picha

Fangasi wanaosababisha mapunye dalili zao na jinsi ya kupambana nao

Fangasi hawa ni maarufu sana kwa mapunye ya kichwani ama kwenye ngozi mikononi ama miguuni.

Fangasi wanaosababisha mapunye dalili zao na jinsi ya kupambana nao

2. Fangasi wa mapunye;

Fangasi hawa ni maarufu sana kwa mapunye ya kichwani ama kwenye ngozi mikononi ama miguuni. Kitaalamu fangasi hawa hujulikana kama tinea” au “dermatophytosis.  Na kwa maarufu sana wanafahamika kama ringworm kwa kuwa wanatoa mabako ya mduara kwenye ngozi.

 

Fangasi hawa wanaweza kukaa kwenye ngozi, kuta, nguo, taulo na maeneo mengine. Miongoni mwa dalili zao ni kuona maduara kwenye ngozi, mara nyingi dalili za fangasi hawa huweza kuonekana kuanzia siku 4 mpaka 14 baada ya ngozi kupata maambukizi ya fangasi hawa. zifuatazo ni katika dalili za fangasi hawa:-

  • Kuwasha kwa ngozi na maumivu wakati mwingine
  • Kuwepo kwa mapele ama ukurutu uliotengeneza umbo la duara
  • Ngoz kuwa nyekundu, kupasuka ama kuwa kavu
  • Kukatika ama kunyonyoka kwa nywele kwenye sehemu iliyo athirika

 

Fangasi hawa wanaweza kukaa katika maeneo mbalimbali ya mwili na kusababisha dalili tofautitofauti kulingana na eneo lililo athirika. Kwa mfano;-

 

Fangasi hawa wakiwa kwenye nyayo (sthlete’s foot) huweza kuonesha dalili kama nyayo kuwa nyekundu, kuvimba ama kujaa maji, ngoxi kutoka ama kubabuka, kuwasha kwa ngozi katikati ya vidole na kidole na mara nyingi kati ya kidole kidogo na kinachomfatilia. Wakati mwingine kisigino na nyayo huweza kuathirika na kuweka mabumbuza.

 

Kwenye kichwa, fangasi hawa huweka maduara yaliyo nyonyoka ngozi, yakiwa na ukurutu, ngozi kavu, na kuwasha. Maduara haya maarufu tunayaita mapunye, yanaweza kuwa mengi na kuungana kufanya duara moja kubwa. Mara nyingi sana fangasi wa kichwani huwapata sana watoto kuliko watu wazima.

 

Kwenye pachipachi za mapaja (jock itch). Fangasi hawa hukaa sehemu ya ndani ya mapaja karibu na sehemu za siri ama kuzungukia eneo hilo, lakini wanashambulia mapaja. Miongoni mwa dalili zao ni mapaja kufanya wekundu, kuwasha na hali inaweza kuwa mbaya mpaka ngozi ikababuka na hatimaye kufanya vidonda kwa kujikuna. Wanaweza kushambulia pia korodani na kufanya ibabuke, iwe nyekundu na kuweka vidonda.

 

Fangasi wa kwenye ndevu (tinea barbae). fangasi hawa wanashambulia maeneo ambayo ndevu zinapatikana kama kwenye kidevu na shavu. Dalili zao ni kuwasha kwa kidevu, shavu, na sehemu ya juu ya shingo. Fangasi hawa wanaweza kuwa hatari zaidi na kusababisha mapele yenye usaha kwenye eneo hili.

 

Huweza kuwapata wenye ndevu ama ambao wananyoa ndevu. Dalilizao  ni kama za fangasi wa maeneo mengine, kama eneo kuwa jekundu, kuwasha kuwa na madoamadoa na kunyonyoka kwa ndevu katika eneo lililo athirika.

 

Walio hatarini zaidi kupata fangasi hawa

Watu wote wanaweza kupata fangasi hawa wa mapunye. Lakini kuna watu wengine wapo hatarini zaidi. Na hii ni kutokana na shughuli zao wanazofanya, mazingira wanayoishi ama staili za maisha yao.

  • Watu wenye mfumo wa kinga dhaifu
  • Watu wanotumia changia sehemu moja ya kuwekea nguo
  • Watu wanaofanya shughuli ambazo hugusana gusana kwa mfano wanaofanya miereka.
  • Watu wanaovaa nguo za kubana sana
  • Watu wanaogusana gusana na wanyama wenye mapunye.

 

Namna ya kujilinda na mapunye

  1. Weka ngozi yako katika hali ya usafi
  2. Vaa viatu ambavyo vinaruhusu hewa kupita kwenye nyayo zako
  3. Usitembee miguu peku hasa kwenye maeneo yenye watu wengi
  4. Kata kucha zako ziwe fupi na ziweke katika hali ya usafi
  5. Badilisha soksi zako na nguo za ndani (chipi, boksa n.k) japo mara moja kwa siku
  6. Usichangie nguo zako na mtu mwingine
  7. Kama uanfanya kazi inayohitaji kugusana gusana kwa ngozi hakikisha unaoga mara kwa mara kwa siku.


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 8015

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 ai web app     👉5 Dua za Mitume na Manabii     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Nini husababisha Fangasi sehemu za Siri

Katika somo hili tutaeleza sababu kuu zinazopelekea kupata fangasi sehemu za siri, mazingira yanayochochea kuongezeka kwa fangasi, pamoja na vitu vinavyochangia maambukizi na kurudia-rudia kwa tatizo.

Soma Zaidi...
Dalilili za Ngozi kuwa kavu

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Ngozi kuwa kavu si mbaya, lakini inaweza kusumbua na isipendeze, ikitengeneza mistari laini na Mikunjo.

Soma Zaidi...
Fahamu Ugonjwa unaohusiana na kuzidi kwa joto mwilini (anhidrosis) ama heatshock

posti hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa na Ugonjwa unaohusiana na joto ambao hujulikana Kama Anhidrosis ni kutoweza jasho kawaida. Usipotoa jasho mwili wako hauwezi kujipoza, jambo ambalo linaweza kusababisha joto kupita. wakati mwingine inaweza k

Soma Zaidi...
YAJUE MARADHI YA KISUKARI

Posti hii itakwenda kuelezea mambo machache kuhusu ugonjwa wa kisukari

Soma Zaidi...
Dalili za minyoo mviringo (ascariasis)

Ascariasis ni aina ya maambukizi ya minyoo mviringo. Minyoo hii ni vimelea wanaotumia mwili wako kama mwenyeji kukomaa kutoka kwa mabuu au mayai hadi minyoo wakubwa. Minyoo ya watu wazima, ambayo huzaa, inaweza kuwa zaidi ya futi (sentimita 30) kwa

Soma Zaidi...
Athari za Ugonjwa wa herpes simplex kwa watoto wadogo.

Posti hii inahusu zaidi athari za Ugonjwa wa herpes simplex kwa watoto wadogo, tunajua kubwa mama kama ana ugonjwa huu anaweza kumwambikiza mtoto na mtoto akazaliwa na Ugonjwa huu.

Soma Zaidi...