishwa kwa dhati moyoni bila ya chembe ya shaka juu ya kuwepo Allah (s.w) na juu ya Utume wa Muhammad (s.a.w).

Rejea Qur’an (49:14-15).

 

2.Shahada ya Matamshi (Ulimini).

-     Ni lazima shahada baada ya kuyakinishwa moyoni itamkwe dhahiri mbele ya umma wa Kiislamu ili kumtabulisha kwao kwa lengo la kujenga udugu naye na kuwa ummah mmoja.

Rejea Qur’an (9:33), (61:9), (48:28), (49:10), (61:4) na (3:102).

 

3.Shahada ya Vitendo.

-     Shahada ya kweli ni ile baada ya kuyakinishwa moyoni na kutamkwa kwa ulimi hudhihirishwa katika vitendo vya maisha ya kila siku ya muislamu.

 

-     Shahada ya matamshi bila kudhihirishwa katika matendo ni udanganyifu kwa mtoaji na ummah wa Kiislamu, na haikubaliki mbele ya Allah (s.w).

Rejea Qur’an (49:14).

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 4328

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 web hosting    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 Dua za Mitume na Manabii    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Kwa nini hakuna haja ya Mtume mwingine baada ya Muhammad

Na tukiutafiti Uislamu kwa makini kama mfumo kamili wa maisha tunaona unadhihiri ukweli wa aya hii ya Qur-an.

Soma Zaidi...
KUAMINI MALAIKA

Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala

Soma Zaidi...
Maana ya kuamini malaika katika maisha ya kila siku

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mitume wa uongo

Wafuatao ni baadhi ya wale waliodai utume wakati Mtume (s.

Soma Zaidi...
Maswali juu ya dini anayostahiki kufuata mwanadamu

Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Sifa za waumini wa ukweli katika uislamu

Je unamjuwq ni nani muumini, na ni zipi sifa za muumini?

Soma Zaidi...
Dalili za kuwepo mwenyezi Mungu

Nguzo za Imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Haki za kielimu za mwanamke katika uislamu

Haki ya ElimuKatika Uislamu kujielimisha ni faradhi inayowahusu Waislamu wote, wanaume na wanawake: "Soma kwa jina ?

Soma Zaidi...
KUAMINI VITABU VYA ALLAH (S.W)

Mtu hawi Muumini wa kweli mpaka awe na yakini juu ya vitabu vya Allah (s.

Soma Zaidi...