Fangasi wanaosababisha mapunye dalili zao na jinsi ya kupambana nao
Fangasi hawa ni maarufu sana kwa mapunye ya kichwani ama kwenye ngozi mikononi ama miguuni.
2. Fangasi wa mapunye;
Fangasi hawa ni maarufu sana kwa mapunye ya kichwani ama kwenye ngozi mikononi ama miguuni. Kitaalamu fangasi hawa hujulikana kama tinea” au “dermatophytosis. Na kwa maarufu sana wanafahamika kama ringworm kwa kuwa wanatoa mabako ya mduara kwenye ngozi.
Fangasi hawa wanaweza kukaa kwenye ngozi, kuta, nguo, taulo na maeneo mengine. Miongoni mwa dalili zao ni kuona maduara kwenye ngozi, mara nyingi dalili za fangasi hawa huweza kuonekana kuanzia siku 4 mpaka 14 baada ya ngozi kupata maambukizi ya fangasi hawa. zifuatazo ni katika dalili za fangasi hawa:-
- Kuwasha kwa ngozi na maumivu wakati mwingine
- Kuwepo kwa mapele ama ukurutu uliotengeneza umbo la duara
- Ngoz kuwa nyekundu, kupasuka ama kuwa kavu
- Kukatika ama kunyonyoka kwa nywele kwenye sehemu iliyo athirika
Fangasi hawa wanaweza kukaa katika maeneo mbalimbali ya mwili na kusababisha dalili tofautitofauti kulingana na eneo lililo athirika. Kwa mfano;-
Fangasi hawa wakiwa kwenye nyayo (sthlete’s foot) huweza kuonesha dalili kama nyayo kuwa nyekundu, kuvimba ama kujaa maji, ngoxi kutoka ama kubabuka, kuwasha kwa ngozi katikati ya vidole na kidole na mara nyingi kati ya kidole kidogo na kinachomfatilia. Wakati mwingine kisigino na nyayo huweza kuathirika na kuweka mabumbuza.
Kwenye kichwa, fangasi hawa huweka maduara yaliyo nyonyoka ngozi, yakiwa na ukurutu, ngozi kavu, na kuwasha. Maduara haya maarufu tunayaita mapunye, yanaweza kuwa mengi na kuungana kufanya duara moja kubwa. Mara nyingi sana fangasi wa kichwani huwapata sana watoto kuliko watu wazima.
Kwenye pachipachi za mapaja (jock itch). Fangasi hawa hukaa sehemu ya ndani ya mapaja karibu na sehemu za siri ama kuzungukia eneo hilo, lakini wanashambulia mapaja. Miongoni mwa dalili zao ni mapaja kufanya wekundu, kuwasha na hali inaweza kuwa mbaya mpaka ngozi ikababuka na hatimaye kufanya vidonda kwa kujikuna. Wanaweza kushambulia pia korodani na kufanya ibabuke, iwe nyekundu na kuweka vidonda.
Fangasi wa kwenye ndevu (tinea barbae). fangasi hawa wanashambulia maeneo ambayo ndevu zinapatikana kama kwenye kidevu na shavu. Dalili zao ni kuwasha kwa kidevu, shavu, na sehemu ya juu ya shingo. Fangasi hawa wanaweza kuwa hatari zaidi na kusababisha mapele yenye usaha kwenye eneo hili.
Huweza kuwapata wenye ndevu ama ambao wananyoa ndevu. Dalilizao ni kama za fangasi wa maeneo mengine, kama eneo kuwa jekundu, kuwasha kuwa na madoamadoa na kunyonyoka kwa ndevu katika eneo lililo athirika.
Walio hatarini zaidi kupata fangasi hawa
Watu wote wanaweza kupata fangasi hawa wa mapunye. Lakini kuna watu wengine wapo hatarini zaidi. Na hii ni kutokana na shughuli zao wanazofanya, mazingira wanayoishi ama staili za maisha yao.
- Watu wenye mfumo wa kinga dhaifu
- Watu wanotumia changia sehemu moja ya kuwekea nguo
- Watu wanaofanya shughuli ambazo hugusana gusana kwa mfano wanaofanya miereka.
- Watu wanaovaa nguo za kubana sana
- Watu wanaogusana gusana na wanyama wenye mapunye.
Namna ya kujilinda na mapunye
- Weka ngozi yako katika hali ya usafi
- Vaa viatu ambavyo vinaruhusu hewa kupita kwenye nyayo zako
- Usitembee miguu peku hasa kwenye maeneo yenye watu wengi
- Kata kucha zako ziwe fupi na ziweke katika hali ya usafi
- Badilisha soksi zako na nguo za ndani (chipi, boksa n.k) japo mara moja kwa siku
- Usichangie nguo zako na mtu mwingine
- Kama uanfanya kazi inayohitaji kugusana gusana kwa ngozi hakikisha unaoga mara kwa mara kwa siku.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
๐1 web hosting ๐2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina ๐3 kitabu cha Simulizi ๐4 Kitabu cha Afya ๐5 Madrasa kiganjani ๐6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Dalili za upungufu wa maji mwilini.
Upungufu wa maji mwilini hutokea unapotumia au kupoteza Majimaji mengi zaidi ya unayonywa, na mwili wako hauna maji ya kutosha na Majimaji mengine ya kufanya kazi zake za kawaida. Usipochukua nafasi ya Vimiminika vilivyopotea, utapungukiwa na maji.
Soma Zaidi...Dalili za Uvimbe kwenye mfuko wa uzazi (uterine fibroid)
Uvimbe kwenye mfuko wa uzaziรย hukua kutoka kwenye tishu laini za misuli ya uterasi. Fibroids nyingi ambazo zimekuwepo wakati wa ujauzito hupungua au kutoweka baada ya ujauzito, kwani uterasi inarudi kwenye ukubwa wa kawaida.
Soma Zaidi...Sababu za maumivu ya uti wa mgongo
Posti hii inahusu zaidi sababu za uti wa mgongo, ni ugonjwa unaotokana na kuwa na maumivu kwenye uti wa mgongo, hasa hasa ugonjwa huu ushambulia watu kuanzia miaka ishilini mpaka kwenye arobaini hivi, zifuatazo ni sababu za maumivu katika uti wa mgongo.
Soma Zaidi...Jinsi ya kujenga afya ya akili katika ulimwengu wa sasa.
โKatika ulimwengu wa kidijitali na wenye kasi kubwa, afya ya akili imekuwa rasilimali muhimu zaidi kwa binadamu. Makala haya yanachunguza mbinu za kisayansi na kivitendo za kujenga ustahimilivu wa kiakili, kudhibiti mfadhaiko wa teknolojia, na kukuza usawaziko wa maisha. Kupitia mwongozo huu, utajifunza jinsi ya kuweka mipaka, kuboresha mahusiano, na kutumia mazoea ya kujijali (self-care) ili kudumisha utulivu wa ndani katikati ya changamoto za kisasa.
Soma Zaidi...Dalili za Kiharusi Cha joto la mwili.
Kiharusi cha joto ni hali inayosababishwa na joto la juu la mwili wako, kwa kawaida kama matokeo ya kufichuliwa kwa muda mrefu au bidii ya mwili katika joto la juu. Aina hii mbaya zaidi ya jeraha la joto, kiharusi cha joto kinaweza kutokea ikiwa joto
Soma Zaidi...