picha

Fangasi wanaosababisha mapunye dalili zao na jinsi ya kupambana nao

Fangasi hawa ni maarufu sana kwa mapunye ya kichwani ama kwenye ngozi mikononi ama miguuni.

Fangasi wanaosababisha mapunye dalili zao na jinsi ya kupambana nao

2. Fangasi wa mapunye;

Fangasi hawa ni maarufu sana kwa mapunye ya kichwani ama kwenye ngozi mikononi ama miguuni. Kitaalamu fangasi hawa hujulikana kama tinea” au “dermatophytosis.  Na kwa maarufu sana wanafahamika kama ringworm kwa kuwa wanatoa mabako ya mduara kwenye ngozi.

 

Fangasi hawa wanaweza kukaa kwenye ngozi, kuta, nguo, taulo na maeneo mengine. Miongoni mwa dalili zao ni kuona maduara kwenye ngozi, mara nyingi dalili za fangasi hawa huweza kuonekana kuanzia siku 4 mpaka 14 baada ya ngozi kupata maambukizi ya fangasi hawa. zifuatazo ni katika dalili za fangasi hawa:-

  • Kuwasha kwa ngozi na maumivu wakati mwingine
  • Kuwepo kwa mapele ama ukurutu uliotengeneza umbo la duara
  • Ngoz kuwa nyekundu, kupasuka ama kuwa kavu
  • Kukatika ama kunyonyoka kwa nywele kwenye sehemu iliyo athirika

 

Fangasi hawa wanaweza kukaa katika maeneo mbalimbali ya mwili na kusababisha dalili tofautitofauti kulingana na eneo lililo athirika. Kwa mfano;-

 

Fangasi hawa wakiwa kwenye nyayo (sthlete’s foot) huweza kuonesha dalili kama nyayo kuwa nyekundu, kuvimba ama kujaa maji, ngoxi kutoka ama kubabuka, kuwasha kwa ngozi katikati ya vidole na kidole na mara nyingi kati ya kidole kidogo na kinachomfatilia. Wakati mwingine kisigino na nyayo huweza kuathirika na kuweka mabumbuza.

 

Kwenye kichwa, fangasi hawa huweka maduara yaliyo nyonyoka ngozi, yakiwa na ukurutu, ngozi kavu, na kuwasha. Maduara haya maarufu tunayaita mapunye, yanaweza kuwa mengi na kuungana kufanya duara moja kubwa. Mara nyingi sana fangasi wa kichwani huwapata sana watoto kuliko watu wazima.

 

Kwenye pachipachi za mapaja (jock itch). Fangasi hawa hukaa sehemu ya ndani ya mapaja karibu na sehemu za siri ama kuzungukia eneo hilo, lakini wanashambulia mapaja. Miongoni mwa dalili zao ni mapaja kufanya wekundu, kuwasha na hali inaweza kuwa mbaya mpaka ngozi ikababuka na hatimaye kufanya vidonda kwa kujikuna. Wanaweza kushambulia pia korodani na kufanya ibabuke, iwe nyekundu na kuweka vidonda.

 

Fangasi wa kwenye ndevu (tinea barbae). fangasi hawa wanashambulia maeneo ambayo ndevu zinapatikana kama kwenye kidevu na shavu. Dalili zao ni kuwasha kwa kidevu, shavu, na sehemu ya juu ya shingo. Fangasi hawa wanaweza kuwa hatari zaidi na kusababisha mapele yenye usaha kwenye eneo hili.

 

Huweza kuwapata wenye ndevu ama ambao wananyoa ndevu. Dalilizao  ni kama za fangasi wa maeneo mengine, kama eneo kuwa jekundu, kuwasha kuwa na madoamadoa na kunyonyoka kwa ndevu katika eneo lililo athirika.

 

Walio hatarini zaidi kupata fangasi hawa

Watu wote wanaweza kupata fangasi hawa wa mapunye. Lakini kuna watu wengine wapo hatarini zaidi. Na hii ni kutokana na shughuli zao wanazofanya, mazingira wanayoishi ama staili za maisha yao.

  • Watu wenye mfumo wa kinga dhaifu
  • Watu wanotumia changia sehemu moja ya kuwekea nguo
  • Watu wanaofanya shughuli ambazo hugusana gusana kwa mfano wanaofanya miereka.
  • Watu wanaovaa nguo za kubana sana
  • Watu wanaogusana gusana na wanyama wenye mapunye.

 

Namna ya kujilinda na mapunye

  1. Weka ngozi yako katika hali ya usafi
  2. Vaa viatu ambavyo vinaruhusu hewa kupita kwenye nyayo zako
  3. Usitembee miguu peku hasa kwenye maeneo yenye watu wengi
  4. Kata kucha zako ziwe fupi na ziweke katika hali ya usafi
  5. Badilisha soksi zako na nguo za ndani (chipi, boksa n.k) japo mara moja kwa siku
  6. Usichangie nguo zako na mtu mwingine
  7. Kama uanfanya kazi inayohitaji kugusana gusana kwa ngozi hakikisha unaoga mara kwa mara kwa siku.


                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 9771

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 ai web app     πŸ‘‰2 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰3 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰4 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

Kupoteza nywele kwa wingi (Hair loss): Sababu na tiba.

​Kupoteza nywele ni jambo linaloweza kuathiri hali ya kujiamini ya mtu yeyote. Ingawa ni kawaida kupoteza nywele 50 hadi 100 kila siku, kupoteza nywele kwa wingi kiasi cha kuacha sehemu wazi kichwani ni ishara kuwa kuna kitu hakiko sawa. Makala haya yanakusaidia kuelewa sababu zinazochochea hali hii na namna unavyoweza kurejesha afya ya nywele zako.

Soma Zaidi...
Dalili za anemia ya upungufu wa vitamin.

Anemia ya upungufu wa vitamini ni ukosefu wa seli nyekundu za damu zenye afya unaosababishwa na kiasi kidogo cha vitamini fulani kuliko kawaida.

Soma Zaidi...
Makosa Yanayofanywa na Wapenzi Wengi

Mahusiano ni safari ya kujifunza kila siku. Makala hii inachambua makosa ya kawaida yanayoweza kuathiri ustawi wa mahusiano, ikitoa mwongozo wa jinsi ya kuyatambua na kuyafanyia kazi ili kujenga uhusiano imara na wenye furaha.

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa Bawasili

Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa Bawasili, ni Dalili ambazo ujitokeza kwa mgonjwa ambaye ana ugonjwa wa Bawasili.

Soma Zaidi...
TIBA YA MINYOO AU DAWA YA MINYOO: praziquantel (biltricide) mebendazole (vermox, emverm) na albendazole (albenza).

TIBA YA MINYOO Moja katika sifa za minyoo ni kuwa wanatibika kwa urahisi pindi mgonjwa akipewa dawa husika.

Soma Zaidi...
Dalilili za pepopunda

postii hii inshusiana na dalili na matatizo ya pepopunda. Pepopunda ni ugonjwa hatari wa kutishia maisha unaosababishwa na sumu ya tetanospasmin inayozalishwa katika majeraha yaliyoambukizwa na kizuizi cha bacillus clostridia. Bakteria ya pepopunda hu

Soma Zaidi...