picha

Fangasi wanaosababisha mapunye dalili zao na jinsi ya kupambana nao

Fangasi hawa ni maarufu sana kwa mapunye ya kichwani ama kwenye ngozi mikononi ama miguuni.

Fangasi wanaosababisha mapunye dalili zao na jinsi ya kupambana nao

2. Fangasi wa mapunye;

Fangasi hawa ni maarufu sana kwa mapunye ya kichwani ama kwenye ngozi mikononi ama miguuni. Kitaalamu fangasi hawa hujulikana kama tinea” au “dermatophytosis.  Na kwa maarufu sana wanafahamika kama ringworm kwa kuwa wanatoa mabako ya mduara kwenye ngozi.

 

Fangasi hawa wanaweza kukaa kwenye ngozi, kuta, nguo, taulo na maeneo mengine. Miongoni mwa dalili zao ni kuona maduara kwenye ngozi, mara nyingi dalili za fangasi hawa huweza kuonekana kuanzia siku 4 mpaka 14 baada ya ngozi kupata maambukizi ya fangasi hawa. zifuatazo ni katika dalili za fangasi hawa:-

 

Fangasi hawa wanaweza kukaa katika maeneo mbalimbali ya mwili na kusababisha dalili tofautitofauti kulingana na eneo lililo athirika. Kwa mfano;-

 

Fangasi hawa wakiwa kwenye nyayo (sthlete’s foot) huweza kuonesha dalili kama nyayo kuwa nyekundu, kuvimba ama kujaa maji, ngoxi kutoka ama kubabuka, kuwasha kwa ngozi katikati ya vidole na kidole na mara nyingi kati ya kidole kidogo na kinachomfatilia. Wakati mwingine kisigino na nyayo huweza kuathirika na kuweka mabumbuza.

 

Kwenye kichwa, fangasi hawa huweka maduara yaliyo nyonyoka ngozi, yakiwa na ukurutu, ngozi kavu, na kuwasha. Maduara haya maarufu tunayaita mapunye, yanaweza kuwa mengi na kuungana kufanya duara moja kubwa. Mara nyingi sana fangasi wa kichwani huwapata sana watoto kuliko watu wazima.

 

Kwenye pachipachi za mapaja (jock itch). Fangasi hawa hukaa sehemu ya ndani ya mapaja karibu na sehemu za siri ama kuzungukia eneo hilo, lakini wanashambulia mapaja. Miongoni mwa dalili zao ni mapaja kufanya wekundu, kuwasha na hali inaweza kuwa mbaya mpaka ngozi ikababuka na hatimaye kufanya vidonda kwa kujikuna. Wanaweza kushambulia pia korodani na kufanya ibabuke, iwe nyekundu na kuweka vidonda.

 

Fangasi wa kwenye ndevu (tinea barbae). fangasi hawa wanashambulia maeneo ambayo ndevu zinapatikana kama kwenye kidevu na shavu. Dalili zao ni kuwasha kwa kidevu, shavu, na sehemu ya juu ya shingo. Fangasi hawa wanaweza kuwa hatari zaidi na kusababisha mapele yenye usaha kwenye eneo hili.

 

Huweza kuwapata wenye ndevu ama ambao wananyoa ndevu. Dalilizao  ni kama za fangasi wa maeneo mengine, kama eneo kuwa jekundu, kuwasha kuwa na madoamadoa na kunyonyoka kwa ndevu katika eneo lililo athirika.

 

Walio hatarini zaidi kupata fangasi hawa

Watu wote wanaweza kupata fangasi hawa wa mapunye. Lakini kuna watu wengine wapo hatarini zaidi. Na hii ni kutokana na shughuli zao wanazofanya, mazingira wanayoishi ama staili za maisha yao.

