Fahamu kuhusu ugonjwa wa vidonda vya tumbo (Peptic ulcers)
Vidonda vya tumbo ni vidonda vilivyo wazi vinavyotokea kwenye utando wa ndani wa umio, tumbo na sehemu ya juu ya utumbo wako. Dalili ya kawaida ya Peptic ulcer ni maumivu ya tumbo. Vidonda vya tumbo ni pamoja na: Vidonda vya tumbo vinavyotokea ndani
Kuna aina mbili za vidonda vya tumbo ni pamoja na:
1.Vidonda vya tumbo vinavyotokea ndani ya tumbo, Vidonda vya umio vinavyotokea ndani ya mirija yenye mashimo vinavyojulikana kama (esophagus) ambayo husafirisha chakula kutoka kooni hadi tumboni mwako.
Vidonda vinavijitokeza kwenye utombo mdogo duodenal vinavyotokea ndani ya sehemu ya juu ya utumbo ndogo ambavyo hujulikana kama (duodenum).
DALILI ZA VIDONDA VYA TUMBO NI KAMA IFUATAVYO;
1.Maumivu ya kuungua ndiyo dalili inayojulikana zaidi ya vidonda vya tumbo (Peptic ulcers). Maumivu hayo husababishwa na kidonda na huchochewa na asidi ya tumbo. (Ulcerated).
2. Maumivu kuanzia chini ya kitovu hadi kupandisha kwenye mfupa wako matiti
3. Maumivu endapo hujala tumbo lipo tupu.
4.Kuwaka moto nyakati za usiku (burning sensation).
5Kutapika damu dalili ikiwa Sugu sana inaweza kupelekea mgonjwa kutapika damu nyekundu au nyeusi kabisa.
4kinyesi kutoka kikiwa na damu nyeusi pia ugonjwa wa vidonda vya tumbo ukiwa chronic sana hupelekea mgonjwa kinyesi kuwa cheusi.
5. Kichefuchefu au kutapika, maumivu ya moto kwenye tumbo hiwa yanapanda hadi kwenye sehemu ya kifuani na haya maumivu hupelekea mgonjwa kupatwa na kichefuchefu.
6. Kupunguza uzito kusikoelezeka, Mgonjwa anaweza kukondonda kutoka na maumivu makali ya umio kwenye tumbo na kudhohofika kwa mwili pia.
7. Hamu kubadilika (appetite changes) kama vile kula, kukosa usingizi, n.k
SABABU ZINAZOSABABISHA VIDONDA VYA TUMBO;
1. Asidi; Vidonda vya tumbo hutokea pale ambopo asidi imezid kwenye njia ya usagaji wa chakula katika sehemu ya ndani ya umiokwenye tumbo au utumbo mdogo. Asidi hii inaweza kusababisha kidonda kinachoumiza ambacho kinaweza kuvuja damu.
2. Kama njia yako ya usagaji chakula imefunikwa na utando wa makamasi (mucous) ambao kwa kawaida hulinda dhidi ya asidi. Lakini ikiwa kiwango cha asidi kikiongezwa au kiwango cha kamasi kimepungua, unaweza kupata vidonda vya tumbo
3.Bakteria. Bakteria ambao hujulikana kama Helicobacter pylori kwa kawaida huishi kwenye utando wa makasi (mucous) unaofunika na kulinda tishu zinazozunguka tumbo na utumbo mdogo. Mara nyingi, bacteria wa Helicobacter pylori hawasababishi matatizo, lakini wanaweza kusababisha kuvimba kwa safu ya ndani ya tumbo, na kusababisha ugonjwa wa vidonda vya vitumbo.Haijulikani jinsi H. pylori huenea. Inaweza kupitishwa kutoka kwa mtu hadi kwa mtu kwa mawasiliano ya karibu, kama vile kumbusu. Watu wanaweza pia kuambukizwa H. pylori kupitia chakula na mamaji.
04.Matumizi ya mara kwa mara ya dawa fulani za kupunguza maumivu. Baadhi ya dawa za za maumivu zinaweza kuwasha utando wa tumbo au utumbo wako mdogo. Dawa hizi ni pamoja na aspirin, ibuprofen (Advil, Motrin IB, zingine), naproxen (Aleve, Anaprox, nyingine), ketoprofen na nyinginezo. Vidonda vya tumbo huwapata watu wazima zaidi wanaotumia dawa hizi za maumivu mara kwa mara.
