image

Fahamu kuhusu ugonjwa wa vidonda vya tumbo (Peptic ulcers)

Vidonda vya tumbo ni vidonda vilivyo wazi vinavyotokea kwenye utando wa ndani wa umio, tumbo na sehemu ya juu ya utumbo wako. Dalili ya kawaida ya Peptic ulcer ni maumivu ya tumbo. Vidonda vya tumbo ni pamoja na: Vidonda vya tumbo vinavyotokea ndani

Kuna aina mbili za vidonda vya tumbo ni pamoja na:

 1.Vidonda vya tumbo vinavyotokea ndani ya tumbo, Vidonda vya umio vinavyotokea ndani ya mirija yenye mashimo vinavyojulikana kama (esophagus) ambayo husafirisha chakula kutoka kooni hadi tumboni mwako.

 Vidonda vinavijitokeza kwenye utombo mdogo  duodenal vinavyotokea ndani ya sehemu ya juu ya utumbo ndogo ambavyo hujulikana kama (duodenum).

 

 DALILI ZA VIDONDA VYA TUMBO NI KAMA IFUATAVYO;

 1.Maumivu ya kuungua ndiyo dalili inayojulikana zaidi ya vidonda vya tumbo (Peptic ulcers). Maumivu hayo husababishwa na kidonda na huchochewa na asidi ya tumbo. (Ulcerated).

 

2. Maumivu kuanzia chini ya kitovu hadi kupandisha kwenye mfupa wako matiti

 

3. Maumivu endapo hujala tumbo lipo tupu.

 

4.Kuwaka moto nyakati za usiku (burning sensation).

 

5Kutapika damu dalili ikiwa Sugu sana inaweza kupelekea mgonjwa kutapika damu nyekundu au nyeusi kabisa.

 

4kinyesi kutoka kikiwa na damu nyeusi pia ugonjwa wa vidonda vya tumbo ukiwa chronic sana hupelekea mgonjwa kinyesi kuwa cheusi.

 

5. Kichefuchefu au kutapika, maumivu ya moto kwenye tumbo hiwa yanapanda hadi kwenye sehemu ya kifuani na haya maumivu hupelekea mgonjwa kupatwa na kichefuchefu.

 

6. Kupunguza uzito kusikoelezeka, Mgonjwa anaweza kukondonda kutoka na maumivu makali ya umio kwenye tumbo na kudhohofika kwa mwili pia.

 

7. Hamu kubadilika (appetite changes) kama vile kula, kukosa usingizi, n.k

 

SABABU ZINAZOSABABISHA VIDONDA VYA TUMBO;

1. Asidi; Vidonda vya tumbo hutokea pale ambopo asidi imezid kwenye njia ya usagaji wa chakula katika sehemu ya ndani ya umiokwenye tumbo au utumbo mdogo. Asidi hii inaweza kusababisha kidonda kinachoumiza ambacho kinaweza kuvuja damu.

 

 2. Kama njia yako ya usagaji chakula imefunikwa na utando wa makamasi (mucous) ambao kwa kawaida hulinda dhidi ya asidi. Lakini ikiwa kiwango cha asidi kikiongezwa au kiwango cha kamasi kimepungua, unaweza kupata vidonda vya tumbo

 

3.Bakteria.  Bakteria ambao hujulikana kama Helicobacter pylori kwa kawaida huishi kwenye utando wa makasi (mucous) unaofunika na kulinda tishu zinazozunguka tumbo na utumbo mdogo. Mara nyingi,  bacteria wa Helicobacter pylori hawasababishi matatizo, lakini wanaweza kusababisha kuvimba kwa safu ya ndani ya tumbo, na kusababisha ugonjwa wa vidonda vya vitumbo.Haijulikani jinsi H. pylori huenea. Inaweza kupitishwa kutoka kwa mtu hadi kwa mtu kwa mawasiliano ya karibu, kama vile kumbusu. Watu wanaweza pia kuambukizwa H. pylori kupitia chakula na mamaji.

 

04.Matumizi ya mara kwa mara ya dawa fulani za kupunguza maumivu.  Baadhi ya dawa za  za maumivu zinaweza kuwasha utando wa tumbo au utumbo wako mdogo. Dawa hizi ni pamoja na aspirin, ibuprofen (Advil, Motrin IB, zingine), naproxen (Aleve, Anaprox,  nyingine), ketoprofen na nyinginezo. Vidonda vya tumbo huwapata watu wazima zaidi wanaotumia dawa hizi za maumivu mara kwa mara.

 

MAMBO HATARI

 Unaweza kuwa na hatari zaidi ya Peptic ulcers kama:

1.Moshi.  Uvutaji sigara unaweza kuongeza hatari ya VidondaVidonvya tjmbo kwa watu walioambukizwa bacteria wa H. pylori.

