Safari ya damu kwa Kila siku
Posti hii inakwenda kukuletea mfumo wa damu mwilini na safari zake za Kila siku
SAFARI YA DAMU KWA KILA SIKU.
picDamu ni tishu iliyopo katika hali ya kimiminika. Bila ya damu mwanadamu hawezi kuishi. Moyo ndio kiungo kikuu wenye mwili chenye kazi ya kuisambaza damu mwili mzima. Ukubwa wa kiungo hichi hufanana na ngumi. Moyo husafirisha damu kwenye mishipa inayokadiriwa kuwa na urefu wa kilomita elfu tisini na saba (97) na hii hufanyika ndani ya sekunde 20 tu.pic
Damu imeundwa kwa seli hai nyekundu za damu, seli hai nyeupe za damu, plasma, maji na seli sahani. Kila moja kati ya hizi ina kazi yake maalumu. Katika makala hii fupi tutaona vitu hivi kwa ufupi tu. Pia itambulike kuwa kuna viumbe hawana damu kama minyoo na baadhi ya samaki. Na hii ni kutokana na jinsi maumbile yao yalivyo. Asilimia 7% ya mwili wa binadamu ni damu na mtu mzima ana damu kuanzia lita 3.7 mapaka lita 5.6.
Seli nyekunsu za damu (red blood cell), hizi kitaalamu huitwa erythrocytes na hutengenezwa kwenye uroto wa mifupa yaani bone marrow. Kwa wastani seli hizi zinaweza kuishi kwa muda wa siku 120 tu baada ya kutengenezwa. Asilimia 40@ ya damu ni seli hizi na ndio ambazo zinaipa damu rangi nyekundu. Seli zina protini na haemoglobin (chembechembe nyekundu) na hizi ndio huipa rangi nyekundu. Kazi ya seli hizi ni kubeba heya ya oxygeni kutoka kwenye mapafu na kuipeleka kwenye moyo ili isambazwe zaidi mwilini. Ka kutoa hewa ya kabondaioksaidi kutoka kwenye moyo na kuipelekwa kwenye mapafu ili itolewe nje. Pia hubeba viinilishe (nutrients) kupeleka sehemu zingine za mwili.
Seli n yeupe za damu (white blood cell) kwa jina la kitaalamu huit wa leukocytes. Kazi kubwa ya seli hizi ni kupambana na maambukizi na wadudu wa baya wanaoshambulia mwili. Seli hizi zinaweza kuishi kuanzia siku moja mpaka mwezi mmoja tu baada ya kutengenezwa. Pia hutengenezwa kwenye uroto wa mifupa. Seli hizi zipo aina nyingi, kuna ambazo hupambana na kula bakteria na wadudu wengine wavamizi mwilini, kuna nyingine zinatoa antibodies kwa ajili ya kusaidia kupambana.
Seli sahani (platelets) kitaalamu huitwa thrombocytes pia hutengenezwa kwenye uroto wa mifupa. Sinaishi siku sita tu baada ya kutengenezwa. Kazi yao kubwa ni kugandisha damu pindi kunapokuwa na jeraha. Plasma sio seli ni maji ya njano ambayo husaidia damu huogelea vizuri kupita kwenye mirija ya damu. Asilimia 90 ya plasma ni maji, ila pia ina madimi, vitamin na viinilishe (nutrients)
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
๐1 Kitabu cha Afya ๐2 Madrasa kiganjani ๐3 Simulizi za Hadithi Audio ๐4 Kitau cha Fiqh ๐5 Bongolite - Game zone - Play free game ๐6 ai web app
Post zinazofanana:
Jinsi ya kuimarish afya ya meno
Katika post hii utajifunza namna ambavyo unaweza kuboresha afya ya meno yakom
Soma Zaidi...Namna ya kuzuia dalili za hatari kwa aliyefanyiwa upasuaji
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuzuia dalili za hatari kwa aliyefanyiwa upasuaji, ni mbinu mbalimbali ambazo utumika ili kujaribu kuepuka Dalili za hatari kwa aliyefanyiwa upasuaji.
Soma Zaidi...Jinsi ya kuhesabu siku za hatari za kupata mimba.
Kujua siku zako za hatari (siku ambazo una uwezekano mkubwa wa kupata mimba) ni njia muhimu sana kwa wanandoa wanaopanga kupata mtoto. Siku hizi hutegemea mchakato wa kupevuka kwa yai (ovulation), ambapo yai huachiliwa kutoka kwenye ovari ili kurutubishwa. Makala hii inaelezea mbinu rahisi ya kalenda unayoweza kutumia.
Soma Zaidi...Maumivu makali ya tumbo wakati wa hedhi: Ni ya kawaida?
โMaumivu ya tumbo wakati wa hedhi, yanayojulikana kitabibu kama dysmenorrhea, ni hali inayowapata wanawake wengi. Kwa kiasi kikubwa, maumivu mepesi hadi ya wastani ni ya kawaida. Hata hivyo, maumivu yanapokuwa makali kiasi cha kuzuia shughuli zako za kila siku, hiyo inaweza kuwa ishara ya tatizo lingine la kiafya linalohitaji uchunguzi. Makala hii inaangazia tofauti kati ya maumivu ya kawaida na yale yanayohitaji tahadhari.
Soma Zaidi...Ukoma (Leprosy): Je, unagundulika vipi leo?
โUkoma, unaojulikana kitaalamu kama Hansenโs disease, ni ugonjwa wa muda mrefu unaosababishwa na bakteria Mycobacterium leprae. Ugonjwa huu huathiri ngozi, neva za pembeni (peripheral nerves), utando wa juu wa njia ya upumuaji, na macho. Licha ya dhana potofu za kale, Ukoma leo unagundulika kwa urahisi na kutibika kikamilifu kwa dawa za antibayotiki, na mgonjwa anapoanza tiba, hawezi tena kuambukiza wengine.
Soma Zaidi...