Posti hii inakwenda kukuletea mfumo wa damu mwilini na safari zake za Kila siku
SAFARI YA DAMU KWA KILA SIKU.
picDamu ni tishu iliyopo katika hali ya kimiminika. Bila ya damu mwanadamu hawezi kuishi. Moyo ndio kiungo kikuu wenye mwili chenye kazi ya kuisambaza damu mwili mzima. Ukubwa wa kiungo hichi hufanana na ngumi. Moyo husafirisha damu kwenye mishipa inayokadiriwa kuwa na urefu wa kilomita elfu tisini na saba (97) na hii hufanyika ndani ya sekunde 20 tu.pic
Damu imeundwa kwa seli hai nyekundu za damu, seli hai nyeupe za damu, plasma, maji na seli sahani. Kila moja kati ya hizi ina kazi yake maalumu. Katika makala hii fupi tutaona vitu hivi kwa ufupi tu. Pia itambulike kuwa kuna viumbe hawana damu kama minyoo na baadhi ya samaki. Na hii ni kutokana na jinsi maumbile yao yalivyo. Asilimia 7% ya mwili wa binadamu ni damu na mtu mzima ana damu kuanzia lita 3.7 mapaka lita 5.6.
Seli nyekunsu za damu (red blood cell), hizi kitaalamu huitwa erythrocytes na hutengenezwa kwenye uroto wa mifupa yaani bone marrow. Kwa wastani seli hizi zinaweza kuishi kwa muda wa siku 120 tu baada ya kutengenezwa. Asilimia 40@ ya damu ni seli hizi na ndio ambazo zinaipa damu rangi nyekundu. Seli zina protini na haemoglobin (chembechembe nyekundu) na hizi ndio huipa rangi nyekundu. Kazi ya seli hizi ni kubeba heya ya oxygeni kutoka kwenye mapafu na kuipeleka kwenye moyo ili isambazwe zaidi mwilini. Ka kutoa hewa ya kabondaioksaidi kutoka kwenye moyo na kuipelekwa kwenye mapafu ili itolewe nje. Pia hubeba viinilishe (nutrients) kupeleka sehemu zingine za mwili.
Seli n yeupe za damu (white blood cell) kwa jina la kitaalamu huit wa leukocytes. Kazi kubwa ya seli hizi ni kupambana na maambukizi na wadudu wa baya wanaoshambulia mwili. Seli hizi zinaweza kuishi kuanzia siku moja mpaka mwezi mmoja tu baada ya kutengenezwa. Pia hutengenezwa kwenye uroto wa mifupa. Seli hizi zipo aina nyingi, kuna ambazo hupambana na kula bakteria na wadudu wengine wavamizi mwilini, kuna nyingine zinatoa antibodies kwa ajili ya kusaidia kupambana.
Seli sahani (platelets) kitaalamu huitwa thrombocytes pia hutengenezwa kwenye uroto wa mifupa. Sinaishi siku sita tu baada ya kutengenezwa. Kazi yao kubwa ni kugandisha damu pindi kunapokuwa na jeraha. Plasma sio seli ni maji ya njano ambayo husaidia damu huogelea vizuri kupita kwenye mirija ya damu. Asilimia 90 ya plasma ni maji, ila pia ina madimi, vitamin na viinilishe (nutrients)
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu
Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Jifunze
Main: Post
File: Download PDF
Share On
Facebook
or
Whatsapp
Views 1112
Sponsored links
👉1
Kitabu cha Afya
👉2
Kitau cha Fiqh
👉3
kitabu cha Simulizi
👉4
Simulizi za Hadithi Audio
👉5
Madrasa kiganjani
👉6
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
hathari zitokanazo na uvutaji wa sigara ,pombe na madawa ya kulevya na mbinu za kujikinga nayo
Posti hii inahusu zaidi utumiaji wa pombe na sigara pamoja na madawa katika jamii. Soma Zaidi...
KITABU CHA MATUNDA
Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho Soma Zaidi...
Kitabu cha Afya 04
Afya inaweza kuathiriwa na vitu vingi sana. Hapa tutaendelea kuona mabo zaidi yanayoathiri afya yako. Soma Zaidi...
kitabu cha afya
Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho Soma Zaidi...
Nina shida hiyo maumivu chini ya tumbo upande wa kushoto na mkojo wa kahawia sana na unatoa arufu
Kama unapatwa na maumivu ya tumbo na ilhali mkojo ni mchafu, ama una harufu sana, basi post hii ni kwa ajili yako. Soma Zaidi...
Dua Sehemu ya 01
Zijue fadhila za kuomba dua, tambua umuhimu na mahimizo juu ya kuomba dua? Soma Zaidi...
Dhana ya uzazi wa mpango na historia yake duniani
Soma Zaidi...
DONDOO 100 ZA AFYA
Pata dondoo 100 za Afya Soma Zaidi...
TAHADHARI KWENYE VYAKULA ILI KULINDA AFYA YAKO
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...
KITABU HA MATUNDA
Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho Soma Zaidi...