 

2.Kunywa pombe.  Pombe inaweza kuwasha na kuharibu utando wa makamasi (mucous) wa tumbo lako, na huongeza kiwango cha asidi ya tumbo inayozalishwa.

 

 MATATIZO YANAYOPELEKEA VIDONDA VYA TUMBO; 

Vidonda vya tumbo visipotibiwa vinaweza kusababisha:

1. Kutokwa na damu kwa ndani.  Kuvuja damu kunaweza kutokea kama upotezaji wa damu polepole ambao husababisha Anemia au upotezaji mkubwa wa damu ambao unaweza kuhitaji kulazwa hospitalini au kutiwa damu mishipani. Kupoteza sana damu kunaweza kusababisha matapishi meusi au yenye damu au kinyesi ccheusi chenye damu.

 

2.Maambukizi.  Vidonda vya tumbo vinaweza kula tundu kupitia ukuta wa tumbo lako au utumbo mdogo, hivyo kukuweka katika hatari ya kuambukizwa kivimbe chako cha tumbo (Peritonitisi).

 

3. Kovu kidonda.  Vidonda vya tumbo pia vinaweza kutoa tishu zenye kovu zinazoweza kuzuia kupita kwa chakula kwenye njia ya usagaji chakula, hivyo kukufanya ujae kwa urahisi, kutapika na kupunguza uzito.

 

 Mwisho; ugonjwa wa vidonda vya tumbo sio mzuri kwahy endapo utapata dalili inapaswa kuwahi hospital na kupata vipimo na matibabu.Ni hadithi potofu kwamba vyakula vikali au kazi yenye mkazo inaweza kusababisha Vidonda vya tumbo sasa inajulikana kwamba maambukizo ya bakteria au baadhi ya dawa sio mkazo au lishe husababisha vidonda vya tumbo.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Mankaa Tarehe 2024-08-08 18:19:19 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 125


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zifazofanana:-

Jifunze zaidi mzunguko wa mfumo wa damu kwa binadamu
Posti hii inahusu zaidi mfumo wa mwili ambao huhusika na kusafirisha damu ,virutubisho na takamwili.mfumo huu unajumuisha damu,mishipa ya damu na moyo.moyo husukuma damu kupitia mishipa ya damu na kufika maeneo yote ya mwili. Soma Zaidi...

Sababu za maumivu ya tumbo kitovuni na dalili zake
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo kitovuni na dalili zake Soma Zaidi...

Vitu vinavyochochea kuwepo kwa Ugonjwa wa ukimwi.
Posti hii inahusu zaidi vitu ambavyo vinasababisha kuongezeka kwa Ukimwi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na baada ya watu kujua Ugonjwa huu na matokeo ila bado ugonjwa unazidi kuongezeka. Soma Zaidi...

Dalili za ugonjwa wa Donda koo
Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa Donda Koo ni ugonjwa unaosababishwa na vimelea viitwavyo kwa kitaalamu corynebacterium diphtheria, ugonjwa huu ushambulia Koo na unaweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya hewa, mate na Soma Zaidi...

Fahamu Ugonjwa wa kifua kikuu kwa watoto chini ya miaka mitano
Posti hii inaonyesha mambo mbalimbali yanayoweza kusababisha Ugonjwa wa kifua kikuu kwa watoto chini ya miaka mitano. Soma Zaidi...

Ni Nini husababisha kinjwaa kutoa harufu mbaya?
Posti hii inaelezea kuhusiana na sababu zinazosababisha kinjwa au mdomo kutoa harufu mbaya? Soma Zaidi...

Fahamu Dalili za Ugonjwa wa Bawasiri
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa wa Bawasiri. Bawasiri ni mishipa iliyovimba kwenye njia yako ya haja kubwa na sehemu ya chini ya puru. Bawasiri inaweza kutokana na kukaza mwendo wakati wa kwenda haja ndogo au kutokana na shinikizo la kuongeze Soma Zaidi...

NJIA YA KUJIKINGA NA UGONJWA WA VIRUSI VYA VYA UKIMWI NA ATHARI ZAKE
Posti hii inahusisha maambukizi ya virusi vya ukimwi .pia  tutangalia  njia za kujikinga na  ugonjwa wa UKIMWI Soma Zaidi...

Dalili za maumivu ya uti wa Mgongo
Posti hii inahusu zaidi dalili za uti wa mgongo ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye tatizo la uti wa Mgongo. Soma Zaidi...

Kupambana na kisukari
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kupambana na kisukari Soma Zaidi...

Dalili za VVU/UKIMWI Ni zipi
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za VVU/ UKIMWI Soma Zaidi...

NINI CHANZO CHA UGONJWA WA MALARIA? NI YUPI MBU ANAYESAMBAZA MALARIA
Malaria husababishwa na vimelea (parasite) ambavyo husambazwa ama kubebwa na mbu aina ya anopheles. Soma Zaidi...