Navigation Menu



image

Mbu (mosquito)

Posti hii inakwenda kukupa sifa za mdudu mbu

MBU (MOSQUITO)

 

Mbu ni katika wadudu wanaopatikana maeneo yenye joto hususan maeneo ynye hali ya hewa ya kitropik. Mbu anafahamika kwa kuwa ndiye msambazaji mkubwa wa malaria pamoja na matende na ngiri maji. Chakula cha mbu ni maji, bakteria pamoja na damu. Mbu dume huweza kumjua mwanamke kwa kutumia sauti ya mbawa. Mbu ni katika wadudu wadogo lakini wana maajabu makubwa. Katika mkala hii tutaangalia kwa ufupi mambo matano kuhusu mbu.

 

Tofauti na kuwa mbu ni mdogo lakini anaweza kunyonya damu iliyokuwa nzito kuliko mwili wake. Yaani sawa na mtu mwenye uzito wa kilo 70 kula chakula chenye uzito wa kili 100. mara mbu anaponyonya damu mwili wake huchukuwa mpaka siku tatu kuweza kuimeng’enya damu ile na kuimaliza. Baada ya hapo mbu atakwenda kunyonya damu tena. Itambulike kuwa chakula cha mbu ni bakteria, maji pamoja na damu. Mbu jike hula damu pindi anapotaka kutaga. Wataalamu wanaeleza kuwa kuna aina 2000 za mbu.

 

picKabla ya mbu kutaga mayai yake anaanza kupima ardhi kama ina majimaji pamoja na joto la kutosha kwa maisha ya mayai yake. Mbu hutaga mayai juu ya maji, ardhi, miti na nyasi pamoja na maeneo mengine yaliyo na majimaji. Pia mbu anaweza kutaga yai lake hata pakiwa na maji kiasi cha tone moja tu. Nayai ya mbu ni chakula kwa samaki pamoja na watutu wengine hivyo mbu huwa makini sana wakati wa kutaga mayai yake.

 

Tofauti na wadudu wengine na ndege mbu anaweza kulizuia yai lake tumboni kulitaga pindia anapohofia usalama wa yai lake. Kuku na ndege wengine yai linapofikia kutagwa hana namna lazima akalitage, lakini hii ni tofauti kwa mbu. Yai la mbu linaweza kukaa kwa muda wa miaka miwili bila ya kufa na ndo maana ni vigumu kutokomeza kabisa mbu.

 

Yai la mbu lina rangi ya njano, tangi hii ni rahisi kulifanya yai hili lionewe na maadui walao mayai ya mbu. Hivyo ifikapo usiku yai la mbu hubadilika rangi na kuwa jeusi. Hali hii husaidia kuliepusha yai la mbu kuliwa na maadua. Pia yai la mbu halizami ndani ya maji, na linaweza kuelea hewani, njia zote hizi husaidia ulinzi wa yai hili lisidhuriwe.

 

Ijapokuwa mbu anakula binadamu lakini na yeye ni chakula kwa viumbe vingine kama popo. Hivyo popo hutusaidia katika mapambano dhidi ya wadudu hawa hatari. mbu pia anaweza kujuwa wati mtu yupo kwa kutumia pumzi anayopumua mwanadamu.






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Mengineyo Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 2088


Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

MAAJABU YA VIUMBE
MAAJABU YA VIUMBE Dunia ina maajabu sana lakini viumbe wana maajabu pia. Soma Zaidi...

MNYAMA ANAYEKIMBIA ZAIDI YA WOTE
4. Soma Zaidi...

Tembo ni katika wanyama wenye kushangaza sana.
Tembo wana maajabu makubwa kama utazingatia kwa umakini umbo lake zuri. Soma Zaidi...

Kitabu Cha ayansi ya viumbe
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet. Soma Zaidi...

Ndege kwenye ulimbo
Wahenga wanaelewa, enzi hizo unaambiwa ndege akinasa basi unakumbuka macho juu asije akayoke. Hukuchinib. hujali kama kuna mjimba ama nini Soma Zaidi...

MAAJABU YA VIUMBE: TEMBO, NYOKA, MBU, SIMBA, CHUI, TAIGA, FARASI, NGAMIA NA WANYAMA WENGINE
Soma Zaidi...

Fast
Jifunze matumizi ya simu yako na namna ya kutatua matatizo mbalimbali kwenye simu na kompyuta.. Soma Zaidi...

ABOUT BONGOCLASS
learn English Vocabulary Soma Zaidi...

mchango
Soma Zaidi...

nataka niunganishe namba yangu kwa mtu mwingne ili kama kuna sms nimetumiwa ianzie kwa huyo mtu
Ikiwa nataka niunganishe namb yangu kwa mtu mwingne il kama kuna sms nime2miwa ianzie kwa huyo mtu nifanyeje? Soma Zaidi...

Bongoclass ni nini, ipo wapi bongoclass na ni zipi kazi zake?
Bonoclass ni muunganiko wa maneno mawili, kutoka katika lugha mbili yaani lugha ya kiingereza na lugha ya kiswahili. Soma Zaidi...

YAJUWE MAAJABU YA MBUZI PORI
1. Soma Zaidi...