MAMBO HATARI
Unaweza kuwa na hatari zaidi ya Peptic ulcers kama:
1.Moshi. Uvutaji sigara unaweza kuongeza hatari ya VidondaVidonvya tjmbo kwa watu walioambukizwa bacteria wa H. pylori.
2.Kunywa pombe. Pombe inaweza kuwasha na kuharibu utando wa makamasi (mucous) wa tumbo lako, na huongeza kiwango cha asidi ya tumbo inayozalishwa.
MATATIZO YANAYOPELEKEA VIDONDA VYA TUMBO;
Vidonda vya tumbo visipotibiwa vinaweza kusababisha:
1. Kutokwa na damu kwa ndani. Kuvuja damu kunaweza kutokea kama upotezaji wa damu polepole ambao husababisha Anemia au upotezaji mkubwa wa damu ambao unaweza kuhitaji kulazwa hospitalini au kutiwa damu mishipani. Kupoteza sana damu kunaweza kusababisha matapishi meusi au yenye damu au kinyesi ccheusi chenye damu.
2.Maambukizi. Vidonda vya tumbo vinaweza kula tundu kupitia ukuta wa tumbo lako au utumbo mdogo, hivyo kukuweka katika hatari ya kuambukizwa kivimbe chako cha tumbo (Peritonitisi).
3. Kovu kidonda. Vidonda vya tumbo pia vinaweza kutoa tishu zenye kovu zinazoweza kuzuia kupita kwa chakula kwenye njia ya usagaji chakula, hivyo kukufanya ujae kwa urahisi, kutapika na kupunguza uzito.
Mwisho; ugonjwa wa vidonda vya tumbo sio mzuri kwahy endapo utapata dalili inapaswa kuwahi hospital na kupata vipimo na matibabu.Ni hadithi potofu kwamba vyakula vikali au kazi yenye mkazo inaweza kusababisha Vidonda vya tumbo sasa inajulikana kwamba maambukizo ya bakteria au baadhi ya dawa sio mkazo au lishe husababisha vidonda vya tumbo.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Dalili za maambukizi kwenye uume
Post hii inahusu zaidi dalili za maambukizi kwenye uume, ni dalili ambazo ujitokeza pale maambukizi yanapotokea kwenye uume.
Soma Zaidi...Maandalizi ya kisaikolojia na kimwili kabla ya kubeba mimba.
Kupanga kupata mtoto ni uamuzi mkubwa na wa furaha katika maisha ya mtu. Hata hivyo, safari hii haihitaji tu matamanio, bali inahitaji maandalizi ya kina. Makala hii inaangazia misingi ya kujiandaa kisaikolojia na kimwili ili kuhakikisha afya ya mama na mtoto, na kuimarisha utayari wa kuwa mzazi katika kipindi chote cha ujauzito
Soma Zaidi...Njia za kuzuia uwepo wa ugonjwa wa Bawasili.
Posti hii inahusu zaidi njia au mbinu ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuepuka kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili kwenye jamii, hizi ni njia za awali za kupambana na kuwepo kwa Ugonjwa wa Bawasili.
Soma Zaidi...Fahamu Ugonjwa wa mshtuko wa sumu.
Ugonjwa wa Mshtuko wa Sumu ni matatizo ya nadra, yanayotishia maisha ya aina fulani za maambukizi ya bakteria. Mara nyingi ugonjwa wa mshtuko wenye sumu hutokana na sumu zinazozalishwa na bakteria.
Soma Zaidi...Tatizo la kutokwa na damu puani: Nini cha kufanya?
Kutokwa na damu puani ni hali inayoweza kumtisha mtu yeyote, hasa kwa sababu ya kuona damu ikitiririka ghafla. Ingawa mara nyingi inaonekana kuwa tatizo kubwa, ukweli ni kwamba sehemu kubwa ya visa hivi ni vidogo na vinaweza kutatuliwa kwa hatua rahisi za nyumbani. Makala haya yanakupa mwongozo wa jinsi ya kudhibiti hali hii kwa usahihi na wakati gani unapaswa kutafuta msaada wa kitabibu.
Soma Zaidi...Dalilili za tetekwanga
posti hii inazungumziaTetekuwanga . Tetekwanga(varisela) ni maambukizi ya virusi ambayo husababisha kuwasha, kama vile upele. Tetekuwanga huambukiza sana watu ambao hawajapata ugonjwa huo wala kupewa chanjo dhidi yake. Kabla ya chanjo ya mara kwa mara
Soma Zaidi...