picha

Cheetah

Posti hii inakwenda kukupa sifa za mnyama cheetah

.Cheetah

 

picHuyu ni katika wanyama jamii ya paka, na anafanana zaidi na mnyama anayeitwa puma. Cheetah ni mnyama mwindaji kama walivyo chui, simba na mbwa mwitu. Ijapokuwa cheetah wanafanana kwa sura na maumbile lakini unaweza kutofautisha mmoja kwa mwingine kwa kutofautisha rangi za kwenye mikia yao. Cheetah ni katika wanyama walio hatarini kwa kuuliwa kwani wapo wachache sana. Wataalamu wa wanyama na watafifi wanaeleza kuwa nchi ya Namibia ndio nchi pekee yenye cheetah wengi zaidi. Inakadiriwa cheetah wanaoishi maeneo haya wanafika 2500. Cheetah anaweza kufika uzito wa kilogramu 39 mpaka 65 (kg 29 - 65).

 

picTafiti zinaonesha kuwa cheetah ndiye mnyama anayekimbia kwa kasi zaidi kuliko wanyama wote wa porini. Cheetah anaweza kukimbia kwa mwendokasi wa kilomita 97 kwa lisaa (97 km/h) na anaweza kuendelea kukimbia kwa mwendokasi huu kwa umbali wa mita 300. Mwili wa cheetah hauna uwezo wa kutoa jasho hivyo anapokimbia kwa umbali huu wa mita 300 bila ya kukpata kiwindwa chake cheetah huachana nae kwa kuhofia mwili wake kupata joto ambalo linaweza kumpelekea kufa.

 

picWanyama hawa wanakaa kwenye makundi ya familia na mara nyingi madume wanapenda kupigana. Wanyama hawa wanapoteza asilimia 10 mpaka 13 ya vile walivyoviwinda kwa simba pamoja na fisi. Tafiti zinaonesha kuwa nusu ya mawindo yao wanafanikiwa kupata chakula. Cheetah ni katika wanyama waliop hatarini sana kwani wana windwa sana na binadamu kwa ajili ya kuuliwa. Mnyama huyu anapenda kuwinda kwenye maeneo yaliyo wazi pasiwe na miti mingia mabayo itamfanya akikose kiwindwa chake kwa urahisi.

 

Cheetah ni katika wanyama ambao wanaweza kuishi muda mrefu bila ya kunywa maji. Kwani anajipatia maji anayohitaji kutoka kwenye mwili wa kiwindwa chake. Pindi anapowinda humnyatio mnyama wake mpaka ukaribu wa mita 10 ndipo humkurupukia na kumkumbiza kwa mwendokasi wa zaidi sana, na hukata tamaa pindi akimkimbiza kwa umbali wa mita 300. 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Mengineyo Main: Post File: Download PDF Views 1989

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Simulizi za Hadithi Audio     πŸ‘‰2 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰3 Bongolite - Game zone - Play free game     πŸ‘‰4 web hosting     πŸ‘‰5 Dua za Mitume na Manabii     πŸ‘‰6 Madrasa kiganjani    

Post zinazofanana:

Mbu (mosquito)

Posti hii inakwenda kukupa sifa za mdudu mbu

Soma Zaidi...
Ni kwa namna gani nyoka husikia ijapokuwa hana masikio

Ingawa nyoka hawana masikio ya nje kama binadamu na wanyama wengine, bado wana uwezo wa kusikia. Hutumia mifupa ya kichwa na viungo vya ndani kutambua mitetemo kutoka ardhini na mawimbi ya sauti yenye mzunguko mdogo.

Soma Zaidi...
ABOUT BONGOCLASS

learn English Vocabulary

Soma Zaidi...
ZOEZI

Zoezi laΒ 1 (a) Ainisha maana ya sunnah kilugha na kisheria.

Soma Zaidi...
Historia fupi ya kuingia kwa wakoloni Tanzania

Hapa utakwenda kujifunza namna ambavyo ukoloni uliingia Tanzania na vipindi vyake. Utajifunza hatuwa ambazo ukoloni uliweza kupiti na hatimay kuitawala Tanzania

Soma Zaidi...