 

Namna ya kujilinda na mapunye

  1. Weka ngozi yako katika hali ya usafi
  2. Vaa viatu ambavyo vinaruhusu hewa kupita kwenye nyayo zako
  3. Usitembee miguu peku hasa kwenye maeneo yenye watu wengi
  4. Kata kucha zako ziwe fupi na ziweke katika hali ya usafi
  5. Badilisha soksi zako na nguo za ndani (chipi, boksa n.k) japo mara moja kwa siku
  6. Usichangie nguo zako na mtu mwingine
  7. Kama uanfanya kazi inayohitaji kugusana gusana kwa ngozi hakikisha unaoga mara kwa mara kwa siku.


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 7731

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 ai web app    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 web hosting    👉5 Dua za Mitume na Manabii    👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

Dalili za maambukizi kwenye figo

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Maambukizi kwenye figo (pyelonephritis) ni aina mahususi ya maambukizi ya njia ya mkojo (UTI) ambayo kwa kawaida huanza kwenye urethra au kibofu chako na kusafiri hadi kwenye figo zako.

Soma Zaidi...
Fahamu mapacha wanavyounganishwa.

Mapacha walioungana ni watoto wawili wanaozaliwa wakiwa wameunganishwa kimwili. Mapacha walioungana hukua wakati kiinitete cha mapema kinapojitenga na kuunda watu wawili. Ingawa vijusi viwili vitakua kutoka kwa kiinitete hiki, wataendelea kushikamana mar

Soma Zaidi...
Fahamu Ugonjwa wa kipindupindu.

Kipindupindu ni ugonjwa wa bakteria ambao kawaida huenezwa kupitia maji machafu. Kipindupindu husababisha Kuhara na Upungufu wa maji mwilini.

Soma Zaidi...
Uvimbe wa mishipa midogo ya Damu kwenye ngozi

Posti hii inazungumzia kuhusiana na uvimbe wenye uchungu wa mishipa midogo ya damu kwenye ngozi yako ambayo hutokea kutokana na ongezeko la joto la ghafla kutokana na halijoto ya baridi. Pia inajulikana kama pernio, chilblain inaweza kusababisha kuwasha,

Soma Zaidi...
Dalili za hatari kwa mtoto aliyezaliwa

Posti hii inahusu zaidi dalili za hatari kwa mtoto aliyezaliwa, ni dalili ambazo ujitokeza tu mtoto anapozaliwa kwa hiyo dalili hizi zinapaswa kuzuiwa ili zisilete madhara makubwa.

Soma Zaidi...
Aina za kifua kikuu.

Posti hii inahusu zaidi aina mbili za kifua kikuu, aina ya kwanza ni ile ya kawaida ambayo ushambulia mapafu na aina ya pili ni ile ambayo ushambulia sehemu mbalimbali za mwili kama vile kwenye limfu node, kwenye sehemu za moyo, kwenye uti wa mgongo, kwen

Soma Zaidi...
Dalili za tezi dume ambayo hazijashuka (cryptorchidism)

Tezi dume ambayo haijashuka si ya kawaida kwa ujumla, lakini ni ya kawaida kwa wavulana waliozaliwa kabla ya wakati.na muda mwingine zikipanda tumboni huwa hazishuki kabisa kwenye korodani.

Soma Zaidi...
DALILI ZA MIMBA BAADA YA TENDO LA NDOA

Je unahitaji kujuwa kama umepata ujauzito baada ya kufanya tendo la ndoa? hakika sio rahisi ila kama utakuwa makini utaweza.

Soma Zaidi...
Dalili za mtu mwenye wasiwasi (anxiety)

Post hii unahusu mtu mwenye ugonjwa wa akili ambao huitwa ugonjwa wa wasiwasi Kwa kitaalamu huitwa anxiety,ni pale mtu anapokuwa na wasiwasi Kwa vitu nafasi mbali mbali kama tutakavoona.

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa sugu wa Figo.

Ugonjwa sugu wa figo, pia huitwa kushindwa kwa figo sugu, huelezea upotevu wa taratibu wa utendakazi wa figo. Figo zako huchuja taka na Majimaji kupita kiasi kutoka kwa damu yako, ambayo hutolewa kwenye mkojo wako. Ugonjwa sugu wa figo unapofikia hatua

Soma Zaidi...