Fangasi wanaosababisha mapunye dalili zao na jinsi ya kupambana nao

Fangasi wanaosababisha mapunye dalili zao na jinsi ya kupambana nao

Fangasi hawa ni maarufu sana kwa mapunye ya kichwani ama kwenye ngozi mikononi ama miguuni.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Fangasi wanaosababisha mapunye dalili zao na jinsi ya kupambana nao

2. Fangasi wa mapunye;

Fangasi hawa ni maarufu sana kwa mapunye ya kichwani ama kwenye ngozi mikononi ama miguuni. Kitaalamu fangasi hawa hujulikana kama tinea” au “dermatophytosis.  Na kwa maarufu sana wanafahamika kama ringworm kwa kuwa wanatoa mabako ya mduara kwenye ngozi.

 

Fangasi hawa wanaweza kukaa kwenye ngozi, kuta, nguo, taulo na maeneo mengine. Miongoni mwa dalili zao ni kuona maduara kwenye ngozi, mara nyingi dalili za fangasi hawa huweza kuonekana kuanzia siku 4 mpaka 14 baada ya ngozi kupata maambukizi ya fangasi hawa. zifuatazo ni katika dalili za fangasi hawa:-

 

Fangasi hawa wanaweza kukaa katika maeneo mbalimbali ya mwili na kusababisha dalili tofautitofauti kulingana na eneo lililo athirika. Kwa mfano;-

 

Fangasi hawa wakiwa kwenye nyayo (sthlete’s foot) huweza kuonesha dalili kama nyayo kuwa nyekundu, kuvimba ama kujaa maji, ngoxi kutoka ama kubabuka, kuwasha kwa ngozi katikati ya vidole na kidole na mara nyingi kati ya kidole kidogo na kinachomfatilia. Wakati mwingine kisigino na nyayo huweza kuathirika na kuweka mabumbuza.

 

Kwenye kichwa, fangasi hawa huweka maduara yaliyo nyonyoka ngozi, yakiwa na ukurutu, ngozi kavu, na kuwasha. Maduara haya maarufu tunayaita mapunye, yanaweza kuwa mengi na kuungana kufanya duara moja kubwa. Mara nyingi sana fangasi wa kichwani huwapata sana watoto kuliko watu wazima.

 

Kwenye pachipachi za mapaja (jock itch). Fangasi hawa hukaa sehemu ya ndani ya mapaja karibu na sehemu za siri ama kuzungukia eneo hilo, lakini wanashambulia mapaja. Miongoni mwa dalili zao ni mapaja kufanya wekundu, kuwasha na hali inaweza kuwa mbaya mpaka ngozi ikababuka na hatimaye kufanya vidonda kwa kujikuna. Wanaweza kushambulia pia korodani na kufanya ibabuke, iwe nyekundu na kuweka vidonda.

 

Fangasi wa kwenye ndevu (tinea barbae). fangasi hawa wanashambulia maeneo ambayo ndevu zinapatikana kama kwenye kidevu na shavu. Dalili zao ni kuwasha kwa kidevu, shavu, na sehemu ya juu ya shingo. Fangasi hawa wanaweza kuwa hatari zaidi na kusababisha mapele yenye usaha kwenye eneo hili.

 

Huweza kuwapata wenye ndevu ama ambao wananyoa ndevu. Dalilizao  ni kama za fangasi wa maeneo mengine, kama eneo kuwa jekundu, kuwasha kuwa na madoamadoa na kunyonyoka kwa ndevu katika eneo lililo athirika.

 

Walio hatarini zaidi kupata fangasi hawa

Watu wote wanaweza kupata fangasi hawa wa mapunye. Lakini kuna watu wengine wapo hatarini zaidi. Na hii ni kutokana na shughuli zao wanazofanya, mazingira wanayoishi ama staili za maisha yao.

 

Namna ya kujilinda na mapunye

  1. Weka ngozi yako katika hali ya usafi
  2. Vaa viatu ambavyo vinaruhusu hewa kupita kwenye nyayo zako
  3. Usitembee miguu peku hasa kwenye maeneo yenye watu wengi
  4. Kata kucha zako ziwe fupi na ziweke katika hali ya usafi
  5. Badilisha soksi zako na nguo za ndani (chipi, boksa n.k) japo mara moja kwa siku
  6. Usichangie nguo zako na mtu mwingine
  7. Kama uanfanya kazi inayohitaji kugusana gusana kwa ngozi hakikisha unaoga mara kwa mara kwa siku.


                   

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 4296

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Dalili za mtu aliyegongwa na nyoka
Dalili za mtu aliyegongwa na nyoka

Post hii inahusu zaidi dalili za mtu aliyegongwa na nyoka, nyoka ni kiumbe ambacho Kina sumu kali na sumu ikiingia mwilini mtu huwa na dalili mbalimbali

Soma Zaidi...
Sababu za kuwepo kwa saratani ya inni.
Sababu za kuwepo kwa saratani ya inni.

Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali za kuwepo kwa saratani ya ini, saratani hii imekuwa tishio kwa wengi ila ni vizuri kujua baadhi ya sababu ambazo uchangia sana kuwepo kwa tatizo hili la saratani ya inni.

Soma Zaidi...
Sababu za vidonda sugu vya tumbo
Sababu za vidonda sugu vya tumbo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za vidonda vya tumbo sugu

Soma Zaidi...
 Sababu za Ugonjwa wa pumu
Sababu za Ugonjwa wa pumu

Pumu ni ugonjwa wa njia ya upumuaji unaojulikana na kizuizi cha muda mrefu cha njia ya upumuaji. Inahusisha mfumo wa upumuaji unaobana njia ya hewa, Inaweza kuwa ya nje (hii hutokea kwa vijana kutokana na mizio) au ya ndani (hutokea kwa wazee)

Soma Zaidi...
  Dalili na ishara za Ugonjwa wa akili.
Dalili na ishara za Ugonjwa wa akili.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa wa akili .

Soma Zaidi...
Aina za kisukari
Aina za kisukari

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu aina za kisukari

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa herpes simplex au vipele kwenye midomo na sehemu za siri
Dalili za ugonjwa wa herpes simplex au vipele kwenye midomo na sehemu za siri

Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa wa vipele kwenye midomo na sehemu za siri ambao kwa kitaalamu huitwa herpes zoster. Kwa hiyo ili kugundua kubwa mtu ana Ugonjwa huu Dalili kama hizi zifuatazo zinaweza kutokea kwa mgonjwa.

Soma Zaidi...
 DAWA MBADALA ZA VIDONDA VYA TUMBO
DAWA MBADALA ZA VIDONDA VYA TUMBO

DAWA MBADALA ZA VIDONDA VYA TUMBO Dawa za kukabiliana na zaidi ambazo zina calcium carbonate (Tums, Rolaids), zinaweza kusaidia kutibu vidonda vya tumbo lakini hazipaswi kutumiwa kama matibabu ya msingi.

Soma Zaidi...