Shahada mbili

Kwenye mada hii tutajifunza shahada mbili,tafsiri ya shahada kstika maisha ya kila siku.

6.2.Shahada Mbili.

 “Nashuhudia kuwa hapana Mola ila Allah”

 

-     Kiutendaji maana yake ni kuahidi kwa dhati utaishi kila kipengele cha maisha yako kwa kumtii Allah (s.w) katika maamrisho na makatazo yake.

 

-     Pia ni kuahidi kuwa hutamtii yeyote isipokuwa Allah (s.w) na kuendesha maisha yote kwa mujibu wa Qur’an na Sunnah.

 

“Na ninashuhudia kuwa Muhammad ni Mtume wa Allah”

 

-    Kiutendaji maana yake ni kuahidi kuishi kwa kufuata mafundisho ya Mtume (s.a.w) na kuacha aliyoyakataza.

Rejea Qur’an (59:7).

 

-    Pia ni kuahidi kufuata mwenendo na tabia za Mtume (s.a.w) kama kiigizo cha maisha yetu yote.

Rejea Qur’an (33:21).

 

 

-     Shahada haikamiliki kwa kutoa shahada ya kwanza tu ni lazima uongeze na ya pili kwa sababu Mtume (s.a.w) ndiye mwalimu aliyeteuliwa na Allah (s.w) kuufundisha wahyi kwa wanaadamu ili kumtambua na kuweza kumuabudu yeye ipasavyo.

 

  1. Shahada ya Moyoni.

-     Ni ile inayoyakinishwa kwa dhati moyoni bila ya chembe ya shaka juu ya kuwepo Allah (s.w) na juu ya Utume wa Muhammad (s.a.w).

Rejea Qur’an (49:14-15).

 

2.Shahada ya Matamshi (Ulimini).

-     Ni lazima shahada baada ya kuyakinishwa moyoni itamkwe dhahiri mbele ya umma wa Kiislamu ili kumtabulisha kwao kwa lengo la kujenga udugu naye na kuwa ummah mmoja.

Rejea Qur’an (9:33), (61:9), (48:28), (49:10), (61:4) na (3:102).

 

3.Shahada ya Vitendo.

-     Shahada ya kweli ni ile baada ya kuyakinishwa moyoni na kutamkwa kwa ulimi hudhihirishwa katika vitendo vya maisha ya kila siku ya muislamu.

 

-     Shahada ya matamshi bila kudhihirishwa katika matendo ni udanganyifu kwa mtoaji na ummah wa Kiislamu, na haikubaliki mbele ya Allah (s.w).

Rejea Qur’an (49:14).

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 4212

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 Dua za Mitume na Manabii    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Makundi ya dini za wanaadamu

Kwenye kipengele hichi tutajifunza makundi ya dini za watu. Na makundi hayo ni matatu.

Soma Zaidi...
Tofauti kati ya Quran na vitabu vingine vya mwenyezi Mungu

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kwa nini hakuna haja ya Mtume mwingine baada ya Muhammad

Na tukiutafiti Uislamu kwa makini kama mfumo kamili wa maisha tunaona unadhihiri ukweli wa aya hii ya Qur-an.

Soma Zaidi...
Lengo la kushushwa vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika Surat ahzab

Na waliposema wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao, "Mwenyezi Mungu na Mtume wake hawakutuahidi ila udanganyifu tu.

Soma Zaidi...
Maana ya Elimu katika uislamu na nani aliye elimika?

Hili ni swali kutoka katika maarifa ya elimu ya dini ya kiislamu kidato cha kwanza (EDK FORM 1)

Soma Zaidi...